Chief Kidaha Makwaia alituwakilisha siku ya kuapishwa Malkia Elizabeth II wa Uingereza

Chief Kidaha Makwaia alituwakilisha siku ya kuapishwa Malkia Elizabeth II wa Uingereza

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1566955289981.jpeg


David Kidaha Makwaia Pichani, yupo na mwingereza Lord Iveagh siku ya kutawazwa kwa malkia Elizabeth mwaka 1956.

Chifu David kidaha, alikuwa ni chifu wa wasukuma, alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 84 ,alikuwa ndio ngazi kati ya ukoloni na machifu ,na baada ya ukoloni barani Afrika na pia alikuwa na urafiki mkubwa na Gavana wa Tanganyika toka mwaka 1949 hadi 1958, Lord Twining.
Mwakwaia alicheza katikati ya viongozi wa Kiingereza na machifu wa majimbo kadhaa ya Tanganyika, alishuhudia Kipindi cha mpito cha Afrika mashariki kutoka kipindi cha ubeberu hadi baada ya Uhuru.

Makwaia alizaliwa na kuwa muislamu akiwa ni mtoto wa Chifu wa kisukuma ,Makwaia Ng'wandu wa Bwiha Mkoa wa Shinyanga Tanganyika, alijifunza kilimo katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwanzoni mwa miaka ya 1940 Kabla ya kuingia Chuo cha Lincoln, Oxford ,ambapo alisoma kanuni na utendaji wa Serikali za mitaa ,Falsafa na Siasa.

Maisha ya Makwaia kisiasa yalitoa fursa nyingi katika dunia ya viongozi wa kikoloni Tanzania ,na viongozi wa kikabila ,alimpokea Baba yake uchifu wa Busiha mwaka 1945 na baadae akaja kuwa chifu mkubwa wa wasukuma ,Taasisi yenye zaidi ya machifu 50 ,yenye ofisi yake na bendera kupitia hili akatambulika kwa waingereza kama sauti ya mzawa mwenye mamlaka ,mwaka huohuo akachaguliwa kuwa kati ya wabunge wawili waafrika kwenye baraza la kutunga sheria (Legco).
1566955235969.jpeg
 
View attachment 1191675

David Kidaha Makwaia Pichani, yupo na mwingereza Lord Iveagh siku ya kutawazwa kwa malkia Elizabeth mwaka 1956.

Chifu David kidaha, alikuwa ni chifu wa wasukuma, alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 84 ,alikuwa ndio ngazi kati ya ukoloni na machifu ,na baada ya ukoloni barani Afrika na pia alikuwa na urafiki mkubwa na Gavana wa Tanganyika toka mwaka 1949 hadi 1958, Lord Twining.
Mwakwaia alicheza katikati ya viongozi wa Kiingereza na machifu wa majimbo kadhaa ya Tanganyika, alishuhudia Kipindi cha mpito cha Afrika mashariki kutoka kipindi cha ubeberu hadi baada ya Uhuru.

Makwaia alizaliwa na kuwa muislamu akiwa ni mtoto wa Chifu wa kisukuma ,Makwaia Ng'wandu wa Bwiha Mkoa wa Shinyanga Tanganyika, alijifunza kilimo katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwanzoni mwa miaka ya 1940 Kabla ya kuingia Chuo cha Lincoln, Oxford ,ambapo alisoma kanuni na utendaji wa Serikali za mitaa ,Falsafa na Siasa.

Maisha ya Makwaia kisiasa yalitoa fursa nyingi katika dunia ya viongozi wa kikoloni Tanzania ,na viongozi wa kikabila ,alimpokea Baba yake uchifu wa Busiha mwaka 1945 na baadae akaja kuwa chifu mkubwa wa wasukuma ,Taasisi yenye zaidi ya machifu 50 ,yenye ofisi yake na bendera kupitia hili akatambulika kwa waingereza kama sauti ya mzawa mwenye mamlaka ,mwaka huohuo akachaguliwa kuwa kati ya wabunge wawili waafrika kwenye baraza la kutunga sheria (Legco).
View attachment 1191674
Sky,
Napenda kuchangia kidogo niyajuayo kuhusu Chief David Kidaha Makwaia.

Kwanza mimi nilipata bahati ya kukutana na Chief Kidaha hapa Dar es Salaam
mwaka wa 1968.

