China haina uwezo wa kustahimili vikwazo vya kiuchumi kama Urusi ilivyoweza kustahimili, ndio maana haina ubavu wa kuivamia Taiwan.

China haina uwezo wa kustahimili vikwazo vya kiuchumi kama Urusi ilivyoweza kustahimili, ndio maana haina ubavu wa kuivamia Taiwan.

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Nchi za magharibi hazijaamini hadi sasa kuwa Urusi imeweza kuhimili vikwazo lukuki vya kiuchumi, kinyume chake nchi za magharibi hususan ulaya magharibi ndizo zilizoumia zaidi. Ilitegemewa kuwa urusi itashindwa kuhimili na hivyo kushindwa kuendesha vita vyake dhidi ya ukraine.

Kwa upande mwingine China japo ina uwezo wa kuivamia na kuishinda Taiwan kwa nguvu za kijeshi, lakini haina ubavu wa kuweza kuhimili vikwazo vya kiuchumi toka nchi za magharibi kama urusi ilivyoweza. Ndiyo maana China haina ubavu hata kidogo wa kuweza kuivamia Taiwan. Itabaki kupiga kelele tu na vitisho vya mazoezi ya kijeshi kuizunguka Taiwan. Mabeberu wa nchi za magharibi wanajua china hana ubavu huo wala hawezi kufanya yale ambayo urusi inafanya leo!!

Sababu kuu kwa nini China haiwezi kuhimili vikwazo vya kiuchumi vya mabeberu:
1. Uchumi wa China unategemea uuzaji wa bidhaa za viwandani na soko lao kubwa ni nchi za ulaya na marekani. Kwa bahati mbaya hizi bidhaa si bidhaa za lazima kiasi kwamba nchi zikigoma kununua zitaathirika, lakini pia kuna bidhaa mbadala toka mataifa mengine.

Hii ni tofauti kabisa na Urusi ambayo yenyewe huuza bidhaa ambazo ni za lazima katika maisha na bidhaa ambazo haziwezi kukosa soko duniani yaani mafuta na gesi!! Ukikataa kununua kwanza lazima uumie na utalazimika kuzitafuta kwa gharama zaidi! Mfano, Poland ilikataa kununua gesi ya urusi kwa sharti la kulipa kwa ruble. Lakini Poland ililazimika kununua gesi hiyo hiyo ya urusi kupitia kwa Ujerumani na kwa bei ya juu zaidi!! Hivi sasa nchi za ulaya wanalazimika kununua gesi kimiminika toka marekani ambayo kwanza haitoshelezi lakini pia ni gharama mara nne zaidi, wakati urusi inauza gesi kwa masoko mengine ya china na India.

2. China inategemea pia viwanda vyake ambavyo vingi vipo huko huko marekani na ulaya! Viwanda hivyo vikipigwa marufuku China haina ubavu wa kuzalisha bidhaa nyingi kuweza kutosheleza masoko yake hata nje ya ulaya na marekani.

3. China haijitoshelezi kwa vyakula na bado hadi leo inategemea kuagiza vyakula toka mataifa mengine hasa marekani na ulaya. Wakinyimwa chakula na kwa vile ni wengi hawawezi kustahimili. Tofauti na Urusi inayojitosheleza kwa vyakula na sehemu kubwa kuuza nchi za nje.

Kwa kadri siku zinavyosonga mbele ndivyo uwezo wa China kuishinda Taiwan kijeshi unavyozidi kupungua maana Taiwan itauziwa silaha za maangamizi na za kujilinda!!

Kama ilivyo kwa Urusi kama ingechelewa zaidi kuivamia ukraine, ingekuta ukraine imejiimarisha zaidi kijeshi.

China inatia huruma lakini haina jinsi zaidi ya kulalamika!! Lakini ni afadhali kutokuthubutu kuliko kuthubutu halafu ukafilisika!!

Kwa Urusi tunavyozungumza, keshaweka kibindoni tayari majimbo matano ikiwemo Crimea na Ukraine hana jinsi zaidi ya kulia lia kwa mabeberu kuomba misaada ya fedha na silaha!! China ubavu huo hana vinginevyo itaaibika!!
 
We ni mjinga sana uchumi wa china ni almost trillion 18 ya GDP unafananisha na Russia ambao hata trillion 2 ya GDP haijafika ujinga ni tatizo kubwa sana Tanzania

Maajabu ni Russia kaweka majimbo matano kibindoni Ila bado anayapigania Hana uthibiti nayo hayo ndo maajabu
 
Tukiweka ushabiki pembeni,

Ukweli ni kwamba tunajua majanga ya nchi za magharibi kwa sababu ya uhuru wa vyombo vya habari uliopo.

