Chuo Kikuu (UDSM) Kufunguliwa na Masharti mapya!

Chuo Kikuu (UDSM) Kufunguliwa na Masharti mapya!

Hebu na tufanye assessment ya nini hao DARUSO walichofanya lets say for the past 10 years.
Mwenye data na atoe...Mimi niiionayo ni kila siku kuitisha mikutano ya migomo tu.....
Kuna data zozote zinazoonyesha kama serikali ya wanafunzi inamsaidiaje wanafunzi wa kawaida wa mwaka wa kwanza?? Kam zipo na za kujitosheleza then tunaweza kutajadili tofauti, kama hakuna...Then ni sawa tu kufungiwa.
Na si vitambulisho pekee tu, washurutishwe kuvaa na sare sasa...Napendekeza suruali/sketi za kijani mpauko na mashati ya kahawia ili waonekane vizuri wakipita mahali....
 
Hebu na tufanye assessment ya nini hao DARUSO walichofanya lets say for the past 10 years.
Mwenye data na atoe...Mimi niiinonayo ni kila siku kuitisha mikutano ya migomo tu.....
Kuna data zozote zinazoonyesha kama serikali ya wanafunzi inamsaidiaje wanafunzi wa kawaida wa mwaka wa kwanza?? Kam zipo na za kujitosheleza then tunaweza kutajadili tofauti, kama hakuna...Then ni sawa tu kufungiwa.
Na si vitambulisho pekee tu, washurutishwe kuvaa na sare sasa...Napendekeza suruali/sketi za kijani mpauko na mashati ya kahawia ili waonekane vizuri wakipita mahali....

Mkuu MZG DARUSO kama DARUSO hakuna la maana, kilichopo pale ni kutafuta umaarufu kwa kuandaaa migomo isiyo na tija, na kikubwa zaidi ni kale kabiashara kanachoendeshwa pale maana hao viongozi wa sasa wa DARUSO wanajifaidia sana kiasi kwamba wengine wamesikika wakijitamba kabisaa the way walivyokuwa wanafaidi pesa ya DARUSO, sasa ngoma ndo imekula kwao ngoja tuone nini kitatokea maana kama hakuna hiyo DARUSO maana yake hata lile jengo la viongozi watapigwa chini hakuna kujifanya ooh mimi ni kiongozi nakaa hapa nani kasema?? yaani i wish ningekuwa home angalau nizunguke zunguke maeneo ya mlimani niangalie vijana wanavyohanganika kwa vitu ambavyo walikuw ana uwezo wa kuvisolve kiurahisi zaidi.
 
Hebu na tufanye assessment ya nini hao DARUSO walichofanya lets say for the past 10 years.
Mwenye data na atoe...Mimi niiinonayo ni kila siku kuitisha mikutano ya migomo tu.....
Kuna data zozote zinazoonyesha kama serikali ya wanafunzi inamsaidiaje wanafunzi wa kawaida wa mwaka wa kwanza??....
Ndio nilitaka kuuliza na mimi kazi za Daruso....tatizo la wale vijana nasikia Chadema waliwadanganya asa ona madhara wanayoyapata
Napendekeza suruali/sketi za kijani mpauko na mashati ya kahawia ili waonekane vizuri wakipita mahali....
kwikwikwikwikwikwi
 
Ningependa kuchangia straight to the point kwenye hii mada; sitaongelea DARUSO anyway. Nionavyo mimi hili swala la Uchangiaji elimu ya vyuo vikuu ndio hasa chanzo cha migomo na matatizo yote yanayotokea chuo kikuu. Na kama migomo hiyo haikukwa ya kinidhamu na inafanywa kiholela je tujiuliza kuwa wanafunzi hawa wakifanywa migomo kwa kufuata sheria wanasikilizwa? au bado wanafanywa wapumbavu na kudharauliwa?
Jambo lingine swala hili la uchangiaji lilijadiliwa wapi? au ulikuwa ni uamuzi wa mtu binafsi au wakuu fulani? Maana ni issue amabayo ina affect jamii na katika different levels, let's say wa kipato cha juu na chini. Nchi yenyewe ipo kwenye record kuwa tunaishi less that a Dollar/day halafu unamwambia mwanafunzi wa chuo kikuu achangie hizo hela atatoa wapi? Ikumbukwe kuwa wanafunzi wengi ni full time students anaingia darasani kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa mbili usiku na wengi wao ni watoto wa wakulima. The whole issue is economical and educational segregation.
Nini kifanyike; kwa nini serikali isiwashirikishe kuchangia hawa wanafunzi kwa njia ya mikopo na wahakikishe hiyo mikopo inarudi as soon as they are employed after their education? Tuachane na mikopo waliyokuwa wanatoa mwanzo maana na yenyewe walikuwa wanapeana tu, na sidhani kama hela zote huwa zinarudi; na kama zote zilikuwa zinarudi kwa nini zisizungushwe kwa wanafunzi hawa wanaoandamana kila siku?
Kama wanataka wanafunzi wachangie basi wawapunguzie masaa ya darasani na wa create part-time jobs for the students so they afford it!Period!
 
