Corona: Tuweni macho na hivi vifo vya ghafla ghafla


Mkuu huwa kuna autopsy. Lakini hapa tuna jipya:

"Vifo vinavyotokea ghafla ghafla katika zama hizi ambazo mamlaka kwa makusudi haina nia ya kufahamu vyanzo vya vifo, akili za kuambiwa changanya na za kwako."

Hapo ndipo hoja zako zote zinapoparaganyika!
 
uchumi ndio maisha na ndio uhai wenyewe bila uchumi dunia ya leo uhai haupo jaribu kukaa bila fedha yeyote mwezi uone kama utaishi

Sent using Jamii Forums mobile app
Meko anawadanganya,uchumi unaweza ukaujenga tena Ila uhai ukitoka ndo imetoka.Ni akili mbovu za kiwango Cha mwanaccm kuamini mtu asiye na hata shilingi mia mfukoni na sawa na yule aliye mortuary au kaburini
 
ulikuwa hujui tuu watu wanakufa sana miaka yote sema ukifahamu kuwa ni hali ya kawaida na yakiasili isiyo epukika utamshukuru mungu azidi kukujalia afya njema na bila.kuendekeza hofu ya ziada

Sent using Jamii Forums mobile app
Siku Covid ikimfyekelea mbali meko ndo mtajua corona inaua
 
Tuambie kifo gan cha gafla kimetokea hapa tz siku za karibuni
unataka siku ya leo na tarehe ya leo?
naogopa kuweka picha zao hapa, lkn kwenye Mitandao wapo kibao
mmoja wa TISS wamempumzisha Mbeya huko
Mwingine Diwani Moshi Kilimanjaro
Mwingine Dr aliwahudumia wenye corona DSM
Mwingine wa karibu TCRA wamempeleka Tanga
jamani Corona ipo, tujikinge tusiambukizane, maana msioamini ndio mnaotuletea
 
Mzee kaiacha Benz yake. Apumzike kwa amani [emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
Hivi ni vile vifo vya ghafla ghafla ambavyo nguvu kubwa sana hapa kwetu imekuwa ikitumika kulazimisha kuwa havikusababishwa na Corona.

Ila ni wazi kuwa habari za mkewe kukutwa Corona, yeye mwenyewe kuwa na Corona na walinzi wake kuwa na Corona ndani ya wiki takribani mbili zilizopita hazikuwa ngeni.

Burundi first lady in Kenya for COVID-19 treatment

Tetesi: - Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza pia apatikana Corona

Ikumbukwe pia kuwa Nkurunziza alikuwa amekataa kuchukua hatua zozote thabiti kuhusiana na Corona akidai kuwa Mungu aliipenda sana Burundi kwa Corona kuwafikia.

Pia alikaidi miito yote kuahirisha shughuli za uchaguzi mkuu mwezi jana na mwezi huu ili kuidhibiti mikusanyiko ya watu. Pia alikaidi kusimamisha mikusanyiko ya makanisani na misikitini.

Maisha nchini kwake yaliachwa kuendelea kama yanavyoendelea hapa kwetu.

Yale yale ya wale wabunge wetu, wakuu wa wilaya, ma OCD na ma OCS yule bwana wa TABOA na wengi wengine. Vifo vya ghafla!

Tangulia kwa amani bwana Pierre kwa hakika umetuachia somo. Hadi litakapoeleweka si muda mrefu utakuwa mwenyeji wetu tu.

Nyuma yako mbele yetu. Twaja mkuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…