Huwa nataka mtu akiri kwanza ndio nimlipue ili usileta sababu za kitoto
Naanza na injili kama ulivyo Nukuu kutoka kwa Yohana 17 transilation ya SUV
- Yesu akasema "Baba, saa imekwisha kufika" Je unaamini Yesu ana Baba ambae yupo mbinguni?
- 1 Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe;
- Yesu anasema amepewa mamlaka juu ya wote wenye mwili na kwamba atawapa wote wenye mwili uzima wa milele, Je unaamini hili?
- 2 kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.
- Yesu anasema uzima wa milele ndio huu wamjue aliemtuma ambae hapo juu Yesu kasema ni Baba yake ndio kamtuma!! upo na unaelewa?
- 3Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
- Yesu anasema amemtukuza Baba yake na amemaliza alichotumwa kufanya , kimetajwa hapo juu atupe uzima wa milele, Unaamini uzima wa milele tunapata kupitia Yesu?
- 4Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
- Yesu anasema alikuwepo kabala ya ulimwengu kuwepo na Alikuwa na Baba pamoja, Yesu hapa najizihirisha Yeye na Baba ni wamoja na kwa ku copy kwako hapa inamaana unaamini Yesu ni Mungu au umejikopia tu vitabu havikuhusu?
- 5 Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.
Nimemaliza maswali yangu bila kuweka hypocrisy jibu hayo maswali? nipo
Code:
* Yesu akasema "Baba, saa imekwisha kufika" Je unaamini Yesu ana Baba ambae yupo mbinguni?
NDIYO KWA SABABU BABA YAKE YESU NDIYE BABA WA WANAISRAEL WOTE:
Yesu anasema
Yohana 20:17
Yesu akamwambia, “Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’ ”
Code:
* Yesu anasema amepewa mamlaka juu ya wote wenye mwili na kwamba atawapa wote wenye mwili uzima wa milele, Je unaamini hili?
HAPANA SIAMINI KWA 7BU YESU ALITUMWA KWA WANAISRAEL TU NAMI SIMWANA WA ISRAEL:
Yesu anasema:
Mathayo 15:24
Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
Lakini pia Yesu siku chache kabla ya mateso aliwagiza wanafunzi wake hivi:
Mathayo 10:23
Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia, Hamtaimaliza miji ya Israeli, hata ajapo Mwana wa Adamu.
Mpaka leo Mwana na Adamu hajarudi lakini kina Paul kitambooo walijigeuzia mazuzu wao kina nyinyi.[emoji2][emoji2][emoji2]
Code:
* Yesu anasema uzima wa milele ndio huu wamjue aliemtuma ambae hapo juu Yesu kasema ni Baba yake ndio kamtuma!! upo na unaelewa?
YOHANA 20:17 imeshamaliza.
* 3Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
Huu ndiyo msingi wa Uislamu,Mungu ni Mungu na Yesu ni Mtume wa Mungu.
Code:
* Yesu anasema amemtukuza Baba yake na amemaliza alichotumwa kufanya , kimetajwa hapo juu atupe uzima wa milele, Unaamini uzima wa milele tunapata kupitia Yesu?
HAPANA KWA SABABU HILI NI KWA WATU WALE TU ALIOPEWA YESU:
YOHANA 17:6
Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.
Na kwa kuthibitisha hilo akaongeza hivi:
YOHANA 17:9
Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;
Code:
* Yesu anasema alikuwepo kabala ya ulimwengu kuwepo na Alikuwa na Baba pamoja, Yesu hapa najizihirisha Yeye na Baba ni wamoja na kwa ku copy kwako hapa inamaana unaamini Yesu ni Mungu au umejikopia tu vitabu havikuhusu?*
YOHANA 20:17 ilishamaliza uchakachuaji wote.[emoji2][emoji23][emoji16]
Yesu ni Mungu mwenye Mungu!Ujinga huo mnao nyinyi tu wapiga makofi kanisani [emoji41][emoji41][emoji41]
KARIBU TENA NIENDELEE KUKUPA TUITION [emoji23][emoji16][emoji3].