Chief Kidaha Makwaia alituwakilisha siku ya kuapishwa Malkia Elizabeth II wa Uingereza

Chief Kidaha Makwaia alituwakilisha siku ya kuapishwa Malkia Elizabeth II wa Uingereza

Shukrani mkuu, Nitaagiza.๐Ÿ™๐Ÿป๐Ÿ™๐Ÿป๐Ÿ™๐Ÿป
Mokaze,
In Shaa Allah.

Bei ni Shs: 10,000.00 ikiwa utanunua Ibn Hazm.
Kwengine ni kati ya 13,000.00 hadi 15,000.00.

Kuna nakala ya Kiingereza (1998) na Kiswahii (2002).
 
Itabidi siku nikipita maduka hayo nijipatie nakala yangu
Nemo,
Hutajutia uamuzi wako.
Kitabu hiki kilipotoka mwaka wa 1998 ilikuwa September.

Mwezi December kabla ya X Mas The East African Magazine ilifanya ''serialisation''
tatu.

Cambridge Journal of African History ikachapa ''book review,'' tatu za mabingwa wa
African History - John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.

Hadi sasa kitabu kimechapwa mara tatu na kinakwenda toleo la nne.
 
Nemo,
Hutajutia uamuzi wako.
Kitabu hiki kilipotoka mwaka wa 1998 ilikuwa September.
Mwezi December kabla ya X Mas The East African Magazine ilifanya ''serialisation''
tatu.
Camridge Jouranl of African History ikachapa serialisation tatu za mabingwa wa
African History - John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.
Hadi sasa kitabu kimechapwa mara tatu na kinakwenda toleo la nne.

Hakika vizazi vijavyo vitatambua mchango wa kazi zako
 
Duh sasa Nyerere kwa nini alikuwa akiwaweka kizuizini watu wote ambao walikuwa na potential ya kumchallenge?

Sasa kwa nini amuweke ndani Chief Makwawia?

Huyu Nyerere kuna haja ya kumuangalia critically pengine sifa tunazompa nyingine zimepitiliza
Struggling for the fittest, asinge fanya hivo angekuwa mzembe! Mkwaiha alikuwa na nafasi nzuri ya kuwa Rais wa kwanza kupitia wakoloni km JOMO KENYATTA alivo kuwa, lkn mzembe alilewa hela ya wakoloni!
 
View attachment 1191675

David Kidaha Makwaia Pichani, yupo na mwingereza Lord Iveagh siku ya kutawazwa kwa malkia Elizabeth mwaka 1956.

Chifu David kidaha, alikuwa ni chifu wa wasukuma, alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 84 ,alikuwa ndio ngazi kati ya ukoloni na machifu ,na baada ya ukoloni barani Afrika na pia alikuwa na urafiki mkubwa na Gavana wa Tanganyika toka mwaka 1949 hadi 1958, Lord Twining.
Mwakwaia alicheza katikati ya viongozi wa Kiingereza na machifu wa majimbo kadhaa ya Tanganyika, alishuhudia Kipindi cha mpito cha Afrika mashariki kutoka kipindi cha ubeberu hadi baada ya Uhuru.

Makwaia alizaliwa na kuwa muislamu akiwa ni mtoto wa Chifu wa kisukuma ,Makwaia Ng'wandu wa Bwiha Mkoa wa Shinyanga Tanganyika, alijifunza kilimo katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwanzoni mwa miaka ya 1940 Kabla ya kuingia Chuo cha Lincoln, Oxford ,ambapo alisoma kanuni na utendaji wa Serikali za mitaa ,Falsafa na Siasa.

Maisha ya Makwaia kisiasa yalitoa fursa nyingi katika dunia ya viongozi wa kikoloni Tanzania ,na viongozi wa kikabila ,alimpokea Baba yake uchifu wa Busiha mwaka 1945 na baadae akaja kuwa chifu mkubwa wa wasukuma ,Taasisi yenye zaidi ya machifu 50 ,yenye ofisi yake na bendera kupitia hili akatambulika kwa waingereza kama sauti ya mzawa mwenye mamlaka ,mwaka huohuo akachaguliwa kuwa kati ya wabunge wawili waafrika kwenye baraza la kutunga sheria (Legco).
View attachment 1191674
Waweja sana mayo..
 
Makwaia mjumbe wa Legco kuna wakati alikuwa anaishi mji wa Moshi,mtaa wa Mkwawa.
 
Bob Makani ni mtoto wa jirani kwa Chifu Makwaia.

