Cocacola kubandika majina ya watu bila ruhusa/malipo, Jacline Wolper aomba wanasheria kuingilia kati

Mkuu kwahiyo unahalalisha haya yote kwakuwa hawajaenda mahakamani?
HAKI HAIPATIKANI MAHAKAMANI TU

Mkuu unamaanisha haki ipi tena?

Mbona naona inshu simple tu, Coca cola wamewapa taarifa wahusika na wahusika wakakubali Zawadi ya Kopo yenye jina lao...Kama unaona jina lako kubwa Ungekataa mapema.

Sasa mpaka picha unapiga halafu unashtuka baadae kuwa ulitakiwa kulipwa?

Kwanza naona Coca Cola ndio wanawatangaza akina Wolper na Si akina Wolper kuitangaza Coca cola.
 
Kopo limeandikwa 'Wolper'.

Hata kama ni jina lake kweli, ana uhakika gani kaandikwa yeye na si Wolper mwingine?

tatizo ni zile picha za wasanii zinazowaonyesha wasanii katika page ya cocacola, sasa picha yako na jina lako bado utasema wolper wapo wengi duniani? na hizopicha wanapost pasipo idhini yao wenyewe, zenye maandishi share cocke with wolper
 

Sawa


Tuambie ni wasanii wapi hao walipigiwa simu wakagoma kwenda?

Pili kama waligoma kwenda na Coca Cola wakaamua tuu kutumia majina yao bila ridhaa yao which is the proper avenue to air their complains?

Kwa nini wasiwasiliane na hiyo kampuni na kulalamika?

Kama kampuni haiwasikilizi au haitaki kuwalipa kwa kutumia majina yao bila ridhaa yako basi waende kwenye vyombo vya sheria kudai haki yao.

Wao si wanaona wana kesi? Waende mahakamani.

Tunarudi pale pale celebrity ni watu wenye ushawishi mkubwa popote duniani na hawa ndio hutumiwa na makampuni duniani kote kufanya matangazo. Ronaldo analipwa mamilioni ya usd just kwakuvaa viatu vya nike na anapewa viatu hivyo bure..... Why?

Kama maselebu wa Bongo wanaona wanaliwa wachukue hatua za kisheria dhidi ya kampuni ya Coca Cola.

Waache kulalama. Wafanye kama alivyofanya Rihanna.


Sasa kama wanajijua ni "brandy" kama unavyodai wewe si waende kwenye vyombo vya sheria wakadai haki zao kwa "brandy" zao kutumika bila ridhaa yao? Tatizo nini? Kutafuta sympathy mitandaoni hakutawasaidia.


Sasa mjinga nani hapo kama siyo wasanii wa kibongo?

Narudia tena Wolper hakukuta kopo limeandikwa wolper ndio akalalamika maana anajua wolper wapo wengi tu, Coke wenyewe ndio wamempigia simu na kumwambia njoo kwenye hafla tukukabithi bango la kopo la coke lenye jina lako

Umejuaje? Kwa kuamini tuu alichokiandika? Do you have any inside information of what exactly happened, au umedakia aliyosema tuu?

Kwa msanii anayejutambua kwake yeye hii ni biashara sababu jina lake na yeye ni brand ya biashara....period
Kwanini hawakumfuata mwajuma wa mbagala wakauze naye sura mlimani city na mapich ya insta?

Labda wasanii ya bongo hawajitambui. Wangekuwa wanajitambua wasingeishia kulalama mitandaoni bali kuchukua hatua stahiki kudai haki zao.

Why wasanii wakubwa ndio wauze sura kwenye hiyo hafla ya kukabidhiwa? Unahitaji kujua kwa undani maana ya marketing kulijua hili

Sihitaji kujua marketing bse it is relevant here. Issue kubwa hapa ni contratual na IP rights ambazo ni za kisheria. Kwamba Coca Cola wametumia majina yao bila ridhaa yao. In any contract, there must be a consent given by both parties. Sasa kama hawa meselebu wanadai, hawaku-consent majina yao kutumia, then they can sue the company for damages.

Au kama wanadhani kuwa majina yao yanalindwa na intellectual property law, basi wakaishtaki hiyo kampuni for infringing their IP rights kama alivyofanya Rihanna. If Coca Cola has infringed their IP rights, mahakama itaamua kuwa hao maselbu walipwe fidia.


Kwa hiyo huku mitandaoni ndiko haki zinapatikana? Mie nilidhani wako serious kumbe walikuwa wanaonyesha madukuduku yao tuu? Shame on them.

