CHRISTMASS ni ya kina Pope Julius I au ni yetu sisi na Yesu wetu?

CHRISTMASS ni ya kina Pope Julius I au ni yetu sisi na Yesu wetu?

Mzee katika Ukristo hakuna sikukuu zinazoamriwa kibiblia. sikukuu zote zimetokana na maazimio ya waumini walioona ni vema kukumbuka ukweli fulani ya imani na kuikumbuka kwenye siku maalumu.
Hakuna amri kukumbuka siku ya kufufuka kwa Yesu (Pasaka) wala hakuna amri ya kukumbuka kufika kwa Roho Mtakatifu kwa watu wengi (Pentekoste) wala kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu (Krismasi).
Kwa Pasaka na Pentekoste hao waumini wa siku za kwnaza waliweza kutumia tarehe zilizotajwa katika Biblia kwa hiyo walipanga tarehe zilizofaa na taarifa (kwa ufahamu wao - maana kalenda zilibadilika hivyo kila tarehe ni ya kibinadamu).
Kuhusu Krismasi hakuna dokezo la tarehe, Hivyo waliteua siku kwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu.
Ambako hakuna ubaya, maana katika Ukristo hakuna amri wala maagizo kutoka Mungu kuhusu tarehe fulani.

Ndugu Waislamu wengi wanapenda sikukuu ya Maulidi, ambayo pia si tarehe ya kuzaliwa ya Mtume bali sikukuu iliyoanzishwa karne kadhaa baadaye. Waislamu wengine wanaipinga wakidai si halali kuanzisha sherehe isiyoamriwa katika Qurani au sunna ya mtume mwenyewe.

Waingereza husheherekea Queens Birthday kwenye mwezi ulioteuliwa kwa sababu hali ya hewa inafaa zaidi kwa sherehe ya umma, si kwenye siku alikozaliwa.

Ubaya wapi?
Suala la kusherehekea Krismas ni suala la MAPOKEO; huu ndio mwanzo wake kwani hakuna, nasema tena, hakuna andiko lolote kwenye BIBLIA linalozungumzia hii sikukuu, tofauti na PASAKA ambayo Yesu Kristo, Aliye Hai ametuagiza tuikimbuke (hata kama ni kupitia kwa Wayahudi - kwenye Agano jipya!). Zaidi ya hapo, wajanja wakaifanya iwe na mtizamo na mwelekeo wa kibiashara zaidi na watu wengi, hata Wakristo, wakaingia mkenge huu. Twende na maandiko ili tusikumbwe na mafundisho ya UONGO na mwisho wake tuikose Mbingu jamani!
 
Suala la kusherehekea Krismas ni suala la MAPOKEO; huu ndio mwanzo wake kwani hakuna, nasema tena, hakuna andiko lolote kwenye BIBLIA linalozungumzia hii sikukuu, tofauti na PASAKA ambayo Yesu Kristo, Aliye Hai ametuagiza tuikimbuke (hata kama ni kupitia kwa Wayahudi - kwenye Agano jipya!). Zaidi ya hapo, wajanja wakaifanya iwe na mtizamo na mwelekeo wa kibiashara zaidi na watu wengi, hata Wakristo, wakaingia mkenge huu. Twende na maandiko ili tusikumbwe na mafundisho ya UONGO na mwisho wake tuikose Mbingu jamani!
SIna uhakika tofauti ya Pasaka (kama kumbukumbu ya ufufuo wa Yesu) na Krismasi unapata wapi? Katika Biblia sijawahi kuona sikukuu ya Pasaka ya Kikristo (usichanganye na ile sherehe ya Pasaka ya Kiyahudi).
Zote mbili ziliundwa kwa hiari yao na waumini ili kukumbuka ukweli fulani wa imani nyao.
 
SIna uhakika tofauti ya Pasaka (kama kumbukumbu ya ufufuo wa Yesu) na Krismasi unapata wapi? Katika Biblia sijawahi kuona sikukuu ya Pasaka ya Kikristo (usichanganye na ile sherehe ya Pasaka ya Kiyahudi).
Zote mbili ziliundwa kwa hiari yao na waumini ili kukumbuka ukweli fulani wa imani nyao.
Tulia na urudi kwenye maandiko au ufanye consultation na viongozi wako wa dini/imani/dhehebu juu ya haya masuala mawili. Labda baadaye nikitulia naweza kukupa maandiko kutoka kwenye Biblia Takatifu juu ya PASAKA.
 