Mwanae Edward Makwaia nilikuwa nasomanae darasa moja St. Josephs Convent
School basi siku moja akaniambia kuwa baba yake amekuja kutoka Nairobi kwa
hiyo nimsindikize kwenda kumwamkia.

Hivi ndivyo nilivyobahatika kumuona Chief Kidaha.

Lakini wakati ule mimi mtoto sikuwa najua kwa nini Chief Kidaha alikuwa anaishi
Kenya.

Chief Kidaha baada ya uhuru aliwekwa kizuizini Tunduru kupitia Preventive Dentition
Act ya 1962 na baada ya kutoka aliamua kuhama nchi na kwenda Kenya.

Chief Kidaha Kidaha ni mtoto wa Chief Makwaia Mohamed Mwandu wa Busiya.

1566962505965.png



Wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes katika miaka ya 1980s nilikutana na
Chief Kidaha Makwaia kwenye Nyaraka za Sykes kupitia barua aliyoandika Dr. Wilbard
Mwanjisi.

Dr. Mwanjisi
alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanganyika African Government Servant
Association (TAGSA) mwaka wa 1951 aliandika makala kali sana katika jarida la chama, makala ambayo aliwashambulia Waingereza kiasi Rashid Kawawa akiwa mwanakamati wa Halmashauri Kuu ya TAGSA aliandika barua kuonya kuwa makala hiyo isichapwe bila ya kujadiliwa na Halmashauri Kuu ya TAGSA.

Katika makala hii Dr. Mwanjisi aliitaja hotuba ya Chief Kidaha Makwaia ndania ya LEGCO
kuwa ni hotuba muhimu sana na akamsifia Chief Kidaha Makwaia kuwa ni mwanasiasa
makini wa kupigiwa mfano (‘Doctor Mwanjisi Speaks to TAGSA’ 22 nd December, 1951
(Sykes' Papers),

Katika hotuba hiyo Chief Kidaha alikuwa anaishauri serikali ya Kiingereza kuondoa ile sheria ambayo ilikuwa inawapiga marufuku Waafrika wafanyakazi wa serikali kujishughulisha na siasa.

Kitu ''interesting,'' katika kipindi hiki ni kuwa Chief Kidaha alikuwa na mazungumzo na Katibu wa TAA, Abdul Sykes, mazungumzo haya yakifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes, Abdul akijaribu kumshawishi Chief Kidaha aingie TAA ili wamchague kama Rais kisha waunde TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Mazungumzo haya hayakufanikiwa.

Baada ya uhuru Dr. Mwanjisi na yeye aliwekwa kizuizini na kama alivyofanya Chief Kidaha baada ya kutoka kizuizini alikwenda kuishi Kenya.

Na bahati mbaya sana waandishi wa historia ya TANU hawakutaka kufanya mahojiano yoyote
na marehemu Ally Sykes katika historia ya TANU na kwa hili historia iliyokuja kuandikwa ikakosa mengi muhimu katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Hii ndiyo sababu Chief Kidaha Makwaia haonekani kokote katika historia ya kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Ningependa kuhitimisha kwa kueleza kuwa baada ya kutawazwa kwa Malkia Elizabeth, uongozi wa TAA ulituma salamu za pongezi kwa Malkia kwa kutawazwa kwake barua ya pongezi ilitiwa sahihi na Rais wa TAA Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi Budohi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes.

1566965992194.png

Chief David Kidaha Makwaia
 
Sky,
Napenda kuchangia kidogo kuhusu Chief David Kidaha Makwaia.

Kwanza mimi nilipata bahati ya kukutana na Chief Kidaha hapa Dar es Salaam
mwaka wa 1968.

Mwanae Edward Makwaia nilikuwa nasomanae darasa moja St. Josephs Convent
School basi siku moja akaniambia kuwa baba yake amekuja kutoka Nairobi kwa
hiyo nimsindikize kwenda kumwamkia.

Hivi ndivyo nilivyobahatika kumuona Chief Kidaha.

Lakini wakati ule mimi mtoto sikuwa najua kwa nini Chief Kidaha alikuwa anaishi
Kenya.

Chief Kidaha baada ya uhuru aliwekwa kizuizini Tunduru na Nyerere na baada ya
kutoka aliamua kuhama nchi na kwenda Kenya.