Topshop walipotumia image ya Rihanna bila ridhaa yake hakukimbilia fasta kwenye social media kutoa madukuduku yake kwa followers wake.

Bali alimtafuta mwanasheria akampa ushauri wa kisheria na mwisho kuishtaki Topshop na kushinda kesi na kufidiwa kama dola milioni 5 za kimarekani hivi. That's what I call being clever in using the law to protect your rights na siyo kuishia kutoa dukuduku kwenye mitandao ili kupata sympathy kwa watu ambao hata hawajui what exactly happened.

Kwenye suala kama hili hakuna cha kwenda kwenye social media au kuitisha media conference. That is a waste of time and money.

Ni ufinyu wa kudadafua mambo kunakopelekea watu kuaminishwa eti coke "wanawaenzi" wasanii kwa kuwapatia hayo mabango ya makopo yenye majina yao wakati kumbe wenzao wanafanya marketing kubwa sana

Mjinga ndiye aliwaye.

Binafsi naweza kusema huu ni mwanzo mzuri wa wasanii kuanza kujitambua kwamba wao kama wao na majina yao ni brand

Mwanzo mzuri? Subiri Octoba watakavyoanza kutumiwa na wanasiasa kama kondomu kwenye kampeni za uchaguzi.

Kuwatumia wasanii kama hivyo sio vibaya isipokuwa kuwepo na makubaliano kabla hata kama itakuwa ni bila malipo na si kukurupuka na kupigiwa tu simu eti njoo mlimani city kunaHafla ya kukabidhiwa kopo lako LENYE JINA LAKO

Waliovyoambiwa waende nao wakakurukupa na kwenda bila hata kuhoji. Baada ya kulishwa huko wanakuja kulalama mitandaoni. Waende zao huko.

Tambua coke wakindika juma basi juma neture hawezi kulalamika wala

Sioni la maana ambalo unawashauri hao masebu. If you really like them, if you really want their interests to be protected wasaidie angalao kwa kuwapa ushauri wa maana.

Kuwaambia eti ni sawa kuelekeza madukuduku yao kwenye mitando huwasaidii chochote. Wakishatoa madukuduku yao so what?

Kama kweli wanadhani wana kesi, basi waichukulie hiyo kampuni hatua stahiki. Waiandikie kampuni kutaka ufafanuzi juu ya kutumia majina yao bila ridhaa yao na kuwa wanastahili kulipwa or their IP rights have been infringed.

Kama hawaridhishwi na majibu yao au kama kampuni inagoma kuwalipa, wawape notice ya kulipa, vingenevyo watawapeleka kwenye vyombo vya sheria. Kama kampuni bado ikigoma, waende mahakamani wakadai haki zao huko.

Ila la muhimu ni kupata ushauri wa kisheria kama kweli wana kesi. Maana waki-rely kwenye hizi sympathy zenu na kwenda kudai kichwa kichwa the so called haki zao, watakuja kujuta kwa sababu sheria haina sympathy na hutakuwa mahakamani kuwatetea kwa kuandika kama ulivyoandika.
 
Mbona hiyo iko wazi sana. Rejea sehemu ulizokwepa hoja na kuanzisha mpya. Hali kadhalika sehemu ulizoshindwa hoja ukaamua kwenda kimya-kimya au kutusi wengine.

Wewe umesema nimejichanganya.

Mimi nimekupa changamoto unionyeshe kimahsusi wapi nilipojichanganya, umeshindwa!

Badala yake unaniambia eti nirejee sehemu nilizokwepa hoja.

Kwa kifupi ni kwamba huwezi kunionyesha nilipojichanganya.

Ungekuwa unaweza ungenionyesha tena mstari kwa mstari.
 
tatizo ni zile picha za wasanii zinazowaonyesha wasanii katika page ya cocacola, sasa picha yako na jina lako bado utasema wolper wapo wengi duniani? na hizopicha wanapost pasipo idhini yao wenyewe, zenye maandishi share cocke with wolper

Hiyo page ya Coca-Cola inapatikana wapi?
 

Mkuu ukisoma vizuri lalamiko la Wolper wala halipo kwenye malipo zaidi isipokuwa makubaliano, na ndio maana akatumia neno kuheshimu umaarufu wao

Coke walichofanya ni ujanja wa kutengeneza kwanza hili bango lenye jina mfano pachanya halafu ndio wanakupigia simu kukuomba uje wakukabidhi na wakuchukue picha uziweke kwenye insta yako na social media za coke wanaweka

Wapo wengi walioamini kuwa kwa kufanya hivyo Coke imewaheshimu na kuwatunza zawadi kwa heshima lakini wapo pia waliokuja kugundua kabla na hata baadae kuwa wametumika kutangaza Coke bila kujijua
Hii haiondoi uhalali wa waliojitambua kuhoji "hapa hatujatumika kweli jamani?"

