Chenge ashikiliwa polisi kwa ajali ya gari iliyosababisha vifo

Chenge ashikiliwa polisi kwa ajali ya gari iliyosababisha vifo

inavyosemekana ni kuwa Chenge na marehemu vicky walikuwa ni marafiki wa muda mrefu.

ila siku ile ya tukio,walikuwa wakipata kinywaji pamoja akiwa na rafiki yake huyo waliepata ajali pamoja. ilipokuwa inakaribia hiyo saa kumi alfajiri walikorofishana chenge na huyo vicky,ndipo wakaamua kuchukua kibajaj waondoke zao kwa hasira. huyu bwana aliporudi akaambiwa jamaa wameshaondoka na kibajaj,ndipo akaamua kuwafukuza alipkuwa karibu kukifikia akajaribu kubloc kwa mbele ndipo ajali ikatokea.

Kwa hiyo habari ndiyo hiyo,mama nae kule mwanza kathibitisha mahusiano ya chenge na binti yake huyo kwa hiyo wasitupige changa la macho.!!!!!!
 
Ajali Dar: Chenge adaiwa kujuana na mmoja wa marehemu

Frederick Katulanda,Mwanza
SAKATA la ajali ya gari la Andrew Chenge ambalo limesababisha vifo vya wanawake wawili, limeingia katika sura mpya baada ya ndugu wa wasichana hao kudai kuwa Chenge alikuwa akimfahamu mmoja wa marehemu.

Chenge ambaye alikuwa Waziri na Mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali, aliingia matatani baada ya gari alilokuwa akiendesha kugonga "bajaji" usiku wa kuamkia juzi na kuua wanawake wawili ambao ni Beatrice Costantine ambaye ni mfanyabiashara wa Mwanza na mmiliki wa saluni ya kike na Vicky George Makanya.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Mwanza baadhi ya ndugu waliohojiwa na Mwananchi Jumapili akiwamo mama mzazi wa Vicky, walisema wanafahamu Chenge kuwa alikuwa akimjua ndugu yao Vicky.

Akizungumza na Mama wa marehemu Vicky, Nazifa Kambi nyumbani kwao Iloganzala ambako kuna matanga alisema amesikitishwa na taarifa za upotoshaji zilizoeleza kuwa mwanae na rafiki yake walikuwa wakienda Zanzibar kwa ajili ya kufunga ndoa jambo ambalo alilipinga na kueleza kuwa alikuwa akija Mwanza baada ya kutoka Zanzibar ambako walikwenda kununua vifaa vya saluni ya mwenzake.

"Ajali hii inanipa mashaka makubwa kutokana na kupokea taarifa za kupotosha za kufunga ndoa," alisema.
Alisema pia amepata taarifa kutoka kwa wafanyakazi wenzake kuwa Chenge walikuwa wakifahamiana na Vicky na kwamba kila mara alipokuwa akifika Mwanza Hotel alikuwa akimtaka kumhudumia vinywaji yeye.

Nazifa alisema marehemu Vicky ambaye alikuwa mfanyakazi wa Mwanza Hotel katika kitengo cha King Casino ambayo kwa sasa inajulikana kama The Stone, hata yeye mwenyewe aliwahi kumsikia mwanaye kuhusu mbunge huyo kumtaka atoke nyumbani kwenda kumhudumia siku ambayo hakuwa kazini.

