Chuki tu: Kawambwa sio tatizo

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Ni makosa na haikubaliki kufanyia utafiti jambo ambalo sababu/majibu yake tayari yapo na yanafahamika kwa watu. Mfano huhitaji kufanya utafiti wa kugundua kwanini unasinsia mchana darasani ili hali unajua kwamba jana ulikesha kwenye sherehe. Inajulikana tayari kuwa usipolala usiku utasinsia/lala mchana na usipolala mchana utasinsia/lala usiku. Sasa kama huo ndo ukweli kuhusu usingizi itashangaza kuona mtu ambaye hakulala usiku lakini pia hasinsii mchana, ama kalala usiku lakini anasinsia tena mchana, hii sasa ndio inayohitaji utafiti maana maana sio kawaida na tabia ya usingizi, tunahitaji kufahamu zaidi kama huyu mtu anakula milungi ndo maana halali, anatumia kinywaji gani, anaumwa, ana msongo wa mawazo, n.k.

Je, kwa mfano huo hapo juu swala la wanafunzi wa kidato cha nne kufeli measurably linahitaji utafiti ama kuundiwa tume gani? Kipi hakifahamiki kinachohitaji utafiti? Waziri mwenye dhamana ya elimu hakufanya nini kuzuia wanafunzi wasifeli mitihani yao?

Ili learning itokee (take place) ni baada ya muunganiko wa mambo/factors mbali mbali yakiwemo:

1.Mwanafunzi mwenyewe: (akili, juhudi, tabia)

2. Walimu: (elimu, juhudi, uzoefu, motisha, tabia)

3. Wazazi: (mahitaji, matibabu, kufuatilia elimu ya mtoto, mazingira bora yanayowezesha kusoma, ada, kufundisha tabia

4. Serikali: (majengo, idadi ya walimu, idadi ya wanafunzi kwa darasa, mishahara ya walimu, vitabu, maabara, usafiri wa wanafunzi na walimu, ukaguzi, elimu za walimu, mitaala, chakula shuleni)

5.Baraza la Mitihani: (alama za wanafunzi kujiunga form I, usimamizi, utungaji na usahihishaji wa mitihani)

6. Jamii: (tabia za wanajamii dhidi ya wanafunzi, vilabu vya pombe kwenye makazi, ngoma na miziki kwenye makazi, usafiri wa daladala, vibanda vya video, ubakaji)

7. Utandawazi: (matumizi ya simu, internet, magazeti na majarida kwa wanafunzi)


Je, vitu hivi havipo Tanzania? Kama mambo sio shwari katika kila kipengele hapo juu hatuhitaji kufanya utafiti tena, ila ni swala la ki-management lisilohitaji utafiti (research) maana sababu za kufeli zinajulikana tayari ni kuchukua hatua tu za kiutendaji.



Je, katika mambo hayo saba niliyoyataja hapo juu Kawambwa kama Kawambwa kahusika na lipi linalomuhitaji yeye ajiuzuru kama Waziri? Hili ni swala la mfumo mzima kuanzia chama tawala, serikali, wananchi, na dunia kwa ujumla, hata ulaya na Marekani wanalalamikia matokeo mabaya kwa watoto wao, na sababu ni hizihizi.


Ukiaangalia shule zilizofanya vizuri kwenye matokeo haya utagundua kuwa walikuwa na wanafunzi bora waliojiunga form 1, wana vitendea kazi, wana wazazi wenye upeo, wana walimu wanaolipwa vizuri, n.k.



Swali la kufeli kwa wanafunzi haliwezi likaachwa juu ya mabega ya Mh. Kawambwa. Anayedai kawambwa ajiuzuri anaropoka na kupayukatu. Kwa hali ilivyo hata ukimtoa Kawambwa peke yake leo hali itabakia ileile. overhaul??!!!


 
Hoja yako ina ukweli lakini kwa matokeo haya serikali ndiyo iliyochangia kwa kiasi kikubwa kwa kuwa na migogoro ya kimaslahi na walimu lakini mbaya zaidi ikatumia mahakama kuwazima bila kutafuta suluhu nao. Lakini hata mambo mengine uliyoyataja serikali ikitengeneza sera nzuri kuhakikisha mtoto anapata elimu nzuri hata kama mtoto hana uwezo hawawezi kufeli kwa kiwango hiki. Wizara ya Elimu ndiyo inayohusika na uandaaji wa sera ya uboreshaji wa elimu na maslahi ya walimu, tunasikiliza bunge la bajeti mara nyingi umemsikia Waziri akiiomba bunge kuboresha maeneo hayo na Wabunge wakamkatalia? Zaidi utamsikia akitetea chai, posho na matumizi ya kawaida hata kiasi cha kutoa machozi. Hivi tatizo katika wizara yako mpaka aone Mbunge? Waziri upo tu.
 
Hivi unataka kutuambia hili la kufeli ni la bahati mbaya?
Serikali,Kawambwa na naibu wake,Ndalichako wote ni wa kufukuzia mbali!
Hawana ubunifu wa matatizo yaliyopo na hawana uelewa wa changamoto za dunia ya sasa.
Kimsingi wanaandaa taifa legelege la mbumbu watupu!!!

Hebu fikiria kidogo tu,Kawambwa miaka michache iliyopita alikuwa akitoa ripoti ya elimu huko Bagamoyo mbele ya Raisi
akasema wamejenga matundu manne(4) ya choo kwa shilingi milioni 728,000,000/= kutoka ktk fedha za halmashauri,akapigiwa makofi,halafu unasema nini wewe!!?
 
tattizo ni wewe na wenzio wasiofikiri kabla ya kijianika jamvini walivyo vilaza wa mawazo na maamuzi.
 