Kama urusi nayo ingekuwa na uhuru kama huo, pengine kuna majanga ya kutisha ndani ya Urusi.

vyombo kawa rt, tass na sputnic huwa hawatoi habari zozote mbaya ndani ya urusi.
 
Nchi za magharibi hazijaamini hadi sasa kuwa Urusi imeweza kuhimili vikwazo lukuki vya kiuchumi, kinyume chake nchi za magharibi hususan ulaya magharibi ndizo zilizoumia zaidi. Ilitegemewa kuwa urusi itashindwa kuhimili na hivyo kushindwa kuendesha vita vyake dhidi ya ukraine.

Kwa upande mwingine China japo ina uwezo wa kuivamia na kuishinda Taiwan kwa nguvu za kijeshi, lakini haina ubavu wa kuweza kuhimili vikwazo vya kiuchumi toka nchi za magharibi kama urusi ilivyoweza. Ndiyo maana China haina ubavu hata kidogo wa kuweza kuivamia Taiwan. Itabaki kupiga kelele tu na vitisho vya mazoezi ya kijeshi kuizunguka Taiwan. Mabeberu wa nchi za magharibi wanajua china hana ubavu huo wala hawezi kufanya yale ambayo urusi inafanya leo!!

Sababu kuu kwa nini China haiwezi kuhimili vikwazo vya kiuchumi vya mabeberu:
1. Uchumi wa China unategemea uuzaji wa bidhaa za viwandani na soko lao kubwa ni nchi za ulaya na marekani. Kwa bahati mbaya hizi bidhaa si bidhaa za lazima kiasi kwamba nchi zikigoma kununua zitaathirika, lakini pia kuna bidhaa mbadala toka mataifa mengine.

Hii ni tofauti kabisa na Urusi ambayo yenyewe huuza bidhaa ambazo ni za lazima katika maisha na bidhaa ambazo haziwezi kukosa soko duniani yaani mafuta na gesi!! Ukikataa kununua kwanza lazima uumie na utalazimika kuzitafuta kwa gharama zaidi! Mfano, Poland ilikataa kununua gesi ya urusi kwa sharti la kulipa kwa ruble. Lakini Poland ililazimika kununua gesi hiyo hiyo ya urusi kupitia kwa Ujerumani na kwa bei ya juu zaidi!! Hivi sasa nchi za ulaya wanalazimika kununua gesi kimiminika toka marekani ambayo kwanza haitoshelezi lakini pia ni gharama mara nne zaidi, wakati urusi inauza gesi kwa masoko mengine ya china na India.

2. China inategemea pia viwanda vyake ambavyo vingi vipo huko huko marekani na ulaya! Viwanda hivyo vikipigwa marufuku China haina ubavu wa kuzalisha bidhaa nyingi kuweza kutosheleza masoko yake hata nje ya ulaya na marekani.

3. China haijitoshelezi kwa vyakula na bado hadi leo inategemea kuagiza vyakula toka mataifa mengine hasa marekani na ulaya. Wakinyimwa chakula na kwa vile ni wengi hawawezi kustahimili. Tofauti na Urusi inayojitosheleza kwa vyakula na sehemu kubwa kuuza nchi za nje.

Kwa kadri siku zinavyosonga mbele ndivyo uwezo wa China kuishinda Taiwan kijeshi unavyozidi kupungua maana Taiwan itauziwa silaha za maangamizi na za kujilinda!!

Kama ilivyo kwa Urusi kama ingechelewa zaidi kuivamia ukraine, ingekuta ukraine imejiimarisha zaidi kijeshi.

China inatia huruma lakini haina jinsi zaidi ya kulalamika!! Lakini ni afadhali kutokuthubutu kuliko kuthubutu halafu ukafilisika!!

Kwa Urusi tunavyozungumza, keshaweka kibindoni tayari majimbo matano ikiwemo Crimea na Ukraine hana jinsi zaidi ya kulia lia kwa mabeberu kuomba misaada ya fedha na silaha!! China ubavu huo hana vinginevyo itaaibika!!
umeongea ukweli mtupu ila ma-LGBT hawajibu kufuatana na ulichoelezea badala yake wanafoka balaa
 
We ni mjinga sana uchumi wa china ni almost trillion 18 ya GDP unafananisha na Russia ambao hata trillion 2 ya GDP haijafika ujinga ni tatizo kubwa sana Tanzania

Maajabu ni Russia kaweka majimbo matano kibindoni Ila bado anayapigania Hana uthibiti nayo hayo ndo maajabu
Pole!! unawaaibisha wazazi wako kuwa hawajakulea vizuri, bila shaka walikuwa wanakutukana!!

