Chuo Kikuu Huria (Open University of Tanzania)

Chuo Kikuu Huria (Open University of Tanzania)

Wakuu mimi ni form 4 .... naomba kuuliza,je naweza kupata nafasi ya kuanza certificate hapo OUT?
Na je wanatoa Faculty zipi (kama nitapewa listi nitashukuru sana)
Unaweza kuanza certificate kama walau Una D nne form four kama Maelekezo ya NACTE yalivyo.
 
Wakuu mimi ni form 4 .... naomba kuuliza,je naweza kupata nafasi ya kuanza certificate hapo OUT?
Na je wanatoa Faculty zipi (kama nitapewa listi nitashukuru sana)
Nakushauri kutembelea website Yao utapata kila kitu.
www.out.ac.tz
 
Hivi inawezekana kusoma degree mbili tofauti kwa mwaka wa masomo huo huo? Yani Nina maana kwamba mtu unasoma degree A,UDOM na wakati huo huo unasoma degree B Open university, je inawezekana?
Hauwezi kusoma shahada mbili kwenye vyuo viwili vilivyo chini ya TCU.
TCU Hawawezi kukupa admission mbili Kwa wakati mmoja lazima uwe deregistered chuo kimoja ili uombe kingine na kama umepata viwili au zaidi Kwa wakati mmoja lazima uconfirm kimoja.
 
Rafiki yangu amedahiliwa ktk foundation course ila ishu za uchumi zimemkalia vibaya kidogo, hivyo anahitaji kufahamu inawezekana akafanya malipo mwakani na kuanza kusoma?
Kama anaweza alipe first payment 210,000 then asajiri kozi zake aanze kusoma taratibu.
Au asajiri kozi chache aanze kusoma
 
Hivi kuna Faculty ya Procurement pale au Pablic relation mwenye kujua anijuze tafadhali
Kuna kozi ya Procurement and Supply Chain Management kuanzia Cheti mpaka shahada iko kitivo cha usimamizi wa biashara.
Pia kuna kozi ya Mass communication ambayo Mtu Wa Public Relations pia inamfaa iko ngazi ya Cheti mpaka Shahada ya uzamivu.
Public Relations yenyewe haipo.
 
Kuna kozi ya Procurement and Supply Chain Management kuanzia Cheti mpaka shahada iko kitivo cha usimamizi wa biashara.
Pia kuna kozi ya Mass communication ambayo Mtu Wa Public Relations pia inamfaa iko ngazi ya Cheti mpaka Shahada ya uzamivu.
Public Relations yenyewe haipo.
Naomba kujua mahali kilipo chuo kikuu huria kwa Dar es Salaam
 
Kuna kozi ya Procurement and Supply Chain Management kuanzia Cheti mpaka shahada iko kitivo cha usimamizi wa biashara.
Pia kuna kozi ya Mass communication ambayo Mtu Wa Public Relations pia inamfaa iko ngazi ya Cheti mpaka Shahada ya uzamivu.
Public Relations yenyewe haipo.
Habar, vip kwa wanaomba transfer-(NACTE) mnawapokea ? Social work nta level 5 march intake ?????
 
Mimi naomba kuuloza kuwa , kuna kozi ya foundation katika chuo cha open university of Tanzania, je mtu akisoma kozi hiyo na kuomba chuo kikuu akapata , je upande wa mkopo wa heslb anaweza kupewa au atasoma kwa gharama zake? Je akifaulu ataruhusiwa kusoma chuo chochote au ni out tu?
 
Mimi naomba kuuloza kuwa , kuna kozi ya foundation katika chuo cha open university of Tanzania, je mtu akisoma kozi hiyo na kuomba chuo kikuu akapata , je upande wa mkopo wa heslb anaweza kupewa au atasoma kwa gharama zake? Je akifaulu ataruhusiwa kusoma chuo chochote au ni out tu?
Hiyo kozi unajisomesha wala sio gharama sana tena ndani ya mwaka mmoja...jipange tu.


#MaendeleoHayanaChama
 
Hiyo kozi unajisomesha wala sio gharama sana tena ndani ya mwaka mmoja...jipange tu.


#MaendeleoHayanaChama
Yaani namaanisha baada ya kumaliza kusoma hiyo Foundation course, nikiomba kusoma Bachelor Degree chuo chochote kilichopo Tanzania naweza kupata? Na je nikiomba mkopo kutoka heslb nitapewa?
 
