CORONAVIRUS: Naongeza miluzi ya tahadhari lockdown iharakishwe

CORONAVIRUS: Naongeza miluzi ya tahadhari lockdown iharakishwe

Pili joto halizuii kuenea kwa huu ugonjwa maana Italia na Spain hasa hapo Madrid ni jiji lenye joto sio baridi kama China, Korea ya Kusini au nchi zingine zilizokumbwa na hili gonjwa.

Ni kweli. I hope research zinaweza kusaidia. Tehran average centigrade ni nyuzi 17 na Milan ni 20 wakati Addis Ababa ni 19 ila huko wao wamekuwa hit very hard. Joto sio sababu. Watu wanajifariji tu kuwa hiki kirusi hakiwezi kuvumilia joto linalozidi centigrade 24. Dar ni 29-32, Nairobi 26, Entebbe 26
 
Mkuu tuanze na maeneo ya starehe, nyumba za ibada, sherehe za harusi n.k.
Tuzuwie watu toka nchi zilizo athirika na janga hasa za Ulaya.

Tufunge mpaka wetu na nchi jirani zenye COVID-19 turuhusu kusafirisha mizigo tu kati ya nchi zetu.


Yaani mfunge bar kisa corona? Tukanywe wapi sisi😥😥😜😜acheni wehu wenu basi
 
Tunaelekea kwenye mvua kawaida huwa ni low season kwa utalii, vyema tufunge sasa tufungue baada ya mwezi au miezi miwili wakati huo tukiianza high season ya june/july

Few years from now you may wish you should have started today...
 
Kwa hiyo usipopima hufi?

Kama wagonjwa tunao wengi ila shida ni ukosefu wa maabara tu maana yake vifo vya kutisha tungeshavishuhudia mitaani zaidi ya Italy na Spain wenye maabara.

Wito wa mtoa mada ni muhimu sana badala ya kusubiri maafa,hata Italy alianza mgonjwa mmoja!!
Cardiovascular disease and diabetes kills more than covid-19

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunaelekea kwenye mvua kawaida huwa ni low season kwa utalii, vyema tufunge sasa tufungue baada ya mwezi au miezi miwili wakati huo tukiianza high season ya june/july

Few years from now you may wish you should have started today...

Nimebarikiwa na signature yako mkuu😊
 
Ni kweli. I hope research zinaweza kusaidia. Tehran average centigrade ni nyuzi 17 na Milan ni 20 wakati Addis Ababa ni 19 ila huko wao wamekuwa hit very hard. Joto sio sababu. Watu wanajifariji tu kuwa hiki kirusi hakiwezi kuvumilia joto linalozidi centigrade 24. Dar ni 29-32, Nairobi 26, Entebbe 26
Kwa vile tuna wagonjwa tayari maeneo ya Dar, Arusha , na Zanzibar basi nachukulia madai hayo ya joto zaidi ya nyuzi 24 siyo yenye uzito sana.
Ingawa kitakwimu ni kweli ugonjwa umeshambulia sana maeneo yenye baridi sana.
Uingereza kuna, Urusi na nchi za Scandinavia zina baridi kubwa kuliko baadhi ya maeneo yaliyoshambuliwa sana na ugonjwa kama ya kule Italia.
 
Kwa vile tuna wagonjwa tayari maeneo ya Dar, Arusha , na Zanzibar basi nachukulia madai hayo ya joto zaidi ya nyuzi 24 siyo yenye uzito sana.
90% ya hao wagonjwa ni imported cases. Yaani wameingia Bongo wakati mzee Corona tayari keshazama ndani. All in all, joto sio sababu kwa kuwa South Africa sasa local transmission zimeshaanza maana kuna wagonjwa kibao ambao hawajasafiri kutoka nje ya Nchi.
 
