Chombo cha anga za juu cha Shenzhou 14 cha China chaleta mbegu za mpunga zilizopatikana katika obiti kwa mara ya kwanza duniani

Chombo cha anga za juu cha Shenzhou 14 cha China chaleta mbegu za mpunga zilizopatikana katika obiti kwa mara ya kwanza duniani

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
Kundi la tatu la sampuli za majaribio ya sayansi ya anga za juu, ambalo lilirudishwa na chombo cha anga za juu cha Shenzhou 14 cha China, lilirejeshwa Beijing alfajiri ya tarehe 5. Sampuli zilizorejeshwa ni pamoja na vifurushi vitatu vya baridi vya sampuli za kibaiolojia na mfuko mmoja wa sampuli usio na kontena.

Miongoni mwao, sampuli tatu za vifurushi baridi vya sampuli za kibaolojia zilikuwa ni sampuli za majaribio za mpunga na Arabidopsis thaliana ambazo zimekua katika anga kwa siku 120, ni mara ya kwanza kwa mbegu za mpunga kupatikana katika obiti duniani. Kwa sasa, sehemu ya sampuli zilirejeshwa kwenye maabara ya Chuo cha Sayansi cha China ili kuendelea kulimwa.

VCG111413086070.jpg


VCG111413086032.jpg
 
Wazioteshe halafu mbegu ikishapatikana ya kutosha, watugawie tuanze kulima mpunga hapa duniani wa kutoka Sayari zingine
 
Kundi la tatu la sampuli za majaribio ya sayansi ya anga za juu, ambalo lilirudishwa na chombo cha anga za juu cha Shenzhou 14 cha China...
Ni wapi huko? Hakuna utafiti ambao umeshaonyesha uwepo wa viumbe hai kwenye anga za juu. Source?
 
Back
Top Bottom