Ameiomba serikali kufanya uchunguzi wa kina kuhusu ajali hiyo ili kupata nini kilichosababisha ajali hiyo.
Kwa upande wa msemaji wa familia ya Beatrice, kaka wa marehemu, Andrew Costantine akiwa Kiseke kwenye matanga alisema wanachofahamu wao ni kuwa dada yake amepatwa ajali akiwa njiani kurejea hotelini walikofikia ya JVL Hotel iliyopo Mwananyamala wakati wakitoka Oysterbay kwa ajili ya kuchukua mizigo yao tayari kwa kuondoka Dar es Salaam kwenda Mwanza.
Andrew alieleza kuwa tayari marehemu na rafiki yake walikuwa wamekwisha kutoka Zanzibar ambako walikwenda kununua bidhaa na vifaa vya saluni ya kike ambavyo vimekutwa hotelini walikokuwa wamefikia.
Alisema marehemu hakuwa amekwenda kufunga ndoa Zanzibar kwa vile alikuwa na mume wake ambaye ni mzungu raia wa Marekani na kwamba mpaka anafikwa na mauti mme wake alikuwa nje ya nchi.
Alisema habari zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa walikuwa wakienda kufunga ndoa siyo za kweli.
"Wakati wakiondoka alimuaga rafiki yake Khadija Hassani ambaye ndiye alimuachia nyumba yake na wakati akiwa Zanzibar alimtumia fedha kwa ajili ya kuwalipia ada ya shule watoto, sasa mambo mengine hakuna anayejua tunaomba uvumulivu msiba uishe," alieleza.

Alisema mpaka sasa Chenge ameahidi kusaidia familia kusafirisha miili ya marehemu hao, lakini bado hawajapokea lolote kutoka kwake na wanaendelea kumsubiria wakati polisi wakikamilisha taratibu za uchunguzi huku na wao wakijipanga kusafirisha miili ya ndugu zao.
Msiba hii imeacha simanzi Jijini Mwanza na kuwa gumzo kubwa huku ukizua minog'ono ya hapa na pale na baadhi ya wakazi wa jiji la Mwanza wengine wakishangazwa na tukio hilo na jinsi jeshi la polisi lilivyounda tume kushughulikia ajali hiyo tofauti na ajali nyingine.
Marehemu hao waliondoka Jijini Mwanza Machi 24, mwaka huu kwa safari ya kibiashara Dar es salaam na baadaye Zanzibar na walikuwa wakitarajiwa kureja Ijumaa Machi 27, Beatrice ameacha watoto wanne ambao wanasoma shule tofauti za bweni na mwenzake Vicky ameacha mtoto mmoja mwenye umri wa miaka mitano.
Hata hivyo, juhudi za kumpata Chege kwa simu jana hazikuzaa matunda jana.

Hizi taarifa sasa zinaleta mkanganyiko mkubwa sana.......there must be something behind the scene!
 
Sasa na yule Bwana Constantine kaka wa marehemu Beatrice kwa nini alisema uwongo au why Beatrice alimwambia kaka yake kuwa rafiki yake huyo Vicky anakwenda Zanzibar kuolewa? Wakati mama wa marehemu anakana hakuna harusi? Nini kinaendelea jamani?
 
inavyosemekana ni kuwa Chenge na marehemu vicky walikuwa ni marafiki wa muda mrefu.

ila siku ile ya tukio,walikuwa wakipata kinywaji pamoja akiwa na rafiki yake huyo waliepata ajali pamoja. ilipokuwa inakaribia hiyo saa kumi alfajiri walikorofishana chenge na huyo vicky,ndipo wakaamua kuchukua kibajaj waondoke zao kwa hasira. huyu bwana aliporudi akaambiwa jamaa wameshaondoka na kibajaj,ndipo akaamua kuwafukuza alipkuwa karibu kukifikia akajaribu kubloc kwa mbele ndipo ajali ikatokea.

Kwa hiyo habari ndiyo hiyo,mama nae kule mwanza kathibitisha mahusiano ya chenge na binti yake huyo kwa hiyo wasitupige changa la macho.!!!!!!

walikuwa wakinywa baa gani au hoteli gani???
 
Huo ndo utaratibu wa Bongo! Hizo sticker nimezinunua sana, na sijawahi kufanyiwa ukaguzi wowote, na sikutoa rushwa.
Hizo sticker ni njia ya kukusanya pesa tu hakuna lingine lolote.
Mheshimiwa Kang,

Kuzinunua hizo sticker bila ukaguzi ndio Rushwa yenyewe, Wewe unazinunua 5000 kukwepa kupeleka gari kukaguliwa, ungepeleka gari ungelipa 3000TShs, Hata kama ni mradi wa kukusanya pesa lakini ndio sheria, haijali kama ni mbaya au nzuri, Msheshimiwa na wewe ni miongoni wa watoa rushwa, ili kutokomeza rushwa inabidi kila mtu atimize wajibu wake.

