Comment 1 kwa kina kuhusu Tiba ya Asili ya tatizo lolote, ambayo 100% unahakika nayo kwa shuhuda binafsi

Ni kweli, nyongeza kwa wale ambao wajomba zao wapo mbali na mpwa wake shangazi pia anaweza kuwa mbadala. Njia nyingine ni hii.

CHUNGU CHA MOTO KAMA TIBA YA UDENDA KWA MTOTO MCHANGA.

Mtoto anapotimiza miezi 3 na zaidi hili tatizo linaanza
Chukua chungu cha udongo kiweke jikoni bila kitu chochote(kikiwa tupu),kiache jikoni kwa dk 30 au zaidi au pungufu kulingana na ukali wa moto.

Kikipata moto vizuri kiipue,weka chini mahali salama mchukue mtoto muinamishie kwenye chungu kabla hakijapoa,udenda ukidondokea kwenye chungu utakauka haraka sana kwa sababu ya chungu ni cha moto na mtoto udenda wake utakauka mdomoni atakuwa hatoi tena udenda.

NOTE: Fanya kwa uangalifu isiwe ni ajali ya maumivu kwa mtoto, usimuinamishie sana kiasi kwamba akapata jotojoto la mvuke wa chungu, kinachotakiwa ni udenda tu udondokee kwenye chungu cha moto.
 

Mkuu sasa matumizi unaweza hata kwa kula kibichi au mpaka pia uchemshe kama suala la mafua?
 
Ukiungua kwa uji, maji ya moto, kurukiwa na mafuta wakati unapika etc paka mafuta ya babycare. Maumivu yatakuwepo kwa masaa ila malegelege hayatatokea kabisa.
 
Unakula majani, mizizi au shina? Mibichi au unachemsha? Kwa wiki au mwezi? Glass moja au zaidi au pungufu?
Magome unabandua unachemsha, glas 3 kwa siku hadi pale utakapohisi kiungulia mara kwa mara ni dalili au ishara ya kuondokewa na kisukari hivyo nenda hospitali kahakikishe kama tiba imefanya kazi,tumia ujuzi huu kuwatibu wengine pia.
 
Kama una tatizo lololote la ngozi upele,mba,chunusi,mpauko na harara kula kabichi week unaikaanga bila kuchanganya na chochote zaidi ya kitunguu unakula ila kama waweza tafuna mbichi ni bora zaidi ndani ya week matokeo utayapata.

Angalizo chunga msije sababisha zikapanda bei
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…