Tulia na urudi kwenye maandiko au ufanye consultation na viongozi wako wa dini/imani/dhehebu juu ya haya masuala mawili. Labda baadaye nikitulia naweza kukupa maandiko kutoka kwenye Biblia Takatifu juu ya PASAKA.
Karibu sana. Ila ukumbuke tunajadili sikukuu ya Wakristo siyo ile Pasaka ya Kiyahudi (=Pessackh). Maandiko kuhusu pasaka ni mengi. Hakuna kuhusu sikukuu ya Kikristo.
Hilyo ndilo swali tunalojadili.
 
SIna uhakika tofauti ya Pasaka (kama kumbukumbu ya ufufuo wa Yesu) na Krismasi unapata wapi? Katika Biblia sijawahi kuona sikukuu ya Pasaka ya Kikristo (usichanganye na ile sherehe ya Pasaka ya Kiyahudi).
Zote mbili ziliundwa kwa hiari yao na waumini ili kukumbuka ukweli fulani wa imani nyao.
fanyeni hivi kwa kunikumbuka.....-Jesus

Anyway.. kina babu chrismas na wale Sungura wa Pasaka waliingiaje kwenye ukristo?
 
Mzee katika Ukristo hakuna sikukuu zinazoamriwa kibiblia. sikukuu zote zimetokana na maazimio ya waumini walioona ni vema kukumbuka ukweli fulani ya imani na kuikumbuka kwenye siku maalumu.
Hakuna amri kukumbuka siku ya kufufuka kwa Yesu (Pasaka) wala hakuna amri ya kukumbuka kufika kwa Roho Mtakatifu kwa watu wengi (Pentekoste) wala kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu (Krismasi).
Kwa Pasaka na Pentekoste hao waumini wa siku za kwnaza waliweza kutumia tarehe zilizotajwa katika Biblia kwa hiyo walipanga tarehe zilizofaa na taarifa (kwa ufahamu wao - maana kalenda zilibadilika hivyo kila tarehe ni ya kibinadamu).
Kuhusu Krismasi hakuna dokezo la tarehe, Hivyo waliteua siku kwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu.
Ambako hakuna ubaya, maana katika Ukristo hakuna amri wala maagizo kutoka Mungu kuhusu tarehe fulani.

Ndugu Waislamu wengi wanapenda sikukuu ya Maulidi, ambayo pia si tarehe ya kuzaliwa ya Mtume bali sikukuu iliyoanzishwa karne kadhaa baadaye. Waislamu wengine wanaipinga wakidai si halali kuanzisha sherehe isiyoamriwa katika Qurani au sunna ya mtume mwenyewe.

Waingereza husheherekea Queens Birthday kwenye mwezi ulioteuliwa kwa sababu hali ya hewa inafaa zaidi kwa sherehe ya umma, si kwenye siku alikozaliwa.

Ubaya wapi?
Mzee, je wewe ni mzuri kiasi gani kwenye Bibilia? Bible imetaja Sikujua za kuzienzi
 
Mzee katika Ukristo hakuna sikukuu zinazoamriwa kibiblia. sikukuu zote zimetokana na maazimio ya waumini walioona ni vema kukumbuka ukweli fulani ya imani na kuikumbuka kwenye siku maalumu.
Hakuna amri kukumbuka siku ya kufufuka kwa Yesu (Pasaka) wala hakuna amri ya kukumbuka kufika kwa Roho Mtakatifu kwa watu wengi (Pentekoste) wala kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu (Krismasi).
Kwa Pasaka na Pentekoste hao waumini wa siku za kwnaza waliweza kutumia tarehe zilizotajwa katika Biblia kwa hiyo walipanga tarehe zilizofaa na taarifa (kwa ufahamu wao - maana kalenda zilibadilika hivyo kila tarehe ni ya kibinadamu).
Kuhusu Krismasi hakuna dokezo la tarehe, Hivyo waliteua siku kwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu.
Ambako hakuna ubaya, maana katika Ukristo hakuna amri wala maagizo kutoka Mungu kuhusu tarehe fulani.

Ndugu Waislamu wengi wanapenda sikukuu ya Maulidi, ambayo pia si tarehe ya kuzaliwa ya Mtume bali sikukuu iliyoanzishwa karne kadhaa baadaye. Waislamu wengine wanaipinga wakidai si halali kuanzisha sherehe isiyoamriwa katika Qurani au sunna ya mtume mwenyewe.

Waingereza husheherekea Queens Birthday kwenye mwezi ulioteuliwa kwa sababu hali ya hewa inafaa zaidi kwa sherehe ya umma, si kwenye siku alikozaliwa.

Ubaya wapi?
Kumbukumbu 16:1 “Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka Bwana, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku Bwana; Mungu wako.

