Cocacola kubandika majina ya watu bila ruhusa/malipo, Jacline Wolper aomba wanasheria kuingilia kati


Ok nini? Umekubali kwamba umechemka?

Mi naomba kujua mtazamo wako
Je kwa mtazamo wako hicho wanachofanya Coke kupitia hawa wasanii wakubwa kibongo bongo sio promo?

Kwa mtazamo wangu ni promo.

Lakini hawatumii wasanii tu.

Wanatumia mtu yeyote apendaye jina lake liwepo kwenye chupa au kopo la soda zao.
 
Ok nini? Umekubali kwamba umechemka?



Kwa mtazamo wangu ni promo.

Lakini hawatumii wasanii tu.

Wanatumia mtu yeyote apendaye jina lake liwepo kwenye chupa au kopo la soda zao.

Kama unakubali ni promo na msanii anapotumika kwenye promo anategemea malipo sasa tatizo la Wolper kuhoji wmetumika kijanja ni nini?
 
Kama unakubali ni promo na msanii anapotumika kwenye promo anategemea malipo sasa tatizo la Wolper kuhoji wmetumika kijanja ni nini?

Mtu yeyote kutumika katika promo si lazima apate malipo na kwa mantiki hiyo si lazima ategemee malipo.

Ndiyo maana nimekuwa nikihoji kama kuna watu humu waliousikia upande wa Coca-Cola ukisema nini kuhusu suala zima.

Ndiyo maana nimeuliza humu kama kuna ambaye anayajua makubaliano au maafikiano ambayo pande zote mbili ziliyafikia, hakuna aliyejitokeza na kusema anajua zaidi ya Le Mutuz ambaye alikuwa mmoja wa waliopewa hayo makopo.

Na alichokisema Le Mutuz humu kinakinzana na kinachosemwa na wengi. Yeye (Le Mutuz) kasema waliohusika na kuchagua majina ya watu kuwekwa kwenye hayo makopo ni kampuni ya ICL na si Coca-Cola wenyewe.

Na kaongeza kuwa hao ICL waliwasiliana na hao watu na wakawaeleza kinachoendelea. Waliokubali walipewa hizo 'zawadi' zao na waliokataa hawakupata kitu hivyo na picha hawakupigwa.

Binafsi nahitaji taarifa zaidi ili niweze kuhitimisha kama kweli kuna unyonywaji au la.

Lakini vilevile nashangaa kuona baadhi ya hao waitwao wasanii, watu ambao mtu ungedhani wana tajiriba ya kutosha na mambo ya mikataba na makubaliano, badala ya kwenda sehemu husika kudai haki yao, wanakimbilia kwenda kwenye mitandao ya kijamii na kulialia.
 
Reactions: EMT

mbona kitu kirahisi hivyo......hii comment ilipaswa kumaliza huu mjadala
 
Mtu yeyote kutumika katika promo si lazima apate malipo na kwa mantiki hiyo si lazima ategemee malipo.

Hapa sasa inategemea wewe msanii au mtu yeyote uanajithaminisha vipi
Do you worth to be paid for promo?
Lemutuz kaona ni "heshima" kupewa hivyo hastahili kulipwa, its ok, no offense
Na Wolper kajithaminisha kaona anathamani ya kulipwa kwa hilo NI HAKI YAKE PIA
 

Mkuu haijalishi Coke walifanya wenyewe direct au walitumia kampuni kufanya hiyo kazi
Kinachojali ni hapa kuna unyonyaji wa wakijanja kutumia wasanii

Kimsingi Coke hawahitaji kuja kujibu lolote sababu waliokubaliana na "zawadi hiyo ya heshima" hawajalalamika zaidi ya kutoa ASANTE KUBWAA kwenye social media zao huku wamekenua meno

Kilichopo ni kwamba le mutuz amegeuka mteteZi wa Coke
Wengi wenu bila kujijua mmepanga foleni nyuma ya Le mutuz na kuanza kushambulia waliohoji kuna harufu ya unyonyaji

Msando kiroho safi kabisa akawashauri anaowasimamia wasishiriki hadi kuwepo maelewano
The next move Lemutuz kaanza kumshambulia Msando eti wakili wa IG anawapotosha wasanii kwenye hii "GOLDEN OPPORTUNITY"
Yaani le mutuz amelivalianjuga utadhani wakili wa coke, kifupi anataka watu wote wafikiri kama anavyofikiri yeye
 
Narudia tena si kila dhuluma lazima imalizwe mahakamani
Wasanii ni watu wakawaida tu kama wewe, kuwa msanii tena wa kibongo hakumaanishi unajua sheria na mikataba

Instagram na social media zingine kwa dunia hii ni sehemu ya maisha ya wasanii, kusema wanalilia insta sio sahihi maana huko wanashare kila kitu na fans wao

Hivi wewe hujasikia huko uliko mara kibao wasanii wanalalamika kwenye social media zao labda fulani kaniibia beat yangu nk?
Ila ikifanyika bongo ni kulialia
 
Unapoiambia serikali ikutetee ni sawa na kuipa coca cola muda wa kuendelea na mauzo kwa hilo jina lako.