Mie nadhani wazazi pia wamechangia hali hii ya baadhi ya wanafunzi kutokurudi vyuoni either kwa uzembe au kwa kukosa uwezo. Kama wazazi wengeshirikiana na wanafunzi katika kufatilia kwa undani zaidi nini cha kufanya ili wanafunzi warudishwe vyuoni hali hisingefika hivi.Swala la kuvaa vitambulisho sio kosa. Kwa sababu hii itawatambulisha ni kina nani ni wanafunzi na kina nani sio wanafunzi. Kwa mfano nchi zilizoendelea kila mwanafunzi anapaswa kuwa ni kitambulisho ili pindi atakapotaka kuingia kokote ndani ya chuo akitumie. Pili kinasaidia kwa usalama wa ndani ya maeneo ya taaluma. Manake kila atakeyeingia katika maeneo fulani hapo chuoni atajulikana ni nani.
Ila sijuhi kwa mazingira ya vyuo vyetu vya kitanzania je hali haitaleta husumbufu kwa watu wengine ambao sio wanafunzi ambao watakuwa wamekwenda hapo chuoni kwa sababu mbali mbali? Manake tamko lililotolewa na Prof Maboko ni kwamba kutakuwa na ukaguzi getini sasa sijuhi kwa watu ambao sio wanafunzi hawataruhusiwa kuingia maeneo ya chuo.
 
Date::1/15/2009
Wabunge: Wanafunzi wote vyuo vikuu warejeshwe
Jackson Odoyo
Mwananchi​

WABUINGE wameitaka serikali isimamie zoezi la kuwarejesha wanafunzi wa vyuo vikuu waliofukuzwa na kuhakikisha kwamba wote wanarudishwa masomoni.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kwa niaba ya wabunge wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, mwenyekiti wa kamati hiyo, Omary Kwaang’ alisema serikali inatakiwa iwe makini katika suala hilo la kurejesha wanafunzi hao chuoni.

Mwenyekiti huyo alitoa kauli hiyo siku moja baada ya vyuo vikuu mbalimbali nchini, kutangaza utaratibu mpya wa kuwarejesha wanafunzi waliofukuzwa mapema mwaka jana kwa sababu za mgomo vyuoni.

Moja ya taratibu hizo ni suala la kujaza fomu na kujiandikisha upya huku wakitakiwa kulipa madeni yote wanayodaiwa chuoni hapo.

Sababu kubwa iliyofanya wanafunzi hao kuanzisha migomo hiyo ni kupinga sera ya uchangiaji wa elimu, wakidai kuwa inawapa upendeleo wanafunzi wanaotoka katika familia zenye uwezo na kuwabana wale wanaotoka katika familia zisizokuwa na uwezo.

"Tunaomba serikali iwe makini katika suala hili la kurudisha wanafunzi vyuo vikuu na kuhakikisha kwamba, hakuna mwanafunzi atakayeachwa katika zoezi hili la kuwarejesha," alisema Kwaang' na kuongeza:

"Hatuoni sababu ya baadhi ya wanafunzi kurejeshwa na wengine kukataliwa. Hiyo si halali hata kidogo".

Kwaang' pia alisema hakuna sababu ya nchi kuendelea kubeba mzigo wa kusomesha watoto wanaotoka familia zenye uwezo wakati kuna watoto wanaohitaji msaada wa serikali.

"Watoto wote wenye uwezo wa kuchangia wanapaswa kuchangia masomo yao, ili serikali iendelee kuwasaidia watoto wasiokuwa na uwezo," aliongeza Kwaang'.

"Ingawa sera ya kuchangia huduma ni jambo la msingi katika jamii, kitendo cha Bodi ya Mikopo kuwagawa wanafunzi katika makundi sita kinaigawa nchi katika makundi mawili na inawaongezea wazazi mzigo."

Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo, George Nyatega alisema ili kukuza kiwango cha fedha zinazotolewa wakati wa mikopo, inapaswa fedha hizo zitozwe riba.

“"Fedha zinazokopeshwa zinapungua thamani yake kila siku, kwa sababu hazitozwi riba, sasa basi ili hali hiyo isiendelee kuwepo inabidi wanafunzi wote wanaopewa mikopo watozwe riba," alisema Nyatega na kuongeza:

"Mikopo inatolewa bila kutoza riba na urejeshwaji wake huchukua muda mrefu (hadi miaka 10) ni dhahiri kwamba thamani yake inapungua."

"Njia pekee ya kulinda thamani ya mikopo hiyo ni kutoza riba inayolingana na mfumuko wa bei".

"Pamoja na kwamba wazo la kutoza riba halikubaliki kwa wadau, bodi itaendelea kulielezea ili liweze kueleweka," alizidi kusisitiza.

Hata hivyo Kwaang' alifafanua kwamba sera ya kuchangia iko katika sekta zote, lakini tatizo ni namna ya kuitekeleza kwani utekelezaji wake inachangia kuwagawa wanafunzi na kwamba, hali hiyo ikiachwa iendelee itawagawa watoto wa Kitanzania kwa maana kwamba kutakuwa na tabaka la watu wenye elimu na wasiokuwa na elimu ndani ya nchi moja.

"Haya makundi ya wanafunzi wanaopewa mikopo yanaongeza mzigo kwa wazazi na pili yanaleta tabaka la elimu ndani ya nchi kiasi ambacho kinatufanya tujiulize maswali mengi," alisema.

"Sera ya uchangiaji haiepukiki, lakini tatizo linalokuja hapa ni utaratibu wa kuwagawa wanafunzi hawa katika makundi sita ya uchangiaji, sasa swali la kujiuliza katika hili ni je, utaratibu huo hauwaachi wanafunzi wanaostahili ? alihoji mwenyekiti huyo.

Katika hatua nyingine, Kwaang' alisema utaratibu huo haustahili hata kidogo kwa sababu inawaongezea wazazi mizigo ambayo haistahili na kwamba inawafanya washindwe kuwasomesha watoto.

