Chief Mangungo 2.0 na Ujinga wa Mwafrika 2013..

Chief Mangungo 2.0 na Ujinga wa Mwafrika 2013..

1. tuendeshe nchi kama wafanya biashara. kwanin waje kuchimba madin, ges na kuchukua wanyama hapa na wasiende kwingine? hapo itatupa uwezo wa kuwabana. hatushindwi kujua wapi kinapatikana nin na kwa gharama gani hapa duniani. wanakopata hivo vitu kwa bei ya bureovyo. 2. tusitegemee waaminifu kwa wanaotusainia mikataba huko maana hawapo. ukimtimua lakin akipewa $5m atajal nin? au atakuhonga usimtimue. 3. mikataba iwe hadharan. 4. husisha vyombo vingi kwenye mchakato. akiweza kuhonga wote atakuwa amefilisika
 
Mojawapo ya mikataba hiyo ule maarufu wa Chifu Mangungo wa Usagara na mingine mingi.
Mikataba siri....

Ujinga wa Mwafrika 2.0

Mkuu Mzee Mwanakijiji, to start with, naomba umtendee haki Chief Magungo ni wa Msovero, shuleni tulifundishwa ni wa Msowero na sio Usagara, unless Msowero ndio was by then na sasa ndio Usagara!
Chief Mangungo wa Msovero.

Nikirudi kwenye issue at hand, mikataba ile ya Karl Peters iliandikwa kwa lugha ya Kijerumani na hakukuwa na mfasiri bali kina Mangungo walidanganywa!. Mikataba hii ya sasa ni ya Kiingereza na sio Kichina!, hapa hatujadanganwa kitu, kila kitu kiko wazi kabisa crystal clear na tumewakubalia!.

Mikataba yote ina kipengele cha "confidentiality" just to protect the rights of contracting parties!. Linapokuja suala la mikataba inayohusu public entities yenye public interest, the contracting parties ni public ya Watanzania, na whoever anasaini huo mkataba, he/she is signing on behalf of The People of Tanzania!, hivyo "we the people" we had "the right to know", each and everything before hand, tena during negotiations period, not otherwise!.

Hawa viongozi wetu hawajifunzi mambo ya Niger Delta, "The Ogoni People" na sasa wanawafanya Wana Mtwara ndio kina Ken Sarowiwa wawanyonge gesi iende Bagamoyo!.

Hili la gesi jamani, mimi mwenzenu nililizungumza hapa kitambo tangu mwezi July, Gesi asili: A "day light robbery?!"- watanzania tunaibiwa Mchana Kweupe!

Mkataba wa Ujenzi wa Bomba la Gesi, nimeuzungumza hapa Tetesi: Bomba la Gesi Mtwara:A "20 -Year Grace Period" ya Mkopo wa Mchina ni "Changa la Macho!".

Watu tumehamanika sana na Mkataba wa Mchina!, laiti tungeujua mkataba wa BG ambao ndio wanaoichimba hiyo gesi, tungelia!. Costs ziko inflated 5 times!, ukiuliza sababu unaambia security risks, "Watanzania hatuna uwezo wa kulinda "oil and gas infrastructures", hivyo makampuni ya bima, yamewalazimisha kutoa tender za ulinzi kwa makampuni ya Afrika Kusini yenye uwezo!. Pia oparations ni very expensive kwa sababu Tanzania hatuna makampuni ya logostics na supply ya consumables yakiwemo maji ya kunywa na vyakula, vyote vinatoka Kenye au South na vinakuwa airlifted!. At the end of the day, anayelipa gharama zote ni sisi!.

Wazungu, Wachina na whoever atakayakuja , has the ability to play on us kwa sababu kila kitu anafanya yeye!, kwa hoja ya msingi kuwa sisi hatujui kitu!.

"Beggars can not be chooses!", we, Tanzanians as a beggars nation, we have to take what we get, not what we want! chini ya principle "if you can't get what you want, just take what you get!"

Ubaya uko wapi?!.

