Chuo cha Ardhi kinapaswa kuchukua hatua dhidi ya mabinti mapacha waliokiri kufanyiana mitihani

Chuo cha Ardhi kinapaswa kuchukua hatua dhidi ya mabinti mapacha waliokiri kufanyiana mitihani

Na mimi nikiri....nishafanyiwa sana pepa na wanangu wakati nikiwa zangu site mikoani naendelea na harakati za kusaka tonge....nikirudi wana nao wananeemeka , usiulize iliwezekana vipi...
 
Na mimi nikiri....nishafanyiwa sana pepa na wanangu wakati nikiwa zangu site mikoani naendelea na harakati za kusaka tonge....nikirudi wana nao wananeemeka , usiulize iliwezekana vipi...
Hahahaha na wewe uende wasafi au EFm ukataje na chuo ulichofanyiwa na ukamtaje aliyekufanyia!
 
Mzumbe pia morogoro kulikuwa na mapacha wa kike wanafanyiana mtihani

Mmoja kichwa anajua hesabu sana anasoma kozi ya BAF mwingine kilaza hajui hesabu anasoma kozi ya marketing

Hivyo yule kichwa akawa anambeba pacha wake maana walikuwa kozi tofauti pepa zinapishana ratiba. Mpaka UE anamfanyia.

Siku ya pepa za hesabu, accounts, na economics pacha kilaza alikuwa anafanyiwa na pacha kichwa.

Inasemekana mpaka necta form 6 alimfanyia pacha wake pepa ya Basic applied Mathematics maana pacha kichwa yeye alikuwa hafanyi BAM yeye alikuwa anafanya pepa ya Pure Mathematics ambayo ilikuwa siku tofauti.
Hao mapacha Wanafanana kweli kweli bila kuwazoea sana huwezi watofautisha
Ila huo ni ujasiri wa hali ya juu
 
Wajinga hao, elimu yao haijawasaidia, wameshindwa kujua ubaya wa kuongea hivyo hadharani, wenyewe wanatamka kama sifa lakini si jambo jema kwao. Labda wakaushiwe ila wakiamuliwa imekula kwako.
 
Tumekuwa tukisikia hapa Duniani hasa Tanzania kuwa huwa kuna degree za bure na wengine wamekuwa wakisema kuna degree za chupi!

Lakini sijawai kusikia au kuona watuhumiwa wakikiri kufanya uhalifu kabisa hadharani!

Chuo cha Ardhi ni chuo kizuri lakini ikifika hatua ya watu kisa tuu mapacha wanaweza kufanyiana mitihani na wana kiri hadharani kuwa walifanyiana mitihani tena ya supplimentary basi ujue hii ni hatua kubwa na dharau kubwa sana kwa taasisi hasa ya Elimu ya juu na inayo aminika!

Hawa mabinti wanasema waliweza kufanyiana mitihani na hakuna aliyegundua na sasa wanakwenda hadharani kusema kuwa waliweza kufanya hivyo ni wazi dharau sana kwa taasisi hii ya Elimu na inathibitisha kuwa taasisi hii haiko makini na kuna walakini kwenye hutoaji wa Elimu!

Watu wana hangaika sana kupata elimu halafu watu wanaidhalilisha elimu kiasi hiki …hii ni aibu kwa chuo cha Ardhi na Wizara ya Elimu pia!

Watu wengi wamekuwa wakitilia mashaka sana Elimu zetu hasa utoaji wake na sasa ni wazi wahalifu wameanza kutoa ushahidi wa mashaka kwenye hizi degree zilizojaa mtaani!

Ni matuamaini yangu taasisi itachukua hatua kali dhidi ya uhalifu huu wa kielemu uliofanywa na hawa mapacha na kwenda kukiri hadharani kwenye chombo cha habari Wasafi FM!

Source: Wasafi FM

View attachment 2926553
Kama siti mtemvu, wema sepetu walifoji hadi vyeti na wakakiri ili washiriki miss tz na hakuna aliyewahi kuwasumbua, wewe wadhani hawa nani atawasumbua.
 
Binadamu huwa tunapaswa tujue mipaka yetu ya kuzungumza kuzingatia hadhira tunayozungumza nayo.

Katika jaribio lao la kunogesha upacha wao wameishia kuhatarisha qualifications zao. Ukute ni uongo hawajawahi hata kufanyiana hiyo mitihani ila walitakana kuongeza vionjo tu kusahau kuwa wanasikika nchi nzima.
 
Binadamu huwa tunapaswa tujue mipaka yetu ya kuzungumza kuzingatia hadhira tunayozungumza nayo.

Katika jaribio lao la kunogesha upacha wao wameishia kuhatarisha qualifications zao. Ukute ni uongo hawajawahi hata kufanyiana hiyo mitihani ila walitakana kuongeza vionjo tu kusahau kuwa wanasikika nchi nzima.
Yani hapo walipo muda huu najua wanajuta kufanya interview😂😂😂😂😂
 
Muda mwingine mdomo huponza kichwa.Hawa wakiitwa chuoni kuelezea hayo maelezo watajiteteaje?
Watasema waliongea hivyo kutafuta umaarufu 'kutrend'. Kusema tu haitoshi chuo lazima kithibitishe kuwa walifanyiana mitihani kitu ambacho ni ngumu na kitaaibisha chuo.
 
Back
Top Bottom