Regards
Kipa
 
kuna jamaa alisema kwamba eneo la ajali hakukuwa na DAMU je kuna ukweli wowote? hii inaweza kuwa clue muhimu.

Ajali hii inaleta shaka kutokana na ukweli kuwa
1. Wahusika wa ajali wanafahamiana sana (Chenge na Vick)
2. Dereva wa bajaj hajapatikana
3. Mmiliki wa bajaj hajajitokeza licha ya kutakiwa na polisi tena kwa kutajwa jina (Zuwena)
4. Wahusika wote inaonekana walitoka eneo moja yaani bar au casino/kwenye ulevi
 
Msheshimiwa Mwiba,

Kweli Wadanganyika tuna safari ndefu, haya ngoja nijaribu na mimi kukuelimisha

Insurance ( Bima ) ndio iliyokwisha 2007 Zanzibar insurance company ni shirika mama la bima lilosajiliwa kwa ajili ya kutoa bima mbalimbali ikiwemo ya magari, shirika hili lina mawakala wako wanoliwakilisha, ukiangalia hiyo sticker iliyokwisha 2007 kwenye maandishi ya juu yaliyozunguka nusu duara utaona Zanzibar insurance.... na katikati ya hiyo sticker utaona jina la wakala wa zanziba insurance.Valididty yake ni mwaka mmoja

Road License ( ni leseni ya barabarani ) kwa kifupi ni ruhusa ya gari kutembea barabarani hii hulipiwa TRA ndio inayoonekana inaisha 2009 hapo kwenye sticker. Validity yake ni mwaka mmoja kama ilivyo bima

Tofauti zake: Wakati leseni ya barabarani inaruhusu gari kutembea barabarani lakini haiwezi kulipia fidia ikitokea ajali kazi ya fidia ni ya bima, zote hizi zinakuwa na details kama vile aina ya gari engine na chasis no tarehe ilipotengenezwa jina na anuani za mmiliki nguvu ya injini, BIMA inakwenda zaidi na kutaja thamani ya gari, Kwajili details hizi ni nyingi haziwezi kukaa zote kwenye sticker inayobandikwa kwenye gari basi hupewa karatasi nyingine yanye vitu hivyo hizo sticker zinakuwa na summary tu.

Kwa mtaji huu WEWE NDIO ULIEDANDIA TRENI MBELE HUKU LIKIWA KWENYE MWENDO KASI ANGALIA UTAGONGWA.

Salaaam
Kipa
 
inavyosemekana ni kuwa Chenge na marehemu vicky walikuwa ni marafiki wa muda mrefu.

ila siku ile ya tukio,walikuwa wakipata kinywaji pamoja akiwa na rafiki yake huyo waliepata ajali pamoja. ilipokuwa inakaribia hiyo saa kumi alfajiri walikorofishana chenge na huyo vicky,ndipo wakaamua kuchukua kibajaj waondoke zao kwa hasira. huyu bwana aliporudi akaambiwa jamaa wameshaondoka na kibajaj,ndipo akaamua kuwafukuza alipkuwa karibu kukifikia akajaribu kubloc kwa mbele ndipo ajali ikatokea.

Kwa hiyo habari ndiyo hiyo,mama nae kule mwanza kathibitisha mahusiano ya chenge na binti yake huyo kwa hiyo wasitupige changa la macho.!!!!!!


