Chinese food zinanishinda kula, kuna wengine wenye tatizo hili?

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Katika starehe ninazopenda hapa duniani ni kula na kulala, huwa ninapenda kujifunza kupika vyakula tofauti, ninapenda kujaribu kula vyakula tofauti na vile nilivyozoea. Katika marafiki niliyowapata nimeweza kumudu kula vyakula vya nchi wanazotoka.

Kitanda changu ninahakikisha ni kisafi mahali ninapoweza kupata usingizi mzuri kwani hii ni starehe unayopata bila malipo.

Katika vyakula nimejaribu kula Chinese nimeshindwa kabisa, siku ya kwanza nilikuwa na wenzangu safarini, group lote waliamua kwenda Chinese restarant, niliingia chakula chote nilichokula nilirudisha change pale, ilibidi niweke tissue mdomoni nikikimbila bafuni. Mara ya pili binamu yangu alinipeleka buffet ya wa-China, nilishindwa kumwambia hiki hakipandi, tumefika nilijikaza, tumerudi nyumbani yaliyonitokea sina haja ya kusema mengi.

Hivi ni mimi tu au kuna ambao chakula cha wa-China hakipandi?
 
Mmmmh! Kuna hii pia
 

Attachments

  • Hatari.jpg
    55.3 KB · Views: 203
Lazima uwe very precise unapoenda kula kwenye Chinese restaurants.

Jamaa wanakula vitu vingi mno. Mbwa, mende, chura, sasa isije ukawa ulikula mix ya Chinese noodles na hizo nyama [emoji3]
 
Lazima uwe very precise unapoenda kula kwenye Chinese restaurants.

Jamaa wanakula vitu vingi mno. Mbwa, mende, chura, sasa isije ukawa ulikula mix ya Chinese noodles na hizo nyama [emoji3]
Wanakuwa na buffet wanakwambia 15,000-20,000 eat as much as you can, sasa hapo ndiyo kasheshe yenyewe inapokuja.
 
Mimi nilikula buffet moja ya kichina, sahani ya kwanza nilikwenda chooni. Nikajaribu ya pili nikaishia huko kwa saa 1 ndio nikatoka. Sikukaa tena juzi nilikwenda Kingston, Jamaica nilikuta jamaa anagombana na mchina kwa kumlisha vyakula vibovu.[emoji1] [emoji1] [emoji111]



Ndukiiiii[emoji125] [emoji125] [emoji125]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rafiki yangu aliishi nyumba moja na mchina, ananiambia wakati wanapika wanakuwa na bakuli ambalo wanaosha kila kitu kitakachotumika kwenye mapishi na mwisho yale maji ya kuoshea yanaongezewa kwenye mchuzi.
 
sasa nenda hongkong uchafuke roho mwisho wa siku utaagiza mwenyewe kiletwe hichohicho chakula.kwenye slaughter houses zao wamejaza mabanda ya mbwa,kuna kipond cha vyura,glass chambers za mijoka,kuna earthworms sehemu flani,bugs,panya weupe,panzi wakubwa...yani utadhani ni kijumba cha ushirikina kumbe ndio msosi...ila wana mchuzi very delicious wewe nenda uagize shark fin soup kule mitaa ya Guangzhou utakipenda sana.keep sampling ukishazoea utatafutaga hayo maeneo kwa bidii za kufa mtu..
 
Wachina wengi sio hygienic. Lakini ni bora mara mia ukaagiza a la carte kuliko buffet.
Ni kweli mkuu, tatizo liliongezeka pale mmoja wa rafiki zangu aliponiambia alikuwa Cambodia akiwa restaurant kuna mzungu alikwenda na mbwa akamfunga nje, aliingia ndani akaoda chakula, kilichelewa kidogo, lakini aliletewa starter ya soup, main course fried rice, dessert ice cream and coffee. Ametoka nje mbwa wake hamuoni, kuuliza anaambiwa ni ile starter uliyokula sorry.
 
Hauko peke yako SE. Mie kwenye restaurant zao kuna harufu fulani hivi siipendi hata kidogo. Na hata nikienda basi huwa ni kwa ajili ya company tu na naishia kugusa gusa tu kusema kweli. Ukiacha hiyo harufu nahofia pia kulishwa nyama ya mbwa.

 
Hauko peke yako SE. Mie kwenye restaurant zao kuna harufu fulani hivi siipendi hata kidogo. Na hata nikienda basi huwa ni kwa ajili ya company tu na naishia kugusa gusa tu kusema kweli. Ukiacha hiyo harufu nahofia pia kulishwa nyama ya mbwa.
Na hata ukienda chooni unakuta vyoo vyao usafi wa plastic, ninashukuru kuwa siko peke yangu.
 
Reactions: BAK
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…