Mfumo unaotumiwa kuchambua uwezo wa kiuchumi wa wazazi wa wanafunzi hao (means testing) huwagawa wanafunzi katika makundi sita. Kundi la kwanza "A", mwanafunzi hupata mkopo kwa asilimia mia, wakati katika kundi "B", mwanafunzi hupata mkopo kwa asilimia 80 na katika kundi la tatu, mwanafunzi hupata mkopo kwa asilimia 60.

Katika kundi la tatu, mwanafunzi hupata mkopo kwa asilia 40 na kundi la mwisho linahusu wanafunzi ambao hawapati mkopo kabisa.

"Tunazingatia uwezo wao kiuchumi wa mwombaji ikiwa pamoja na historia ya elimu ya mwombaji, kiwango cha elimu ya wazazi ama walezi wake, shughuli za kiuchumi za mwombaji na wazazi au walezi," alisema Nyatega.
 
Mimi naunga mkono kwa nguvu zote uhuru wa wanafunzi, lakini uhuru nao bila ya mipaka inakuwa karaha. Nimejaribu kuwasiliana na wadau wengi waliowahi kupitia pale ambao walikuwa wanafunzi wa kawaida tu na kuwauliza ni faida gani waliyoipata kutoka kwa uongozi wao wakiwa kama wanafunzi wa kawaida. Jibu ni la kusikitisha sana. Hakuna cha maana walichokitaja, mmoja wao ndio alinihuzunisha sana baada ya kuniambia kuwa jamaa hawakujali hata dispute ndogo tu za mgawanyo wa vyumba, sasa kama hivi kuna maana gani ya kuwa na uongozi.
Tunapigia kelele sana uongozi wa serikali kuwa ni butu lakini kama tunataka kuangalia haki, basi kila uitwao uongozi uwe fair game kwa critisism.....
Kutoka kwenye vyombo vya habari mishipa ya shingo imekutoka unapiga kelele eti unadai haki, haki ipi? mbona ukiwa kama kiongozi hatukupigii kelele kwa kushindwa majukumu yaliyo ndani ya uwezo wako??
Tunafahamu sana na "uongozi" wa chuo nao una uoza wake vilevile ambao utaniumiza vidole vyangu kuandika hapa, lakini kwa sasa napendekeza DARUSO ipumzishwe kwanza, itie akili, viongozi watakiwe kujieleza ni kwa nini uongozi wao ni muhimu uwe na ushahidi wa vielelezo, then wapewe probationary period kuassess kama wanaweza then ndio wapewe full rights...
For Now...!!! Posho ya wanayoipata na ikatengeneze madawati ya watoto wa darasa la pili pale shule ya msingi mwananyamala komakoma slaa slaa nukta nukta kwa kidala shop. Nawakilisha...
 
1. sasa watanzania tunawaiga Makaburu na sera yao ya apartheid kwani wabantu ktk maeneo yaliyotengwa ( reserved bantuland) walitakiwa kuvaa vitambulisho.
2. Kuna tatizo gani kama mtu ataingia darasani halafu asifanye mtihani? Siono haja ya watu kuonyesha vitambulisho ndio aingie darasani.
3. "PhD holders are people who are very deep in the ocean but at a very shalow water to the extent that their backs are seen". Usomo wao uko wapi ktk masuala madogo kama haya?

tulisemega toka enzi zile
Kitovu cha kwanza kinachodidimiza elimu na uchumi kwa Tz ni UDSM.

hiki ndicho chuo kinachotoa wahitimu wengi karibu kila fani na maamuzi mara nyingi kutoka vyuo vingine huwa wana desa usdm wakiamini ni chuo kikongwe na chenye wasomi wa kubobea
Lakini kinyume chake ni sahihi maamuzi ya ma bwana hawa wasomi waliobobea yanatia shaka sana kwa maamuzi yao mimi nakwenda mbali zaidi kuhoji usomi wao na kubeza elimu yao hawa jamaa sio WASOMI ,Tangu leo natilia msisitizo huo.
kukokotoa ma namba sio usomi huo hata kumputa inazikokotoa namba kwani komputa ni SOMI ama ina phd?
 
Pamoja na kuwa hili limetangazwa na uongozi wa chuo, lakini siyo siri kwamba ni agizo la serikali. Badala ya kuwa na utaratibu wa kukaa meza moja na uongozi wa DARUSO ili kuyazungumza matatizo mbali mbali yanayowakabili wanafunzi wa UDSM na wa vyuo vingine vya elimu ya juu nchini, wameona ni bure waifutilie mbali DARUSO.

Huku ni kufilisika kimawazo hawana sera mpya na kwa uwezo wao finyu waliokuwa nao wanadhani kuifuta DARUSO ndiyo kutamaliza matatizo chungu nzima yanayowakabili wanafunzi wa elimu juu nchini mwetu wakiwemo wale wa UDSM.

Huu ni mwaka 2008 tengenezeni utaratibu wa kukaa meza moja na viongozi wa wanafunzi wa vyuo mbali mbali nchini ili msikie matatizo yao na kujadili njia mbali mbali za kuyatatua matatizo hayo badala ya kuwa na fikra za mwaka 47 na kuwanyima wanafunzi hao haki yao ya kikatiba ya kujichagulia viongozi wao wanaotaka katika vyuo vya elimu ya juu nchini.
 
