Chombo Huru kichunguze tukio la Binti kubakwa na kulawitiwa, Kauli za Polisi zinatia shaka kupatikana Haki yake

Chombo Huru kichunguze tukio la Binti kubakwa na kulawitiwa, Kauli za Polisi zinatia shaka kupatikana Haki yake

Black Butterfly

Senior Member
Joined
Aug 31, 2022
Posts
130
Reaction score
368
Kwa takriban mwezi sasa Polisi bado wanahangaika na uchunguzi wa tukio la Binti aliyeonekana katika Video akifanyiwa vitendo vya Ukatili na Wanaume Watano na bado kumekuwa na kauli za kutia shaka kuhusu haki ya huyo binti. Baadhi ya Askari wamekuwa wakitoa kauli zinazoonesha wazi kumkandamiza huyo Binti.

Lakini kuchelewa kupelekwa Mahakamani kwa Jalada la Uchunguzi wa tukio hilo kunazidi kuibua sintofahamu wakati tangu Agosti 9, 2024 Polisi walisema uchunguzi umekamilika sasa nini kinachelewesha kufikishwa Mahakani watuhumiwa waliokamatwa?

Hili jambo hadi sasa linahitaji Uchunguzu wa Tume Huru itakayoundwa kutoka nje ya Jeshi la Polisi na Vyombo vingine ambavyo baadhi vimeonekana kulinda au kuwaficha wahusika. Ikumbukwe tayari inasemekana mmoja waliowatuma wabakaji ni Afande. Sasa hali hiyo tu inaingiza mgangano wa kumaslahi.

Kama wananchi wenye uchungu na haki zetu tunaomba Uchunguzi wa Vyombo huru katika suala hili ili tuwe na amani ya matokeo. Bila hivyo tutapata wasiwasi kwa kulinganisha na matukio mengine ambayo polisi wamekuwa wakichunguza laki ni hakuna matokeo ya kueleweka yanayokuja.
 
Shida watateuliwa hao hao Polisi kuchunguza hii nchi kuanzia juu mpaka chini vitongojini inajiendea tuuu.
 
Naunga mkono hoja Mkuu,

Haki inapopatikana ndio hupunguza watu kujichukulia sheria mkononi.
 
Kwa takriban mwezi sasa Polisi bado wanahangaika na uchunguzi wa tukio la Binti aliyeonekana katika Video akifanyiwa vitendo vya Ukatili na Wanaume Watano na bado kumekuwa na kauli za kutia shaka kuhusu haki ya huyo binti. Baadhi ya Askari wamekuwa wakitoa kauli zinazoonesha wazi kumkandamiza huyo Binti.

Lakini kuchelewa kupelekwa Mahakamani kwa Jalada la Uchunguzi wa tukio hilo kunazidi kuibua sintofahamu wakati tangu Agosti 9, 2024 Polisi walisema uchunguzi umekamilika sasa nini kinachelewesha kufikishwa Mahakani watuhumiwa waliokamatwa?

Hili jambo hadi sasa linahitaji Uchunguzu wa Tume Huru itakayoundwa kutoka nje ya Jeshi la Polisi na Vyombo vingine ambavyo baadhi vimeonekana kulinda au kuwaficha wahusika. Ikumbukwe tayari inasemekana mmoja waliowatuma wabakaji ni Afande. Sasa hali hiyo tu inaingiza mgangano wa kumaslahi.

Kama wananchi wenye uchungu na haki zetu tunaomba Uchunguzi wa Vyombo huru katika suala hili ili tuwe na amani ya matokeo. Bila hivyo tutapata wasiwasi kwa kulinganisha na matukio mengine ambayo polisi wamekuwa wakichunguza laki ni hakuna matokeo ya kueleweka yanayokuja.
Una hoja lakini tukio lenyewe liko wazi wala halihitaji uchunguzi, video zipo ni kuwatambuwa tu wahusika.
 
Aliongea akiwa amelewa!

20240819_140603.jpg
 
Kwa takriban mwezi sasa Polisi bado wanahangaika na uchunguzi wa tukio la Binti aliyeonekana katika Video akifanyiwa vitendo vya Ukatili na Wanaume Watano na bado kumekuwa na kauli za kutia shaka kuhusu haki ya huyo binti. Baadhi ya Askari wamekuwa wakitoa kauli zinazoonesha wazi kumkandamiza huyo Binti.