2 Nawe umchinjie pasaka Bwana, Mungu wako, katika kundi la kondoo na la ng’ombe, mahali atakapochagua Bwana apakalishe jina lake”.
 
fanyeni hivi kwa kunikumbuka.....-Jesus

Anyway.. kina babu chrismas na wale Sungura wa Pasaka waliingiaje kwenye ukristo?
"Fanyeni hivi kwa kunikumbuka" - hii si kuhusu sikukuu yoyote, ni kuhusu aina ya ibada ya ekaristia (chakula cha Bwana). Sungura wa Pasaka, mayai ya Pasaka ni desturi za baadaye ya kieneo zilizoanza Ulaya miaka 1500 baada ya Kristo.
krismasi ni sikukuu ambayo tuna habari zake mapema, baada ya mwaka 300 hivi.
 
Kumbukumbu 16:1 “Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka Bwana, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku Bwana; Mungu wako.

2 Nawe umchinjie pasaka Bwana, Mungu wako, katika kundi la kondoo na la ng’ombe, mahali atakapochagua Bwana apakalishe jina lake”.
Nilivyosema pale juu: Pasaka ya Kiyahudi (kufuatana na aya unyotaja; Kiingereza "Passover") ambayo ni kumbukumbu ya kutoka kwa Wanaisraeli katika utumwa nchini Misri ni jambo tofauti na ile Pasaka ya Kikristo inayokumbuka habari ya ufufuo wa Kristo.

Sababu ya kuwa na majina ya kufanana kwa Kiswahili (si kwa Kiingereza na lugha nyingine! - Passover as Jewish holiday -Easter as as Christian holiday, hakuna anayechanganya hizo) ni kwamba Yesu alikamatwa na kuhukumiwa baada ya kusheherekea sikukuu ya Kiyahudi.
 
Sasa shida hapo iko wapi?? Kama warumi walikuwa wanaabudu na kusherehekea sikukuu ya Mungu jua tar. 25.. kisha Papa akaona huo ni upuuzi na ni afadhali hiyo siku tumsherehekee Mungu wa kweli, hapo ubaya upo wapi? Maana siku zote na tarehe ni vya Mungu... Inaonekana kinachokusumbua wewe ni siku hiyo ya tarehe 25... Ila elewa kuwa kwa wakristo suala kubwa sio tarehe wala siku bali ni kuzaliwa kwa mwokozi.. na hata pasaka ni hivyo hivyo ishu sio siku wala saa bali kufa na kufufuka.
Acheni ujinga kwa nini isitafutwe sherehe kwenye mwezi wa mimba au tuhesabu miezi 9 ndio itafutwe siku badala ya kupaka asali kitu kilichooza?
 
Tahere siyo issue, ila ukweli ni kwamba yesu alizaliwa na alivyozaliwa watu walisheherekea.

Mimi bibi yangu hajui tarehe ya kuzaliwa ila kila ikifika 01 january huwa tunasheherekea birthday yake.
 
yerickonyerere_20201227_182247_0.jpg
 
wasaalam, wakuu

Ninaandika haya huku , nikijua nitapingwa zaidi kuliko kuungwa mkono.

Naandika huku nikitaraji pia dhihaka na kashfa kuliko majadaliano yenye mapenzi mema

Naandika sio kwa vile naelewa athari za upagani katika dini na madhehebu yetu

Naandika kwa sababu naelewa ,maafa ya kibinaadamu ambayo wapagani na nyingi zao mila na desturi ambazo zimeacha nyuma katika madhehebu yetu na dini zetu.

Naandika kwasababu pia mimi sio wa kwanza kuandika hapa na wala si wa mwisho kuandika haya.

Naandika kwasababu nilitamani kuandika hiki na nmeandika.

Tumezoea makala za namna hii kwingi tuendako katika majira haya ,lakini kila zama zinavyozidi kujongea taswira mpya inajengeka ndivyo navyo tunazidi kukumbushana kwa hekima njema

Basi

Kama utauliza popote duniani kuhusu 'christ mass' majawabu yake yatakuwa ni sikukuu ya kuzaliwa bwana yesu....lakini moja kwa moja hilo sio jibu la kweli la swali hilo ......kama ungeli ipata na ungelirejelea vitabu vya history ya kale na biblia kwa ujumla ungelipata sababu ya kupinga na kupangua kumbukizi hii ya mazazi ya kiongozi na mwokozi yesu kristo.
View attachment 1655856
Katika injili zote haijapata kuwepo thibati, ya bwana YESU eti ya kwamba alizaliwa majira yapi?? na tarehe zipi.