Pasco.

 
huko kwingine wanachimbaje? mazingira yakoje? tuwe kama busines people. kama ingekuwa hiyo gesi na wese mali yako binafsi ungefanyaje? chunguza wenye gesi kama wew waliofanikiwa wamefanikiwaje halafu iga. mbona mengine hatuoni aibu kuiga? sasa tatizo wanaotuwakilisha wakitumwa wakajifunze hayo mambo wanaenda kujifunza jins ya kupiga dili effectively. tatizo letu uzalendo uko chin, uaminifu mdogo, viongoz wetu ndo hvo tena, ubunifu hamna. tusingeshindwa asilani
 
lete ushahidi wa unachosema
tusiwe tunajadili vitu vya kudhani dhani
Kwa wale wenzangu na miye watavikumbuka vizuri "Mfululizo" wa vitabu vya "Ujinga wa Mwafrika". Vitabu hivi vilikuwa kwa muda mrefu sehemu ya simulizi la "Mazungumzo Baada ya Habari" na vilisimulia hadithi fulani ya maisha wakati wa ukoloni au baada ya ukoloni na jinsi gani Waafrika tulikuwa hatujui vitu vya wageni na hivyo tulijikuta tunafanya vitu ambavyo baadaye tukivifikiria tunacheka.

Lakini mojawapo ya vitu ambavyo vinatokana na somo hilo ni habari ya jinsi gani mababu zetu walivyoweza kuuza utajiri wa ardhi yao kwa wafanyabishara ya ukoloni ambao kinara wao alikuwa Carl Peters (Mkono wa Damu)- Mjerumani. Sasa Carl Peters ndiye kwa kiasi kikubwa alisababisha Ujerumani itafute makoloni Afrika na alifanya hivyo baada ya kuona Waingereza na Wabelgiji (Chini ya Mfalme Leopold II) wakitanua maeneo ya mamlaka yao.

Carl Peters alipokuja maeneo haya ya Tanganyika enzi hizo alijileta kama Mwakilishi wa Ujerumani na akabuni mikataba mbalimbali ambayo aliingia na machifu na watawala mbaalimbali (akiwemo Sultani wa Zanzibar na Kabaka Mwanga wa Uganda) na alifanya mikataba hiyo kwa niaba ya kampuni aliyoiunda ya German East African Company (mliosoma historia mtaikumbuka).

Mojawapo ya mikataba hiyo ule maarufu wa Chifu Mangungo wa Usagara na mingine mingi. Katika mikataba yote hiyo machifu walikuwa wanakubali kuyaachilia maeneo ya ardhi yao kuwa chini ya ulinzi wa Mjerumani na kutumiwa kwa faida ya Mjerumani kwa milele yote. Wengi tunafahamu kuwa wazee hawa walikubali kwa sababu moja kubwa walikuwa hawajui kilichomo kwenye mikataba hiyo na hivyo hata walipokuja kugundua kuwa wameuza ardi yao "mikataba" ile ilikuwa halali na Ujerumani ilikuwa tayari kuhakikisha inasimama hata kwa vita (Kilimanjaro ni mfano mmoja wapo).

Mikataba hii ilifichwa kwa wenyewe na ilifanywa na watawala wao; wakulima na wanakijiji wengine hawakujua kuwa machifu wao wameuza ardhi yao. Na hata kama wangetaka kujua wasingeweza kujua kwani mikataba ilikuwa ni siri kati ya watawala na kampuni hiyo ya kigeni. Na hivyo ndivyo kihistoria eneo ambalo baadaye lilikuja kujulikana kama Tanganyika lilivyoangukia mikononi mwa Ujerumani - hii ilijumuisha Rwanda na Burundi. Hii ilibadilika baada ya vita ya kwanza ya dunia ambapo Tanganyika ikawekwa chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa kupitia Uingereza.

Mjerumani kwa kutumia kampuni ya GEAC kujenga reli, kuanzisha mashamba ya katani, pamba n.k na vyote hivi vilifanywa si kwa ajili ya kuwanufaisha wazawa au wananchi bali hatima yake mazao yanayopatikana yapelekwe Ujerumani kuwa malighafi katika viwanda vyao na zile nyingine za kuuzwa sehemu nyingine kuwa chanzo cha mapato kwa Ujerumani. Wananchi hawakuwa na uchaguzi wowote wa nini kinapandwa, nani anasimamia na hata hawakuwa na uamuzi juu ya matumizi ya faida ambayo Mjerumani alikuwa anapata. Hapa ndipo ulipokuwa Ujinga wa Mwafrika.