Lakini kuchelewa kupelekwa Mahakamani kwa Jalada la Uchunguzi wa tukio hilo kunazidi kuibua sintofahamu wakati tangu Agosti 9, 2024 Polisi walisema uchunguzi umekamilika sasa nini kinachelewesha kufikishwa Mahakani watuhumiwa waliokamatwa?

Hili jambo hadi sasa linahitaji Uchunguzu wa Tume Huru itakayoundwa kutoka nje ya Jeshi la Polisi na Vyombo vingine ambavyo baadhi vimeonekana kulinda au kuwaficha wahusika. Ikumbukwe tayari inasemekana mmoja waliowatuma wabakaji ni Afande. Sasa hali hiyo tu inaingiza mgangano wa kumaslahi.

Kama wananchi wenye uchungu na haki zetu tunaomba Uchunguzi wa Vyombo huru katika suala hili ili tuwe na amani ya matokeo. Bila hivyo tutapata wasiwasi kwa kulinganisha na matukio mengine ambayo polisi wamekuwa wakichunguza laki ni hakuna matokeo ya kueleweka yanayokuja.
Hili limeshavhukuliwa hatuna mkuu,hata RPCwa Dodoma katolewa kwenye nafasi yake!
 
Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzake. Sikutegemea msemaji wa Polisi aseme Eti yule bint alikuwa anajiuza, Mkuu wa Taasisi ya haki za binadamu Tanzania bado yuko kimya. Dr Gwajima ambaye huwa very reactive ikitokea mwana Jamii hasa mama au mtoto Kate Sewa ukatili hukiwasha mara moja, safari hii yuko kimya. Mwisho Rais wa Jamhuri ambaye ana 'maumbile ya kike' hana habari na hili. Sijui yuko busy na Kizimkazi festival. Mama sema neno moja tu, na roho zetu zipone.
 
Harufu kali ya FEMINISTS kuuteka mjadala! Yule kijana wa Manyara aliyedhalilishwa na Waziri yuko kwenye hali gani kwa sasa?
 
Matendo ya namna hii ya vyombo vyetu vilivyopewa dhamana ya kusimamia na kulinda haki za wananchi ndiyo wakati mwingine husababisha matukio ya mauaji na watu kuumizana kwa sababu mtu anaona hana njia nyingine ya kupata haki yake zaidi ya kulipa kisasi.
Natoa rai kwa wale wote wenye dhamana ya kulinda haki za wananchi watimize wajibu wao bila upendeleo wa namna yoyote na hasa kwa wale wanaoamini uwepo wa Mungu wajue wazi siku ya hukumu itafika na watawajibika kwa matendo yao maovu,duniani tunaishi kwa muda mfupi sana na siku ya siku ikifika huyo wanayemkingia kifua hatoweza kuwasaidia chochote mbele ya hakimu wa kweli Baba Mungu wetu.
 
Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzake. Sikutegemea msemaji wa Polisi aseme Eti yule bint alikuwa anajiuza, Mkuu wa Taasisi ya haki za binadamu Tanzania bado yuko kimya. Dr Gwajima ambaye huwa very reactive ikitokea mwana Jamii hasa mama au mtoto Kate Sewa ukatili hukiwasha mara moja, safari hii yuko kimya. Mwisho Rais wa Jamhuri ambaye ana 'maumbile ya kike' hana habari na hili. Sijui yuko busy na Kizimkazi festival. Mama sema neno moja tu, na roho zetu zipone.
Nani aliyekwambia Dr Gwajima yupo kimya wakati yeye ndiye aliyeongea na waziri wa mambo ya ndani?

Unadhani IGP amefanya hivyo kwa kupenda?

IMG-20240819-WA0031.jpg
 
Twende tu scotland yard tukaombe msaada, haya mambo yashatushinda.
 
Mwandishi na mhariri wa hili gazeti wachukuliwe hatua pia. Hiki kichwa cha habari kimekaa kimkakati kupunguza makali ya ukatili kwa kutweza utu wa binti
Ilipaswa iandikwe 'Kahaba' kunukuu maneno ya huyo RPC Dodoma.
 
Back
Top Bottom