Heshima mbele,nadhani ni vizuri kuzidi kumwombea mwenzetu chidi benzi ili Mungu ampe ujasiri na nguvu ya ku overcome chochote ambacho kimekuwa kinamsukuma kutumia madawa ya kulevya.kama ni kwasababu ya stress,hasira,upweke nk basi Mungu amsaidie ku overcome.Wakuu,biashara ya drugs haitakaa iishe kwasababu ndio biashara inayolipa zaidi na inaendeshwa na watu wakubwa sana.wafanya biashara wakubwa na viongozi wakubwa.all over the world..sasa cha kufanya sisi wananchi ni kuendelea kupiga kelele kwenye media,kuelimisha jamii zinazotuzunguka na zaidi watoto wetu kuhusu madhara ya madawa ya kulevya.zaidi kuelimisha watoto wetu kwasababu ndio wako targeted zaidi.ila kufikiria kwamba matumizi ya madawa ya kulevya yatapungua ni ndoto za mchana.hili tatizo ni kubwa sana zaidi ya chidi benzi.kama halijakukuta wewe linaweza kumkuta mwingine yoyote kwenye familia yako.be blessed