Sasa ujinga si ugonjwa au tusi; ujinga ni hali ya kutokujua (ignorance). Mtu aliye mjinga akijuzwa anaerevuka na ujinga humtoka katika lile jambo ambalo alikuwa halijui. Na kila mwanadamu ana ujinga wa aina fulani na hivyo katika maisha yote anatakiwa awe tayari kujifunza. Lakini kwenye eneo ambalo ufahamu upo tayari na unapatikana mtu hatakiwi kuendelea kuwa mjinga. Ujinga wa aina hiyo ambao mtu anauchagua ndio huitwa upumbavu au wengine wanaitwa ujuha kwani ni mtu ambaye hata akijuzwa hajui na hawezi kujua kwa sababu hayuko tayari kujua!

Leo hii watawala wetu wametuambia mikataba ni siri na kuwa mikataba hiyo ikiwekwa wazi basi wawekezaji wanaweza kukimbia na kuwa mikataba hiyo ni siri kati ya 'serikali na wawekezaji' hata kama inahusu ardhi ya umma na mali umma. Ujinga ni kuwa tumekubali kuwa hilo ni kweli! Na ujinga zaidi ni kuwa watawala wetu wanaingia mikataba na wanaamini ni vizuri kuifanya siri na hivyo hatujui nini kilichomo. Mkataba ule wa Carl Peters na Chief Mangungo ulikuwa na kipengele kinachosema kuwa ardhi hiyo ingeweza kutumiwa "exclusively" kwa matumizi ya Mjerumani.

Kwanini nimesema hili....

Well, mkataba wa ujenzi wa bomba la gesi kati ya Kampuni ya Kichina na serikali (Chief Mangugu wa leo) una kipengele kinachosema kuwa sehemu ya gesi ambayo itakuwa inachimbwa huko itauzwa kwa China. Hivyo Wachina wamehakikishiwa gesi ya Mtwara na kutokana na ujuzi wa mtu aliyenisimulia hili na ameona mkatbaa huo anasema Wachina wamehakikishiwa kwa asilimia...

Na sisi tumekubali, Wabunge wamekubali

Mikataba siri....

Ujinga wa Mwafrika 2.0
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji, to start with, naomba umtendee haki Chief Magungo ni wa Msovero, shuleni tulifundishwa ni wa Msowero na sio Usagara, unless Msowero ndio was by then na sasa ndio Usagara![/qoute]

Ni mwanafunzi mzuri wa historia; alikuwa ni chifu wa Msovero, Usagara.
 
Mambo haya yanaamusha hari na molali kwa wananchi na kupandwa na hasira tumeona kwenye dhahabu hatujanufaika na chochote tumeachiwa mashimo matupu, dawa ni kumwondoa huyu mkoloni mweusi
 
Mjalada huu ungekuwa vizuri kama tutazungumzia Chief Mangungo na ujinga wa Mtanzania.Tukijadili sana masuala ya ujinga wa mwafrika kwa maana ya raia kutoka Rwanda,Burundi,Uganda,kenya etc na tukaacha kuzungumzia ujinga wa mtanzania tutakuwa wanafiki.Ni unafiki kwa maana matatizo yetu yatatatuliwa na sisi watanzania wenyewe na si vinginevyo.Kwa wale waliopitia kitabu cha Mathayo Mt.7:3-5 watakubaliana na mimi kwa maelezo aliyoyatoa Bwana Yesu Kristu kwamba nanukuu ''Basi mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako na boriti iliyondani ya jicho lako mwenyewe hauiangaliii?,Au utamwambiaje nduguyo,niache nikitoe kibanzi katika jicho lako na kumbe mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe.Mnafiki wewe,itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako''.Hivyo wanajamii,tujadili moja kwa moja kwa kuitoa boriti iliyopo kwenye jicho la mtanzania na si kuangaika kwa kukitoa kibanzi kilichopo kwa mwafrika ambaye ndiye ndugu yetu.Leo hii utasikia watanzania kutoyazungumzia matatizo yanayowakabili wakiamini kuwa matatizo tuliyonayo yanafanana na matatizo ya waafrika wenzetu kitu ambacho si kweli,mfano mdogo tu suala la usafi wa mji kwa Dar es Salaam limetushinda,Je usafi uliopo kigali unalingana na DSM na je ni suala la ujinga wa Mwafrika au ni ujinga wa mtanzania?
 
