Tetesi: Corona inapukutisha watu Dar. Kuna wanaolalamika ndugu zao kuzikwa kinguvu na Mamlaka Dar huko Bahari Beach, Buza na Mbweni

Angalia tena video ya jana

Hakuna mpambe nyuma yake

Mkutano umefanyika ndani ya nyumba lakini kajipa distance ya kutosha na wakuu wa vyombo vya ulinzi na sidhani ata kama alienda kuwapa mikono baada ya kuongea nao

Hao wakuu wenyewe wamepeana big gap kwenye meza zao

Sasa kama wanaamini Corona sio tatizo kwanini wajihami ivyo.

Abiria chunga mzigo wako
 
Hizi mindset za kuwaza upinzani ni sawa na corona kweli tuna safari ndefu.
Ninyi wanasiasa pande zote ni tatizo kuliko hata hiyo corona yenyewe, kuna wakati nawaza labda mna mbingu yenu. Nyakati zote ninyi kwa kila jambo mnawazia ustawi Wa itikadi zenu ambazo hata hazieleweki hasa mnalenga nini zaidi ya kuboresha maslahi yenu kwa migongo ya wananchi wenu. Issue hii haihitaji hizo porojo zenu hata kidogo lakini hamshtuki asilani.
 
inawezekana haupo Dar wewe. na kama upo Dar basi Chanika huko!
 
Mkuu hivi ndugu wa dk Ulimboka, Lissu na wengine walilalamika wapi? Mie sikumbuki eti
 
Mkuu siyo kwamba immunity haikioni bali immunity at that age inauwezo mkubwa wa kupambana na vinelea vya magonjwa ukilinhanisha na hao walioenda umri.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nilihisi hivyo hivyo kwamba kwakua watoto wadogo bado immunity yao inaendelea kutambua vimelea basi ni rahisi kwa immunity yao kudetect hivi virusi hata kabla havijaingia kwenye seli. Ila sijaprove hicho ninachohisi.

Sasa tumefeli wapi kujifunza juu ya hili? Kwamba watu wa umri huo dunia nzima immunity yao works the same? Na tunatofautiana, rangi, lishe, makazi n.k
 
Hali ni mbaya, tujitahidi kunawa mikono mara kwa mara na kuvaa barakoa.
 
huyo jamaa yako ni nani mbali na jina, naomba kujua
 
Kwa lugha nyingine ulikiwa waambiwa hiyo virus haina tiba hivyo jaribu kutumia njia mbadalabkadiri uwezavyo ili mradi tu uendelee kuishi...

Kwenye suala la uhai hauhitaji hadi uambiwe na mtu/Rais ni jinsi gani unapaswa kufanya ili uendelee kuwa hai, jilinde na uwalinde wanao kuzunguka kadiri uwezavyo...
Mimi bado nina mshangao tu kuwa Rais amesema tujifukize sijui kawaza nini mheshimiwa
 
Hahaha...

Sasa sehemu kama hiyo inaweza geuka jehanamu, akiupata mmoja tu huko au mtu akiupeleka tu huko...balaa litaanzia hapo
Kuna jamaa yangu kaichukua familia yake yote ameipelekea Mafia kisiwani

Kanipigia anasema sehemu pekee salama kwa sasa ni huko

Nami nimemuahidi hata kwa kuogelea nitakwenda na wapendwa wangu
 
Hahaha...

Sasa sehemu kama hiyo inaweza geuka jehanamu, akiupata mmoja tu huko au mtu akiupeleka tu huko...balaa litaanzia hapo
Huko kisiwani jamaa kakodi nyumba nzima iko nje kabisa ya mji maisha yako chini sana amefanya manunuzi ya chakula cha mwezi na nusu hadi miwili hakuna cha daladala ni mwendo baiskeli tu
 
CIA wanajua ukweli unaofichwa na viongozi wetu ndio maana wakaamua kuondoa wamarekani wote juzi
 
Kuna jamaa yangu kaichukua familia yake yote ameipelekea Mafia kisiwani

Kanipigia anasema sehemu pekee salama kwa sasa ni huko

Nami nimemuahidi hata kwa kuogelea nitakwenda na wapendwa wangu
Hilo ndio linalotakiwa sasa, siyo kila siku mnatupigia kelele humu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabla ya corona hapakuwa na ambulance hapo dar?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tembeleeni usiku wa manane sehemu zilizotajwa kama Buza makaburini mkajionee
Bahari beach eneo la kondo Buza na Mbweni acheni kusifia mapambio ya mwami wa kihutu anaetupeleka kuzimu

Watu wanaokufa ni wengi sana aisee anakoongelea mfano Makaburi ya Kondo kila siku usiku wanazika zaidi ya watu wanne ......jana kuna mtu ndugu yao kazikwa pale Wachimbaji wakawaambia washazika zaidi ya 30 hadi jana ....sasa acha hayo makaburi mengine yakiwamo ya Mloganzila ...watu wanaotangazwa ni wale ambao ni public figure.
Lakini pia kuna kashfa ya watu wanaokufa kwa CONVID19 na ndugu zao wanafanya ujanja ujanja wanaachiwa wakazike wenyewe ......kuna ex IGP kapewa mke wake akazike na wengine wengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…