Unaweza kufanya ujinga lakini baadae ukishtuka unajiuliza, sababu next time wengine pia watakua aware wasirudie makosa
So wapo waliokubali hawalalamiki na wapo waliokubali lakini wakakataa kupiga hizo picha na wapo waliokataa kabisaa

Hapa sasa inaonekana kwasababu walikubali basi hakuna hoja ya unyonyaji, unyonyaji upo kwasababu walionyonywa hawajitambui kama wana haki hiyo

Hata siku moja coke haiwezi kumtangaza wolper katu hayo ni mawazo ya kitumwa mno mkuu
Siku zote Coke ndio itawatumia celebrity kujitangaza kupitia fans wao
Unajua social media za hawa zina followers wangapi? Hawa ndio coke imewalenga
Ni sawa na wewe kufungua JF ukakuta bango la Tigo ambao wamelipia jf liwepo pale

Ndio maana nasema uelewa wa watu wengi kuhusu marketing ni mdogo mno na haswa wasanii wetu wenye imani kama yako kuwa makampuni makubwa ndio yatakutumia wewe kukutangaza msanii kumbe wanakutumia wewe kuwatangaza wao

Unajua Diamond analipwa mamilioni mangapi kuitangaza coke? Au ile utaita coke wanamtangaza Diamond?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kwahiyo unahalalisha haya yote kwakuwa hawajaenda mahakamani?
HAKI HAIPATIKANI MAHAKAMANI TU

Sasa kama wamenyonywa haki yao waende kuipata wapi?

Na mahakama zipo kwa minajili gani?
 
Sasa kama wamenyonywa haki yao waende kuipata wapi?

Na mahakama zipo kwa minajili gani?

Haki haipatikani wala kudaiwa mahakamani tu mkuu

Huwezi kuondoa hoja ya msingi sababu tu hawajaenda mahakamani
 

Acha ujinga wewe. Ningekuwa mimi ilikuwa case.
 
Haki haipatikani wala kudaiwa mahakamani tu mkuu

Sasa huku kwenye mitandao ya kijamii ndo wataipata haki yao? Mahakama zipo kwa minajili gani?

Huwezi kuondoa hoja ya msingi sababu tu hawajaenda mahakamani

Hiyo unayoiita hoja ya msingi na yenyewe ina matobo mengi tu.

Kwanza hatujui kiuhakika makubaliano ya hizo pande mbili yalikuwaje maana tayari kuna mkanganyiko. Ukimsoma Le Mutuz (mmoja wa watu waliopewa hayo makopo) na ukimsoma huyo Wolper, masimulizi yao yanakinzana.

Pili, hatujasikia kutoka upande wa Coca-Cola (labda kama wewe umeshasikia) wao wanasemaje.
 
Mkuu kwahiyo unahalalisha haya yote kwakuwa hawajaenda mahakamani?
HAKI HAIPATIKANI MAHAKAMANI TU

Inapatikana wapi then? Instagram?

Halafu hata hukusoma post yote b'se kwani cease and desist letter nayo huwa inatumwa mahakamani?

Kama ulikuwa hujui kwa kifupi ni kwamba a "cease and desist letter, also known as "infringement letter" or "demand letter," is a document sent to an individual or business to halt purportedly-unlawful activity ("cease") and not take it up again later ("desist")"

Je, hao wasanii wanaolalamika majina yao kutumiwa bila ridhaa yao, wameshaiandikia kampuni husika an infringement letter?
 
Mkuu ukisoma vizuri lalamiko la Wolper wala halipo kwenye malipo zaidi isipokuwa makubaliano, na ndio maana akatumia neno kuheshimu umaarufu wao

Oh right. Kwa hiyo suala hapa ni makubaliano siyo?

Kwamba there was no agreement to that effect or there was an agreement, but there has been a breach by one party to the that agreement? Hiki ndicho unachomaanisha?

Let's assume kulikuwa hakuna makubaliano, then hao wasanii watatakiwa kufanya nini?

Or let's assume kulikuwa na makubaliano, lakini kampuni husika is in breach of the agreement.

Utamshauri nini huyu Wolper ukizingatia kwamba anaomba juhudi zihamishiwe kwenye kutetea haki zake?