Jamani sio kila wakati tuwe watu wa kutoa lawama tu pasipo na sababu za msingi, chuo kuamua kuifuta daruso mimi naona wapo sahihi kabisa maana hiyo daruso ilishapoteza mwelekeo wake na ikabakia kuanzisha migomo isiyokuwa na msingi, WHY nimesema hivi:-

Hebu nambieni shuo kimetoa masharti kwa mwanafunzi anayetaka kurejea chuoni ni lazima ajaze forms za kuomba kudahiliwa upya na awe ameambatanisha risiti za ada na awe amemaliza ada yote then azitume kwa registre kabla ya tar 2 january 2009,, wapo waliotimiza haya masharti na wapo wengine walijaza forms na kutokulipa ada wakitegemea chuo watalegeza masharti na watarudi bila kumalizia ada kama ilivyokuwa huko nyuma kwenye migomo mingine, chuo kwa kuwaonea huruma wakawaongezea muda wale ambao walisubmit forms bila kumaliza ada wakawapa mpaka tar 15 january 2009 then tar 16 up 2 17 jan watatoa batch ya pili ya majina ya wale walioweza kufikisha sifa za kurudishwa chuoni, sasa kilichotokea ni kwamba chuo wamekuwa na msimamo mmoja tu kuwa atakayemaliza ada ndiye atakayeruhusiwa kurudi chuo, na asiye maliza basi huyo hataki kusoma. na kwa kiasi kikubwa wanafunzi wameweza kwenda kulipa ada ili waweze kurejeshwa chuoni, sasa haya yaliyopelekea chuo kuamua kuifuta DARUSO ni kwamba:- Juzi tu hapa huyu raisi wa wanafunzi somebody Machibya ameenda kufanya pressconference kuutangazia uma wa wanafunzi wote kuwa ifikapo tarehe 19 January 2009 wanafunzi wote waripoti chuoni wawe wamemaliza ada au hawajamaliza ada waende chuoni na wataingia darasani kama kawaida, sasa hebu niambie wewe ambaye unalaumu why DARUSO imefutwa hii ni kutafuta haki au kutafuta choko choko zisizo na msingi kwa serikali?? Wewe ni nani mpaka utake kutengua maamuzi ya wakuu wako ambao wanakufundisha hapo chuoni na utake kutengua maamuzi ya serikalli? kanini usingekuwa mpole tu? na alipoulizwa kama yeye amelipa au la akasema kwa kujiamini kabisa kuwa hajalipa na hatalipa na chuoni atarudi tu sasa hii ni haki?? wanafunzi wenzako 8000 wameenda kulipa ada wewe unautangazia uma kuwa hutalipa ada na chuoni utarudi tu who are you?? Chuoni kila mtu alienda kwa wakati wake na usia alipewa na wazazi wake na anapofuikuzwa anaondoka peke yake kurudi kwa wazazi wake peke yake hakuna solidarity tena zaidi ya kujawa na hofu utaenda kujibu nini kwa mzazi wako ambaye ni mkulima. Sasa chuo ndo kimeshaamua hivyo no way hakuna DARUSO mpaka hapo itakapotungwa sheria mpya na si daruso tu hakuna society yoyote ya wanafunzi inayotambulika kwa sasa mpaka hapo chuo kitakapotoa utaratibu mpya na kutangaza kwenye gazeti la serikali out off that unajitafutia kuumia tu,, mbaya zaidi nasikia kwamba wamevunjiwa sehemu yao pale nje walipokuwa wanakaanga chips na bar yao walikuwa wanasubiriwa wamalize stock ya vinywaji vilivyopo the waifunge kabisa na ofisi zao walishaambiwa watoe wanachokiona ni chao watafute sehemu nyingine si kwenye majengo ya chuo.

Na pressconference aliyoifanya huyu raisi wa DARUSO ndo imepelekea chuo kutoa maamuzi ya kuwataka wanafunzi wavae kitambulisho watakachopewa upya maana inspection inaanzai getini, unafika pale unaangalia jina lako lipo unaruhusiwa kuingia ndani ya chuo kwa ajili ya registration na unatakiwa kukiacha pale kitambulisho chako cha zamani,, ukiangalia hii yote ni kutaka kuwabana wale ambao wamegoma kulipa ada na wanataka kuja kusoma bure na ndo hao hao waanzisha migomo isiyokuwa na msingi, hebu tufikirie kwanza kabla ya kulalama tu kuna ncho ambayop inatoa elimu bure kwa sasa hivi? ukinambia sweedn, Finland, Norwey nitakucheka maana hao wanakusomesha lakini joto ya jiwe utakuja kuiona huko mbele ukishamaliza shule na umepata kazi so SERA YA UCHANGIAJI KATIKA ELIMU NA AFYA NI LAZIMA na tena nashangaa kwa nini tunakomalia elimu tu na tusikomalie afya iwe free....

Ni hayo tu waungwana si vyema tukaegamia upande mmoja tu kila wakati, madogo wanachemka na ni lazima kaka zao hapa JF tuwaelekeze maana nasi tulipita hapo

Nchi karibu zote za ulaya mashariki ni free tuition fee mfano hapa poland na
unapeleka slary slip ya wazazi wako chuoni wanaigawa pesa wanayopata kwa mwezi kwa wanafamilia wote ikipungua kiasi fulani basi wanakupa na fedha za matumizi ,malazi yani kila kitu.
Na ukifanya vizuri darasani mfano kwa mwisho wa mwaka wenye gpa 4-5
wote wanakula pesa nzuri hapo bila kujali uwezo wa familia.
wenye gpa 3.5-3.9 unakula fungu la kawaida
gpa 3.3-3.5 unakula fedha yako vile vile
Na ukimaliza shule yako hakuna wa kukufuatilia sasa .Hao wa westn country wengi wao wana fedha za kuwasomesha watoto wao usi tulinganishe na sisi bwana.
Watanzania bado sio wanahitaji mkopo bali bado tunahitaji free education kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

Serikali wanabana kitu ambacho hakibaniki na wanadhani kubana watu ili watoe mkopo watasomesha watu wengi kumbe kinyume chake ni sahihi.