.......The Plot Thickens.....!
 
mwizi ni mwizi na hatosheki....
hata insurance huna....
halafu kwa confidence zote unasema ulikua speed kati ya 80 -100 kmph kwenye maeneo ya makazi ya watu. hiyo ni speed kubwa sana kwenye maeneo ya watu.

huyu jamaa hana akili nina shindwa kueluewa hivyo vyeti vyake alivipataje
1. mara ya kwanza alivyoulizwa swali akajibu vijisenti
2. leo anatuambia alikua speed 80 -100 kwa confidence jamani huyu kweli ni
mwanasheria, ndio maana mikataba mingi ilikua mibovu chini yake

asante sana
 
Jamani hebu waandishi/familia idai kuona taarifa ya posmoterm.
Je, kifo kimesababishwa na ajali ya gari la Chenge, au kitu/gari lingine?
Je, dereva wa bajaji alikuwapo na aliumia na kuchukuliwa na polisi????
Je, gari alilosema Chenge lililokuwa nyuma yao ni la nani? Lilifanya nini?
Chenge alikuwa na kiongozi mwingine wa CCM toka kanda ya ziwa, walitoka wapi?
Bajaji haikugongana na gari la Chenge, iligongwa kwa nyuma, walikuwa wakifukuzana?
Wanafahamina, kwanini wengine walipanda bajaji, au waligombana?
 
Jamani hebu waandishi/familia idai kuona taarifa ya posmoterm.
Je, kifo kimesababishwa na ajali ya gari la Chenge, au kitu/gari lingine?
Je, dereva wa bajaji alikuwapo na aliumia na kuchukuliwa na polisi????
Je, gari alilosema Chenge lililokuwa nyuma yao ni la nani? Lilifanya nini?
Chenge alikuwa na kiongozi mwingine wa CCM toka kanda ya ziwa, walitoka wapi?
Bajaji haikugongana na gari la Chenge, iligongwa kwa nyuma, walikuwa wakifukuzana?
Wanafahamina, kwanini wengine walipanda bajaji, au waligombana?

...mungu wangu, kesi inazidi kuongezeka wigo. Wanaume wawili, wanawake wawili, walikuwa wanakunywa pamoja;

wanawake 'wakawatoroka' kwa kutumia usafiri wa Bajaj, wanaume wakawakimbiza kwa hilo Toyota,... Ajali, ...

au;

Walishauwawa kitambo, halafu hiyo bajaji ikaegeshwa hapo na miili (maiti) kisha Toyota ikaja igonga?

WHY? kwanini?
 
statement ya chenge, kupitia habarileo::::


"""“Bajaj ile ilikuwa inataka kupita gari jingine lililokuwa likitoka Morogoro Stores, bahati mbaya kukawa na gari lingine linakuja, ile bajaj ikabana upande wangu na mimi nilikuwa katika mwendo wa kati ya kilometa 80 hadi 100 kwa saa,“ alidai Chenge. Alidai kuwa baada ya kuona bajaj ile inakwepa gari la mbele wasigongane uso kwa uso, alirudi upande wa kulia ndipo alipoigonga ubavuni kushoto. "Gari la nyuma lingesimama, dereva wake angeweza kueleza vizuri, ila baada ya ajali nikasikia watu wanaita 'Chenge! Chenge!’ nikajua niko salama, nikashuka,“ alidai. ""

Conclusion yangu ni kuwa:::

Chenge ndiye aliyekuwa anataka kuipita bajaj kwa mwendo wa kasi, na alipoona kuna gari linakuja upande wa kulia akakwepa head on collision ndio akarudi kwenye lane iliyokuwa bajaj, na kuigonga kwa upande wake wa kushoto.

Swali gumu nalopata ni kwanini dereva wa bajaj kakimbia?? Sioni sababu yoyote ya yeye kukimbia?? Je amekimbia au kawekwa sehemu?? Nadhani utata wote upo hapo, lakini kiutaalamu hii accident picha na maelezo ya chenge, conclusion ni hiyo tu, yeye ndiye aliyekuwa anataka kuovertake.

MImi ningekuwa ndo chenge nisingeongea neno hata limoja maana GIVING REASONS IS A VERY BIG WEAKNESS CHENGE...YOU ARE JUST TOO MUCH!!!!
 
