Chombo Gani cha habari cha Kimataifa kinatoa habari za uhakika

Chombo Gani cha habari cha Kimataifa kinatoa habari za uhakika

ngara23

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2019
Posts
9,091
Reaction score
21,087
Kila nikisikiliza media kubwa zilizoaminika kwasasa ni kama TBC tu

Iwe BBC Swahili, VOA, CNN au Al Jazeera zote ni ovyo tu zinatoka habari za kuendelea na za uongo na uzushi sana
Wanainanga Russia, Parestina, Libya, North Korea nk
Lakini katu wanawasifu wahalifu kama Ukraine, Rwanda, Israel nk
Kwa Sasa angalau kidogo DW
 
Kila nikisikiliza media kubwa zilizoaminika kwasasa ni kama TBC tu

Iwe BBC Swahili, VOA, CNN au Al Jazeera zote ni ovyo tu zinatoka habari za kuendelea na za uongo na uzushi sana
Wanainanga Russia, Parestina, Libya, North Korea nk
Lakini katu wanawasifu wahalifu kama Ukraine, Rwanda, Israel nk
Kwa Sasa angalau kidogo DW
Biashara ya Media inategemea matangazo, angalia alichofanyiwa Elon musk Aliachia kidogo habari za Palestina wakampiga pin ya maana, sasa hivi yupo Busy kuhamasisha Ubaguzi.

Njia nzuri ya Kutumia angalia Media kwa matukio ya sehemu husika. Mfano tumia BBC kuangalia matukio ya Uingereza, Tumia DW matukio ya Ujerumani, Al jazeera Matukio ya Middle East etc Ukisema utumie BBC ama CNN kupata Habari za China kuna Uwezekano mkubwa kulishwa Matango Pori.
 
Wewe mkuu una lako jambo, unataka Urusi asifiwe kwa kuvamia? Palestine hakuna anayehangaika nayo wanaotafutwa ni Hamas ni kama kule Afghanistan waliokuwa wanaotafutwa ni Al qaida.
Al qaida si ndio hao wanasaidiwa na Ukraine Mali mbona hawatafutwi tena? Na Tunajua nani anamsaidia Ukraine.

Comment yako hii inaelezea Exactly kwanini mleta mada ameuliza hili swali.
 
Binafsi nilishanipoteza ham ya kuangalia habari; fikiria unarudi nyumbani jioni umepigika ukikaa mezeni umewasha kativii kako; ni habari za majonzi tuuuuuuu, hata ham ya kula inakwisha; hakuna habari za kutia mtu matumaini........

ILA kama hupendi kupata habari za motomoto, usiangalie TVs za nje, badala yake angalia TBC utapata habari za ukweli na uhakika; ni ushauri tu!
 
Media ipe mtazamo uliochanganywa na akili zako mwenyewe, usimeze kila kitu. Hakuna media bora ila kuna zenye unafuu kuliko nyingine. Wewe fuatilia zote ila ujue kuchuja, kama ni habari inahusu China jiulize ni habari mbaya au nzuri kisha jiulize chombo kilichoitoa kina affiliation na China au hakina. China Daily, People's Daily, Global Times, CCTV4, CGNT, South China Morning Post, etc hivyo ni vyombo vya China haviwezi isemea vibaya. Ukisoma taarifa zake linganisha na taarifa za vyombo vingine ila zingatia nchi marafiki wa China na nchi adui wa China.

Mfano Urusi ni rafiki wa China ila usitarajie taarifa njema ya China kutengeneza jet engine yenye ubora zaidi itaifurahisha Urusi ambayo inategemewa na China kwenye hiyo teknolojia. So hapo chombo cha China kikisema engine iko vizuri, na vyombo vya Ulaya vikasema hata vya Urusi vikiponda ujue iko vizuri.

Hata kwa Urusi Sputnik, Zvezda, RT, RIA Novosti zikisema kitu chuja vilevile. Wakiisema vibaya Uingereza, na Aljazeera ikaisema vibaya, na Fox News hapo ni sawa. Ila sio Sputnik ishangilie Waziri Mkuu wa Uingereza kujiuzuru iseme alikuwa mbovu, na anayekuja itamchukia, na aliyetangulia, na atakayefuata tena ambaye bado hatumjui.

Aljazeera watakuwa neutral kuliko vyombo vingi vya Kiarabu ila juu ya Israel watapotosha na juu ya Saudi Arabia wanaponda sana na kukuza mambo. Waandishi wa habari wa Aljazeera kadhaa wameuwawa na Israel wakiwa na silaha na mjumuiko wa makundi ila utasikia Aljazeera inawaita waandishi wake. Sasa mwandishi aliyevaa kiraia na bunduki akiwa kwenye handaki wapi na wapi. Akiuwawa mwandishi amevaa PRESS, helmet na lile vazi la blue hapo ndio kosa.
 
Media ipe mtazamo uliochanganywa na akili zako mwenyewe, usimeze kila kitu. Hakuna media bora ila kuna zenye unafuu kuliko nyingine. Wewe fuatilia zote ila ujue kuchuja, kama ni habari inahusu China jiulize ni habari mbaya au nzuri kisha jiulize chombo kilichoitoa kina affiliation na China au hakina. China Daily, People's Daily, Global Times, CCTV4, CGNT, South China Morning Post, etc hivyo ni vyombo vya China haviwezi isemea vibaya. Ukisoma taarifa zake linganisha na taarifa za vyombo vingine ila zingatia nchi marafiki wa China na nchi adui wa China.

Mfano Urusi ni rafiki wa China ila usitarajie taarifa njema ya China kutengeneza jet engine yenye ubora zaidi itaifurahisha Urusi ambayo inategemewa na China kwenye hiyo teknolojia. So hapo chombo cha China kikisema engine iko vizuri, na vyombo vya Ulaya vikasema hata vya Urusi vikiponda ujue iko vizuri.

Hata kwa Urusi Sputnik, Zvezda, RT, RIA Novosti zikisema kitu chuja vilevile. Wakiisema vibaya Uingereza, na Aljazeera ikaisema vibaya, na Fox News hapo ni sawa. Ila sio Sputnik ishangilie Waziri Mkuu wa Uingereza kujiuzuru iseme alikuwa mbovu, na anayekuja itamchukia, na aliyetangulia, na atakayefuata tena ambaye bado hatumjui.

Aljazeera watakuwa neutral kuliko vyombo vingi vya Kiarabu ila juu ya Israel watapotosha na juu ya Saudi Arabia wanaponda sana na kukuza mambo. Waandishi wa habari wa Aljazeera kadhaa wameuwawa na Israel wakiwa na silaha na mjumuiko wa makundi ila utasikia Aljazeera inawaita waandishi wake. Sasa mwandishi aliyevaa kiraia na bunduki akiwa kwenye handaki wapi na wapi. Akiuwawa mwandishi amevaa PRESS, helmet na lile vazi la blue hapo ndio kosa.
Umenena vyema mkuu
 
Back
Top Bottom