Chidi Benz ampiga Ray C

Huu ndio ubaya wa kutumia unga wa Pakistan ambayo ni cheap ukikwama utoki ndugu angu Pole sana Makwilo.
 
Hilo gazeti linaripoti .kiJUHA sana, hiyo habari haijulikani kama ni ya mwaka huu au miaka mitatu iliyopita kwa vile haina tarehe. Hakuna background ya kazi ya Ray C kama ni ofisi ya muziki, utangazaji, ofisi ya kubwia unga au danguro....Kwa uandishi huu acheni tuendelee kuwadharau
 
ukiona mwanaume anampiga mangumi na mateke mwanamke ujue huyo mwanaume ana tatizo kubwa kuliko mnaloliona na kuliko atakalosema yeye analo!. Huyo chizi benz siku moja alitaka kumchokoza Kala Pina wa kikosi cha mizinga akiwa jukwaani. Kala pina akamwambia Chidi 'shuka mara moja hapo jukwaani'. Chidi akashuka kama kifaranga kimemwagiwa maji! Sasa anaogopa wanaume,amekazana kuwapiga wanawake tu!
 

Naona hufuatilii yanayojiri hivi sasa.

Ray C ana ofisi yake ya taasisi yake inayoitwa Ray C Foundation. Hii ni asasi inayowasaidia waathirika wa madawa ya kulevya kuachana nayo kwa msaada wa kitabibu. Inasaidia kuwapa wathirika hao dawa za kuondoa sumu mwilini itokanayo na matumizi ya dawa za kulevya, yaani, "narcotics rehabilitation medicine" na kwa namna nyingine "narcotics detoxification". Ni sumu hizi ndizo zinazoleta "utegemezi" (soma "uteja") kwani zinapoingia mwilini husababisha mtumiaji awe anahitaji kutumia dawa hizo za kulevya, kimsingi huwa HAPONI mpaka ziondolewe.

Ni tatizo ambalo limewakumba vijana wengi wa Kitanzania, haswa wasanii wa muziki wa kizazi kipya, ambako Ray C alipitia, mzazi mwenziwe na "Chidi Benz", Mariam alipitia, na pia hata hao wengine wanaodaiwa kuhusika na matumizi ya dawa hizo, kama vile "Chidi Benz".

Binafsi niliwahi kuongea kwa simu na "Chidi Benz". Nilichokiona kwake ni kwamba si mtu anayejiheshimu kwani majibu yake ni ya "ovyo". Nadhani hata hao "mapromota" wa muziki huu wa kizazi kipya wamemkacha kutokana na tabia zake za ajabu ajabu, kuwa na kesi lukuki. Ninachoshangaa ni kwamba Mahakama zetu hazijampa hukumu inayostahili. Je, ni pesa zake anazowahonga makarani na mahakimu ndizo zinazomkwepesha kwenda jela? Hivi akiwekwa ndani MWAKA MMOJA TU, hatabadilika?

Wenye kuwajua wanasheria watoe hoja hiyo - haswa kuhusu kesi ya Mwanaisha - ili Mahakama ichukue hatua ya kuyanusuru maisha yake. Iko siku "Chidi Benz" atakanyaga pabaya na atagombana na mtu ambaye atajihami kwa silaha! Akila "shaba" nani atafaidika na kifo chake?

Mimi ni mjumbe tu na mjumbe hauwawi. Fikisheni ujumbe kwa wahusika. Maisha ya "Chidi Benz" yapo hatarini!

Nimemaliza.
 
Huyo amezidi akifungwa na kuonja jela as ana kesi zingine bado hajaukumiwa na anatenda mengine ni afungwe tu. Amezidi
 

Umeona eeeh, hadi nimeuliza ndio nimepata background, je ni wasomaji wote wa hicho chanzo cha habari wana fursa ya kuuliza? Kwa hiyo mwandishi angeweka sentensi moja tu kuhusu Ray C foundation. Then kuripoti alhamisi, au jumatano bila tarehe halisi inaacha maswali maana kila wiki kuna hizo siku. Anyway inategemeana na wasomaji na upeo wao.
 
Chidi ni kama anapotea,majuzi aliripotiwa alifanya shoo Dodoma uku akiwasha bangi jukwaani.
 

Ulichoandika wewe hakikuwa kwenye mfumo wa swali bali kubeza zaidi.

Jaribu kuuliza kama huelewi, utaelimishwa.
 
Huyu jamaa anapotea kabisa!halafu anaonekana ni MTU mwenye kibri na asieshaurika!Mimi yangu macho tu.
 
hii habari haipo balance kabisa kwanini wameshindwa kumtafuta Chid Beenz nae asikike anasemaje!
tutaamini vipi kama asingiziwi kwa tabia zake za nyuma!?
 
Madawa

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 

Umeongea maneno ya watu milioni 45. Saluti kwako.
Ova.
 
hii habari haipo balance kabisa kwanini wameshindwa kumtafuta Chid Beenz nae asikike anasemaje!
tutaamini vipi kama asingiziwi kwa tabia zake za nyuma!?

kumbe wewe hujaisoma vizuri habari hii, wanasema walimtafuta Chid ili adhibitishe tuhuma hizi ila simu yake ilikuwa imezimwa au kwa lugha nyingine alikuwa hapatikani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…