Ni hivi corona iliyopo tz idadi kama ni ndogo hawapungui 200+lakini hawaonekani na wala haionekani kuwa na madhara kivile hivo ww mleta mada usitutie hof acha tuendelee kujitafutia kipato utakapotukuta ni hapo. Ww unalalamika unataka wafunge miji wazuie watu kutembea ili tule nn ss mengine ni kutuogopesha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu tuanze na maeneo ya starehe, nyumba za ibada, sherehe za harusi n.k.
Tuzuwie watu toka nchi zilizo athirika na janga hasa za Ulaya.

Tufunge mpaka wetu na nchi jirani zenye COVID-19 turuhusu kusafirisha mizigo tu kati ya nchi zetu.
Unajua baa na manight clab yameajir watu wangapi ww em tuache jaman tusije kufa kwa stress kabla ya crona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
COVID-19 inachofanya kule Italia na Spain sio mzaha,

Hali imekuwa mbaya sana kwa hizo nchi kiasi cha maiti kuhifadhiwa makanisani. Pamoja na tamaduni zao kuchangia hali kuwa mbaya lakini kuna uzembe flani ambao hata sisi tunaendelea kuufanya, hutujifunzi kwao.

Vifo sasa vinawafuata vijana, mwanzo vilikuwa dhidi ya wazee lakini kadri siku zinavyo zidi kwenda na ndivyo umri wa wanaokufa kwa huu ugonjwa unashuka.

Hali ya hewa ya joto sio kizuizi kwa huu ugonjwa kuenea. Sema joto nahisi linasaidia kidogo wagonjwa kujisikia nafuu kuliko ukiugua kifua na mafua mahali penye baridi kali.

Italia na Spain zimefikiaje hali mbaya kiasi hiki? Jibu: Walichelewa kuchukua hatua ya kufunga mipaka viwanja vya ndege, train na magari. Kosa kubwa zaidi walichelewa kufunga mitaa au kuzuwia mizunguko ya watu mitaani (lockdown of streets).

Daktari bingwa wa upasuaji aliye badilisha kazi yake na kuwa mhudumu wa kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU) cha wagonjwa wa COVID-19 Dr. Emanuela Catenacci anasema.

"Try to stop, try to stop - isolate people, stop contact in everything because otherwise the situation is, like, a tsunami, is a tsunami, when it starts to grow it's really… it explodes,"

"Don't think that it is happening here and [think] it can't happen everywhere else - because it will if you don't do anything to stop it."

Msome hapa Coronavirus: 'Everyone dies alone': Heartbreak at Italian hospital on brink of collapse

Spain inakaribia kuwa nchi ya pili kwa kasi ya maambukizi ya huu ugonjwa na vifo ikikaribia kuipita Iran.
Spain imefikia hapa sababu ya kupuuzia mambo na wenye mamlaka kuwaza pesa (uchumi) kuliko maisha.

Mfano Meya wa jiji la Madrid alikataa kusitisha tukio (Event) moja la kimataifa lilofanyika kwenye mji wake karibuni kwa kuhofia kukosa kipato kupitia watalii walio hudhuria tukio husika.
Alizembea hivi na kutetea kama sisi kwamba zitawekwa sanitizer za kutosha ukumbini, hii yote ni tamaa ya $500 milioni tu za hao watalii.

Gharama za matibabu na maisha ya raia wake wanaougua na kufa kwa hili gonjwa inazidi mara dufu ya hii fedha. Someni hapa sababu za kuenea gonjwa kwa kasi Spain na Italia Why did coronavirus hit hard in Italy and Spain? Some blame a lack of social distancing — and a lot of social kissing.

Tujifunze kitu kimoja muhimu hapa, pesa sio maisha ya watu. Pili joto halizuii kuenea kwa huu ugonjwa maana Italia na Spain hasa hapo Madrid ni jiji lenye joto sio baridi kama China, Korea ya Kusini au nchi zingine zilizokumbwa na hili gonjwa.

Kauli ya dada yangu wa wizara inayo husu haya mambo kwamba "tuombe Mungu kwakweli, maana hatuwezi kudhibiti(control)" ni mzaha mkubwa na utani na maisha ya watu.