Ukisomesha watu bure kwa kujibana ndani ya miaka 10 ktk miaka hii ambapo wananchi wamejuwa nini maana ya elimu baada ya miaka 15 utajikuta unafaida kubwa na umesomesha watu wengi kuliko kulazimisha kukamuwa ng'ombe dume maziwa ama kujaribu kumkopa nyoka miguu.

Mfano ni wengi wenu hapo wazazi walipojibana kuwanunulia uniform za shule za msingi harafu badae ,kasomeshwa bure na MWL Nyerere matunda wazazi wenu wameyaona na jirani zenu wanavuta udenda.

LAkini kwa wazazi wale waliokuwa mkono wa birika badala ya kuwapeleka vijana wao shule kwa kuwanunulia zile shati nyeupe na bukta za kaki ama sketi za blue ama kijani na wakaamuwa kununua ng'ombe ama mbuzi na wakiamini hiyo ndiyo njia sahihi leo wengi wao wakikuona wewe wanajuta.

Serikali iache ubahili na UMANGIMEZA kitendo cha kumwomba JONGOO MACHO si matusi tu bali ni URACIST na U SKIN HEAD na UHOOLIGAN wakupindikia kwanini.
wanafunzi wengi ni watoto wa wakulima na waalimu na wafanyakazi wa halmashauri wakati serikali ikiwalipa baba wazazi wao elfu 70.Na wakati huo huo ikimtaka mzazi huyo atoa atleast laki tano kwa mwaka.Maajabu kabisa
 
Last edited:
Sowing the seeds of revolution/chaos...katika enzi hizi za fikira tofauti ni wazi kitakachofuata sasa ni aina mpya ya siasa za wanafunzi...nachelea kusema kuwa leadership vacuum inayotengenezwa hapo itawasha moto usioweza kuzimika tena....

Tanzanianjema
 
Date::1/14/2009
Daruso yafutwa, sheria mpya UDSM zatangazwa
Latifa Karugila na Hussein Kauli

CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimeweka masharti magumu ya kudhibiti usajili wa wanafunzi waliodahiliwa upya kuingia chuoni hapo kuanzia Januari 19, mwaka huu.

Vile vile, kimetangaza rasmi kufutwa kwa sheria za chuo zinazotambua kuwepo kwa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo hicho (Daruso).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Naibu Makamu Mkuu wa chuo (Taaluma), Profesa Makenya Maboko, ilionyesha kuwa wanafunzi wote watakaotimiza vigezo vya kujiunga tena na chuo, watapewa vitambulisho vipya pamoja na taratibu za namna ya kuishi chuoni hapo.

Profesa Maboko alieleza kwenye taarifa hiyo kuwa, mwanafunzi atakayekutwa ndani ya chuo bila ya kuvaa kitambulisho atakuwa amesababisha uvunjifu wa amani na utulivu, hivyo atachukuliwa hatua za kisheria juu ya kitendo hicho.

"Wanafunzi watakaokuwa wamevaa vitambulisho hivyo ndio watakaoruhusiwa kuingia darasani," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Ili kutekeleza masharti hayo, Profesa Maboko alisisitiza kuwa kila mwanafunzi atakayekamilisha taratibu za usajili atapaswa kupatiwa kitambulisho kipya, vinginevyo hatatambuliwa kama mwanafunzi aliyetimiza vigezo vya kujiunga tena na chuo.

Akizungumzia kuhusu Serikali ya Wanafunzi wa UDSM (Daruso), Profesa Maboko alisema taasisi zote za wanafunzi zilizokuwa zikitambuliwa na sheria ya chuo ya mwaka 2007, kabla ya kusimamishwa kwao, hazitatambuliwa tena.

Alisema taasisi hizo zitapitishwa upya na baraza la chuo na kuchapishwa kwenye gazeti la serikali kwa kufuata sheria zinazokiongoza chuo hicho.

"Taasisi mpya za wanafunzi zitapitishwa upya na baraza la chuo na kuchapishwa kwenye gazeti la serikali kwa kufuata sheria zinazokiongoza chuo hicho," aliongeza Profesa Maboko.

Wanafunzi waliosajiliwa upya watatakiwa kuripoti chuoni hapo kuanzia Januari 19 hadi 22, mwaka huu, kwa utaratibu maalumu uliotolewa na chuo.
Source: Mwananchi 15/01/2009


Uongozi wa UDSM ulichelewa kuifuta hii DARUSO, to me DARUSO haikuwa ikikidhi mahitaji na matakwa ya wanachuo zaidi ya kuwa jukwaa la kuendesha siasa na kuwanyima haki wale ambayo wapo kwa nia ya kusoma. Ifike mahali wanafunzi waelewe kuwa kazi yao hapo UDSM ni kusoma na wale siyo kuendesha Chuo. Kazi za kuendesha Chuo ziachwe kwa Viongozi wa Chuo vinginevyo wanafunzi wanachukua muda mwingi kufanya yale ambayo haya wahusu kimsingi.
Bravo kwa kuifuta DARUSO
 
Ni kosa kubwa kwa mkusanyiko mkubwa wa wanafunzi pale UDSM kutokuwa na chombo chao kinachowaongoza katika mambo mbali mbali ndani na nje ya chuo hicho. Wanafunzi wanaweza kabisa kuunda DARUSO yao ya chini meza na kutaarifiana mambo mbali mbali kuhusiana na yale yanayowapa karaha mbali mbali katika muda ambapo wapo pale kama wanafunzi.
 



