#COVID19 Corona Tanzania ni vita kati ya Mungu na wasiomwamini kuwa aweza shinda Corona Mungu atashinda hajawahi shindwa

“Mwamini Mungu, lakini mfunge vizuri Ngamia wako”-Mtume Muhammad SAW.

Mungu huwa halipi maombi bali hulipa jitihada!Kupiga maombi wakati hakuna mipango pamoja na vitendo(Actions) madhubuti vya kupambana na Corona ni kumkejeli Mungu.
 
Upo sahihi sana ndugu yangu. Kikubwa ni imani thabiti kwa Mungu wetu huku tukifuata maelekezo yote kutoka kwa wataalamu wetu (wizara ya afya).
Mungu daima milele ndo maana amekupa akili ujitambue na kutatua matatizo yako na kutatua kwa kutumia chanjo!
Ukifa kijinga atakuhukumu kwa ujinga wako!UJINGA NI DHAMBI!
 
Mungu daima milele ndo maana amekupa akili ujitambue na kutatua matatizo yako na kutatua kwa kutumia chanjo!
Ukifa kijinga atakuhukumu kwa ujinga wako!UJINGA NI DHAMBI!
Inasemekana kuna wachina walimuomba mungu alete corona na sasa imesambaa dunia nzima!
Kama wataalam wa afya wanamuacha mh raisi wetu kwenye umati bila kumshauri avae barakoa kazi ipo.
 
Huyo Mungu mbona anawaua hata wanaomwamini? Hayuko fair na haeleweki
 
Inasisimua Sana kuona China Magufuli aka Jiwe anavyosisitiza tusimame na Mungu. Incredible!
 

Attachments

  • VID-20210219-WA0081.mp4
    16.2 MB
Huyo Mungu mbona anawaua hata wanaomwamini? Hayuko fair na haeleweki
Mungu huyu huyu ndiye aliruhusu mwanae wa pekee Yesu Kristo ateswe na kuuwawa, kumbe alishapanga kumfufua siku ya tatu!
 
Mungu huyu huyu ndiye aliruhusu mwanae wa pekee Yesu Kristo ateswe na kuuwawa, kumbe alishapanga kumfufua siku ya tatu!
Na Mungu huyu huyu mwingi wa rehema na mwenye huruma atatuchoma moto wa milele siku ya mwisho.
 
ameen
 
yap! ni kwa uzinzi wako na ushirikina uliokithiri..
Ni yeye aliyeruhusu watu kuwa wazinzi na washirikina, katuumba na udhaifu huo...angeweza kutuumba vile anavyotaka yeye tuwe.
Anatengeneza tatizo halafu anatuhukumu.
 
Watanzania acheni kumdhihaki M/MUNGU. Wapi yamefanyaka maombi M/MUNGU awaepushie hili janga la CORONA. Mkuu wa nchi anasema CORONA haipo watendaji wake wooooote wanasema kuna changamoto wa UPUMUAJI. Emu nambieni ni MUNGU gani anaeweza jibu maombi yenu na anajibu nini mnachomuomba kama nyie hamjaelewa nini kinakusumbua.
Acheni undenzi mataga nyie
 
Na Mungu huyu huyu mwingi wa rehema na mwenye huruma atatuchoma moto wa milele siku ya mwisho.
Naam!

Msingi wa Imani yangu ni Biblia. Kitabu cha kumbukumbu la Torati 28 kimeandika faida za kumuamini na kumtumikia Mungu. Hizi faida zinapatikana hapa hapa Duniani. Kitabu hiki sura 19 kimeandika hasara za kutomwamini Mungu. Hizi nazo zinatokea humu humu Duniani. Ndio kusema Moto wa milele tunaanza kuteseka nao hapa hapa Duniani.
 
Kiimani, kusema covid-19 ipo ni kukubali kushindwa. Ndiposa Imani inaelekeza kukataa mabaya (yaani hata kama yapo unasema hakuna kitu kama hicho). Ndio tofauti ya Sayansi na Imani!
 
Mungu yupi anaombwa na taifa la Tanzania?
 
Mungu anayeabudiwa Vatican na wakatoliki, Mecca na Waislamu, India na Wahindu na China na Wabudha ni huyo huyo mmoja?
Mungu ni mmoja.
Ila wengine wameamua kumtegemea MZUNGU.
HAPO NDIPO SHIDA INAPOKUJA..
 
Ni yeye aliyeruhusu watu kuwa wazinzi na washirikina, katuumba na udhaifu huo...angeweza kutuumba vile anavyotaka yeye tuwe.
Anatengeneza tatizo halafu anatuhukumu.
KILA KITU KIMERATIBIWA NI WEWE TU KUCHAGUA NJIA INAYOKUFAA! ULIJUAJE KMA NI YEYE ALIUMBA YOTE HAYO?🙂 MAANAKO UZINZI NA USHIRIKINA TUNAOFANYA NI MAKOSA YA MUNGU?
 
Mungu yupi anaombwa na taifa la Tanzania?
Wakiwapo walau watu 10 wenye Imani jadidi, wakamwomba Mungu tutaibuka washindi. Kumbuka ubishi wa Abraham kwa Mungu kabla Sodoma na Gomora haijalipuliwa na mvua ya Moto!

My opinion: wenye Imani waendelee kumwomba Mungu atuponye, wataalamu wanasayansi pia wapewe nafasi tutumie maarifa Yao. Maana Mungu ndie ameumba wanasayansi na mi yeye ndiye anasimamia mawazo na fikra zao. Yaani anafanya njia kupitia Scientists.
 
Hayo mataifa mengine hayana walau watu 10 wenye imani ili waibuke washindikama mnavyotegemea Tanzania itaibuka mshindi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…