CONFIRMED: Manara alikuwa anaihujumu Simba SC

CONFIRMED: Manara alikuwa anaihujumu Simba SC

Leo kwenye kipindi cha sports HQ kinachorushwa na E-fm aliyewahi kuwa msemaji wa club ya simba 'simba sports club' Ndg. Haji Manara ameweka bayana kuwa hajawahi kuipenda club hiyo na hajawahi kuwa miongoni mwao. Kwa kinywa chake haji manara amesema "sijawahi kuwa simba"

Itakumbukwa kuwa ni wiki chache zimepita tangu msemaji huyo aaminishe mashabiki wa simba na Watanzania kuwa aliipenda club hiyo kutoka moyoni na kuwa alijitolea kwa nguvu zake zote kwa jasho na damu kuipigania kufa na kupona hadi kufikia hapo ilipofikia.

Lakini kwa kauli yake aliyoitoa leo naungana na wana soccer wengine kuamini pasina shaka kwamba huyu bwana alikuwa yupo simba kwa kazi maalum ya kuhijumu na baada ya kushitukiwa na kutimuliwa ameamua kujitangaza hadaharani kwa kinywa chake mwenyewe.

Kufuatia kauli yake hiyo, mimi kama mdau wa soccer na mkereketwa wa Dar es Salaam Young africans 'Yanga' naishauri kuwa makini na huyu mtu kwa sababu 'what goes around is what comes around'. Kama mtu huyu huyu alitumiwa na wao kututukana na kutukejeli leo amewageuka wale wale waliomtuma na kumlipa kututukana basi ipo siku hata sisi atarudi tena kutugeuka na kututukana vile vile na hapo ndipo msemo wa "what goes around is what comes around" unapodhihirika. Tuwe makini na huyu walking bomb he can erupt anytime.
Katika maisha kuweka akiba ya maneno ni jambo muhimu sana.
 
Wakati mgumu ni kwa nyie, lakini yeeye account yake inasoma ana wakati mgumu upi?mbona ktk maisha ni mambo ya kawaida tu, ni wanasiasa wangapi walitukana sana walipokuwa leo wako wapi?sembuse taaluma?
Hata kama unapokea Millions of money kama huna amani ya moyo, ni kazi bure

Tafakari chukua hatua
 
Halafu nimegundua humu jf kuna misukule inajidanganya eti manara msukule mwenzao anawavuruga wapenzi wa mnyama ukipenda tuite "kolo" ...mngejua tuna enjoy sana na jinsi msukule wenu ujavyopata taabu!

Tunawasubiri uwanjani msaliti alishamaliza kazi yake tukamtimua
Manara anawavuruga Kolo FC hatarii
 
Barbara aliona mbali sana kutimua huyu lopo lopo.

Hawa ndiyo walikuwa wanatoboa chombo wanachosafiria wote.

Huyu asijibiwe kitu ajione mjinga, na kuna mahali Simba wanamtegea akiingia tu king kaisha.
 
Katika maisha kuweka akiba ya maneno ni jambo muhimu sana.
Huyu mwenzetu yanamtoka tu anasahau kama kuna leo na kuna kesho hata hivyo acha tuone huko mbele itakuwaje maana kama ni kuharibu ameshaharibu beyond the repair
 
Barbara aliona mbali sana kutimua huyu lopo lopo.

Hawa ndiyo walikuwa wanatoboa chombo wanachosafiria wote.

Huyu asijibiwe kitu ajione mjinga, na kuna mahali Simba wanamtegea akiingia tu king kaisha.

Nawashauri watani zangu muendelee kumlia buyu hivyo hivyo mkimjibu ni mtakuwa mnampa headlines hasizostahili na tangu ajiunge kwetu naona anawazungumzia nyie tu badala ya kuizungumzia club yetu na kama uongozi utaendelea kumchekea ipo siku ataitumbukiza club kwenye migogoro na taasisi mbali mbali kwa sababu ya uropokaji wake
 
Kuna ile miduanzi sijui inajisikiaje ilikuwa inamtetea Manara. Yaani jitu linasema kabisa kwamba manara ndiye Aliyemfanya kuwa shabiki wa simba doh
 
Manara anawavuruga Kolo FC hatarii
Manara anaongea weeeeeee simba ipo kambini,wanakula kulala na ku train vizuri,manara anaongea weeeee Simba wanazindua jezi zao,Manara anaongea weeeeeee Simba wapo busy kuandaa tamasha lao! Halafu mbaya zaidi hakuna kiongozi amabae anamjibu,anajibiwa na washabiki tu,tofauti kipindi kile alikuwa mwakalebela anamjibu wakati anaisema yanga! Ajabu mkuu unakuja kusema eti Haji anawavuruga kolo(simba) kivipi sasa anawavuruga wakat kila kitu kinaenda sawa?
 
Hizo ni kauli tu...yule yupo kibiashara zaidi
Kama yupo kibiashara naisikitikia club yangu ya yanga maana anaweza kuvujisha siri zetu za ndani endapo atawekewa dau na timu pinzani.
 
Hapo utakuta kapewa hela ili ayaseme hayo
Njaa mbaya sana especially kwa mswahili anauza utu wake kwa lolote lile
 
Back
Top Bottom