Titicomb
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 12,823
- 21,210
COVID-19 inachofanya kule Italia na Spain sio mzaha,
Hali imekuwa mbaya sana kwa hizo nchi kiasi cha maiti kuhifadhiwa makanisani. Pamoja na tamaduni zao kuchangia hali kuwa mbaya lakini kuna uzembe flani ambao hata sisi tunaendelea kuufanya, hutujifunzi kwao.
Vifo sasa vinawafuata vijana, mwanzo vilikuwa dhidi ya wazee lakini kadri siku zinavyo zidi kwenda na ndivyo umri wa wanaokufa kwa huu ugonjwa unashuka.
Hali ya hewa ya joto sio kizuizi kwa huu ugonjwa kuenea. Sema joto nahisi linasaidia kidogo wagonjwa kujisikia nafuu kuliko ukiugua kifua na mafua mahali penye baridi kali.
Italia na Spain zimefikiaje hali mbaya kiasi hiki? Jibu: Walichelewa kuchukua hatua ya kufunga mipaka viwanja vya ndege, train na magari. Kosa kubwa zaidi walichelewa kufunga mitaa au kuzuwia mizunguko ya watu mitaani (lockdown of streets).
Daktari bingwa wa upasuaji aliye badilisha kazi yake na kuwa mhudumu wa kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU) cha wagonjwa wa COVID-19 Dr. Emanuela Catenacci anasema.
"Try to stop, try to stop - isolate people, stop contact in everything because otherwise the situation is, like, a tsunami, is a tsunami, when it starts to grow it's really… it explodes,"
"Don't think that it is happening here and [think] it can't happen everywhere else - because it will if you don't do anything to stop it."
Msome hapa Coronavirus: 'Everyone dies alone': Heartbreak at Italian hospital on brink of collapse
Spain inakaribia kuwa nchi ya pili kwa kasi ya maambukizi ya huu ugonjwa na vifo ikikaribia kuipita Iran.
Spain imefikia hapa sababu ya kupuuzia mambo na wenye mamlaka kuwaza pesa (uchumi) kuliko maisha.
Mfano Meya wa jiji la Madrid alikataa kusitisha tukio (Event) moja la kimataifa lilofanyika kwenye mji wake karibuni kwa kuhofia kukosa kipato kupitia watalii walio hudhuria tukio husika.
Alizembea hivi na kutetea kama sisi kwamba zitawekwa sanitizer za kutosha ukumbini, hii yote ni tamaa ya $500 milioni tu za hao watalii.
Gharama za matibabu na maisha ya raia wake wanaougua na kufa kwa hili gonjwa inazidi mara dufu ya hii fedha. Someni hapa sababu za kuenea gonjwa kwa kasi Spain na Italia Why did coronavirus hit hard in Italy and Spain? Some blame a lack of social distancing — and a lot of social kissing.
Tujifunze kitu kimoja muhimu hapa, pesa sio maisha ya watu. Pili joto halizuii kuenea kwa huu ugonjwa maana Italia na Spain hasa hapo Madrid ni jiji lenye joto sio baridi kama China, Korea ya Kusini au nchi zingine zilizokumbwa na hili gonjwa.
Kauli ya dada yangu wa wizara inayo husu haya mambo kwamba "tuombe Mungu kwakweli, maana hatuwezi kudhibiti(control)" ni mzaha mkubwa na utani na maisha ya watu.
Mungu yupo lakini kama hatutumii akili na utashi aliotupatia nawaambia tutaangamia kweli kweli na wala huyo Mungu hatatuokoa na mkono wa COVID-19. Nasema tusimjaribu Mungu kwa kusubiria miujiza.
Ina maana sisi ndio hatuna dhambi sana kuliko walikotutengenezea makusanyo ya vitabu vya Biblia huko Italia kwa warumi?
Are we more Christians than Romans? Ina maana sisi ndio tuna uislam safi kuliko huko Uarabuni na Uajemi ambako mtume (S.A.W) na maswaaba wake walikuwa wanafanya kazi yao ya kuhimarisha dini ya uisalam?