Tatizo letu nambari one ni Kijakazi...Kijakazi hawakilishi mtu moja, anawakilisha wengi na wote mtazamo wao ni kama wa huyu Kijakazi wetu wa JF hapo juu. Kijakazi ni zaidi ya jina, ni utamaduni, ni tabia na ni udhaifu unaosababishwa na uelewa finyu. Tukiitoa CCM hatuwezi kurudi hapa tena kujadili yale yale...tunajadili yale yale kwa sababu tuko pale pale na watu wale wale na mfumo ule ule, hapana, mabadiliko hayaji hivyo. Tukiitoa CCM tumepiga hatua na tumepiga baragumu, tunamtangazia yeyote yule anayekuja kwamba uvumilivu sasa basi, usipotimiza na wewe unaondoka. Huo mfano kwa sasa hatuna kwani pamoja na CCM kupoteza dira, akina Kijakazi bado wamejazana mle mle, hawajui watokako wala wanakoelekea, wapo wapo tu!

Nikirudi kwenye mada ya Mwanakijiji, nakiri watawala wetu ni werevu, ni kama walivyokuwa Wajerumani na sisi wananchi, kama Chifu Mangungo, ndio wajinga. Tunayoyashuhudia ni mavuno ya yale tuliyoyapanda wenyewe na kwa hiari yetu...inakuwaje mtu na akili zako timamu unampa uongozi mtu asiye na sifa wala historia ya kupigania haki? CCM inapata kiburi kwa sababu sisi wenyewe tumeiruhusu, viongozi wetu hawatetei maslahi yetu kwa sababu tumeshindwa kuyadai na serikali yetu inaingia mikataba ya hovyo kwa sababu tumeshindwa kuwawajibisha. Kijakazi, unatoa mfano wa Ufaransa, je yupo kiongozi wa Ufaransa anayeweza kuwaambia wananchi wake na wabunge kuwa mkataba serikali yao iliyoingia na mwekezaji ni siri, thubutu!

Kama kawaida umeandika na kuleta kejeli bila kujibu na kuelezea yale niliyoandika, kwa maana ni rahisi siku zote kukebehi kuliko kujibu, sasa nataka unijibu, kama ukiweza, kama kweli unafikiri kwamba tatizo ni CCM ni kwa nini wanaoitwa wapinzani hawapingi kwa nguvu zote kutumia pesa zetu kwenda kutibu Viongozi (PAMOJA NA WAPINZANI) nje ya nchi?
Huo utetezi wao wa mwananchi wa kawaida uko wapi? Kama wao watakuwa tofauti na CCM pindi waingiapo madarakani wangetuonyesha ni jinsi gani wanapinga uonevu huu wa kuwaacha Watanzania kufa mahospitalini kusipokuwa na dawa ilihali wao pamoja na jamaa zao wanakwenda kutibiwa nje ya nchi? Mambo ya kupigania sijui Gesi hayana maana yoyote, kama kweli wanamjali Mtanzania wangeanzia hapa kwa maana ndipo maisha ya Mtanzania yanapoguswa moja kwa moja, kumbuka kwamba Upinzani hawajahi kuongoza nchi hii, hivyo ili tuwaamni ni lazima watuonyeshe wako tofauti na hapo ndipo pa kuanzia sio sijui Mnazi Bay, sijui Songo songo, hapana,nataka jibu hapo, Naomba usizunguke nipe tu jibu kuhusu hilo, kama ukiweza!

 
Labda na mimi niuulize swali, tuseme mikataba yote iwekwe wazi, ni nini kitabadilika? hata kama ikijulikana Gesi yote kapewa Mchina au mwingine yoyote ni nini kitabadilika? Ni mangapi sasa tunayajua na yako wazi ni nini kimefanyika? Kuna fungu kubwa la kupeleka viongozi wote wa Serikali na Chama (pamoja na Upinzani) kwenda kutibiwa nje ya nchi pindi wauguapo kila mtu anajua hilo, kuna lolote linafanyika? Mbona tuko kimya? kuna usaliti mkubwa zaidi ya huo ukichukulia watu wanakufa wodini kwa kukosa tu dawa?