Coca cola hawana wasi wasi maana hata hakimiliki kwenu ni shida na mnapenda kuandikwa bila manufaa.

Igeni mifano ulaya, utajiri wa 50 ulitokana na mauzo ya coca cola kwa sehemu kubwa.
 

Haueleweki
Wananyonywa na wakiomba msaada serikalini hutaki lakini unataka wafaidike kama 50cent

Mnaojua haya mambo toeni ufafanuzi na sio na nyie mnaishia kutuhumu tu
 
Mi nadhani watanzania wanashindwa kuelewa, hapa coca cola walichokifanya ni kuwapa heshima wasanii na wtu wetu maarufu, kumbuka hii ni poromo pia kwa watu hao, kwani coca cola wanashida gani na jina lako, wao wameona watoe heshima, acheni hizo
 

Sio tz tu hata Kenya vibandiko (visude) vyote vya coka vina mjina ya watu sijaelewa nini kinaendelea
 
hueleweki,what is your point?
 
Narudia tena si kila dhuluma lazima imalizwe mahakamani

Humalizwa wapi sasa? Kitaa?

Wasanii ni watu wakawaida tu kama wewe, kuwa msanii tena wa kibongo hakumaanishi unajua sheria na mikataba

Kama hujui hata ABC za mikataba na sheria zinazoongoza fani yako basi hustahili kuwepo kwenye hiyo tasnia. Tafuta shughuli zingine za kufanya.

Instagram na social media zingine kwa dunia hii ni sehemu ya maisha ya wasanii, kusema wanalilia insta sio sahihi maana huko wanashare kila kitu na fans wao

Mtu anayekimbilia kwenye mitandao ya kijamii kwenda kulalamika ni anatafuta huruma tu huyo.

Hivi wewe hujasikia huko uliko mara kibao wasanii wanalalamika kwenye social media zao labda fulani kaniibia beat yangu nk?

Huku Ikungulyabashashi sijawahi kusikia.

Ila huko majuu huwa nasikia mara kibao tu wasanii wakiwashitaki mahakamani watu mbalimbali.

Majuzi tu hapa Beyonce kashitakiwa kwa kutumia sauti ya mtu kwenye wimbo wake wa 'drunk in love' bila idhini ya huyo mtu.

Bofya hapa uisome hiyo habari.

Na kama ukitaka naweza kukuwekea habari zingine hata 1,000 za wasanii wakiwashitaki watu mbalimbali kwa kutumia utambulisho wao bila idhini yao. Nikuwekee?
 

umenena vyema.
 
EMT hivi Wolper angeenda mahakamani ndio ungeona madai yake ni valid

Sasa tutajuaje kama madai yake ni valid? Kwa kulalamika tuu mitandaoni? Au kwa kusikiliza hoja ya upande mmoja na kuishia kuweka conclusion?


Unatumia msuli mkubwa sana kuelezea hatua ya mwisho(mahakamani) badala ya awali ( kosa lipo au la) itakayopeleka hiyo ya mwisho kufanikiwa au la

Nyie mnaomtetea ndo mnatumia msuli mkubwa. My simple argument is that kama kweli anadhani ana kesi badi achukue hatua za kisheria. Msuli hapo upo wapi?

Ni kama sasa hawana haki ya kulalamika sababu hawajenda mahakamani or the so called blah blah blah latter

Kuishia kulalama bila kuchukua hatua stahiki ni sawa na bure. Of course, sishangai wewe kusema hivyo bse Watanzania ndiyo tulivyo. Tunapenda sana kulalama, lakini ikifika wakati wa kuchukua hatua stahiki haonekani mtu.


Yes Rihana hakukurupuka kwenda mahakamani alikaa na wataalamu wakadadafua wakaona ipo kesi. Sasa Wolper kafanya hivyo? Au kulalama mitandaoni ndo kutokukurupuka?

Kwa kweli siono hata unachojaribu kutetea hapa zaidi ya kukubaliana na mimi probably bila hata kujijua kuwa kama Wolper anadhani ana kesi, then badala ya kulalama mitandaoni afanye kama alivyofanya Rihanna kwa kutafuta washauri wamshauri kama ana kesi na kama anayo basi awapeke wahusika mahakamani.

Kwa jicho huru kabisa naomba soma tena alicho andika Wolper then rudi hapa kujibu She is just a layman anayeona kunakitu hakipo sawa na anaomba utaalamu......thats all

Yes, she just a layman na huko insta siyo ofisi za malawyer ya kuomba utaalamu.

Hawa maselebu wa Kibongo wanatafuta sympathy tuu. Ukienda YouTube, kuna watu wameweka video zao kibao possibly bila ridhaa zao lakini umeshawasikia wakiilalamikia Google kwa hizo video kuwepo youtube bila ridhaa zao?

Au unataka kuniambia kuwa video zote za wasanii wa kibongo kule YouTube zimewekwa baabda ya kupata ridhaa yao?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…