Chuki makazini huletwa na nini?

Chuki makazini huletwa na nini?

Habari wote…nimebananika kidogo nipatapo muda napitia comments zetu…yawezekana nisipate muda wa kureply lakini ninazisoma na tunazifanyia kazi.

Kwa yeyote aliyecomment, natanguliza Shukrani za dhati🙏.
 
Kuna mwamba kasema hapo juu kuwa ni mtu kuwa na uwezo mdogo wa utendaji kwa hyo anajikomba kwa boss kwa kupeleka taarifa za uzandiki ili akubaliwe na boss...huyu nakubaliana nae kwa 100%...na kuprove hilo...kila msaidiz wa boss akibadilishwa...lazma aanze kuweka mazingira ya kuwa nae karibu ili amrushie taulo pale anapoboronga...hii ipo sanaa kweny private institutions
 
Habari ya wakati huu ni matumaini yangu nyote mpo salama.

Moja kwa moja niende kwenye mada husika.

Najua binadamu tuko tofauti lakini ningependa kupata comments tofauti tofauti kujua nini hasa hupelekea. Chuki, visasi, roho za kutendeana ubaya, malipizi, na mengineyo yasiyopendeza huletwa na nini?

Je, ni kwakuwa hujui na unaonekana mzigo?

Je, unajua zaidi yao na unaonekana kama tishio?

Au ni basi tu mtu anaamua kukuchukia bila sababu ya msingi na kukuombea kila uchwao ukumbwe na baya?

Ninakaribisha maoni.

Shimba ya Buyenze , Mshana Jr Watu8 , Omerta, @Da’Vinc , na wapendwa wengine karibuni.


Mwenye CHUKI hana sababu.

Kukwaruzana kipo lakini kuchukiana ni Kwa watu wenye roho Mbaya
 
Kama ilivyo UPENDO usivyo na Sababu Maalumu ndivyo ilivyo Kwa CHUKI haina sababu maalum.

Mwenye chuki rohoni atakuchukia hata kama hujamfanyia chochote.
Mwenye Upendo atakupenda bila sababu yoyote yaani mpaka unashangaa.

Asije akakuambia mtu kuwa mtu Fulani anakuchukia Kwa sababu Fulani, Big No.
Kuna tofauti ya Kuchukia na kukasirika,
Kuna tofauti ya Kutamani na Kupenda.

Hasira huchochea Chuki
Na Wakati mwingine Tamaa huchochea Upendo
 
Jambo la kwanza, roho mbaya mtu huzaliwa nayo, na huwa inasubiri majira, nyakati na mazingira sahihi ili iweze kuanza kufanya kazi...

Binafsi katika kumtumikia kote mkoloni sijawahi kukutana na watu wa namna hiyo, isipokuwa nimekuwa nikipata kusikia visa hivyo toka kwa watu wa karibu...

Sababu ambazo nimekuwa nikizisikia huwa ni tofauti tofauti, lakini zote ni matokeo ya mtu kuwa na roho mbaya 'roho nyeusi'...

1. Ubinafsi - Hawa ni wale watu wenye umimi, kwamba kila kizuri kiwe chao na vibaya viwe vya wengine

2. Ufukara - Kuna watu ambao maisha yao yamegubikwa na ufukara wa mali, hivyo hujawa na chuki pale wanapoona mtu fulani yupo kwenye nafasi ya kupokea mkate mnono zaidi yao, au hata maisha yake nyumbani ni ya juu kuwazidi katika mali alizonazo

3. Kukosa weledi - Kuna watu waliopata vyeo au nafasi kwa ngekewa tu na wala sio kwa uwezo wa kiakili au taaluma, sasa kule kutokujiamini kwamba mtu anaweza akapokwa nafasi yake hufanya ajenge chuki kama njia ya kujilinda

4. Ukabila - Kuna maofisi ambayo watu wa kabila fulani ni kama wamechanjiwa kuwa wao ni wa ofisi hiyo tu, ikitokea wewe mwenyeji wa mkoa mwingine umeajiriwa au kupangiwa hapo, cha moto utakuona

5. Tofauti za kimaumbile/hulka/ulimbwende na utanashati - Imezoeleka kusikika kuwa watu wafupi huwa wakorofi sana, dhana hii ipo pia makazini ambapo kuna watu hukosa kujiamini kutokana maumbile yao, hujiona sii warembo au watanashati au hujiona wana kasoro fulani za kimaumbile ambazo zinawafanya wamuone mtu fulani kawazidi

6. Tofauti za kiimani - Kama ilivyo tofauti za kimaumbile, hata imani nayo huwa ni chanzo cha chuki baina ya mtu na mtu. Kuna ofisi ambazo imani fulani ya dini ina nguvu kuliko nyinginezo.
Pia kuna watu ambao huwa ni washirikina, hupelekea kuwachukia wale walio wacha Mungu.

