Chuo Kikuu cha Biashara (CBE) chamtunuku David Kafulila ngao ya heshima kwa kusimamia ukuzwaji wa sera za Uchumi Jumuishi nchini

Chuo Kikuu cha Biashara (CBE) chamtunuku David Kafulila ngao ya heshima kwa kusimamia ukuzwaji wa sera za Uchumi Jumuishi nchini

View attachment 3101816
===
Chuo Cha Usimamizi wa Fedha na Biashara Cha CBE nchi Tanzania kimemtunuku Mhe David Zacharia Kafulila ngao ya heshima kwa uchapakazi wake uliotukuka kwa Taifa lake.

Mkuu wa chuo hicho Prof. Eddnah Luoga asema chuo chake kimeamua kumtunuku ngao hiyo ya heshima katika kutambua juhudi zake kwenye kumpata mbia mwekezaji toka sekta binafsi atakayejenga mabweni katika chuo hicho yatakatokuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi elfu 12 kwa mara moja.

Mwekezaji huyo atawekeza kwa sharti la Ubia ili kukabiliana na changamoto za wanafunzi kuishi mbali na eneo la chuo hicho jambo ambalo hupunguza zaidi ari, ufaulu na nguvu za kimasomo kwa wanafunzi.

David Zacharia Kafulila Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi Tanzania PPPC amekuwa akisisitiza wakati wote kuwa lazima Tanzània ifike wakati ambao Serikali yetu itapunguziwa mzigo katika kutekeleza miradi yake ya maendeleo hasa ile yenye sura ya kibiashara.

Mkurugenzi huyo anasema kwa kufanya hivyo kutaipunguzia Serikali mzigo na kuifanya itekeleze baadhi ya miradi yake ya maendeleo nje ya bajeti yake hasa ile yenye sura ya kibiashara ( projects contraction outside the government balance sheet )
===

View attachment 3104529
Safi
 
Vyuo huwa vinatoa digrii za heshima hayo ya ngao Chuo kutoa ndio nayasikia leo

Ngao mara nyingi hutolewa na machifu kwa mhusika

CBE wameanza kutoa ngao kama chuo?
Ipo siku kitatoa kombe la mbuzi
 
Zile Blocks E, F na G unazifahamu vema?

CBE ASA club je?

Elimu Kiganjani Mabweni ni mambo ya Ujima ya akina Mabibo 😂😂😂
Mabweni yanajengwa wapi, Mwanza, Dodoma au Dar kote huko kuna CBE
 
Kafulila asisitize Serikali iuze Shirika la ndege (ATCL), asisitize wawekezaji binafsi katika umeme kuondoa monopoly ya TANESCO
ChoiceVariable
TANESCO kutafutiwa washindani wengine nakubaliana na wewe, ATCL kubinafsishwa haiwezekani.

Kila taifa duniani linakuwa national carrier yake binafsi, shirika la ndege lenye kumilikiwa na taifa.
 
Vikiitwa vya jalalani wanahamaki, unatoaje tuzo kwa proposal? Mradi ukiyeyuka kama kawaida ya wabongo unarudi kumnyan'ganya?
 
Kwa nini Serikali iuze ATCL? Hao wawekezaji Binafsi si wanzishe shirika lao, kama ilivyo Precision? Ethiopian Mpaka leo linamilikiwa na Serikali, na linafanya vizuri. KQ Serikali imeongeza %age ya umiliki....Usafiri wa anga ni strategic area kwa serikali kuumiliki, sio kuachia watu binafsi kama walivyoachiwa ATC kwa wale SAA wakati ule - si uliona kilichtokea?
Nishati ndio inaweza kupokea wawekezaji wengi bila ya tatizo kuja kutokea mbele ya safari. Kila serikali makini inamiliki shirika lake binafsi la ndege.

Wanaita national carrier, lazima iwepo. Mwalimu Nyerere alipofariki 1999 alifuatwa na ndege ya ATC iliyoongozwa na RIP Mazula kule Uingereza, ingekuwa ni aibu kwa serikali kukodisha ndege ya Precision kuufuata mwili wa Nyerere.

Yapo mengi yanayofanywa na ndege inayomilikiwa na serikali, linapokuwepo shirika lenye kumilikiwa na serikali inakuwa ni heshima kwa nchi.
 
Tumbili kama tumbili.
image-insert-your-face-monkey-baby-animal-34515.jpg
 
Kajitahidi kufanya nini au mnaridhika na maneno tu, katika yote aliyowahi kusema ni mradi upi umezinduliwa au kukamilika?
Najitahidi namna ya kukujibu ,ila nashindwa hata nimsaidie wapi huyu tumbili wa werema...hamna kitu pale.
 
Karne hii mnajenga Hostel?

😂😂😂😂
Wanazidi ku-diviate kwenye jukumu la msingi badala ya kuongeza majengo waongeze vitivo waweze kupata kipato zaidi hostels achia sekta binafsi huko wawekeze kumaintain hostels ni gharama zaidi ya madarasa
 
Hata TTCL ni majanga sana, haya ndiyo maeneo ayatupie macho sasa ili kuleta ufanisi na tija
Anahangaika na petty issues asikike wakati shirika kama ttcl liko/lilikuwa kwenye uwezo wa kufanya biashara ya data/ Internet na kupata faida mara dufu kabla hata ya makampuni mengine hayaweka mkazo huko
 
View attachment 3101816
===
Chuo Cha Usimamizi wa Fedha na Biashara Cha CBE nchi Tanzania kimemtunuku Mhe David Zacharia Kafulila ngao ya heshima kwa uchapakazi wake uliotukuka kwa Taifa lake.

Mkuu wa chuo hicho Prof. Eddnah Luoga asema chuo chake kimeamua kumtunuku ngao hiyo ya heshima katika kutambua juhudi zake kwenye kumpata mbia mwekezaji toka sekta binafsi atakayejenga mabweni katika chuo hicho yatakatokuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi elfu 12 kwa mara moja.

Mwekezaji huyo atawekeza kwa sharti la Ubia ili kukabiliana na changamoto za wanafunzi kuishi mbali na eneo la chuo hicho jambo ambalo hupunguza zaidi ari, ufaulu na nguvu za kimasomo kwa wanafunzi.

David Zacharia Kafulila Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi Tanzania PPPC amekuwa akisisitiza wakati wote kuwa lazima Tanzània ifike wakati ambao Serikali yetu itapunguziwa mzigo katika kutekeleza miradi yake ya maendeleo hasa ile yenye sura ya kibiashara.

Mkurugenzi huyo anasema kwa kufanya hivyo kutaipunguzia Serikali mzigo na kuifanya itekeleze baadhi ya miradi yake ya maendeleo nje ya bajeti yake hasa ile yenye sura ya kibiashara ( projects contraction outside the government balance sheet )
===

View attachment 3104529
Kafulila ni mtu mzuri
 
Back
Top Bottom