Mungu yupo lakini kama hatutumii akili na utashi aliotupatia nawaambia tutaangamia kweli kweli na wala huyo Mungu hatatuokoa na mkono wa COVID-19. Nasema tusimjaribu Mungu kwa kusubiria miujiza.
Ina maana sisi ndio hatuna dhambi sana kuliko walikotutengenezea makusanyo ya vitabu vya Biblia huko Italia kwa warumi?

Are we more Christians than Romans? Ina maana sisi ndio tuna uislam safi kuliko huko Uarabuni na Uajemi ambako mtume (S.A.W) na maswaaba wake walikuwa wanafanya kazi yao ya kuhimarisha dini ya uisalam?

Are we more Islams than Arabs and Persians? We can't be serious!! Let's hope we're more Buddhists than Chinese who have nearly won the war against this pandemic disease. If we are doing nothing to help ourselves out of this tragedy but rather wait for God to save us, then surely we shall be forsaken!

Hivi kwanini hatuzuii nyumba za ibada, hatuzuii raia toka nchi zenye huu ugonjwa hasa za Ulaya na Afrika ya Kusini? Kufanya hivi ndio kujaribu kudhibiti tatizo. Fedha ya utalii itatutokea puani na yote ile tuliyo ingiza miaka 2 iliyopita na ya kipindi hiki cha ugonjwa itaishia kwenye kutibu na kupima, na kuzika watu walikumbwa na COVID-19.

Serikali mtaniwia radhi sina nia ya kutisha watu na kupotosha ndio maana nimeweka na rejea kwa njia ya internet hyperlinks. Najua mnajua lakini someni na hapa, pitieni hizo link. Fungeni mipaka na taasisi za ibada angalau kwa siku 21 (majuma matatu).

Tuombeane uzima, na kutakiana kila la kheri.

Rais Magufuli na serikali kwa ujumla. Tunao uhakika kuwa maudhui ya nyuzi hizi yanawafikia.

Mtakuwa na mioyo migumu kuliko ya Farao kama miito hii haiwahusu.

Hadi tufe wangapi ndipo mgutuke?
 
Ni hivi corona iliyopo tz idadi kama ni ndogo hawapungui 200+lakini hawaonekani na wala haionekani kuwa na madhara kivile hivo ww mleta mada usitutie hof acha tuendelee kujitafutia kipato utakapotukuta ni hapo. Ww unalalamika unataka wafunge miji wazuie watu kutembea ili tule nn ss mengine ni kutuogopesha

Sent using Jamii Forums mobile app

Mawazo duni kabisa. Utakuwa huku soma kilichoandikwa wala kuelewa.
 
Yaani mfunge bar kisa corona? Tukanywe wapi sisi😥😥😜😜acheni wehu wenu basi
Ha ha haaa..
Kwani ukichukua six pack yako, mzinga wa whisk au kreti la bia ukanywea nyumbani haulewi?
Tukizembea utazikosa kabisa hizo kitu, dead people don't drink.
 
Ni hivi corona iliyopo tz idadi kama ni ndogo hawapungui 200+lakini hawaonekani na wala haionekani kuwa na madhara kivile hivo ww mleta mada usitutie hof acha tuendelee kujitafutia kipato utakapotukuta ni hapo. Ww unalalamika unataka wafunge miji wazuie watu kutembea ili tule nn ss mengine ni kutuogopesha

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijamaanisha total lockdown bali baadhi ya huduma au shughuli za mikusanyiko.
Na mipakani kuzuia wageni hasa toka nchi zenye wagonjwa wengi wa COVID-19.
 
Wengi wanalaumu serikali kwann haifungi mipaka, Mara kupiga mikusanyiko ya bar, sokon, na mabasi ya mkoa na daladala.

Swali kwao Kama unajua n hatari hvyo kwann usijikinge wewe kwa kuanza kuepuka mikusanyiko Kama hyo?