Si afadhali Chenge anajulikana moyo wake mkavu hana huruma, mimi hao maafande wanaojichekesha ndio hata sielewi kilicho funny kuhusu ajali ni nini yani.

Halafu hatufundishwi toka utoto kuwa ajali ni noma, usalama barabarani ni muhimu, watoto wanaachiwa waje kupiga chabo katikati ya scene of an accident, katoto kamoja kakilimwa na truck hapo sijui itakuwaje.
1520.jpg

Haaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa yani kumbe hapa ni eneo la ajali na chenge anachekelea hivi???
 
Jamani hebu waandishi/familia idai kuona taarifa ya posmoterm.
Je, kifo kimesababishwa na ajali ya gari la Chenge, au kitu/gari lingine?
Je, dereva wa bajaji alikuwapo na aliumia na kuchukuliwa na polisi????
Je, gari alilosema Chenge lililokuwa nyuma yao ni la nani? Lilifanya nini?
Chenge alikuwa na kiongozi mwingine wa CCM toka kanda ya ziwa, walitoka wapi?
Bajaji haikugongana na gari la Chenge, iligongwa kwa nyuma, walikuwa wakifukuzana?
Wanafahamina, kwanini wengine walipanda bajaji, au waligombana?

Mkuu wangu Halisi,

Mbona makubwa hayo tena? Waligombana na kuanza kufukuzana?

Umri kama wa Chenge, saa 10 usiku bado anavinjari viwanja mjini?

Hawa wabunge wanakuwa majimboni kwao saa ngapi?
 
Habari zinasema leo angepelekwa mahakamani, jee hilo limefanyika? au anasubiriwa yule mwanasheria wake wa Marekani/Uingereza? Tupasheni habari mlio nazo
 
Habari zinasema leo angepelekwa mahakamani, jee hilo limefanyika? au anasubiriwa yule mwanasheria wake wa Marekani/Uingereza? Tupasheni habari mlio nazo

Amepelekwa mahamani kwa mbwembwe na waandishi wengi walizuiwa kuingia mahakamani. Na tayari amepata dhamana kiulaini kabisa. Anakwenda kulala home kwake. Alifika kwa gari la polisi hyundai na kuingia moja kwa moja kizimbani na hakimu akaingia saa hiyo hiyo kama walipanga muda na mchezo ukaisha.

Upelelezi haujakamilika!
 
Amepelekwa mahamani kwa mbwembwe na waandishi wengi walizuiwa kuingia mahakamani. Na tayari amepata dhamana kiulaini kabisa. Anakwenda kulala home kwake. A.lifika kwa gari la polisi hyundai na kuingia moja kwa moja kizimbani na hakimu akaingia saa hiyo hiyo kama walipanga muda na mchezo ukaisha. Upelelezi haujakamilika!!!!!

Chenge amesomewa mashtaka matatu likiwepo la kusababisha vifo vya watu wawili.

Ni kwa Hakimu Mkuu Mkazi wa Wilaya ya Kinondoni Emirius Mchaura.
Mwendesha Mashtaka Mrakibu Msaidizi wa Polisi David Mafimbo.
Chenge anadaiwa kufanya makosa hayo Machi 27 mwaka huu majira ya 10:30 alfajiri katika barabara ya Haile Selasie, karume eneo la Osterbay, Kinondoni.

Mafimbo:
Katika shitaka la kwanza Chenge unashitakiwa kwa kusababisha kifo kupitia uendeshaji wa kizembe katika barabara ya umma, na maelezo ya kosa ni kwamba ukiwaunaendesha gari yenye Namba T. 513 ACE Toyota Hilux Double Cabin uliendesha gari hiyo kizembe na kushindwa kuchukuwa tahadhari kama inavyotakiwa huku ukiendesha upande wa kulia zaidi uliigonga Bajaji yenye namba T 736 AXC, kweli au si kweli?.

Chenge: Si kweli.