Kwanza hujajua wala hujaielewa hoja yangu. Sijasema kuwa uchumi wa Urusi ni mkubwa kuliko wa China. Nimesema uchumi wa China japo ni mkubwa lakini HUAUWEZI KUHIMILI VIKWAZO VYA KIUCHUMI toka nchi za magharibi. Sababu ni kuwa uchumi wa China umejengwa juu ya uuzaji wa bidhaa za viwandani na soko kuu ni marekani na ulaya magharibi!! Tatizo ni kuwa bidhaa zenyewe sehemu kubwa si za lazima sana kiasi cha kutokuwa na mbadala duniani. Tofauti na Urusi inayouza mafuta na gesi bidhaa ambazo ni za lazima na hakuna mbadala wake duniani!! Usiponunua wewe atanunua mwenzako na wewe huwezi kukaa bila bidhaa hiyo na utalazimika kuinunua kwa bei ya juu zaidi!! Ulaya wamesusia mafuta India na china wakayachukua!!! Ulaya na Marekani wakisusia bidhaa za China niambie ni nani wa kuziba pengo hilo??
Usipojua kuwa hujui ni mzigo mkubwa sana!!
 
Tukiweka ushabiki pembeni,

Ukweli ni kwamba tunajua majanga ya nchi za magharibi kwa sababu ya uhuru wa vyombo vya habari uliopo.

Kama urusi nayo ingekuwa na uhuru kama huo, pengine kuna majanga ya kutisha ndani ya Urusi.

vyombo kawa rt, tass na sputnic huwa hawatoi habari zozote mbaya ndani ya urusi.
Je BBC hutoa habari mbaya kivile ndani ya Uingereza? Hivi sasa kuna mgomo mkubwa sana wa wauguzi nchini Uingereza na wanaandamana mara kwa mara, lakini hutasikia BBC wameipa uzito habari hiyo. Lakini maanamano yakitokea Iran au China hiyo habari itashikiwa bango live!!!!
 
We ni mjinga sana uchumi wa china ni almost trillion 18 ya GDP unafananisha na Russia ambao hata trillion 2 ya GDP haijafika ujinga ni tatizo kubwa sana Tanzania

Maajabu ni Russia kaweka majimbo matano kibindoni Ila bado anayapigania Hana uthibiti nayo hayo ndo maajabu
Mkuu...mbona kama ww ndio mjinga sasa...Jamaa kaandika vzr sana...ww una muatack...next time jitahidi kuwa mtulivu pls.

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Pole!! unawaaibisha wazazi wako kuwa hawajakulea vizuri, bila shaka walikuwa wanakutukana!!

Kwanza hujajua wala hujaielewa hoja yangu. Sijasema kuwa uchumi wa Urusi ni mkubwa kuliko wa China. Nimesema uchumi wa China japo ni mkubwa lakini HUAUWEZI KUHIMILI VIKWAZO VYA KIUCHUMI toka nchi za magharibi. Sababu ni kuwa uchumi wa China umejengwa juu ya uuzaji wa bidhaa za viwandani na soko kuu ni marekani na ulaya magharibi!! Tatizo ni kuwa bidhaa zenyewe sehemu kubwa si za lazima sana kiasi cha kutokuwa na mbadala duniani. Tofauti na Urusi inayouza mafuta na gesi bidhaa ambazo ni za lazima na hakuna mbadala wake duniani!! Usiponunua wewe atanunua mwenzako na wewe huwezi kukaa bila bidhaa hiyo na utalazimika kuinunua kwa bei ya juu zaidi!! Ulaya wamesusia mafuta India na china wakayachukua!!! Ulaya na Marekani wakisusia bidhaa za China niambie ni nani wa kuziba pengo hilo??
Usipojua kuwa hujui ni mzigo mkubwa sana!!
Upo sahihi
 
Tukiweka ushabiki pembeni,

Ukweli ni kwamba tunajua majanga ya nchi za magharibi kwa sababu ya uhuru wa vyombo vya habari uliopo.