NI ajabu kushangaa wanafunzi wa kidato cha 4 kushindwa mitihani wakati waliingia kidato cha 1 hawajui kusoma wa kuandika. Ina maana miaka 7 awakuambulia kitu, je miaka 4 ingetosha kuwafanya wafaulu?
 
tattizo ni wewe na wenzio wasiofikiri kabla ya kijianika jamvini walivyo vilaza wa mawazo na maamuzi.
Tatizo hutaki kujishughulisha kufikiri mtoa mada ameeleza point za msingi sana, tatizo unataka wapitishwe kama darasa la 7 na form 2 wakiwemo wasiojua kusoma na kuandika
 
tatizo hutaki kujishughulisha kufikiri mtoa mada ameeleza point za msingi sana, tatizo unataka wapitishwe kama darasa la 7 na form 2 wakiwemo wasiojua kusoma na kuandika
ivi wewe mwehu wakati unasoma wasiojua kusoma na kuandika hawakuwepo au hawakufaulu?unadhani ni kwanini kuna wazira inayosimamia haya mambo?kama wizara haiwajibiki unategemea hao wanafunzi na walimu kuwajibika???funga bakuli lako maana huwezi hata kufikiri kabla hujasema neno.
 
Umenena kama GT!Hata mimi siamini ni Kawambwa pekee ndiye ajiuzulu bali ni kuondoa mfumo mzima wa uongozi kwani umeshindwa ku adress pamoja na mambo mengine, changamoto tunazopata kwenye elimu.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Ndio maana watoto wanaandika matusi kwenye paper na kuandika mapenzi kumbe kuna walezi wa aina hiii
 
ndio maana watoto wanaandika matusi kwenye paper na kuandika mapenzi kumbe kuna walezi wa aina hiii
wewe mwehu kwa mwanangu haiwezi kutokea nahangaika kwa ajili yao so najitahid nilipe izo ada kubwa kewnye izo shule za mafisad maana i have no choice.lakini ufikilie kuna wazazi wangapi wasiojua kusoma na kuandika na waliwekeza nguvu zao zote kwa hawa watoto walifail sababu ya serikali dhaifu wakitegemea watoto wao wawasaidie in the future.ukiongea uwajibikaji wa wazazi usijiangalie wewe na jirani yako ambao mmejikuta mpo mjini na mlifanikiwa kusoma.kilaza
 
Hapo ndio tunapotofautiana mimi na wewe mtu ashindwe kujua kusoma na kuandiaka kwa miaka 7 ya shule ya msingi then unasema mzazi anawekeza ili mtoto afaulu form 4 kweli jamani kuna miujiza gani itayofanyika hapa ajue kusoma na kuandika then afaulu within 4 yrs na hapo mzazi anategemea mtoto afaulu, na ndio maana mtoa mada aliainsha mambo ya msingi sana na wala hajatetea serikali kuwa haiwajibiki ila ameeleza wajibu wa kila mtu kwenye ufaulu wa mtoto sasa sijaua wewe unalenga kitu gani
 

Tumia lugha nzuri utaeleweka tu mama.
 
mamajack usiwe mshabiki wa matukio, jaribu kutumia akili yako kupambanua mambo. Hivi kwa akili yako wewe Kawambwa ndo kasababisha matokeo ya vijana wetu yawe mabaya? kati ya mambo saba niliyoyataja ya kufanikisha kusoma tutampaje kawambwa yote? wanafunzi, walimu, wazazi, serikali, baraza, jamii na utandawazi kila mtu achukue kipande chake akifanyie kazi kwa wakati wake. Kawambwa anahusika na kipengele kimoja tu cha serikali, hata hivyo Kawambwa sio rais, na wala sio yeye aliyekataa kuwalipa walimu mishahara minono. Lakini hata kama walimu watalipwa mishahara minono bila ya kushughulikia yale mengine bado tutabaki palepale
 
ndo maana nakwambia wewe na wenzia akili zenu ndogo ka piliton,inakuwa asiyejua kusoma na kuandika akafaul la saba na tumewapa mamlaka ya kusimamia elimu,pesa tunawapa kwenye bajeti mazoomba and then leo unaniambia mtu hajui kusoma wala kuandika then anapas la saba.wazazi wa huko vijijini hawajui mamboa yenu ya elimu na wakati mwingine mnawakamata wasipowapeleka hao watoto sec skul.wewe na huyo waziri mnaupeo sawa wa kufikiri.after all huyo kawambwa mwenyewe hana historia ya kusimamia wizara ikafanya vizuri kwa hiyo wewe na yeye hamuwezi kuona tatizo lenu liko wapi.
 
Wazi kama Mamajack hawakosi mtoto ama ndugu atakaeandika matusi kwenye mitihani, kama mzazi una lugha ya matusi hata mtoto ni rahisi kuiga. mtoto wa mbwa ni mbwa pia
 

mkuu invisible tunaomba kitufe cha dislike tafadhali, na ziwe zanaonekana chini ya post ya mhusika. Utatupunguzia sana ban
 
Haya bwana sio lazima wote tuwe na fikra au mitazamo inayolingana kwa heri
 
Unaweza ukaona wenzio wehu kumbe weye ndi mwehu kabisa kama mwanao anasoma st fisadi utajuaje matatizo ya wa2 wengine ww
 
Hili jambo ni vema likaangaliwa kwa mapana yake badala ya kunyoosheana vidole
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…