Are we more Islams than Arabs and Persians? We can't be serious!! Let's hope we're more Buddhists than Chinese who have nearly won the war against this pandemic disease. If we are doing nothing to help ourselves out of this tragedy but rather wait for God to save us, then surely we shall be forsaken!
Hivi kwanini hatuzuii nyumba za ibada, hatuzuii raia toka nchi zenye huu ugonjwa hasa za Ulaya na Afrika ya Kusini? Kufanya hivi ndio kujaribu kudhibiti tatizo. Fedha ya utalii itatutokea puani na yote ile tuliyo ingiza miaka 2 iliyopita na ya kipindi hiki cha ugonjwa itaishia kwenye kutibu na kupima, na kuzika watu walikumbwa na COVID-19.
Serikali mtaniwia radhi sina nia ya kutisha watu na kupotosha ndio maana nimeweka na rejea kwa njia ya internet hyperlinks. Najua mnajua lakini someni na hapa, pitieni hizo link. Fungeni mipaka na taasisi za ibada angalau kwa siku 21 (majuma matatu).
Tuombeane uzima, na kutakiana kila la kheri.
UPDATES
==================
Link ya taarifa rasmi ya serikali ya Singaore hii hapa Coronavirus disease 2019: Cases in Singapore
Wazungu wanasema seing is believing.
Singapore na Tanzania hasa Dar es Salaam tunafanana sana hali ya hewa, wastani wa joto hapa kwetu ni 29°C.
Hali imekuwa mbaya sana kwa hizo nchi kiasi cha maiti kuhifadhiwa makanisani. Pamoja na tamaduni zao kuchangia hali kuwa mbaya lakini kuna uzembe flani ambao hata sisi tunaendelea kuufanya, hutujifunzi kwao.
Vifo sasa vinawafuata vijana, mwanzo vilikuwa dhidi ya wazee lakini kadri siku zinavyo zidi kwenda na ndivyo umri wa wanaokufa kwa huu ugonjwa unashuka.
Hali ya hewa ya joto sio kizuizi kwa huu ugonjwa kuenea. Sema joto nahisi linasaidia kidogo wagonjwa kujisikia nafuu kuliko ukiugua kifua na mafua mahali penye baridi kali.
Italia na Spain zimefikiaje hali mbaya kiasi hiki? Jibu: Walichelewa kuchukua hatua ya kufunga mipaka viwanja vya ndege, train na magari. Kosa kubwa zaidi walichelewa kufunga mitaa au kuzuwia mizunguko ya watu mitaani (lockdown of streets).
Daktari bingwa wa upasuaji aliye badilisha kazi yake na kuwa mhudumu wa kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU) cha wagonjwa wa COVID-19 Dr. Emanuela Catenacci anasema.
"Try to stop, try to stop - isolate people, stop contact in everything because otherwise the situation is, like, a tsunami, is a tsunami, when it starts to grow it's really… it explodes,"
"Don't think that it is happening here and [think] it can't happen everywhere else - because it will if you don't do anything to stop it."
Msome hapa Coronavirus: 'Everyone dies alone': Heartbreak at Italian hospital on brink of collapse
Spain inakaribia kuwa nchi ya pili kwa kasi ya maambukizi ya huu ugonjwa na vifo ikikaribia kuipita Iran.
Spain imefikia hapa sababu ya kupuuzia mambo na wenye mamlaka kuwaza pesa (uchumi) kuliko maisha.
Mfano Meya wa jiji la Madrid alikataa kusitisha tukio (Event) moja la kimataifa lilofanyika kwenye mji wake karibuni kwa kuhofia kukosa kipato kupitia watalii walio hudhuria tukio husika.
Alizembea hivi na kutetea kama sisi kwamba zitawekwa sanitizer za kutosha ukumbini, hii yote ni tamaa ya $500 milioni tu za hao watalii.
Gharama za matibabu na maisha ya raia wake wanaougua na kufa kwa hili gonjwa inazidi mara dufu ya hii fedha. Someni hapa sababu za kuenea gonjwa kwa kasi Spain na Italia Why did coronavirus hit hard in Italy and Spain? Some blame a lack of social distancing — and a lot of social kissing.