7. Kuwa sehemu isiyo sahihi wakati usio sahihi - Isijekuwa pia upo mahali pasipo sahihi kwako iwe ni idara, ofisi au kitengo kiasi kwamba unazuia 'deals' za watu kufanikiwa, mathalani umezungukwa na wapigaji wakati wewe si mpigaji n.k

8. Mwisho, muhimu zaidi jichunguze wewe mwenyewe huenda una tabia isiyoridhisha inayosababisha watu kuwa na chuki nawe. Huenda chanzo ni wewe mwenyewe na si wengine.

Pitia huu uzi, utakusaidia kama umekumbwa na kadhia hii kwa sasa...
Thread 'Saikolojia: Kushindana na wanaobeba Chuki' Saikolojia: Kushindana na wanaobeba Chuki
Umemaliza kila kitu hapa...
 
Sababu ni zile zile tu Mwanadamu asiyempenda Mungu wala jiran yake..

Wagalatia 5:19-21
....uasherati, uchafu, ufisadi,
[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
 
Jamii zetu hasa sisi watanzania tunakuwa na chuki kazini sababu ya mambo yafuatayo

Wivu _hii uja endapo mnapokea mshahara sawa ila wanahisi kuna jambo unawazidi ambalo sio tu wanaweza litimiza kirahisi ila ni mpaka waingie mikopo .

Husuda _ hii huja baada ya wivu ni pale sasa wafanyakazi wenzio wanapoona hawakuwezi tena sasa ni husda tu ili wakufelishe

Background zetu _ ukikutana na wafanyakazi wenzio ambao wengi wametokea familia za kimasikini aisee ndugu tegemea kila rangi ya ajabu hapo kazini , hasa ukiwazidi baadhi ya vitu au wakigundua uko na background nzuri dhidi yao , watajipendekeza kwako ila ni unafiki sana maana wanakuchora.

Hivyo dawa ni kuwa wewe kama Wewe timiza majukumu yako , nenda kaendelee maisha na familia yako

TEKERI.
 
Habari ya wakati huu ni matumaini yangu nyote mpo salama.

Moja kwa moja niende kwenye mada husika.

Najua binadamu tuko tofauti lakini ningependa kupata comments tofauti tofauti kujua nini hasa hupelekea. Chuki, visasi, roho za kutendeana ubaya, malipizi, na mengineyo yasiyopendeza huletwa na nini?

Je, ni kwakuwa hujui na unaonekana mzigo?

Je, unajua zaidi yao na unaonekana kama tishio?

Au ni basi tu mtu anaamua kukuchukia bila sababu ya msingi na kukuombea kila uchwao ukumbwe na baya?

Ninakaribisha maoni.

Shimba ya Buyenze , Mshana Jr Watu8 , Omerta, @Da’Vinc , na wapendwa wengine karibuni.
Makazini kuna mitandao ya ukwapuaji pesa, sasa ukijifanya hutaki au ikiletwa mtumishi mpya wanajua unakuja kukanyaga dili zao za ulaji lazima ule wa chuya
 
Jambo la kwanza, roho mbaya mtu huzaliwa nayo, na huwa inasubiri majira, nyakati na mazingira sahihi ili iweze kuanza kufanya kazi...

Binafsi katika kumtumikia kote mkoloni sijawahi kukutana na watu wa namna hiyo, isipokuwa nimekuwa nikipata kusikia visa hivyo toka kwa watu wa karibu...

Sababu ambazo nimekuwa nikizisikia huwa ni tofauti tofauti, lakini zote ni matokeo ya mtu kuwa na roho mbaya 'roho nyeusi'...

1. Ubinafsi - Hawa ni wale watu wenye umimi, kwamba kila kizuri kiwe chao na vibaya viwe vya wengine

2. Ufukara - Kuna watu ambao maisha yao yamegubikwa na ufukara wa mali, hivyo hujawa na chuki pale wanapoona mtu fulani yupo kwenye nafasi ya kupokea mkate mnono zaidi yao, au hata maisha yake nyumbani ni ya juu kuwazidi katika mali alizonazo

3. Kukosa weledi - Kuna watu waliopata vyeo au nafasi kwa ngekewa tu na wala sio kwa uwezo wa kiakili au taaluma, sasa kule kutokujiamini kwamba mtu anaweza akapokwa nafasi yake hufanya ajenge chuki kama njia ya kujilinda

4. Ukabila - Kuna maofisi ambayo watu wa kabila fulani ni kama wamechanjiwa kuwa wao ni wa ofisi hiyo tu, ikitokea wewe mwenyeji wa mkoa mwingine umeajiriwa au kupangiwa hapo, cha moto utakuona