Na mpaka ilipofikia mwaka 349 AD dunia haikuwahi kuwa na sikukuu ya kusherekea mazazi ya bwana yesu.

Kila ifikapo tarehe 25 Disemba watu husherekea kuzaliwa kwa bwana yesu na Wengi wetu kwa pumbao letu tulilo nalo tunaamini hiyo ni siku haswa bwana mwokozi alipoletwa duniani na mama yake, mama mwema , mtakatifu, mkarimu, mweupe wa moyo na nafsi alietakasika kabisa MARIAMU hata ALLAH (s.w) katika QUR'AN akamtaja na kuwa mwanamke pekee aliyetajwa katika maandishi hayo matukufu Sio kumtaja tu LaHashaa! ALLAH (s.w) akampa sura yake kabisa Mama wa Yesu (amani za mwenyezimungu ziendelee kuwa naye huko aliko)

Lakini ni kweli bwana YESU alizaliwa 25 disemba???
View attachment 1655857
Ninajua kwamba bwana Yesu Hakuzaliwa mwishoni mwa mwaka,, kama ni hivyo sitakuwa na mashaka nikikuambia ya kwamba ninajua pia bwana yesu alizaliwa katikati ya mwaka wa 6 kuelekea wa 5 B.C.

Thibati hiyo ya Bwana Yesu kuzaliwa Katikati ya mwaka wa 6 kwenda wa 5 BC Pia imetambulika na Biblia ijulikanayo kwa jina la
Life Application Study Bible , katika ukurasa wa A20 .

Lakini hata maelezo yameeleza kwa ufupi kuzaliwa kwa bwana yesu na yanatosha kuonyesha 25 disemba sio sikukuu ya kuzaliwa bwana


Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, kwa msichana mmoja bikira aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu, ewe uliyejaliwa neema na Mungu! Bwana yuko nawe!” Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: Maneno hayo yanamaanisha nini? Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu..... LUKA 1:26-31

Mafundisho hayo yanagongea msumari , kwamba habari za kupokea taarifa za mimba kwa Mariamu kulitokea mwezi wa sita ,na kama ujuavyo mwezi huo kwa jamii za kale nyingi hata zama za sasa ni mwezi wa katikati ya mwaka.....
wasomi wa histori wengi wamejaribu kuonyesha mwezi wa saba napo ndipo Mama mariamu alichukua mimba yake na akazaa kwa utimilifu pasi na kasoro yoyote.... kwa maana mtoto hakuwa na kasoro yoyote ya muda.

ikawa katika kukaa huko siku zake za kuzaa zikatimia ,akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni. LUKA 2: 6-7

Pasi na shaka bwana yesu alizaliwa katika mda timilifu kabisa

Tutake nini tena??? tuombe tujue na tusijue


pia ukirejelea mwanzo na takwimu hizo, hata mwaka wa kwanza A.D bwana Yesu tayari alikuwa na umri wa miaka mitatu na Nusu,, Na hapo pia panakinzana na ile dhana inayosemwa na wengi kuwa Bwana Yesu alipozaliwa ndipo miaka ikaanza kuhesabiwa....(ni vyema ukaingia mtandaoni kupata taarifa kwa uyakinifu zaidi)

POPE JULIUS WA I

Hilo fundisho kuhusu Bwana Yesu kuzaliwa tarehe 25, ya mwezi wa Disemba ni POPE shupavu wa roman aitwae Julius I alitangaza rasmi kuwa tarehe 25 Disemba ndiyo itakuwa siku ya kusheherekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo.......Pia hii ilikuwa siku ambayo wapagani wa walikuwa wakisherehekea kuzaliwa kwa Mungu wao, mungu jua na mwanzo wa majira ya michepuo ya mimea basi JULIUS akaingiza siku hiyo kwa minajili ya mungu wao wapagani wa rumi ili afanyiwe matukuzo na kuwatia katika makufuru wana wa Adamu
View attachment 1655853
Katika majira hayo hayo pia kulikuwa na sikukuu ya wapagani wa Kirumi inajulikana sana kwa jina la “Roman Saturnalia” ambayo pia Waroma walikuwa wanampa heshima mungu wao SATURN, ambaye wao walikuwa wanamwabudu....Mungu huyu ni sayari ya SATANI
Waroma walikuwa wanasherekea sherehe hiyo kila tarehe 19 ya mwezi wa Disemba na ilikuwa inaadhimishwa kwa kufulululiza kwa siku saba hadi tarehe 25 ya mwezi huo wa Disemba ndipo maadhimisho ya siku kuu hiyo yalipohitimishwa.
View attachment 1655860
Pia ilipofika miaka ya elfu na miamoja (1100s )AD Warumi walitangaza kuwa sikukuu (christmass) hii ni ya kidini na wakaweka ulazima pasi na shuruti kwa mataifa yaliyo chini ya makoloni yake kuifata na kutenga fedha kwa ajili ya sikukuu hii....pasi hiari

Kuna kiongozi wa ukatoliki wakati huo mjanja mjanja mmoja bwana nicholas....alifanikiwa kuzishawishi nchi nyingi za ulaya kuipokea sikukuu hii kama ndiyo sikukuu ya kidini na kitaifa ,, umashuhuri wa christmass ukaongezeka na uliendelea kuwa mkubwa miaka ya 1500 AD.