Kwa maana nyingine badala ya kupiga ramli hapa utamshauri nini Wolper ili aweze kutetea haki zake dhidi ya kampuni husika kutumia jina lake bila ridhaa yake?
 
Huwezi kuondoa hoja ya msingi sababu tu hawajaenda mahakamani

Kama mtu ana hoja ya msingi ya kupinga haki yake kufunjwa, s/he can't just sit there na kuishia kulalama kwa followers wake.

S/he must take concrete actions to defend and protect his/her rights.

You gotta fight for your rights and not just sitting on them, urging for "wanaharakati, wabunge, wanasheria pamoja na serikali" to step into his/her shoes and fight for him/her.

Kama kweli ana hoja ya kutetea haki zake at least atuonyeshe what she has done so far kutetea haki zake.

Kama kuna sehemu amekwama atasaidiwa, but only kama ana hoja ya msingi backed by clear and valid evidence na siyo hizi hearsay.
 

Narudia tena kutokwenda mahakamani hakumfanyi mfanyakosa kuwa yupo sahihi.......period

Tunaacha kujadili kama kunatatizo na tuanze kujadili kwanini hawajaenda mahakamani?
Lipitie vizuri andiko la Wolper utaona ni mtu amabaye anaona kuna kitu hakipo sawa na anahitaji msaada wa ufafanuzi kitaalamu
Lakini mnaishia kumuita malaya na mwenye njaa sababu akina le mutuz wanaona hakuna tatizo
 
Narudia tena kutokwenda mahakamani hakumfanyi mfanyakosa kuwa yupo sahihi.......period

Okay, sasa kwenye hii ishu mwenye makosa ni nani? Na kama yupo, wewe hilo hitimisho umelifikiaje?

Tunaacha kujadili kama kunatatizo na tuanze kujadili kwanini hawajaenda mahakamani?

Ndiyo. Kwa sababu mahakama ndiyo utaratibu ambao tumejiwekea kuutumia endapo tuna matatizo yahusuyo haki.

Lipitie vizuri andiko la Wolper utaona ni mtu amabaye anaona kuna kitu hakipo sawa na anahitaji msaada wa ufafanuzi kitaalamu

Sasa huo msaada wa ufafanuzi wa kitaalamu ndo anauhitaji huko Instagram? Hahahaaaa duuuh!!

Lakini mnaishia kumuita malaya na mwenye njaa sababu akina le mutuz wanaona hakuna tatizo

Mimi sijamwita Wolper malaya na wala sijasema ana njaa.
 
EMT hivi Wolper angeenda mahakamani ndio ungeona madai yake ni valid

Unatumia msuli mkubwa sana kuelezea hatua ya mwisho(mahakamani) badala ya awali ( kosa lipo au la) itakayopeleka hiyo ya mwisho kufanikiwa au la

Ni kama sasa hawana haki ya kulalamika sababu hawajenda mahakamani or the so called blah blah blah latter

Rihana hakukurupuka kwenda mahakamani alikaa na wataalamu wakadadafua wakaona ipo kesi then wakasonga front........ Hichi ndicho anachoulizia wolper kwa watu wenye uelewa na mambo haya
Lakini sasa ninyi mnaojifanya mnajua sana hamutaki kumshauri badala yake mnamuona hana haki sababu hajaenda mahakamani tu

Kwa jicho huru kabisa naomba soma tena alicho andika Wolper then rudi hapa kujibu
She is just a layman anayeona kunakitu hakipo sawa na anaomba utaalamu......thats all
 
Last edited by a moderator:
Hapa kuna mtu alitumia id yako?

Hii inaonyesha upo kiubishani zaidi

Unaona sasa usivyo makini?

Wewe umenukuu bandiko langu nikimjibu huyo jamaa aliyeleta kiunganishi cha Mange.

Ndo mimi nikamjibu hivyo kwamba huyo changudoa (Mange) hakuna analojua.

Rudi tena kwenye hilo bandiko ubofye hicho kiunganishi alichokiweka jamaa uone kitakupeleka wapi.

Hakuna nilipomwita Wolper malaya. Hakuna. Hakuna. Hakuna.
 
Nimeamua kukusaidia.

Sasa hebu bofya hicho kiunganishia (kinachosema "COCA COLA YAWANYONYA WASANII WA TANZANIA") alichokiweka HarakatiNews halafu unambie kinakupeleka wapi.

Ok
Mi naomba kujua mtazamo wako
Je kwa mtazamo wako hicho wanachofanya Coke kupitia hawa wasanii wakubwa kibongo bongo sio promo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…