Yaani namaanisha baada ya kumaliza kusoma hiyo Foundation course, nikiomba kusoma Bachelor Degree chuo chochote kilichopo Tanzania naweza kupata? Na je nikiomba mkopo kutoka heslb nitapewa?
Ndio unaweza kupata mkopo mana moja ya kigezo cha kupata mkopo ni kuwa admitted na chuo kwa masomo ya shahada..vigezo vingine hutolewa na bodi hivyo jitahidi kufahamu vigezo vya bodi kwa mwaka husika.

#MaendeleoHayanaChama
 
Ndio unaweza kupata mkopo mana moja ya kigezo cha kupata mkopo ni kuwa admitted na chuo kwa masomo ya shahada..vigezo vingine hutolewa na bodi hivyo jitahidi kufahamu vigezo vya bodi kwa mwaka husika.

#MaendeleoHayanaChama
Shukrani kiongozi wangu
 
Mfano bacherol yoyote ile unatakiwa kusoma maximum unit 40 minimum 36 3years hivyo basi kuna mitihani aina mbili moja special annual examination unaweza andika muda wowte pale tangazo la kusajili masomo kwa ajili ya mtihani pili annual examination hivyo basi unaweza ukawa umesajili course 10 zenye unit 18 kwa mwaka wa kwanza tatu zenye unit 6 ukapiga kama special na nyingine ukaandika annual sasa unajikuta utamaliza unit zako ndani ya mda au chini ya mda sasa kumbuka ww ulisajiliwa intake gani kama ni January,April,July au October hivyo basi utasubilia intake yako ifike kwa mda muafaka huku ukiwa ushamaliza na kusubili mahafari kisha kuchukua cheti au transcript ila transcript nasikia unaweza pewa mapema tuuu
Safi sana Shukrani kwa ufafanuzi mzuri 🙏
 
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (kwa Kiingereza: Open University of Tanzania) ni chuo kikuu kinachotoa kozi za cheti, stashahada na shahada kupita masomo ya mbali (Distance Learning). Makao makuu yako Dar es Salaam, Tanzania. Chuo Kikuu Huria kina takribani wanafunzi 70,000 kutoka ngazi mbalimbali za kitaaluma.

Historia
Kilianzishwa mwaka 1992 kwa kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge namba 17 ya mwaka 1992. Sheria hiyo ilipata nguvu ya utendaji rasmi tarehe 1 Machi 1993 kwa mujibu wa tangazo la serikali namba 55 ya gazeti lake rasmi.

Mwaka 1994, Januari 19 Makamu Mkuu wa kwanza wa Chuo alishika madaraka na mwezi huohuo walisajiliwa wanafunzi wa awamu ya kwanza.

Mwaka 2007 kwa mujibu wa sheria ya vyuo vikuu, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kilianza kutumia sheria na taratibu zake za ndani ya chuo toleo la mwaka (2007) katika shughuli zake za kiutawala.

Taaluma
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinatoa stashahada, diploma na shahada mbalimbali kupitia elimu ya kimtandao au elimu ya masafa ya juu kwa njia ya tehama au nyenzo nyingine mbalimbali za kiteknolojia. Shughuli za chuo zinafanyika na kutoa huduma katika viwango vya utendaji na usimamiaji wa baraza la vyuo vikuu Tanzania (TCU). Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinatoa programu takribani 125.

Vituo
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kina vituo kwenye mikoa zaidi ya 30 nchini Tanzania; hii ni kujumlisha na vituo vya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar (Unguja na Pemba), Kenya vituo viwili (Chuo cha Egerton na Njoro), Rwanda (eneo la Kibungo), Uganda na Namibia (Chuo cha Triumph).

Vituo vingine vya mashirikiano ya ndani ni ACDE-TCC (African Council for Distance Education- Technical Collaboration Committee), CECED (Centre for Economics and Community Economic Development), SADC ODL CoS TE (SADC Centre of Specialization in Teacher Education).

