Chuo Kikuu Cha Uhasibu Arusha kinahitaji wanafunzi zaidi ya 2000 kurudia mitihani wakati walishafanya mitihani na matokeo yalitoka

Chuo Kikuu Cha Uhasibu Arusha kinahitaji wanafunzi zaidi ya 2000 kurudia mitihani wakati walishafanya mitihani na matokeo yalitoka

HANADA

New Member
Joined
Sep 12, 2024
Posts
1
Reaction score
3
Uongozi wa Chuo cha Uhasibu Arusha, umetaka wanafunzi zaidi ya 2000 kurudia mtihani ingawa walishafanya mtihani huo wa semister ya 2.

Chanzo ni kutolipa ada ya kufanya mtihani, hii sio haki.

Uongozi umeshindwaje kutambua toka kipindi chote hadi wamefanya mtihani na matokeo yameshatoka. Na istoshe, wazazi watatoa wapi kiasi cha pesa cha ada, maana mtihani ni tarehe 23 mwezi huu na wanafunzi wapo likizo.

Mifumo ya vyuo na wanafunzi wamefanya mtihani kwa sababu ya mifumo yao mibovu hadi mtu anapata namba ya kufanya mtihani. Je, Jamii Forums nani wa kumlaumu?

Wasaidieni wadau, hali sio nzuri na hii sio haki.

IMG-20240911-WA0044.jpg
 
Kama kiuchumi hauko poa n bora usisome mana unaiangaisha familia hela nyingi halaf hakuna unachokuja kukipata baada ya hayo masomo n bora izo hela ufanyie biashara utatoboa
 
Ada shilingi ngapi ? Watu wanachangia harusi ya siku moja mpaka milion10 ila kulipa ada ambayo haifiki hata mil 3 tena kwa mwaka nzima mtoto anapata elimu hawataki .

Kuna haja ya kujitathmini kama jamii upya .
 
Wanafunzi wengi wanaendekeza starehe baada ya kulipa ada hasa wenye boom na wakaze hvohvo hasa kwa wenye mikopo ya serikali, lakn kwa wasiokua na mikopo wawafikilie upya hali ni mbaya kwa wazazi mlishe mtoto na alipe ada, lakn wale wanaokula ada mjtafakari mnatoka familia gani mspende kuiga fanya kulingana na kpato chenu nyumbani. mwsho kabsa sio haki uzembe ni wao wajitathmini wao na mifumo yao kwahyo wasiwabebesha mzgo wanafunzi kwa ujnga wao wenyewe
 
Nashukuru miaka 4 ya pale Campus, sikuwahi pata tatizo kuhusu ada, au fedha juu ya mambo ya chuo.

Wazazi wangu mbarikiwee sanaa, [emoji120][emoji120][emoji120]
 
Huwezi kuta hii kwenye vyuo
Nashukuru miaka 4 ya pale Campus, sikuwahi pata tatizo kuhusu ada, au fedha juu ya mambo ya chuo.

Wazazi wangu mbarikiwee sanaa, [emoji120][emoji120][emoji120]
Ulikuwa na asilimia 100 za Magu?
 
IAA ndo pamekuwa pa kiboya ivyo sa hivi rector prof Manamba,BATE vipi yupo?
 
Back
Top Bottom