Hata kama nitaonekana kwako ni mpuuzi hio hainifanyi kuacha kuuonyesha huo upuuzi wangu kila unapoleta upuuzi wako utapata jibu la kipuuzi toka kwangu.
Hujaelewa .Wewe hujui kuwa si lazima inayosemekana ni dawa itibu hayo anayejiita mzinduzi anasema inatibu?
Kwani ile ya Madagascar haikuzinduliwa? Kwani yaliyosemekana inatibu hayakusemwa? Mbona baada ya kuifuata kwa mbwembwe walioileta waliufyata kama hawakuwahi hata kuisikia?
Vipi mzee mzima babu wa loliondo? Kwani hakuwa na dawa na orodha ya alivyokuwa akitibu?
Kamwulize jiwe na wenzao walioonekana wakifakamia vikombe vya jero jero kama maswahiba yao yaliyowafikisha huko kama yalitoweka, kwisha au hata kupata nafuu.
Nani asiyejua kuwa aliyesema za kuambiwa changanya na za kwako aliona mbali sana?
Hujaelewa .
Mnaosema korona haipo ile dawa nibya nini?
Hapana ndugu, tunataka serikali itoe tamko kuwa nchi inakabiliwa na janga la corona na iwatake wananchi kuchukua tahadhari moja mbili tatu. Si lazima iwe lock down kwani huko kwa wenzetu wenye nazo walishindwa.Hivi mnaotaka Serikali iseme kuna CORONA mnaotaka iweje?baadhi wanataka Serikali ikiri na kuchukua hatua kali km lockdown na tuletewe misaada/kukopeshwa chanjo.Hatua ya Serikali kutokukir ni bora zaid.KAMA mtu anataka Karantin ajiweke mwenyewe.