Wakati wa ukoloni vibarua waliokuwa wanafanya kwenye mashamba ya katani Tanga na kwingeneko ujira waliokuwa wanalipwa ingawaje ulikuwa mdogo lakini uliwatosha kula mpaka pale ujira mwingine ulipofika, leo hii kibarua pesa anayopata haitoshi hata wiki moja, na kusema kwamba mazao yaliwanufanisha wao (Wajerumani) tu sio kweli kmaana Wakulima wa Kilimanjaro (Waafrika) tayari walikuwa wanashindana na wakulima wa Kijerumani kwa Uzalishaji wa Kahawa, leo wamerudi nyuma miaka 100!

Kwa hiyo tuna kazi kubwa ya kukaa na kujitafakari sisi kama Watz, tatizo letu ni nini na liko wapi, turudi nyuma tuangalie tulipokosea, kuanza kukaa na kulaumu na kutafuta visingizio hakutatusaidia kitu, tujiulize ni kwa nini tunashindwa kusimamamia maslahi yetu?

Usiri wa Mikataba sio tatizo, utakuta kuna nchi nyingi pia Mikataba ni siri lakini cha muhimu wale wanaosaini hiyo Mikataba HAWAWEZI kukubali kuikandamiza nchi yao kama sisi tunavyofanya, sasa swali ni KWA NINI?

Ukiangalia hivi majuzi Raisi Kikwete alikuwa Ufaransa kuna picha wamepiga na Raisi wa Ufaransa na watu wake kwenye meza, nina uhakika kuna Mkataba umesainiwa pale na siajabu pia watu wa Ufaransa hawaujui lakini nina uhakika wale waliousaini kwa upande wa Ufaransa maslahi ya nchi yalizingatiwa kwanza, lakini sisi kwetu Mungu ndio anajua, sasa kwa nini?Tutafute jibu hapo, yani ni kwa nini mtu awe tayari kuweka nchi yake na watu wake rehani kwa miaka 99? Bila kupata hilo jibu hatuwezi kutatua hili tatizo tutabaki tu kufikiri tatizo ni CCM, tutaitoa na baada ya muda tutarudi hapahapa tena kuanza kujadili yale yale wakati huo adui hatakuwa CCM tena!

Hizo sababu ulizozitaja ndizo zinatufanya wananchi tutake mikataba iwe wazi. Ulichokisema ni kuwa waafrika hawana uzalendo. Ni kweli. Ndiyo maana mikataba iliyosainiwa na viongozi wa kiafrika inabidi iwe wazi ili watu wajiridhishe kuwa hawajachakachua kwa kupewa fungu la kumi. Wachina wanajulikana kwa kuwahonga viongozi wa kiafrika hata China kwenyewe rushwa imeshamiri ji jambo la kawaida. Sasa huku kwetu kupewa asilimia ya gesi unafikiri ni kitu kidogo tu sisi tunyamaze.
Ninavyojua wabunge wanatakiwa kukagua shughuli za serikali na kuisimamia. Ni kipengele gani cha katiba kinachozuia serikali kuweka shughuli zake wazi kukaguliwa na wawakilishi wa ananchi ambao ni wabunge?
Hivyo tunawajibu wa kuhakikisha mikataba inakuwa wazi.
 
Ni kweli na ndio maana nasema upande mwingine ni hawa watawala ndio wenye kubeba lawama. sijui kama umepata nafasi ya kusoma mikataba ya Richmond au ile ya Airbus 320 na ya Dash 8; au mikataba ya ununuzi wa magari ambayo kina Mataka wa ATCL waliingia... imeandikwa na watu wenye akili lakini imeandikwa kwa makusudi kuwa ilivyo. Sasa bila kuweka kanuni za kuongoza serikali inapoingia mikataba na zikawa kanuni zenye kulinda nchi na maslahi yake wawekezaji tutaweza vipi kulinda maslahi yetu?

Lakini Bw. Tayari swali dhahiri ni hili tunaweza vipi kuwakatalia wawekezaji wanapokuja na masharti ya kutubana wakitishia kuwa tusipokubali wanaenda nchi nyingine?