Chief Kidaha Kidaha ni mtoto wa Chief Makwaia Mohamed Mwandu wa Siha.

View attachment 1191693


Wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes katika miaka ya 1980s nilikutana na
Chief Kidaha Makwaia kwenye Nyaraka za Sykes kupitia barua aliyoandika Dr. Wilbard
Mwanjisi.

Dr. Mwanjisi alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanganyika African Government Servant
Association mwaka wa 1951 aliandika makala kali sana katika jarida la chama makala
ambayo aliwashambulia Waingereza kiasi Rashid Kawawa akiwa mwanakamati aliandika
barua kuonya kuwa makala hiyo isichapwe bila ya kujadiliwa na Halmashauri Kuu ya
TAGSA.

Katika makala hii Dr. Mwanjisi aliitaja hotuba ya Chief Kidaha Makwaia ndania ya LEGCO
kuwa hotuba muhimu sana na akamsifia Chief Kidaha Makwaia kuwa ni mwanasiasa
makini wa kupigiwa mfano (‘Doctor Mwanjisi Speaks to TAGSA’ 22 nd December, 1951
(Sykes' Papers),

Katika hotuba hiyo Chief Kidaha Makwaia alikuwa anaishauri serikali ya Kiingereza kuondoa
ile sheria ambayo ilikuwa inawapiga marufuku Waafrika wafanyakazi wa serikali kujishughulisha
na siasa.
Shukran mzee
 
Sky,
Napenda kuchangia kidogoniyajuayo kuhusu Chief David Kidaha Makwaia.

Kwanza mimi nilipata bahati ya kukutana na Chief Kidaha hapa Dar es Salaam
mwaka wa 1968.

Mwanae Edward Makwaia nilikuwa nasomanae darasa moja St. Josephs Convent
School basi siku moja akaniambia kuwa baba yake amekuja kutoka Nairobi kwa
hiyo nimsindikize kwenda kumwamkia.

Hivi ndivyo nilivyobahatika kumuona Chief Kidaha.

Lakini wakati ule mimi mtoto sikuwa najua kwa nini Chief Kidaha alikuwa anaishi
Kenya.

Chief Kidaha baada ya uhuru aliwekwa kizuizini Tunduru kupitia Preventive Dentition Act ya 1962 na baada ya kutoka aliamua kuhama nchi na kwenda Kenya.

Chief Kidaha Kidaha ni mtoto wa Chief Makwaia Mohamed Mwandu wa Busiya.

View attachment 1191693


Wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes katika miaka ya 1980s nilikutana na
Chief Kidaha Makwaia kwenye Nyaraka za Sykes kupitia barua aliyoandika Dr. Wilbard
Mwanjisi.

Dr. Mwanjisi
alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanganyika African Government Servant
Association (TAGSA) mwaka wa 1951 aliandika makala kali sana katika jarida la chama, makala ambayo aliwashambulia Waingereza kiasi Rashid Kawawa akiwa mwanakamati wa Halmashauri Kuu ya TAGSA aliandika barua kuonya kuwa makala hiyo isichapwe bila ya kujadiliwa na Halmashauri Kuu ya TAGSA.

Katika makala hii Dr. Mwanjisi aliitaja hotuba ya Chief Kidaha Makwaia ndania ya LEGCO
kuwa ni hotuba muhimu sana na akamsifia Chief Kidaha Makwaia kuwa ni mwanasiasa
makini wa kupigiwa mfano (‘Doctor Mwanjisi Speaks to TAGSA’ 22 nd December, 1951
(Sykes' Papers),

Katika hotuba hiyo Chief Kidaha alikuwa anaishauri serikali ya Kiingereza kuondoa ile sheria ambayo ilikuwa inawapiga marufuku Waafrika wafanyakazi wa serikali kujishughulisha na siasa.

Kitu ''interesting,'' katika kipindi hiki ni kuwa Chief Kidaha alikuwa na mazungumzo na Katibu wa TAA, Abdul Sykes, mazungumzo haya yakifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes, Abdul akijaribu kumshawishi Chief Kidaha aingie TAA ili wamchague kama Rais kisha waunde TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Mazungumzo haya hayakufanikiwa.

Baada ya uhuru Dr. Mwanjisi na yeye aliwekwa kizuizini na kama alivyofanya Chief Kidaha baada ya kutoka kizuizini alikwenda kuishi Kenya.