Uongozi wa UDSM ulichelewa kuifuta hii DARUSO, to me DARUSO haikuwa ikikidhi mahitaji na matakwa ya wanachuo zaidi ya kuwa jukwaa la kuendesha siasa na kuwanyima haki wale ambayo wapo kwa nia ya kusoma. Ifike mahali wanafunzi waelewe kuwa kazi yao hapo UDSM ni kusoma na wale siyo kuendesha Chuo. Kazi za kuendesha Chuo ziachwe kwa Viongozi wa Chuo vinginevyo wanafunzi wanachukua muda mwingi kufanya yale ambayo haya wahusu kimsingi.
Bravo kwa kuifuta DARUSO

Kama vile kazi za siasa waachiwe wanasiasa na sisi wengine tukae pembeni maana hayatuhusu kimsingi. Na hizi ndio fikira za watanzania wanaolalamika na ufisadi na maisha magumu....

Kazi ipo

Tanzanianjema
 
Nini kifanyike; kwa nini serikali isiwashirikishe kuchangia hawa wanafunzi kwa njia ya mikopo na wahakikishe hiyo mikopo inarudi as soon as they are employed after their education? Tuachane na mikopo waliyokuwa wanatoa mwanzo maana na yenyewe walikuwa wanapeana tu, na sidhani kama hela zote huwa zinarudi; na kama zote zilikuwa zinarudi kwa nini zisizungushwe kwa wanafunzi hawa wanaoandamana kila siku?
Kama wanataka wanafunzi wachangie basi wawapunguzie masaa ya darasani na wa create part-time jobs for the students so they afford it!Period!

DARUSO...nadhani wamesema vyama hivi vinaweza kuanzishwa upya kwa kufuata sheria zilizowekwa na chuo (students included,I would think).That being the case,what's the fuss all about?Wafuate sheria,waanzishe DARUSO upya.Au red-tapeism nako huku.

Mikopo...hii kurudi kwake,kutategemea uwepo wa strategy nzuri ya urudishwaji ingawa mpaka sasa,hili halijafanyiwa kazi ipasavyo.

Naunga mkono hoja ya utolewaji wa work study opportunities for university students.Preferably at their respective campuses.
However,kwa kufanya hivyo,itabidi tufikirie pia njia ya kuaccomodate current employees in areas where students are able and more likely to take over.
Tukiweza kusolve hili (and I haven't given much thought as to how,yet) inawezekana kabisa tukatatua tatizo hili sugu la funding kwa wanafunzi wetu.

Ingawa bado tutahitaji kufanyia kazi attitudes za wanafunzi...maana masista du wenzangu,kakameni kutuona na ufagio kisa tu extra cash to cover for our fees,itakuwa kimbembe!I guess,the vice versa applies.
 
Ukistaajabu ya Mussa, je ya Firauni si ndio utazimia! nakubali kabisa Daruso inamapungufu yake lakini sikubali kabisa uamuzi wa kuifuta. Chakushangaza ukiwakuta walimu wa chuo wanavyoelezea au kuchambua namna ya kutatua migogoro utasema wao ndio kila kitu lakini mgogoro utokee waite watatue utaona madudu wanayoyafanya, zipo hatua nyingine mbadala za kumaliza migogoro ya wanafunzi lakini jamaaa kila kukicha solutions zao ni hizo hizo bila kuzingatia mazingira yanabadilika na watu pia ni tofauti.

Binafsi ningewashauri kubomoa utawala wote wa chuo na kuweka utawala mpya kuliko recycling inayoendelea hapo, na wafanyakazi wa utawala pia wanatakiwa kuondoka niliona wanavyowajibu vijana hapo monday this week nikajiuliza hivi mwanafunzi wa chuo ni mteja au ni mhalifu, kuna chumba no.104 undergraduate noma, utafikiri magereza hao watu waliokuwa humo balaa.

Kufuta Daruso bado hakujatatua tatizo la msingi linaloleta migomo ya kila kukicha, manake Daruso yetu iligoma na ya sasa imegoma na hakuna hata mtu mmoja aliyekuwepo mwaka 2001 leo yuko Daruso lakini migomo kama kawa. Makamu wa chuo na timu yake waache kufikiria majibu rahisi katika swala linalogusa maisha ya watu wengi, kama kazi imemshinda apishe wengine wasongembele.
 
Kosa lingine ni letu wazazi. Vijana wanagoma wakiangalia uwezo wa sisi wazazi wao. Sisi tunakaa kimya kana kwamba hayatuhusu. Tunawasaliti vijana na kwa kufanya hivyo tunajisaliti wenyewe. Tunapaswa kupaza sauti zetu na kumuuliza JK, mbona watoto wa maskini wanakosa elimu wakati ulisema haitatokea hivyo?