Jibu n kuwa wazuie wasizuie huu ugonjwa watanzania wanautafuna kwa ud na uvumba juz kila mtu 80% waliokuwa na viela mfukon walianza kufanya showoff Mara kununua mask, Mara midawa, Mara shopping ya vyakula alafu kesho yake ndo wakwanza kutokunawa mikono, wakwanza kutoa mkono wa kwanza kuhag. N mungu tuu anatulinda Ila watanzania kuishi kwa bajet ya siku tatu tuu n shida Yan hata mtu awe na kilakitu ndan atajitia kiherehere Cha Mara yupo baa, Mara sokon Yan full mzaha
 
Mkuu recommendations ni nini?tufanyeje?
  1. Tufanye lockdown baadi ya maeneo ya mikusanyiko inayowezekana kuzuiwa kwa muda kama majuba ya ibada.
  2. Tuzuie wageni hasa toka nchi zilizo shambuliwa sana na huu ugonjwa.
  3. Tuache ndege na magari ya mizigo tu na ya huduma muhimu za kibinadamu.
  4. Mikahawa na vilabu vya pombe (restaurants and bars) viwe vya kuchukua huduma na kuondoka na bidhaa.
  5. Majumba ya sinema yafungwe.
  6. Kutolewa muongozo wa shughuli za mazishi na mikusanyiko yake, Mfano liwekwe shari watu wakae mbali mbali na wanaobeba jeneza wavae golves, mask, na wawe wachache tu, sehemu kubwa jeneza libebwe na magari.
  7. Zizuiwe sherehe za kijamii kama harusi zinazokusanya watu wengi kumbini, zifanyike viwanja vya nje na watu wakae umbali wa miata 3 au zisitishwe kwa muda.
Unaweza kuongezea, nashauri hii ifanyike angalau majuma matatu tu kwa majaribio, tusisubirie majanga kisha tuje kuwaomba radhi waliotoa tahadhari wakashughulikiwa kama ilivyo tokea China kwa yule Daktari alie toa angalizo kwa umma.
 
Waziri Mkuu Majaliwa linganisha mawazo yako:

Majaliwa awataja wanaoruhusiwa kutoa taarifa kuhusu corona

na maudhui yaliyotolewa kwa unyenyekevu, heshima na taadhima kiasi hiki katika uzi huu.

Tunaamini mamlaka mliyo nayo yanawawajibisha kututendea haki sisi raia wenu.

Pana hatari ya kuja kuanza kulaumiana muda si mrefu kutoka sasa.

Mungu ni mwema janga hili linatukuta wakati tulikuwa na muda wote wa kujifunza toka kwa wenzetu katika kipindi chote kabla ya ugonjwa na hata baada ya ugonjwa kutufikia.

Historia itakuwapo kutuhukumu.

Eeh Mungu wetu utusamehe sisi wakosaji.
 
  1. Tufanye lockdown baadi ya maeneo ya mikusanyiko inayowezekana kuzuiwa kwa muda kama majuba ya ibada.
  2. Tuzuie wageni hasa toka nchi zilizo shambuliwa sana na huu ugonjwa.
  3. Tuache ndege na magari ya mizigo tu na ya huduma muhimu za kibinadamu.
  4. Mikahawa na vilabu vya pombe (restaurants and bars) viwe vya kuchukua huduma na kuondoka na bidhaa.
  5. Majumba ya sinema yafungwe.
  6. Kutolewe muongozo wa shughuli za mazishi na mikusanyiko yake, Mfano liwekwe shari watu akae mbali mbali na wanaobeba jeneza wavae golves, mask, na wawe wachche tu, sehemu kubwa jeneza libebwe na magari.
  7. Zizuiwe sherehe za kijamii kama harusi zinazokusanya watu wengi kumbini, zifanyike viwanja vya nje na watu wakae umbali wa miata 3 au zisitishwe kwa muda.
Unaweza kuongezea, nashauri hii ifanyike angalau majuma matatu tu kwa majaribio, tusisubirie majanga kisha tuje kuwaomba radhi waliotoa tahadhari wakashughulikiwa kama ilivyo tokea China kwa yule Daktari alie toa angalizo kwa umma.

Kweli serikali hii bado tu haisikii?

Mbona balaa?
 
Back
Top Bottom