China aichumbia gesi ya Russia inayouzwa nchi za Ulaya

China aichumbia gesi ya Russia inayouzwa nchi za Ulaya

Sikirimimimasikini

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2019
Posts
2,926
Reaction score
15,634
China imeazimia kutotegema tena gesi asilia toka kwa mataifa pinzani, ambayo ni Marekani na Australia. Na badala yake inawekeza ktk project ya kujenga bomba jingine jipya la gesi toka Russia ili kuongeza zaidi kiwango cha gesi inayonunua toka Russia.

Bomba la awali (lililopo sasa) hupeleka gesi toka Russia kuingia China kiwango cha mita za ujazo bilioni 38 kwa mwaka, ambazo ni sawa na lita trilioni 38.

Ktk mradi huu wa bomba jipya la gesi, China itaongeza kiwango cha mita za ujazo bilioni 10 kwa mwaka (sawa na lita trilioni 10 za gesi).

Pia Russia ipo ktk mchakato wa ujenzi wa bomba jingine la tatu la gesi (Power of Siberia 2 Pipeline), ambalo litapitia Mongolia kupeleka gesi China na litakuwa na uwezo wa kupeleka gesi mita za ujazo bilioni 50 (sawa na lita trilioni 50) nchini China.

Mabomba hayo kwa ujumla yataiwezesha China kununua gesi ya Russia mita za ujazo bilioni 100 (sawa na lita trilioni 100) kwa mwaka, ambayo ni takriban nusu ya gesi inayonunua China toka nchi za nje (China hununua gesi kiasi cha mita za ujazo bilioni 200 kwa mwaka toka nchi za nje). Kwa upande wake Russia, atanufaika kwa kupata soko jipya ambapo atakuwa akiuza karibu nusu ya ile gesi aliyokuwa akiipeleka Ulaya. Russia amekuwa akiuza takriban mita za ujazo bilioni 170 hadi 200 kwa mwaka ktk nchi za Ulaya.

 
Ni harakati za mfa maji tuu.Walichoongeza ni lita b10,000
Mzee unajua hata maana ya billion!?
Let say Russia akiuza kila Litre $0.5
Litre bilion laki moja.
Bilion ipo na zero 9 ongeza zero tano mbele. Maana atauza liter billion laki moja.

Maana yake 100,000,000,000,000 x $0.5
Unapata $50,000,000,000,000
Ni sawa na $50T.

Ukiondoa operation cost na mengine. Hapo Russia hakosi $10T.
 
Ni harakati za mfa maji tuu.Walichoongeza ni lita b10,000
Endelea kujifariji Mkuu, Marekani yenyewe ilitahadharisha mwezi wa kwanza mwaka huu (kabla hata ya vita hii kuanza) kuwa bomba la gesi la 'Power of Siberia 2' litazifanya nchi za Ulaya na China zigombanie gesi ya Russia

Soma habari hiyo toka Voice of America

SmartSelect_20220313-085117_Chrome.jpg



 
China imeazimia kutotegema tena gesi asilia toka kwa mataifa pinzani, ambayo ni Marekani na Australia. Na badala yake inawekeza ktk project ya kujenga bomba jingine jipya la gesi toka Russia ili kuongeza zaidi kiwango cha gesi inayonunua toka Russia.

Bomba la awali (lililopo sasa) hupeleka gesi toka Russia kuingia China kiwango cha mita za ujazo bilioni 38 kwa mwaka, ambazo ni sawa na lita bilioni 38,000.

Ktk mradi huu wa bomba jipya la gesi, China itaongeza kiwango cha mita za ujazo bilioni 10 kwa mwaka (lita bilioni 10,000 za gesi).

Pia Russia ipo ktk mchakato wa ujenzi wa bomba jingine la tatu la gesi (Power of Siberia 2 Pipeline), ambalo litapitia Mongolia kupeleka gesi China na litakuwa na uwezo wa kupeleka gesi mita za ujazo bilioni 50 (lita bilioni 50,000) nchini China.

Mabomba hayo kwa ujumla yataiwezesha China kununua gesi ya Russia mita za ujazo bilioni 100 (lita bilioni 100,000) kwa mwaka, ambayo ni takriban nusu ya gesi inayonunua China toka nchi za nje (China hununua gesi kiasi cha mita za ujazo bilioni 200 kwa mwaka toka nchi za nje). Kwa upande wake Russia, atanufaika kwa kupata soko jipya ambapo atakuwa akiuza karibu nusu ya ile gesi aliyokuwa akiipeleka Ulaya. Russia amekuwa akiuza takriban mita za ujazo bilioni 170 hadi 200 kwa mwaka ktk nchi za Ulaya.

Andika vizuri hesabu! Mita za ujazo bilioni 10 ungesema ni sawa na lita trilioni 10!
 
tanzania yetu ndio nchi ya furaha na ka mdundo kwa juu, imagine tuna gesi kwenye aridhi yetu ambayo sio ya kwetu tena😂
 
Back
Top Bottom