Tujiulize pia, hivi watoto wote wanaotaka mkopo wakipewa asilimia 100 kuna shida yoyote? La msingi ni kuwabana walipe, period. Ni kama nataka kulima, naenda benki kukopa, benki inanipa hela za kulimia tu na inasema za kuipanda na kupalilia nijitegemee wakati sina uwezo huo. Je nikilima tu huo mkopo utarudi? Si bora wanikoppeshe hadi gharama za kuvuna na kuuza ili hayo mauzo ndiyo nilipe mkopo?. Serikali tumia akili.

Tatizo linakuwa gumu kwani JK, mkuu wa nchi alitoa msimamo wake mapema sana juu ya suala la sera ya uchangiaji kuwa haitabadilishwa. Ni kosa kubwa kwa rais kutoa misimamo kama hiyo kwani wewe ndiye mkuu kabisa, Sasa tuone kama hatakula matapishi yake.
Akisema sera ibaki hivyohivyo - kala matapishi yake maana watoto wa maskini hawatasoma. akisema ibadilishwe - kala matapishi yake maana alishasema haitabadilishwa. KAZI KWELIKWELI.


Kamakabuzi asante sana kuangalia upande wa pili wa shilingi!

Mimi ni mhadhiri hapo chuo, nimekuwa nikpigana na hali hii, hali si nzuri maana vita hivi viko individuala zaidi, sitashangaa kuona waadhiri wakikaa kimya kuhusu hili swlaa, Yes, kwani wana shida gani?? fedha wanazo!

Wenzangu na mie watu wa chini ndio hao wanapinga migomo, wanawabeza watoto, hali si nzuri jamani!

nashindwa niongee nini, nianzie wapi, kwa namna gani. ila tulipofik hali si nzuri... na wala siamini!

sio siri, naona hata kukaa na kufanya kazi ndani ya hiki chuo, ni kama kutembea uchi wa mnyama! nafikiria kuonyesha reaction yangu ni kuacha kazi mahali hapa, kwa uchungu.

Historia itatuhukumu, hakika itatuhukumu

makanisa yako wapi? misikiti mnafanya nini jamani?, vyama vya siasa mnasubiri nini?, wanaharakati, vyombo vya kimataifa! mko wapi?? nani wa kuwaonea huruma hawa vijana??. tunafanya hivi kwa taifa linaloongoza kwa umaskini duniani? huku wenzetu wakiwaza watoto wasome, taifa liendelee, huku tunawaza kuwadidimiza. fedha zipo za kuwakopesha, ni kipaumbele tu na uzalendo!

WAZAZI AMKENI JAMANI!!!!!!!!!!!

Waberoya
 
Jamani sio kila wakati tuwe watu wa kutoa lawama tu pasipo na sababu za msingi, chuo kuamua kuifuta daruso mimi naona wapo sahihi kabisa maana hiyo daruso ilishapoteza mwelekeo wake na ikabakia kuanzisha migomo isiyokuwa na msingi, WHY nimesema hivi:-

Hebu nambieni shuo kimetoa masharti kwa mwanafunzi anayetaka kurejea chuoni ni lazima ajaze forms za kuomba kudahiliwa upya na awe ameambatanisha risiti za ada na awe amemaliza ada yote then azitume kwa registre kabla ya tar 2 january 2009,, wapo waliotimiza haya masharti na wapo wengine walijaza forms na kutokulipa ada wakitegemea chuo watalegeza masharti na watarudi bila kumalizia ada kama ilivyokuwa huko nyuma kwenye migomo mingine, chuo kwa kuwaonea huruma wakawaongezea muda wale ambao walisubmit forms bila kumaliza ada wakawapa mpaka tar 15 january 2009 then tar 16 up 2 17 jan watatoa batch ya pili ya majina ya wale walioweza kufikisha sifa za kurudishwa chuoni, sasa kilichotokea ni kwamba chuo wamekuwa na msimamo mmoja tu kuwa atakayemaliza ada ndiye atakayeruhusiwa kurudi chuo, na asiye maliza basi huyo hataki kusoma. na kwa kiasi kikubwa wanafunzi wameweza kwenda kulipa ada ili waweze kurejeshwa chuoni, sasa haya yaliyopelekea chuo kuamua kuifuta DARUSO ni kwamba:- Juzi tu hapa huyu raisi wa wanafunzi somebody Machibya ameenda kufanya pressconference kuutangazia uma wa wanafunzi wote kuwa ifikapo tarehe 19 January 2009 wanafunzi wote waripoti chuoni wawe wamemaliza ada au hawajamaliza ada waende chuoni na wataingia darasani kama kawaida, sasa hebu niambie wewe ambaye unalaumu why DARUSO imefutwa hii ni kutafuta haki au kutafuta choko choko zisizo na msingi kwa serikali?? Wewe ni nani mpaka utake kutengua maamuzi ya wakuu wako ambao wanakufundisha hapo chuoni na utake kutengua maamuzi ya serikalli? kanini usingekuwa mpole tu? na alipoulizwa kama yeye amelipa au la akasema kwa kujiamini kabisa kuwa hajalipa na hatalipa na chuoni atarudi tu sasa hii ni haki?? wanafunzi wenzako 8000 wameenda kulipa ada wewe unautangazia uma kuwa hutalipa ada na chuoni utarudi tu who are you?? Chuoni kila mtu alienda kwa wakati wake na usia alipewa na wazazi wake na anapofuikuzwa anaondoka peke yake kurudi kwa wazazi wake peke yake hakuna solidarity tena zaidi ya kujawa na hofu utaenda kujibu nini kwa mzazi wako ambaye ni mkulima. Sasa chuo ndo kimeshaamua hivyo no way hakuna DARUSO mpaka hapo itakapotungwa sheria mpya na si daruso tu hakuna society yoyote ya wanafunzi inayotambulika kwa sasa mpaka hapo chuo kitakapotoa utaratibu mpya na kutangaza kwenye gazeti la serikali out off that unajitafutia kuumia tu,, mbaya zaidi nasikia kwamba wamevunjiwa sehemu yao pale nje walipokuwa wanakaanga chips na bar yao walikuwa wanasubiriwa wamalize stock ya vinywaji vilivyopo the waifunge kabisa na ofisi zao walishaambiwa watoe wanachokiona ni chao watafute sehemu nyingine si kwenye majengo ya chuo.