Yani kati ya wale wapambe wa karibu na Chifu Baba yake Bob Makani ni mmoja wao.

Wa karibu tunajua.

Sent using Jamii Forums mobile app
Chief Makwaia Baba yake David Makwaia,alikuwa mjomba wa Bob Makani. Mama Yake Bob Makani ni mtoto wa Chief.
 
Duh sasa Nyerere kwa nini alikuwa akiwaweka kizuizini watu wote ambao walikuwa na potential ya kumchallenge?

Sasa kwa nini amuweke ndani Chief Makwawia?

Huyu Nyerere kuna haja ya kumuangalia critically pengine sifa tunazompa nyingine zimepitiliza
Watu wote waliojaribu kutaka kuonekana wana hoja za kuzidi zile za Nyerere walikiona cha mtema kuni. Fuatilia:
  1. Joseph Kasela Bantu
  2. Christopher Kassanga Tumbo
  3. James Mapalala
  4. Chief Abdallah Said Fundikira
  5. Chief Paul David Kidaha Makwaia
  6. Oscar Kambona
  7. John Dunstan Lifa Chipaka
  8. Michael Marshall Mowbray Kamaliza
  9. Gray Likungu Mataka
  10. Bibi Titi Mohamed
  11. Tuntemeke Sanga
  12. na wengine wengi walioleta ubishi
 
Watu wote waliojaribu kutaka kuonekana wana hoja za kuzidi zile za Nyerere walikiona cha mtema kuni. Fuatilia:
  1. Joseph Kasela Bantu
  2. Christopher Kassanga Tumbo
  3. James Mapalala
  4. Chief Abdallah Said Fundikira
  5. Chief Paul David Kidaha Makwaia
  6. Oscar Kambona
  7. John Dunstan Lifa Chipaka
  8. Michael Marshall Mowbray Kamaliza
  9. Gray Likungu Mataka
  10. Bibi Titi Mohamed
  11. Tuntemeke Sanga
  12. na wengine wengi walioleta ubishi
Kuna makala iliandikwa na Daily Mail Nyerere alipofariki, ilieleza jinsi alivyokuwa na uwezo wa kujenga hoja, kutumia lugha ya Kiingereza na kuweka kuwashawishi watu waikubali hoja yake. Ilikuwa makala nzuri sana ilieleza pia Ujamaa ulivyoharibu mifumo ya maendeleo iliyoachwa na Waingereza.
 
Kuna makala iliandikwa na Daily Mail Nyerere alipofariki, ilieleza jinsi alivyokuwa na uwezo wa kujenga hoja, kutumia lugha ya Kiingereza na kuweka kuwashawishi watu waikubali hoja yake. Ilikuwa makala nzuri sana ilieleza pia Ujamaa ulivyoharibu mifumo ya maendeleo iliyoachwa na Waingereza.
Alishindwa kujenga hoja dhidi ya hawa watu ikabidi awanyamazishe kwa vyombo vya dola. Marehemu Kasanga Tumbo alikuwa akizungumza kwa uchungu sana jinsi alivyotoka UK miaka ya 1960's akiwa balozi akashuka airport Dar pale diplomatic passport ikachukuliwa kwanza, ubalozi ukaishia pale uwanjani! Akasindikizwa mpaka kwao Tabora akiwa na pair kadhaa za suti ambazo alisema hakupata tena fursa ya kuzivaa kwa maisha ya kijijini ambapo aliwekwa kwenye aina fulani ya detention ambayo hakuruhusiwa kutoka nje ya kijiji chake hadi Nyerere alipostaafu 1985. Na alisema zile suti alikuja akazifungasha akaenda nazo Dar kwa treni mwaka 1992 kwenda kushiriki kongamano la vyama vingi mfumo huo uliporuhusiwa.
 
Kuna makala iliandikwa na Daily Mail Nyerere alipofariki, ilieleza jinsi alivyokuwa na uwezo wa kujenga hoja, kutumia lugha ya Kiingereza na kuweka kuwashawishi watu waikubali hoja yake. Ilikuwa makala nzuri sana ilieleza pia Ujamaa ulivyoharibu mifumo ya maendeleo iliyoachwa na Waingereza.