Mafimbo: Katika shitaka la pili, Chenge unashitakiwa kwa kusababisha vifo vya watu wawili, na maelezo ya kosa ni kwamba mnamo Machi 27 mwaka huu majira ya 10:30 alfajiri katika barabara ya Haile Selasie, karume Osterbay wilaya ya Kinondoni ukiendesha gari bila kuchukuwa taadhari uliigonga Bajaji na kusababisha vifo vya watu wawili Victoria Gorge na Beatrice Constantini, kweli au si kweli?

Chenge: Si kweli.

Mafimbo : Shitaka la Tatu ni kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha uharibifu wa bajaji, jibu kweli au si kweli?

Chenge: Si kweli.
Baada ya Chenge kukana mashtaka yake yote ASP Mafimbo alimweleza Hakimu Mchauru kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Hakimu Mchauru aliweka wazi masharti ya dhamana ambapo alimweleza mshtakiwa kuwa anatakiwa kusaini hati ya dhamana ya milioni 1/- NA kuwa na mdhamini mmoja atakayesaini hati ya dhamana ya milioni 1/-.

Chenge alikamilisha masharti hayo ya dhamana aliyotakiwa kuyatekeleza na kesi imeahirishwa hadi 30 April mwaka huu.

Kesi iifanyika chumba kidogo cha mahamama alichukuwa takribani dakika 10 hadi 15 tangu Chenge alipowasili mahakamani hapo, ambapo alifika na kupitiliza moja kwa moja kwenye chemba na hakimu kuanza kuendesha kesi huku waandishi wa habari wakisikiliza kesi wakiwa nje ya chumba kutokana na chumba hicho kuwa na nafasi ndogo isiyotoshereza watu wengi kuingia.

Nje ya mahakama ndugu wa Chenge walisikika wakiwasema vibaya waandishi wa habari waliokuwa wakifuatilia kesi hiyo na kutaka kuwazuia wasimpige picha Chenge.

“Hivi mnazani kwakumpigapicha ndugu yetu mtaondokana na umaskini? Kama mnadhani mtatajirika kutokana na kesi hii ya leo basi tutaona kama mtaondokana na umaskini,” alisikika mmoja wa ndugu wa Chenge akiwaambia waandishi wa habari.

Umati wa watu ulifurika katika mahakama hiyo waliofika ili kumshuhudia Kiongozi huyo wa serikali akifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka yake.

Chenge alifikishwa mahakamani hapo majira ya saa 6 mchana akiwa kwenye gari ya polisi na baada ya kuachiwa kwa dhamana aliondoka na gari binafsi yenye namba T ASP 362.
 
chenge kamgonga huyo mwanamke kwa makusudi ili amuue
MASWALI YA KUJIULIZA
1.chenge kila akienda mwanza hotel anapiga simu huyo muhudumu aje kumuhudumia hata kama ni usiku wa manane/hata kama yuko off.( maana yake ni uhusiano wa kimapenzi) je humu ndani wana JF ambao mmeajiriwa sehemu siyo mali yenu mnaweza mkafanya kwa mteja kiasi hicho?
2. huyo mfanyakazi bora mwanza hoteli( vicky marehemu) anakunywa baa moja na chenge usiku wa manane (huo ni uhusiano)
3. kwa wanaume wa JF, mwanamke ametoka Z'bar kununua vifaa vya saloon. Je hivi vifaa vya saloon sio chenge ndio amevinunua??? huyo mwanamke kwa kazi yake ya mwanza hoteli asingeweza kwenda Z'bar kununua vifaa vya saloon alafu awe anakula maisha usiku wa manane maana yake angemaliza mtaji wote wa saloon? Ni jambo la kawaida kwa wanaume tanzania kuwafungulia wanawake saloon, botique na vinginevyo.
4. Chenge kila siku akienda mwanza anampigia huyo mwanamke simu aje kumuhudumia, iweje ashindwe kumpa lift usiku ule? iweje ashindwe kumkodia tax ya maana usiku ule mpaka mwanamke kakimbilia cheap option bajaji? jibu UGOMVI
 
Back
Top Bottom