Na pressconference aliyoifanya huyu raisi wa DARUSO ndo imepelekea chuo kutoa maamuzi ya kuwataka wanafunzi wavae kitambulisho watakachopewa upya maana inspection inaanzai getini, unafika pale unaangalia jina lako lipo unaruhusiwa kuingia ndani ya chuo kwa ajili ya registration na unatakiwa kukiacha pale kitambulisho chako cha zamani,, ukiangalia hii yote ni kutaka kuwabana wale ambao wamegoma kulipa ada na wanataka kuja kusoma bure na ndo hao hao waanzisha migomo isiyokuwa na msingi, hebu tufikirie kwanza kabla ya kulalama tu kuna ncho ambayop inatoa elimu bure kwa sasa hivi? ukinambia sweedn, Finland, Norwey nitakucheka maana hao wanakusomesha lakini joto ya jiwe utakuja kuiona huko mbele ukishamaliza shule na umepata kazi so SERA YA UCHANGIAJI KATIKA ELIMU NA AFYA NI LAZIMA na tena nashangaa kwa nini tunakomalia elimu tu na tusikomalie afya iwe free....

Ni hayo tu waungwana si vyema tukaegamia upande mmoja tu kila wakati, madogo wanachemka na ni lazima kaka zao hapa JF tuwaelekeze maana nasi tulipita hapo

Sera ya CCM imesema wazi kuhusu kuchangia elimu hivyo DARUSO walikua na muda tosha kupiga kampeni kuiangusha CCM kwenye uchaguzi uliopita kama wanapinga sera hiyo. Uhuru wa kusema umeletwa na SERA YA VYAMA VINGI, hivyo DARUSO wajue kua ingekua ni enzi za CCM pekee labda sasa hivi wangekua SERO ama kupigwa viboko.
Migomo inaangusha sana viwango vya elimu na hadhi ya vyuo vyetu hivyo wanachuo waimairishe mbinu zao katika kushiriki kwenye uchaguzi badala ya kupigania kupinga/kugomea ama kubadili sera, wakumbuke tupo kwenye mfumo wa vyama vingi vyenye sera tofauti. Nadhani wanafunzi hawatapenda CCM ipite tena 2010 maana ikipita tena wajue SERA YA KUCHANGIA ELIMU imependwa na wengi, wakiwemo wazazi wao.
DARUSO inavuna walichopanda. Kwa namna yeyote ile, DARUSO ni batili kuendesha mazunguzo na waandishi wa habari kuhusu namna ya kuendesha CHUO. Sera ya kulipia ni ya CCM wala si CHUO na huiondoi sera ya CCM kwa kugomea CHUO bali kwa kuiangusha CCM.
 
Inaelekea watu wengi wanaochangia humu jamvini wanashindwa kutofautisha kati ya DARUSO na UONGOZI WA DARUSO. DARUSO ni jumuiya ya wanafunzi wa chuo kikuu ch Dar es Salaam. Wanafunzi wana haki ya kikatiba ya kujumuika pamoja na haki hii kisheria haiwezi kuporwa na Uongozi wa Chuo.

Sioni ni vipi chuo kinaweza ku-deal na wanafunzi 8000 bila some form of representation. Kuna matatizo mengi yanawapata wanafunzi kama jumuiya ambayo itakuwa vigumu kwa mwanafunzi mmoja mmoja kuyatatua kivyakevyake. Wanaosema DARUSO haijafanya lolote na hivyo haipaswi kuwapo sidhani kama wanaelewa vizuri wanachokisema.

Ni kweli inawezekana kabisa Uongozi wa DARUSO kama viongozi wengine wengi katika jumuiya na taasisi nyingine wameshindwa kutimiza majukumu yao. Lakini hii haiwezi kuwa sababu ya kuiondoa DARUSO kama jumuiya kwa sababu DARUSO si ya viongozi ni ya wanafunzi. Ninachokiona ni jitihada dhalimu za viongozi wa chuo (na serikali) kujaribu kuwatisha vijana hawa na kutengeneza mazingira ambayo maamuzi na vitendo vyao havitaweza kuhojiwa na wanafunzi.

Kwa mfano, huwezi kuweka utaratibu ambao utafanya vijana karibu 2000 kushindwa kuendelea na masomo halafu utegemee watu wakae kimya. Inashangaza na kuhuzunisha kwamba watanzania wengi hili haliwashtui hata kidogo! Leo angalau nimefarijia kuanza kusikia sauti za wabunge wakianza kuhoji na kutaka wanafunzi wote warudishwe chuoni.

Chanzo cha matatizo yanayotokea vyuo vikuu vya umma si wanafunzi pekee. Bodi ya mikopo, wizara (serikali) pamoja na vyuo vyenyewe vinachangia. Mbona hawa hatuoni wakiwajibika?
 
Last edited:
Back
Top Bottom