Na hapo ndipo uliponza kujitokeza mgawanyiko mkubwa mno katika ukristo,,jambo lililopelekea kuanzishwa kwa madhehebu mengi ya kikristo ya kiprostentanti, mpaka sasa yanakadiriwa kufikia takribani 3000..

Lakini mgawanyiko huo wa madhehebu ulisaidia sana kufichua mambo mbalimbali na kutoa uhuru wa mafundisho mengi mengi na hapo wakristo wengi walipata mwanya wa kueleza namna na maana ya christmass ni UPAGANI tena ni sherehe ya kutungwa.

Haya mafundisho yalifanya UINGEREZA kuiondoa sikukuu hiyo mwaka 1600 AD, kama sikukuu yake ya kitaifa na kidini hata katika makoloni yake yote.
View attachment 1655866
Hata hivyo tamaduni ya sherehe hizi zilirudi kwa sura ya pili ya kikristo.....ambapo mtindo wa kusherekea wa sasa uliambatana na kupambwa kwa miti ya krismass katika makanisa na kutumina kadi za salam zilizosheheni maandiko ya biblia takatifu na maadhimisho yakazidi kupamba moto kila mwaka hata sasa katika zama zetu za kina SANTA CLAUS
View attachment 1655864

DA'VINCI XV
Samahan Kwa kuchelewa,hv jina halis jamaa alilopewa na Maria Ni lipi Jesus Christ,Yesu,Masia au...........
 
Hata kalenda unayotumia ni kalenda ya Papa. Inaitwa Gregorian Calendar. Ya papa Gregorian

Sasa unaonaje ukaamua kuachana na matumizi ya kila kinachotoka kwa papa ikiwamo kalenda?
wakina papa ndo wa anzilishi wa uchafu wote huu wakuchafua maandiko.watu mpaka Leo.wanajua siku inaisha saa6 usiku.wametu aminisha mungu.ana mtoto.tumekubali ukiwauliza mungu alizaa na nani uyo mtoto.wana kwambia ni mambo ya kiroho zaidi.japo Mimi ni mkristo ila sikubali kwamba mungu ana mtoto.maana nikujitoa akili.mungu.anazaha..
 
Mkuu yesu hajazaliwa mwezi wa 12...Hata muulize padri wako hili kila mtu analijua...mwezi wa 12 ni msimu wa baridi sna lakini Yesu anazaliwa kuna wachungaji walikuwa wanachunga kitu ambacho hakiwezekani msimu huo..Yesu atakuwa alizaliwa kati ya mwezi wa3 - wa 5...
Lakini sikukuu ya tar25 mwezi wa 12 ilikuwepo hata kabla ya yesu kuzaliwa..Waroma waliisherekea hiyo sherehe ya Jua kuzaliwa maana Tarehe za mwisho za december kuelekea January Ndo Jua linarudi ndomaana juu ya mti wa chrismass wanaweka Nyota ikimaanisha Jua linarudi,,,Ndomaana ukiangalia picha za Yesu wa kiroma utaona nyuma ya kichwa chake kuna mwanga kama Jua hivi...likiashiria Mungu Jua...Hence Sunday mambo ni mengi mkuu
Hoja yako ni nini sasa? nimeandika kwamba kuhusu tarehe mwezi yawezekana ukawa sahihi lakini ulichokielewa kwenye Biblia ilikuwa ndiyo hoja yangu.
 
wakina papa ndo wa anzilishi wa uchafu wote huu wakuchafua maandiko.watu mpaka Leo.wanajua siku inaisha saa6 usiku.wametu aminisha mungu.ana mtoto.tumekubali ukiwauliza mungu alizaa na nani uyo mtoto.wana kwambia ni mambo ya kiroho zaidi.japo Mimi ni mkristo ila sikubali kwamba mungu ana mtoto.maana nikujitoa akili.mungu.anazaha..
Kweli kabisa haiwezekani akazaha
 
Back
Top Bottom