CORD Raises Credibility Concerns Of Results Being Released.

Duh, kaazi kweli kweli, sidhani kama Raila akishindwa atakubali kiulaini, hali ya hewa imeanza kuchafuka!
 
Jamani tokea asubuhi matokeo ni: Uhuru 53.38/% -Raila 42.04% mbona haya matokeo hayaongezeki? halafu kwenye taarifa yao Citizen kila baada ya dakika kadhaa wanasema wanataka kila mtu akubali matokeo kwa lolote litakalo tokea!
 
Kutoka kule Boma wamedai watu waendelee kua na subira matokeo rasmi ni hapo kesho!
 
Halafu hawa Citizeni katika front page yao ya TV yao wameweka neno KIVUMBI 2013! Hili neno linaashiria maana mbaya sana! Tusubiri tuone.
 
hahhahahahahahahahahahhaha mkuu hujasikia Mnyika anasema kamiss maandamano so analianzisha soon mpaka kwa waziri wa maji.

Wewe nawe unaboa sana sasa! Haya ya CDM hapa yamefikaje? Ndio nyinyi tunaosema mmesahau mpaka kuhudumia familia zenu kisa,uchaguzi wa Kenya aaarrrgh!
 
Halafu hawa Citizeni katika front page yao ya TV yao wameweka neno KIVUMBI 2013! Hili neno linaashiria maana mbaya sana! Tusubiri tuone.

Wakenya si unajua kiswahili mgogoro kwao wahurumie.

Kuna jamaa yangu mmoja mkenya alifaulu mtihani, mbongo akamwambia hongera. Jamaa mkenya akajibu hongere baba Moi. Yaani jamaa alikuwa anajua sentensi yenye neno hongera lazima iishie na baba Moi. Alikuwa hajui matumizi ya neno hongera...

Na ile story ya kingunge Moi si unaijua? au story ya mahayati.
 
tusubiri kidogo tu mungiki wataanza kazi. very soooooooooooooooooon
 

Duh! Africa...
 
Nimekuwa nafuatilia mtiririko mzima wa matukio yanayoendelea huko haiashirii mwisho mzuri kuna dalili ya machafuko kuzuka tena mwaka huu tuombe Mungu apishile mbali.Hivi ni kwa nn ukabila unawatesa sana wenzetu?litawagharimu sana hili wakae chini watafakari tena jinsi ya kuuondoa ukabila Kenya.Tusubiri na tuone.
 
Wakikuyu wakikuyu i hate them these viroboto
 
KUFICHULIWA KWA SIRI KUBWA ZA UCHAKACHUAJI WA MATOKEO YA
UCHAGUZI MKUU NCHINI KENYA YASABABISHA MATOKEO YOTE
YA URAIS KUSITISHWA MARA MOJA KUTANGAZWA


Matangazo ya kura za urais nchini Kenya zasitishwa ghaflla mpaka hapo kesho tangu KUFUJA KWA UCHAKACHUAJI MKUBWA wa matokeo na Injinia asiye mwaminifu pale makao makuu ya kampuni ya simu nchini humo SafariCom.

Kila mahali hadi hivi sasa ni watu kuchanganyikiwa hasa katika kundi lililokua likipendelewa na hayo matokeo ya kuchonga. Pamoja na yote, watu wengi wameonyesha kushangazwa sana na matamshi ya Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Kinana, kule kukimbilia kwake kuhimiza vyama vikubali matokeo ilhali akifahamu kashfa hii nzito tayari imesababisha tume kushitisha matangazo zaidi ya matokeo.

Sote tuendelee kuwaombea majirani zetu kamwe wasisukumwe tena kwenye vitendo vya umwagaji damu kwani Mwenyekiti wa Tume ameweka wazi kwamba kamwe hatoendelea tena kuyatumea matokeo toka SafariCom.

Naam, kwa taarifa zaidi hatua hiyo ya tume imeelezewa kufikiwa kufuatia kwa kujulishwa kwao kutokea kuchezewa kwa kiasi kikubwa hivyo kaahidi kutangaza matokeo rasmi hapo kesho moja kwa moja toka kwenye makaratasi toka mashinani
.
 

Tupe source mkuu, hizi story za namna hii kila anayeshindwa anaweza kuzitengeneza ili kupata huruma ya jamii. Please, kwa maslahi ya wakenya na kwa ustawi wa wakenya acheni kueneza uvumi wa aina hii, ambao utasababisha hasira zisizo za lazima na kupelekea kuuana kama kwa mwaka 2007. Tafadhari kama hakuna reliable source, tusiendelee kuweka kwenye mitandao habari hizi.
 
Kule kuna ccm wana engineer wizi ndiyo maana wakajifanya kukaa kimya. IT Engineers wa hapa wapo huko na wanafanya kilekile walichofanya Tz, isitoshe Uhuru ana hela kama mchanga wa ufukweni mwa ziwa Tanganyika, na rushwa Africa ndiyo iko kileleni!
 

Mkuu,
Ni kweli kabisa maana JamiiForums yetu ni ya viwango na hivyo ''Vyanzo/source'' ya habari inatokea wapi ni muhimu.

Maana mitandao ya kijamii Kenya mingi wakati huu wa uchanguzi wa 2013 Kenya imefungiwa kwa kukosa viwango vyetu vya JamiiForums ya Tanzania.

Hivyo inawezekana jamaa zetu waKenya wamekosa mahali pa kupandikiza taarifa zisizo sahii kupitia JamiiForums.
 
sasa mbona wananchi watakuwa wameshajua, wewe si umeitoa hiyo siri humu jF na wakenya wengi ni members humu?
 
Sometimes, ni bora hata ya ukabila, angalau kunakuwa na mipaka kati ya kabila moja na lingine, kuliko udini ambapo mnaishi kwenye maeneo mchanganyiko. Yaani yakijatokea machafuko ya kidini Tanzania, hali yetu itakuwa mbaya mara kumi ya ilivyokuwa Kenya.
 
Source: Uwezo Tunao. Cha zaidi kafuatilie kama kuna matangazo zaidi ya matokeo ya Urais nchini humo tangu usome taarifa hii humu.

Tume sasa kutangaza matokeo kuanzia hapo kesho kwa kutegemea na kutumia makaratasi na wala si zile za ki-elektroniki ambazo tayari zimechakachuliwa kule SafariCom.

 

Kwahiyo unadhani Mombasa hakuna wakikuyu au Eldoret hakuna wakamba?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…