Kama urusi nayo ingekuwa na uhuru kama huo, pengine kuna majanga ya kutisha ndani ya Urusi.

vyombo kawa rt, tass na sputnic huwa hawatoi habari zozote mbaya ndani ya urusi.
Unachosema ni sahihi kabisa!

Mara nyingi, vyombo vya habari vya nchi za magharibi vimekuwa na uwezo na ujasiri wa kukosoa ama kutangaza masuala hasi kuhusu serikali za nchi zao kitu ambacho ni tofauti kabisa na media za upande mwingine (Urusi, China, Korea Kaskazini n.k.).
 
We ni mjinga sana uchumi wa china ni almost trillion 18 ya GDP unafananisha na Russia ambao hata trillion 2 ya GDP haijafika ujinga ni tatizo kubwa sana Tanzania

Maajabu ni Russia kaweka majimbo matano kibindoni Ila bado anayapigania Hana uthibiti nayo hayo ndo maajabu
Soma uchumi buda acha kupayuka. High GDP and per caputa income does not necessarily mean high standard of living/welfare. Kuna factors nyingi sana.
 
Je BBC hutoa habari mbaya kivile ndani ya Uingereza? Hivi sasa kuna mgomo mkubwa sana wa wauguzi nchini Uingereza na wanaandamana mara kwa mara, lakini hutasikia BBC wameipa uzito habari hiyo. Lakini maanamano yakitokea Iran au China hiyo habari itashikiwa bango live!!!!
Hiyo BBC unayoisema hii hapa. Huo mgomo unaosema hausikiki BBC, huu hapa. Umewekewa mpaka na ratiba na maeneo ambayo maandamano yanafanyikia.

Nikuulize swali: Urusi na media zake inaweza kufanya hivi kwaajili ya wananchi wake?
 
Je BBC hutoa habari mbaya kivile ndani ya Uingereza? Hivi sasa kuna mgomo mkubwa sana wa wauguzi nchini Uingereza na wanaandamana mara kwa mara, lakini hutasikia BBC wameipa uzito habari hiyo. Lakini maanamano yakitokea Iran au China hiyo habari itashikiwa bango live!!!!
hapa ndipo unapofanya tukudharau na kudharau kila unachoposti humu kwa sababu umeweka mahaba mbele kuliko uhalisia.
 
Nionavyo urusi wana mfumo kama wa north korea ambapo ni heri adui akushinde kiuchumi lakini sio akushinde uwezo wa kuamua hatima yako(kijeshi).
kama mambo yapo shwari ndani ya urusi unadhani ni kwa nini wananyima uhuru wa vyombo vya habari??
kwa akili zako unadhani makampuni makubwa yaliyokuwa yanafanya kazi urusi yalipoondoka hayajasababisha hata unemployment??
ushawahi kuona RT wanatangaza habari hiyo?
 
Tukiweka ushabiki pembeni,

Ukweli ni kwamba tunajua majanga ya nchi za magharibi kwa sababu ya uhuru wa vyombo vya habari uliopo.

Kama urusi nayo ingekuwa na uhuru kama huo, pengine kuna majanga ya kutisha ndani ya Urusi.

vyombo kawa rt, tass na sputnic huwa hawatoi habari zozote mbaya ndani ya urusi.
Hapa umemaliza kila kitu.
 
Nionavyo urusi wana mfumo kama wa north korea ambapo ni heri adui akushinde kiuchumi lakini sio akushinde uwezo wa kuamua hatima yako(kijeshi).
kama mambo yapo shwari ndani ya urusi unadhani ni kwa nini wananyima uhuru wa vyombo vya habari??
kwa akili zako unadhani makampuni makubwa yaliyokuwa yanafanya kazi urusi yalipoondoka hayajasababisha hata unemployment??
ushawahi kuona RT wanatangaza habari hiyo?
Takriban kampuni elfu zimefungwa, hapa inaonesha serikali imepoteza kodi na ajira kwa watu wake. Ajira laki mbili si mchezo, hapo hatujagusia askari waliopoteza maisha.

Kama laki mbili ajira zimefungwa, ni mambo mengi mno yamekwama hapo russia. Sikumbuki ni lini ila humu Jf ilishawahi kuletwa thread ikielezea Bank kuu ya Russia ikitoa financial statement inayoonesha mapato tu bila kuelezea matumizi.

Nakubaliani na wewe, vyombo vya habari vingekuwa huru Russia, hakika pasingekalika.
 
Back
Top Bottom