5. Tofauti za kimaumbile/hulka/ulimbwende na utanashati - Imezoeleka kusikika kuwa watu wafupi huwa wakorofi sana, dhana hii ipo pia makazini ambapo kuna watu hukosa kujiamini kutokana maumbile yao, hujiona sii warembo au watanashati au hujiona wana kasoro fulani za kimaumbile ambazo zinawafanya wamuone mtu fulani kawazidi

6. Tofauti za kiimani - Kama ilivyo tofauti za kimaumbile, hata imani nayo huwa ni chanzo cha chuki baina ya mtu na mtu. Kuna ofisi ambazo imani fulani ya dini ina nguvu kuliko nyinginezo.
Pia kuna watu ambao huwa ni washirikina, hupelekea kuwachukia wale walio wacha Mungu.

7. Kuwa sehemu isiyo sahihi wakati usio sahihi - Isijekuwa pia upo mahali pasipo sahihi kwako iwe ni idara, ofisi au kitengo kiasi kwamba unazuia 'deals' za watu kufanikiwa, mathalani umezungukwa na wapigaji wakati wewe si mpigaji n.k

8. Mwisho, muhimu zaidi jichunguze wewe mwenyewe huenda una tabia isiyoridhisha inayosababisha watu kuwa na chuki nawe. Huenda chanzo ni wewe mwenyewe na si wengine.

Pitia huu uzi, utakusaidia kama umekumbwa na kadhia hii kwa sasa...
Thread 'Saikolojia: Kushindana na wanaobeba Chuki' Saikolojia: Kushindana na wanaobeba Chuki
Naunga mkono hoja.
Nini kifanyike
1. Penda kutulia ofisini kwako usiwe mtu wa kushinda kwenye makorido/ofisi za watu
2. Tumia masaa yako 9 vizuri ili umalize au ufanye kwa ukubwa kazi yako
3. Masaa ya kazi yakiisha beba kilicho chako nenda nyumbani au kwenye mishe zako
3. Usipende kucheka cheka, tumia system ya kijerumani/kirusi. Unacheka ukiwa na sababu
4. Kama umebarikiwa kuwa na kalamu ya endorsement, fanya bila upendeleo
5. Usipende kufanyia kazi majungu yanayoletwa na X kutoka kwa Y, kuna muda pokea yapitie upande wa pili au kusanya XY uwaambie nk
6. Usiwe mwoga kwenye kufanya maamuzi na usipende kuwa chawa kwa aliye juu yako.
7. Usipende kushea mambo yako ya nyumbani ofisini.
NB: Sehemu kubwa ya hayo juu ukiyafanya si rahisi mtu kukuelewa nini kilichoko kichwani kwako na si rahisi kukuletea mazoea ya kijinga. Ni vigumu kumridhisha kila mtu, pia hata ufanye nini wanadamu hawataacha kufanya yao. Kikubwa zingatia weledi wako wa kazi
 
Habari ya wakati huu ni matumaini yangu nyote mpo salama.

Moja kwa moja niende kwenye mada husika.

Najua binadamu tuko tofauti lakini ningependa kupata comments tofauti tofauti kujua nini hasa hupelekea. Chuki, visasi, roho za kutendeana ubaya, malipizi, na mengineyo yasiyopendeza huletwa na nini?

Je, ni kwakuwa hujui na unaonekana mzigo?

Je, unajua zaidi yao na unaonekana kama tishio?

Au ni basi tu mtu anaamua kukuchukia bila sababu ya msingi na kukuombea kila uchwao ukumbwe na baya?

Ninakaribisha maoni.

Shimba ya Buyenze , Mshana Jr Watu8 , Omerta, @Da’Vinc , na wapendwa wengine karibuni.
Ni wivu tu
Hasahasa ukiwazidi kwa jambo flani
 
Roho mbaya na hapo ukute umemzidi kitu ndiyo usiseme
 
Makazini kuna mitandao ya ukwapuaji pesa, sasa ukijifanya hutaki au ikiletwa mtumishi mpya wanajua unakuja kukanyaga dili zao za ulaji lazima ule wa chuya
Wewe ndio umesema kiini cha tatizo kuu lilipo, mtu hawezi kukuchukia hivi hivi tu, eti ni hulka, umaskini, udini, au kutojiamini, hayo yote ni sawa kwa kiwango kidogo cha tabia za wasiojua kuishi bila ubaguzi.

Ila

MASLAHI (PESA, Wealthy) NDIYO YALIYOKUPELEKA KAZINI WALA SIO (NAFASI) KAZI YENYEWE.

Mkono mtupu haulambwi

Kimtishacho Mfanyabiashara ni Mshindani wake na Mamlaka za Kodi tu.

Na kwa nini nchi na nchi huchukiana kiasi cha kupigana.





Sent from my TA-1004 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom