China yajitosa Ujenzi wa SGR ya Tanzania

China yajitosa Ujenzi wa SGR ya Tanzania

Umkonto

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2018
Posts
2,652
Reaction score
4,593
Imeripotiwa na gazeti la Mwananchi la leo, januari 6;

Chato. Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya China, Wang Yi anatarajiwa kutua nchini Tanzania kesho Januari 7, ambapo pamoja na mambo mengine atashuhudia utiaji saini mkataba wa ujenzi wa awamu ya tano ya reli ya kisasa (SGR) inayotoka Mwanza hadi Isaka yenye urefu wa kilometa 341.

Kwa sasa ujenzi wa reli hiyo kutoka Dares Salaam hadi Mwanza unatekelezwa na kampuni ya Yapi Merkezi.

Akizungumza na waandishi wa habari wilayani Chato leo Januari 6, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi amesema awamu hiyo ya ujenzi itagharimiwa na Serikali ya Tanzania kwa jumla ya Sh3.0617trillion na itajengwa na kampuni mbili kutoka nchini China.

Pia, Profesa Kabudi amesema Waziri huyo atakayetua katika uwanja wa ndege wa Chato Januari 7 jioni, atafanya mazungumzo na Rais John Magufuli na kuzindua chuo cha ufundi wilayani Chato na kutembelea mwalo wa ziwa Victoria wilayani humo kuangalia shughuli za uvuvi.

Amesema Waziri Wang Yi yupo kwenye ziara ya siku tano katika bara la Afrika ambapo kwa Tanzania atakuwepo kwa siku mbili akishiriki mazungumzo binafsi na Rais John Magufuli kisha kufanya mazungumzo rasmi ya kiserikali ya yeye na ujumbe wake.
 
Hivi pale kamata walikosea wakapavunja kile kipande cha kuvuka reli maeneo ua gold star?

Kuna kipindi palikuwa pashaungwa ghafla nikapita pako chini
 
Naomba kujua mashart nafuu tutakayopewa ambayo wenzetu walishindwa kuyafuata na hivyo bandari na airports zao kuendeshwa na uchina
 
Hapa ndipo naipenda serikali yangu. Awamu ya IV walikabidhi ujenzi wa SGR kwa Wachina lakini alipoingia rais wetu Magufuli tukaambiwa Wachina ni wezi na ule mkataba ni ufisadi mtupu kwahiyo hatuwataki, na Sie wafuasi wake tukashangilia na kutamba. Sasa inakuaje tena leo hii mradi unarudishwa kwa wale wale ambao mkataba wao wa awali ulikuwa na masharti ya kifisadi?
 
Naomba kujua mashart nafuu tutakayopewa ambayo wenzetu walishindwa kuyafuata na hivyo bandari na airports zao kuendeshwa na uchina
" Profesa Palamagamba Kabudi amesema awamu hiyo ya ujenzi itagharimiwa na Serikali ya Tanzania kwa jumla ya Sh3.0617trillion na itajengwa na kampuni mbili kutoka nchini China"

Muda ni msema ukweli
 
Hapa ndipo naipenda serikali yangu. Awamu ya IV walikabidhi ujenzi wa SGR kwa Wachina lakini alipoingia rais wetu Magufuli tukaambiwa Wachina ni wezi na ule mkataba ni ufisadi mtupu kwahiyo hatuwataki, na Sie wafuasi wake tukashangilia na kutamba. Sasa inakuaje tena leo hii mradi unarudishwa kwa wale wale ambao mkataba wao wa awali ulikuwa na masharti ya kifisadi?
Muda ni msema ukweli
 
Mazungumzo binafsi na rais Magufuli!
 
Baada ya hapo bila Shaka mtawaachia wale Wachina Mabosi wa ile Bank ya China Commercial Bank ambao mmewashikilia kwa kesi ya uhujumu uchumi.
 
Isaka adi Rwanda ishawekewa mkataba, kagame alihusika, nahisi alifanya hvyo ili nchi jiran ichangie na si kunufaika bila kutia nguvu, ni kama kumjengea jiran yako ukuta ataofaidika nao bila kuchangia
Good move Magufuli
Kwa hiyo itatoka Dar mpaka Mwanza. Halafu ikifika Mwanza ndio inaenda Kigali, Bujumbura na Goma.
Na Bandari ya Mwanza inaunga na bandari ya Uganda. Huu mradi utatukwangua na kutukamua na kutuacha na madeni makubwa mno.
 
Hapa ndipo naipenda serikali yangu. Awamu ya IV walikabidhi ujenzi wa SGR kwa Wachina lakini alipoingia rais wetu Magufuli tukaambiwa Wachina ni wezi na ule mkataba ni ufisadi mtupu kwahiyo hatuwataki, na Sie wafuasi wake tukashangilia na kutamba. Sasa inakuaje tena leo hii mradi unarudishwa kwa wale wale ambao mkataba wao wa awali ulikuwa na masharti ya kifisadi?
Tunaingia mkataba upya usio na wizi
 
Isaka adi Rwanda ishawekewa mkataba, kagame alihusika, nahisi alifanya hvyo ili nchi jiran ichangie na si kunufaika bila kutia nguvu, ni kama kumjengea jiran yako ukuta ataofaidika nao bila kuchangia
Good move Magufuli
Huku jamii forum kumekufa sasa hivi kuna great thinker kweli
 
Wiki nzima hii mapambio kibaooo. Si mlisema wachina wezi
 
Kwa sasa ujenzi wa reli hiyo kutoka DSM hadi MWANZA unatekelezwa na kampuni ya Yapi Merkezi.
Acha upotoshaji!
 
Kwanini wameamua kupeleka reli Mwanza na si Kigoma ilihali tunaona wakongo wengi wakija kufunga mizigo Kkoo kuliko Waganda..huu ni upuuzi mkubwa unafanyika unakamilishaje tawi wakati reli kuu ya kati mwisho ni Kigoma?
scientific research bobezi imefanyika na kuonyesha italipa but KIGOMA NI ENEO HASWA MUHIMU ZAIDI [DRC BURUNDI RWANDA] Suala ni kuongezea tu meli ya kisasa ya uhakika mle ziwani.
 
Back
Top Bottom