Sahihi kabisa brother nilikomenti nimefuta baada ya kuona comment yakoKwa mtihani wa form six haiwezekani
Always BAM hufanyika pamoja na Pure Math's kwa sababu hakuna anayesoma hayo masomo kwa pamoja
Hivo kila mwaka ratiba yake huwekwa kufanyika mda mmoja
Hahahaha na wewe uende wasafi au EFm ukataje na chuo ulichofanyiwa na ukamtaje aliyekufanyia!Na mimi nikiri....nishafanyiwa sana pepa na wanangu wakati nikiwa zangu site mikoani naendelea na harakati za kusaka tonge....nikirudi wana nao wananeemeka , usiulize iliwezekana vipi...
Ni warembo lakini akili hawana maana walicho ongea kinaweza waharibia maishaNi warembo lkn hawana hekima wala busara, maana hekima ni kuliweka kila jambo mahala pake,,,sasa kama hawajui walichofanya ni kosa na kama haitoshi wanajisikia sifa kuongea hadharani,basi ni wapuuzi Sana
Ila huo ni ujasiri wa hali ya juuMzumbe pia morogoro kulikuwa na mapacha wa kike wanafanyiana mtihani
Mmoja kichwa anajua hesabu sana anasoma kozi ya BAF mwingine kilaza hajui hesabu anasoma kozi ya marketing
Hivyo yule kichwa akawa anambeba pacha wake maana walikuwa kozi tofauti pepa zinapishana ratiba. Mpaka UE anamfanyia.
Siku ya pepa za hesabu, accounts, na economics pacha kilaza alikuwa anafanyiwa na pacha kichwa.
Inasemekana mpaka necta form 6 alimfanyia pacha wake pepa ya Basic applied Mathematics maana pacha kichwa yeye alikuwa hafanyi BAM yeye alikuwa anafanya pepa ya Pure Mathematics ambayo ilikuwa siku tofauti.
Hao mapacha Wanafanana kweli kweli bila kuwazoea sana huwezi watofautisha
AKija na ID ya mwenzake utamjuaje sio yeye?Hadi registration number?
Kama siti mtemvu, wema sepetu walifoji hadi vyeti na wakakiri ili washiriki miss tz na hakuna aliyewahi kuwasumbua, wewe wadhani hawa nani atawasumbua.Tumekuwa tukisikia hapa Duniani hasa Tanzania kuwa huwa kuna degree za bure na wengine wamekuwa wakisema kuna degree za chupi!
Lakini sijawai kusikia au kuona watuhumiwa wakikiri kufanya uhalifu kabisa hadharani!
Chuo cha Ardhi ni chuo kizuri lakini ikifika hatua ya watu kisa tuu mapacha wanaweza kufanyiana mitihani na wana kiri hadharani kuwa walifanyiana mitihani tena ya supplimentary basi ujue hii ni hatua kubwa na dharau kubwa sana kwa taasisi hasa ya Elimu ya juu na inayo aminika!
Hawa mabinti wanasema waliweza kufanyiana mitihani na hakuna aliyegundua na sasa wanakwenda hadharani kusema kuwa waliweza kufanya hivyo ni wazi dharau sana kwa taasisi hii ya Elimu na inathibitisha kuwa taasisi hii haiko makini na kuna walakini kwenye hutoaji wa Elimu!
Watu wana hangaika sana kupata elimu halafu watu wanaidhalilisha elimu kiasi hiki …hii ni aibu kwa chuo cha Ardhi na Wizara ya Elimu pia!
Watu wengi wamekuwa wakitilia mashaka sana Elimu zetu hasa utoaji wake na sasa ni wazi wahalifu wameanza kutoa ushahidi wa mashaka kwenye hizi degree zilizojaa mtaani!
Ni matuamaini yangu taasisi itachukua hatua kali dhidi ya uhalifu huu wa kielemu uliofanywa na hawa mapacha na kwenda kukiri hadharani kwenye chombo cha habari Wasafi FM!
Source: Wasafi FM
View attachment 2926553
Yani hapo walipo muda huu najua wanajuta kufanya interview😂😂😂😂😂Binadamu huwa tunapaswa tujue mipaka yetu ya kuzungumza kuzingatia hadhira tunayozungumza nayo.
Katika jaribio lao la kunogesha upacha wao wameishia kuhatarisha qualifications zao. Ukute ni uongo hawajawahi hata kufanyiana hiyo mitihani ila walitakana kuongeza vionjo tu kusahau kuwa wanasikika nchi nzima.
Umenena vema. Vyuo ni extended high schoolKuna elimu hapa bongo au tunakaririshwa tu
Watasema waliongea hivyo kutafuta umaarufu 'kutrend'. Kusema tu haitoshi chuo lazima kithibitishe kuwa walifanyiana mitihani kitu ambacho ni ngumu na kitaaibisha chuo.Muda mwingine mdomo huponza kichwa.Hawa wakiitwa chuoni kuelezea hayo maelezo watajiteteaje?