Chuo Kikuu Huria kina vituo vya kusomea takribani 69 ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Vitivo
Ina:

•Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii
•Kitivo cha Elimu
•Kitivo cha Sheria
•Kitivo cha Uongozi wa Biashara
•Kitivo cha Sayansi, Teknolojia na Masomo ya Mazingira
•Taasisi ya kuyaendeleza masomo
•Taasisi ya Teknolojia ya Elimu
•Kurugenzi ya Huduma za Mikoa
•Kurugenzi ya Utafiti na Masomo ya baada ya Shahada
Makao makuu yake sio Dar es salaam ni Pwani Kibaha kwa mathius kushoto kama unaenda morogoro ina range 3km kutoka barabara ya lami kimepakana na makao makuu ya Efatha ministry
 
Makao makuu yake sio Dar es salaam ni Pwani Kibaha kwa mathius kushoto kama unaenda morogoro ina range 3km kutoka barabara ya lami kimepakana na makao makuu ya Efatha ministry
Ni kweli panaitwa bungo ila temporary headquarters ni kinondoni ambako mambo mengi hufanyika hapo
 
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (kwa Kiingereza: Open University of Tanzania) ni chuo kikuu kinachotoa kozi za cheti, stashahada na shahada kupita masomo ya mbali (Distance Learning). Makao makuu yako Dar es Salaam, Tanzania. Chuo Kikuu Huria kina takribani wanafunzi 70,000 kutoka ngazi mbalimbali za kitaaluma.

Historia
Kilianzishwa mwaka 1992 kwa kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge namba 17 ya mwaka 1992. Sheria hiyo ilipata nguvu ya utendaji rasmi tarehe 1 Machi 1993 kwa mujibu wa tangazo la serikali namba 55 ya gazeti lake rasmi.

Mwaka 1994, Januari 19 Makamu Mkuu wa kwanza wa Chuo alishika madaraka na mwezi huohuo walisajiliwa wanafunzi wa awamu ya kwanza.

Mwaka 2007 kwa mujibu wa sheria ya vyuo vikuu, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kilianza kutumia sheria na taratibu zake za ndani ya chuo toleo la mwaka (2007) katika shughuli zake za kiutawala.

Taaluma
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinatoa stashahada, diploma na shahada mbalimbali kupitia elimu ya kimtandao au elimu ya masafa ya juu kwa njia ya tehama au nyenzo nyingine mbalimbali za kiteknolojia. Shughuli za chuo zinafanyika na kutoa huduma katika viwango vya utendaji na usimamiaji wa baraza la vyuo vikuu Tanzania (TCU). Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinatoa programu takribani 125.

Vituo
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kina vituo kwenye mikoa zaidi ya 30 nchini Tanzania; hii ni kujumlisha na vituo vya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar (Unguja na Pemba), Kenya vituo viwili (Chuo cha Egerton na Njoro), Rwanda (eneo la Kibungo), Uganda na Namibia (Chuo cha Triumph).

Vituo vingine vya mashirikiano ya ndani ni ACDE-TCC (African Council for Distance Education- Technical Collaboration Committee), CECED (Centre for Economics and Community Economic Development), SADC ODL CoS TE (SADC Centre of Specialization in Teacher Education).

Chuo Kikuu Huria kina vituo vya kusomea takribani 69 ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Vitivo
Ina:

•Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii
•Kitivo cha Elimu
•Kitivo cha Sheria
•Kitivo cha Uongozi wa Biashara
•Kitivo cha Sayansi, Teknolojia na Masomo ya Mazingira
•Taasisi ya kuyaendeleza masomo
•Taasisi ya Teknolojia ya Elimu
•Kurugenzi ya Huduma za Mikoa
•Kurugenzi ya Utafiti na Masomo ya baada ya Shahada
Ninajiandaa kusoma Shahada ya Sociology Lakini cha kuhuzunisha about Open University ni kwamba yaani ni ngumu kupata taarifa za kozi yako na msaada mfano ningetegemea kuona kuna Group hata la Telegram la Open university Students mahali ambapo wana share vitu vingi ikiwemo pastpapers kuelekezana na kutiana moyo ila naona ni kama giza
 
Ninajiandaa kusoma Shahada ya Sociology Lakini cha kuhuzunisha about Open University ni kwamba yaani ni ngumu kupata taarifa za kozi yako na msaada mfano ningetegemea kuona kuna Group hata la Telegram la Open university Students mahali ambapo wana share vitu vingi ikiwemo pastpapers kuelekezana na kutiana moyo ila naona ni kama giza
Baada ya kutafuta bila mafanikio Group linalowaunganisha wanafunzi wa centers zote na kozi zote wa Chuo kikuu huria cha Tanzania nimeamua kutengeneza Link kwa ajiri ya wanafunzi wa Chuo kikuu huria ili kuwaleta pamoja waweze kusaidiana katika kupeana moyo, kujadiri mambo mbali mbali lakini pia kupeana msaada wa ki masomo. Wanafunzi wakiwa kwenye group kwa pamoja wataweza kupeana msaada wa wakati yaan ontime help.

Link ya Telegram: Open University Of Tanzania
 
Back
Top Bottom