Nyerere alikuwa na quality zifuatazo

1. Charm/Bashasha
Nyerere alikuwa na uwezo wa kukufanya ujifeel so good around him, kwa jokes, tabasamu.

2. Sharp mind
Nyerere alikuwa ana akili inayofanya kazi fasta sana, alikuwa na uwezo wa kutambua gaps kwenye hoja za wenzie na kuzitumia against wao. Na kama hoja ina mashiko alikuwa ana uwezo wa kumfanya mwenye hoja asijiamini

3. Alikuwa ni mtaalam wa kusuka alliances
Pindi akiona kuwa anahitaji uungwaji mkono katika jambo lake alikuwa na uwezo wa kutafuta kuungwa mkono mapema kabisa kabla hajaleta hoja barazani. Ukifuatilia harakati za uhuru utaona jinsi alivyokuwa akiwapanga wajumbe wanaojua kuzungumza kiswahili vizuri mapema ili hoja ikiletwa mezani then mmoja baada ya mwingine wanaanza kusimama na kuitetea.
Hata alivyomsaidia Mkapa kumshinda JK ndani ya CCM ni. kutokana na uwezo wa Nyerere kuwashawishi wajumbe wa Zanzibar wamuunge mkono.

4. Alikuwa ni mobilizer mzuri
Viongozi wenye kufuata mirengo ya kijamaa huwa ni wazuri kwenye kumobilize masses, Hata Nyerere alikuwa na kipaji cha kurally Taifa zima kusapoti agenda zake kama vile kuvunjilia mbali mfumo wa kichifu, Kuondoa mifumo ya nyarubanja, kumpiga Iddi Amini, Kuunga mkono azimio etc

Udhaifu wa Nyerere
1. Alipenda sana power
Ndo maana reform za msingi za kumpunguzia rais madaraka aliziintroduce alipokuwa anakaribia kung'atuka au akiwa ameng'atuka

2. Wakati mwingine Ukatoliki wake ulimshinda nguvu kwenye fairness

Hii inadhihirishwa na kuamua kuitia nchi katika kuunga mkono waasi wa Biafra, baadhi ya wachambuzi wanaeleza kuwa hii ni kutokana na Biafra kuwa inaungwa mkono na Vatican kutokana majority huko kuwa ni wakatoliki.

3. Alikuwa stubborn
Pindi alipokuwa akiamini kitu alikuwa hakubali mawazo mbadala kirahisi, mfano mzuri ni sera zake za uchumi baada ya azimio la arusha, zilikuwa za populism zaidi

4. Alikuwa mwema kwa loyalists hata kama wanaharibu
Kipindi cha Nyerere so long as una imani na CCM na yeye na wala humchsllenge kutishia power yake au ya chama, pindi ukiharibu kazini basi ungeweza kuhamishiwa shirika jingine
 
View attachment 1191675

David Kidaha Makwaia Pichani, yupo na mwingereza Lord Iveagh siku ya kutawazwa kwa malkia Elizabeth mwaka 1956.

Chifu David kidaha, alikuwa ni chifu wa wasukuma, alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 84 ,alikuwa ndio ngazi kati ya ukoloni na machifu ,na baada ya ukoloni barani Afrika na pia alikuwa na urafiki mkubwa na Gavana wa Tanganyika toka mwaka 1949 hadi 1958, Lord Twining.
Mwakwaia alicheza katikati ya viongozi wa Kiingereza na machifu wa majimbo kadhaa ya Tanganyika, alishuhudia Kipindi cha mpito cha Afrika mashariki kutoka kipindi cha ubeberu hadi baada ya Uhuru.

Makwaia alizaliwa na kuwa muislamu akiwa ni mtoto wa Chifu wa kisukuma ,Makwaia Ng'wandu wa Bwiha Mkoa wa Shinyanga Tanganyika, alijifunza kilimo katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda mwanzoni mwa miaka ya 1940 Kabla ya kuingia Chuo cha Lincoln, Oxford ,ambapo alisoma kanuni na utendaji wa Serikali za mitaa ,Falsafa na Siasa.

Maisha ya Makwaia kisiasa yalitoa fursa nyingi katika dunia ya viongozi wa kikoloni Tanzania ,na viongozi wa kikabila ,alimpokea Baba yake uchifu wa Busiha mwaka 1945 na baadae akaja kuwa chifu mkubwa wa wasukuma ,Taasisi yenye zaidi ya machifu 50 ,yenye ofisi yake na bendera kupitia hili akatambulika kwa waingereza kama sauti ya mzawa mwenye mamlaka ,mwaka huohuo akachaguliwa kuwa kati ya wabunge wawili waafrika kwenye baraza la kutunga sheria (Legco).
View attachment 1191674
Umeeleza vr kabisa cheef makwaia ni baba yangu mzaa bibi yangu kabisa mzaa wa mama yangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom