Chuo Kikuu (UDSM) Kufunguliwa na Masharti mapya!

Kwani lazima chama cha wanafunzi kitambuliwe na uongozi wa chuo? Pengine huu ndiyo wakati muafaka wa wanafunzi kuwa na chama ambacho kitawakikilisha wao bila kuingiliwa na mamlaka ya Chuo. Ikibidi waende mpaka mahakamani kudai haki yao ya msingi ya uwakilishi halisi na si huu wa kilemba cha ukoka! Aluta Continua.

Amandla...........
 
Kuwa na wanafunzi huru wa vyuo vikuu ni swala muhimu la kitaifa. Wanafunzi wa chuo kikuu wanapashwa kuunda serikali yao wenyewe. Wakiundiwa na viongozi wa chuo, basi inakuwa ni serikali ya vibaraka.

UDSM ilikuwa na serikali huru ya wanafunzi iliyoitwa DUSO (Dar es Salaam University Students Organisation). Viongozi wa sasa wa chuo walisoma wakati wa DUSO, na hata JK alisoma chini ya DUSO.

DUSO ilivunjwa wakati CCM ilipoamua kuweka vyama vyote vya wanafunzi chini yake. Miaka kadhaa baadaye, wanafunzi wa mlimani walipewa ruhusa ya kuwa na serikali yao tena, na ikaitwa DARUSO. Hilo jina lilipachikwa na wakubwa.

Wanafunzi wa chuo kikuu wanapashwa kuunda serikali yao wenyewe, na jina lake wachague wenyewe. Ni kosa viongozi wa chuo kuchagua jina la serikali ya wanafunzi.

Hatutaki wanafunzi ambao ni waoga kiasi cha kukubali kulazimishwa kuvaa vitambulisho wakati wote. Mahali ambapo kinahitajika kitambulisho (eg cafeteria) wanafunzi watatoa na kurudisha tena mfukoni.

Ili kutayarisha viongozi bora wa kesho, inabidi wanafunzi wa vyuo vikuu wasiwe mabwege yanayovalishwa vitambulisho kwa nguvu na kupachikwa serikali ya vibaraka.
 
Sidhani kama kuutwa kwa DARUSO ni kumaanisha kuwa wanafunzi hawatakuwa na representation. Ni obvious kwamba kutakuwa na chombo kipya kwa ajili ya wanafunzi. Kama jinsi JUWATA ilivyokufa ikaja OTTU, TUGHE, TUICO etc... Kwa hawa wanafunzi wa UDSM kulikuwa na haja ya kufuta chama chao ikiwa ni mojawapo ya mbinu ya kuweka bayana kuwa wanakuja upya kama wanafunzi wapya. Hii ilisababishwa pia na kitendo cha kiongozi wa iliyokuwa DARUSO kuwatangazia wanafunzi kupitia vyombo vya habari kuwa wafike chuoni hata kama hawajatimiza masharti, sasa hapa kama wana JF wenzangu hamuoni kuwa the late DARUSO ilikuwa ni tatizo kwa hali ya utulivu na maelewano then labda tukubali tu kutofautiana kimawazo.
 
We should not manipulate UDSM students. It's up to them to change DARUSO, if they so desire. It is their government, not ours.

I support their leaders' call for all of them to report back. They should keep their previous leaders until they themselves decide to replace them. No one should usurp their democratic rights.

As Mandela said, freedom is worth fighting for. It is also worth suffering for. UDSM students should fight for the right of equal access to education for all of them
 

Sasa zemarcopolo,
hiyo representation itatoka wapi na kwa utaratibu upi?nani atakayechagua au kuteua students representatives?kuna vikao mbalimbali vinafanyika kuanzia kwenye kamati mbalimbali za chuo hadi kwenye senate ambako wanafunzi huwa na wawakilishi wao ambao huchaguliwa na wanafunzi wenyewe.
Na kwa jinsi hiyo DARUSO kupitia kwenye katiba yao wameainisha kwamba ni nani amepewa mamlaka au uwezo wa kuwawakilisha wanafunzi katika vikao vinavyohitaji uwakilishi wao.Swali nalotaka ulijibu ni hili: wakati bado huo utaratibu mpya haujawekwa, wanafunzi watakuwa represented au hawatakuwa?na kama watapata representative ataokea wapi na kwa utaratibu upi?na je itachukua muda gani hadi utawala wa chuo kuweka utaratibu mpya utakaowawezesha wanafunzi kuweza kujumuika na kuendelea na jumuia zao kama zamani?Hata huyo kiongozi wa daruso aliyetangaza kwamba hata wale wasiolipa ada waripoti siku hiyo kama alikosea kwanini asishughulikiwe yeye na badala yake wameamua kuvunja jumuia zote za wanafunzi?au ni kwanini wasingeivunja daruso pekee?hapa makundi mengine au jumuia zingine zinahusikaje?
 

Tatizo ndilo hilo mkuu! Alipokurupuka kutoa uamuzi 'HAIWEZEKANI' Ndipo alipoharibu. Tunaizika Elimu huku tukiimba ndoto za kuwa na uchumi bora na maisha bora kwa kila mtanzania!
 
uchaguzi ni mwakani, basi hata mwakani sukumeni shangingi la kikwete akija kupiga kampeni huko. wamewaumiza kimtindo, na ninyi waumizeni kwenye kura mwakani. hiyo ndo sulution. huu ni u shauri wangu.
 
Hivi viongozi wa chuo wameshindwa kujua kuwa tatizo sio DARUSO au mpango wao ni kuwaundia chombo kingine na kutunga kila kitu kwenye katiba mpya?......Viongozi wetu hawajui kuwa fikra za mtu/watu huwezi kuziua kwa urahisi hivi hivi, uta-suppress kwa muda lakini zitakuja kuibuka tu tena.
 
Ni mawazo hasi kusema kila siku mimi maskini basi nisaidie!!!

Tanzania na watu wake sii nchi maskini!

Mimi sikubali kuwa Tanzania ni maskini na kwa hiyo watu wake hawawezi kuchangia elimu ya juu ya watoto wao waliowazaa!

Taratibu mkuu, watakuhoji uraia sasa hivi!
 

Mkuu wewe ni kati ya wale 2000 au umefanikiwa kutimiza masharti?
 
Chuo Kikuu hakiwezi kuendeshwa kama kambi ya jeshi. Uhuru unahitajika vyuo vikuu vyote duniani. UDSM haina wanafunzi wa kimataifa? Watavumiliaje unyanyasaji huu?

Naomba kama kuna mwenye University of Dar es Slaam Act atuwekee hapa ili tuone wenyewe kama kuna sheria zinavunjwa na hawa watawala.

Cheo ni dhamana. Maprofesa wasitumie vyeo vyao kudumaza vijana wetu. Kijana unayempangia wapi apite, nini avae, nini aseme, nani amtawale, etc., atakuwa bwege lisilo na faida yoyote kwa taifa. Maprofesa wasikubali kuwa vibaraka wa seriakali wa kugeuza UDSM iwe kama kambi ya jeshi.

Wananchi wote wanapashwa kujiuliza ni nani ana haki ya kusoma chuo kikuu: ni watoto wa matajiri tu? Ni jukumu la wananchi, na makundi maalum kama UDASA, kupigania haki sawa katika Elimu.
 

Hapa sasa ndipo watakapojenga kizazi cha akina "ndio mzee".
Wameshindwa kutatua tatizo,sasa wanatumia mabavu...Kuna taarifa kuwa kwa leo hii geti la kuingilia hawaruhusu gari la aina yeyote kuingia.Na watu waingiao wanaingia kama wanaingia uwanja wa taifa kushuhudia pambano la mpira!!!
 


Augustine hapo umenena vyema mkuu sina la kuon geza. Inabakia ukweli tu kwamba haingii akilini maamuzi kama haya kufanywa na maprofesa ambao ndo jamaa yote ina amini ni watu wenye hekima.
 
Hivi Mkuu wa Chuo angelikua Prof. Viktor au Prof. Peter au Prof. Mbogo-watu wapole na wastaarabu na wasio na papara na kifu fesa chuo kikuu kweli kingelikwenda njia inayokwenda sasa.

Ninadhani chini yao fedha inayozalishwa na Chuo Kikuu katika miradi yake mbalimbali ingelionekana na ingelitumika kuwalipia wale wasioweza kuafodi fuli malipoz!!
 
Once again Prof. Maghembe has proven himself to be a waste of time.....hivi huu U-Prof alitunukiwa wapi vile
 

Mkuu
Tatizo mwalimu anasema mtoto alipiwe ada na mzazi (serikali) na sio mwalimu (chuo). Mtoto na mzazi wakigombana, mwalimu halimuhusu, wakae kivyao wayamalize. Kwa mtazamo huo mzazi anasema mtoto lazima asome hata kama kwa kukalia misumari na anamhiza mwalimu kumwadhibu mtoto wake yeyote atakayeshindwa kufuata masharti ya mzazi na mzazi atamsaidia kwa nguvu zote kudumisha nidhamu ya watoto shuleni (ffu=jeshi)
 
Last edited:
Leo katika maeneo ya Manzese tulikosa umeme kuanzia saa 12 kasoro hadi kilipoisha kipindi cha hapa na pale kinacharushwa na ITV. Ninaongelea Manzese kwa sababu wakati huo nilikuwa maeneo hayo ya Manzese. Baada ya kipindi hicho umeme ulirudi. Ninachouliza ni kwamba je kwenye maeneo mengine nchini umeme ulikuwa je? Ulikatika pia? Hata ilipofika saa moja kamili usiku wakati wa kipindi cha Taarifa ya habari cha Channel Ten umeme pia ulikatika. Chakushangaza zaidi ilipoakaribia saa 2.00 kamili jioni umeme ulikatika tena. Wakati huo ni wakati wa taarifa ya habari za ITV na TBC one. Nilijiuliza kukatika kwa umeme kulipangwa ili tusipate matukio yaliyojiri UDSM kuhusiana na udahili wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam au ni tatizo la kiufundi?
 
inauma kwa kweli...solution ni kulipua bunge likiwa in sessions while holding big banners saying TFC (Tulio fukuzwa Chuo)
 

Hata Mbagala ulikatika. Nilihisi kitu fulani ila ngoja nisiseme zaidi. Pengine ilikuwa 'genuine' faulty.
 

Hata Mbagala ulikatika. Nilihisi kitu fulani ila ngoja nisiseme zaidi. Pengine ilikuwa 'genuine' fault.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…