Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kumtunuku Rais Magufuli Shahada ya Falsafa

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kumtunuku Rais Magufuli Shahada ya Falsafa

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kitamtunuku Rais wa Tanzania, John Magufuli Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa kutokana na uongozi wake hasa ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Akizungumza leo Jumatano Novemba 20, 2019 Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Faustine Bee amesema shahada hiyo itatolewa kesho katika mahafali ya 10 ya chuo hicho.

“Shahada hii itatolewa kwa Rais kwa uongozi wake uliotukuka hususan katika ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa kuwekeza katika elimu, miundombinu, mawasiliano, nishati, utalii na kuimarisha utawala bora na mapambano dhidi ya rushwa," amesema.

Amesema mwaka 2010 shahada hiyo ilitolewa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete na Rashid Kawawa (marehemu).

Profesa Bee amesema wahitimu 6,488 watatunukiwa Astashahada, Shahada, Stashahada ya juu, Shahada ya Umahiri, na Shahada ya Uzamivu.
 
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kinatarajiwa kumtunikia Rais Dk. Magufuli Shahada ya Heshima ya Daktari wa Falsafa kwa uongozi wake uliotukuka hususani katika ujenzi wa uchumi wa viwanda na kuwekeza kwenye miundombinu na kuimarisha utawala bora na mapambano ya rushwa.

IMG_20191120_150655.jpeg
 
Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kinatarajiwa kumtunikia Rais Dk. @MagufuliJP shahada ya heshima ya Daktari wa Falsafa kwa uongozi wake uliotukuka hususani katika ujenzi wa uchumi wa viwanda na kuwekeza kwenye miundombinu na kuimarisha utawala bora na mapambano ya rushwa. View attachment 1267468

Da ndugu watanzania tulipofika sasa ni mapabaya sana.historia za watu kama wakina musolini,hitler,na wengineo walitumia njia ya makundi mbali mbali kuwasafisha na kuwaabudu
 
Kuna kitabu cha literature nilisoma kinaitwa A MAN OF THE PEOPLE. Humo unakutatana na genge la viongozi ktk kitaifa flani wanapeana HONOURS za kijinga jinga na masifa kibao.Sasa nayaona live zama hizi.


Hovyo kabisa
 
Back
Top Bottom