Wawekezaji, hawezi kukimbia kwasababu wananlindwa na Bilateral Foreign Investment Protection Agreements.
Kwa mfano Tanzania ina na Bilateral Foreign Investment Protection Agreements na Uingereza na iko kwenye mchakato mwingine wa kusaign mwingine na Canada.Hii mikataba ndio mwiba halisi wa Mikataba mibovu . Ndio maana unaona hata makamouni ya Canada , au nchii nyingi za ulaya zinazo kuja kuwekeza Tanzania zinatokea Uingereza kwa kutumia loopholes za hizi Bilateral agreement.
IPPAs (Investment Promotion)
Canada's Foreign Investment Promotion and Protection Agreements (FIPAs)
Kama tukiwa na sheria nzuri zinazosimamia maslahi ya Taifa, Kwanza italeta Legal certainty na Itazuia ufisadi.
Kuna option mbili za kufanikisha hili.
1. Nikupitisha sheria ambayo itaweka Limitation ya matumizi ya “Stabilisation clauses” katika mikataba.Matatizo mengi ya mikaba yetu yanatokana na excessive use of “stabilisation clause”.Kwa kufanya hivi itasaidia kuwa inform Investors the rule of the game. Hakuna rule of game now, everything ni shamba la bibi , na kwa kutumia
2. Parliamentary scrutiny of proposed contracts-
 

Attachments

Ebana eeh, vipi kuhusu mishahara ya viongozi kuanzia rais on down? Unaijua? Staki unambie niende idara ya utumishi maana huko nahisi najua tu jibu ntakalolipata...

Wanadai ni siri. Unamlipa mwajiriwa mshahara kila mwezi lakini hujui unamlipa kiasi gani.
 
Mzee Mwanakijiji, Rejea swali lako la mjinga ni nani? Kati ya wanaopiga kura kuchagua viongozi, zaidi ya 80% hawana elimu wala mawasialiano hivyo hupiga kura kwa kurubuniwa na tshirt pombe na mlo wa siku moja. Nyinyi 20% vs wao 80% nani mwenye maamuzi ?
 
Sizani kama ni lazima hata kuweka hii mikataba hadharani, Ila kuna ulazima ku safeguard kwa Kuhakikisha kwamba kiongozi wa Upinzani Bungeni anapata nakala zote za mikataba, then serekali kwa kushirikiana na Upinzani wanaweza kutengeneza talking point za mkataba ambazo zitakuwa verifibale.

Waafrika nadhani tuna curse si bure huu ujinga umezidi. Utadani tulizaliwa kwa bahati mbaya.
 
tunao mangungo wengi sana leo hapa tanzania.... sijui hata tuanzie wapi kutajana
 
Tukianza kwenye family level Tujiulize ni wazazi wangapi huwaandalia watoto wao maisha ya baadae. Then taifa na makuiz pia je tunajifunza nini juu ya kurithisha mali. Je mzee wa miaka 50 anaweza kuwekeza aundio kauli ngoja nile nife maana nikitunza nani atakula. That is why all money stolen huishia kwa viamda na watoto kutumia kwa unga.SHAME ON US AFRICA.
 
Swali linaweza kuulizwa: ni nani aliye mjinga baina yetu? Wao wanaotuambia kuwa mikataba iliyosainiwa ni siri yao tuwaamini au sisi tunaokubali kuwa ni siri tukiamini walichotuambia?

hapa umepiga jichoni.....WAJINGA ni sisi tunaopokea kila kitu na tunalazimishwa ama kuhamasishwa tukubali kuamini na tuna amini.tulipaswakuwa kama watu wa MTWARA MPAKA KIELEWEKE.
 
Kama kawaida umeandika na kuleta kejeli bila kujibu na kuelezea yale niliyoandika, kwa maana ni rahisi siku zote kukebehi kuliko kujibu, sasa nataka unijibu, kama ukiweza, kama kweli unafikiri kwamba tatizo ni CCM ni kwa nini wanaoitwa wapinzani hawapingi kwa nguvu zote kutumia pesa zetu kwenda kutibu Viongozi (PAMOJA NA WAPINZANI) nje ya nchi?
Huo utetezi wao wa mwananchi wa kawaida uko wapi? Kama wao watakuwa tofauti na CCM pindi waingiapo madarakani wangetuonyesha ni jinsi gani wanapinga uonevu huu wa kuwaacha Watanzania kufa mahospitalini kusipokuwa na dawa ilihali wao pamoja na jamaa zao wanakwenda kutibiwa nje ya nchi? Mambo ya kupigania sijui Gesi hayana maana yoyote, kama kweli wanamjali Mtanzania wangeanzia hapa kwa maana ndipo maisha ya Mtanzania yanapoguswa moja kwa moja, kumbuka kwamba Upinzani hawajahi kuongoza nchi hii, hivyo ili tuwaamni ni lazima watuonyeshe wako tofauti na hapo ndipo pa kuanzia sio sijui Mnazi Bay, sijui Songo songo, hapana,nataka jibu hapo, Naomba usizunguke nipe tu jibu kuhusu hilo, kama ukiweza!