Tujifunze kitu kimoja muhimu hapa, pesa sio maisha ya watu. Pili joto halizuii kuenea kwa huu ugonjwa maana Italia na Spain hasa hapo Madrid ni jiji lenye joto sio baridi kama China, Korea ya Kusini au nchi zingine zilizokumbwa na hili gonjwa.
Kauli ya dada yangu wa wizara inayo husu haya mambo kwamba "tuombe Mungu kwakweli, maana hatuwezi kudhibiti(control)" ni mzaha mkubwa na utani na maisha ya watu.
Mungu yupo lakini kama hatutumii akili na utashi aliotupatia nawaambia tutaangamia kweli kweli na wala huyo Mungu hatatuokoa na mkono wa COVID-19. Nasema tusimjaribu Mungu kwa kusubiria miujiza.
Ina maana sisi ndio hatuna dhambi sana kuliko walikotutengenezea makusanyo ya vitabu vya Biblia huko Italia kwa warumi?
Are we more Christians than Romans? Ina maana sisi ndio tuna uislam safi kuliko huko Uarabuni na Uajemi ambako mtume (S.A.W) na maswaaba wake walikuwa wanafanya kazi yao ya kuhimarisha dini ya uisalam?
Are we more Islams than Arabs and Persians? We can't be serious!! Let's hope we're more Buddhists than Chinese who have nearly won the war against this pandemic disease. If we are doing nothing to help ourselves out of this tragedy but rather wait for God to save us, then surely we shall be forsaken!
Hivi kwanini hatuzuii nyumba za ibada, hatuzuii raia toka nchi zenye huu ugonjwa hasa za Ulaya na Afrika ya Kusini? Kufanya hivi ndio kujaribu kudhibiti tatizo. Fedha ya utalii itatutokea puani na yote ile tuliyo ingiza miaka 2 iliyopita na ya kipindi hiki cha ugonjwa itaishia kwenye kutibu na kupima, na kuzika watu walikumbwa na COVID-19.
Serikali mtaniwia radhi sina nia ya kutisha watu na kupotosha ndio maana nimeweka na rejea kwa njia ya internet hyperlinks. Najua mnajua lakini someni na hapa, pitieni hizo link. Fungeni mipaka na taasisi za ibada angalau kwa siku 21 (majuma matatu).
Tuombeane uzima, na kutakiana kila la kheri.
UPDATES
==================
Mkuu recommendations ni nini?tufanyeje?
- Tufanye lockdown baadhi ya maeneo ya mikusanyiko inayowezekana kuzuiwa kwa muda kama majumba ya ibada.
- Tuzuie wageni hasa toka nchi zilizo shambuliwa sana na huu ugonjwa.
- Tuache ndege na magari ya mizigo tu na ya huduma muhimu za kibinadamu.
- Mikahawa na vilabu vya pombe (restaurants and bars) viwe vya kuchukua huduma na kuondoka na bidhaa.
- Majumba ya sinema yafungwe.
- Kutolewe muongozo wa shughuli za mazishi na mikusanyiko yake, Mfano liwekwe shariti watu wakae mbali mbali na wanaobeba jeneza wavae golves, mask, na wawe wachache tu, sehemu kubwa jeneza libebwe na magari.
- Zizuiwe sherehe za kijamii kama harusi zinazokusanya watu wengi kumbini, au zifanyike viwanja vya nje na watu wakae umbali wa miata 3 au zisitishwe kwa muda.
Singapore wana wastani wa joto la 27°C lakini kuna kesi za wagonjwa ambao hawana uhusiano na kuutoa nje ya nchi.90% ya hao wagonjwa ni imported cases. Yaani wameingia Bongo wakati mzee Corona tayari keshazama ndani. All in all, joto sio sababu kwa kuwa South Africa sasa local transmission zimeshaanza maana kuna wagonjwa kibao ambao hawajasafiri kutoka nje ya Nchi.
Link ya taarifa rasmi ya serikali ya Singaore hii hapa Coronavirus disease 2019: Cases in Singapore
Wazungu wanasema seing is believing.
Singapore na Tanzania hasa Dar es Salaam tunafanana sana hali ya hewa, wastani wa joto hapa kwetu ni 29°C.