Na bahati mbaya sana waandishi wa historia ya TANU hawakutaka kufanya mahojiano yoyote
na marehemu Ally Sykes katika historia ya TANU na kwa hili historia iliyokuja kuandikwa ikakosa mengi muhimu katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Hii ndiyo sababu Chief Kidaha Makwaia haonekani kokote katika historia ya kudai kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Ningependa kuhitimisha kwa kueleza kuwa baada ya kutawazwa kwa Malkia Elizabeth, uongozi wa TAA ulituma salamu za pongezi kwa Malkia kwa kutawazwa kwake barua ya pongezi ilitiwa sahihi na Rais wa TAA Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi Budohi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes.

View attachment 1191697
Chief David Kidaha Makwaia


Nadhani hii ni moja kati ya historia muhimu zilizofichwa makusudi katika siasa za kudai uhuru wa nchi yetu, kwani historia za aina hii zipo nyingi.

Tunataraji sikumoja atatokea mwanahistoria uliyehuru na kuandika upya historia ya kudai uhuru upya bila upendeleo, historia itakayokuwa tunu kwa vizazi vyetu na kutoa heshima kwa wale wote waliochangia vilivyo katika harakati za kudai uhuru lakini kwa makusudi mifumo ilijengwa ili wasahaulike.

It is a high time for dedicated historians to unveil the deliberately hidden history.
 
Nadhani hii ni moja kati ya historia muhimu zilizofichwa makusudi katika siasa za kudai uhuru wa nchi yetu, kwani historia za aina hii zipo nyingi.

Tunataraji sikumoja atatokea mwanahistoria uliyehuru na kuandika upya historia ya kudai uhuru upya bila upendeleo, historia itakayokuwa tunu kwa vizazi vyetu na kutoa heshima kwa wale wote waliochangia vilivyo katika harakati za kudai uhuru lakini kwa makusudi mifumo ilijengwa ili wasahaulike.

It is a high time for dedicated historians to unveil the deliberately hidden history.
Imeandikwa tayari hii hapa...
tapatalk_1545239823039.jpeg
 
View attachment 1191675

David Kidaha Makwaia Pichani, yupo na mwingereza Lord Iveagh siku ya kutawazwa kwa malkia Elizabeth mwaka 1956.

Chifu David kidaha, alikuwa ni chifu wa wasukuma, alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 84 ,alikuwa ndio ngazi kati ya ukoloni na machifu ,na baada ya ukoloni barani Afrika na pia alikuwa na urafiki mkubwa na Gavana wa Tanganyika toka mwaka 1949 hadi 1958, Lord Twining.
Mwakwaia alicheza katikati ya viongozi wa Kiingereza na machifu wa majimbo kadhaa ya Tanganyika, alishuhudia Kipindi cha mpito cha Afrika mashariki kutoka kipindi cha ubeberu hadi baada ya Uhuru.

Makwaia alizaliwa na kuwa muislamu akiwa ni mtoto wa Chifu wa kisukuma ,Makwaia Ng'wandu wa Bwiha Mkoa wa Shinyanga Tanganyika, alijifunza kilimo katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwanzoni mwa miaka ya 1940 Kabla ya kuingia Chuo cha Lincoln, Oxford ,ambapo alisoma kanuni na utendaji wa Serikali za mitaa ,Falsafa na Siasa.

Maisha ya Makwaia kisiasa yalitoa fursa nyingi katika dunia ya viongozi wa kikoloni Tanzania ,na viongozi wa kikabila ,alimpokea Baba yake uchifu wa Busiha mwaka 1945 na baadae akaja kuwa chifu mkubwa wa wasukuma ,Taasisi yenye zaidi ya machifu 50 ,yenye ofisi yake na bendera kupitia hili akatambulika kwa waingereza kama sauti ya mzawa mwenye mamlaka ,mwaka huohuo akachaguliwa kuwa kati ya wabunge wawili waafrika kwenye baraza la kutunga sheria (Legco).
View attachment 1191674
Kumbe wasukuma walianza kukumbatia mabeberu muda mreeeefu sana. Ndio maana wakati wa harakati za uhuru walikuwa bardiiiiiii kama timu flani.
 
Back
Top Bottom