JIBU KAMA HUONI TOFAUTI KATI YA CCM na CDM basi we ni KILAZA. Huenda pia ikawa hata hujui kama una tetea mafisadi ACHA U-POYOYO
 
Mjalada huu ungekuwa vizuri kama tutazungumzia Chief Mangungo na ujinga wa Mtanzania.Tukijadili sana masuala ya ujinga wa mwafrika kwa maana ya raia kutoka Rwanda,Burundi,Uganda,kenya etc na tukaacha kuzungumzia ujinga wa mtanzania tutakuwa wanafiki.Ni unafiki kwa maana matatizo yetu yatatatuliwa na sisi watanzania wenyewe na si vinginevyo.Kwa wale waliopitia kitabu cha Mathayo Mt.7:3-5 watakubaliana na mimi kwa maelezo aliyoyatoa Bwana Yesu Kristu kwamba nanukuu ''Basi mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako na boriti iliyondani ya jicho lako mwenyewe hauiangaliii?,Au utamwambiaje nduguyo,niache nikitoe kibanzi katika jicho lako na kumbe mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe.Mnafiki wewe,itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako''.Hivyo wanajamii,tujadili moja kwa moja kwa kuitoa boriti iliyopo kwenye jicho la mtanzania na si kuangaika kwa kukitoa kibanzi kilichopo kwa mwafrika ambaye ndiye ndugu yetu.Leo hii utasikia watanzania kutoyazungumzia matatizo yanayowakabili wakiamini kuwa matatizo tuliyonayo yanafanana na matatizo ya waafrika wenzetu kitu ambacho si kweli,mfano mdogo tu suala la usafi wa mji kwa Dar es Salaam limetushinda,Je usafi uliopo kigali unalingana na DSM na je ni suala la ujinga wa Mwafrika au ni ujinga wa mtanzania?

WE UMETUMWA KUJAZA SEVER?,Mwandishi ameoNgelea ujinga wa nchi JIRANI?,Khaaa magamba mmeathirika mpaka kufikiri kwenu kume DHOOFIKA,si lazima ua-ndike ,Watu wanajadili namna ya kujikomboa toka kwa huyu mkoloni mweusi we unakuja na POROJO za kujaza sever KAKOJOE UKALALE KIMA FUNGU NA WENZIO.
 
lete ushahidi wa unachosema
tusiwe tunajadili vitu vya kudhani dhani

usha chimba dawa au ndo unaenda?,kama tiyari ka-kae jirani na dereva uone bara bara inavyokuja kwa kasi.kilaza mtoto hapa sio kizota
 
huko kwingine wanachimbaje? mazingira yakoje? tuwe kama busines people. kama ingekuwa hiyo gesi na wese mali yako binafsi ungefanyaje? chunguza wenye gesi kama wew waliofanikiwa wamefanikiwaje halafu iga. mbona mengine hatuoni aibu kuiga? sasa tatizo wanaotuwakilisha wakitumwa wakajifunze hayo mambo wanaenda kujifunza jins ya kupiga dili effectively. tatizo letu uzalendo uko chin, uaminifu mdogo, viongoz wetu ndo hvo tena, ubunifu hamna. tusingeshindwa asilani

kiwete Ka zurura DFUNIA nzima kaona watu wanavyo endeleza nchi zao na walivyo na uzalendo ye hata kugundua kwa nini nchi yake maskini haja jua kuna kitu hapo?,mbunge wa mtwara kwenda trnida and tobago kaona wananchi wanavyo faidika na malighafi toka kwao kaja hapa anashinikizwa akubali kuchakachua kisa eti alipelekwa nje.CCM WAPUUZI,,,,...!
 
Back
Top Bottom