Coronavirus, Tanzania: Shule zote kuanzia za Awali, Msingi na Sekondari zafungwa. Mikusanyiko ikiwemo ya Kisiasa yasitishwa

Panic mode

Malaria ni hatari zaidi ya korona Ila huwezi Iona hii panic mode

Kisukari kinaua maelfu ya watu kila mwaka Ila huwezi ona hii panic mode

Tulieni chukueni tahadhari Ila msipanic sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bora wameamua hivyo kuliko kusubiri iuwe watu wengi
Ni njia sahihi kabisa na tujiandae kwa kuporomoka kwa uchumi vibaya kwani joto hili Ulaya na nchi nyingi zimeshawakumba tayari na makampuni mengi yanafungwa
UK kuanzia Leo hakuna Safari mpaka dharura kwa muda wa siku 30 na baada ya hapo kama hali itazidi kuwa mbaya watafunga Airport zote
Hasara ila bora salama
Mungu tusaidie


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Kuna watu wanasema hii kitu ipo overhyped yaani kiuhalisia ni nyepesi!!!....

Serikali yetu inasimamia hiki kitu kwa utulivu tofauti na mataifa mengine. Natumai tumejiandaa vizuri sana japo mlipuko wa kipindupindu tu huwa unatutoa jasho
 
Kwenye public transport watu wasijae sana, wakae wachache, Polisi ipo wapi?
Quarantine zipo? wageni airport wakae siku 14.

Mmekalia sanitizer, bado mtafunguka tu.
 
Ila siasa bana...hata nchi nzima kukiwa na total lockdown, bado kuna watu wataoilaumu serikali tu.

Wapo wataosema hakuna haja hiyo na wapo wataosema hiyo haitoshi!
Kuna watu hawajui total lockdown ikoje. EU wanaandaa pesa kulipa watu watakaokuwa nyumbani bila kazi, Tz itaweza? Kuna watu kula mpaka tutoke nje ukahangaike on daily basis, kukaa nyumbani maana yake ni kukosa hela ya kula.
 
Sababu kubwa kwa nini serikali yetu haifungi mipaka hasa kwa wageni wa kizungu ni mapato. Serikali inategemea sana mapato ya utalii, sasa ikifunga mipaka na kutangaza watalii wasije itakosa pesa za kuendeshea serikali.

Hali ni mbaya ndani makusanyo hakuna sasa wazifunga mipaka watalii wasije watashindwa kuendesha serikali.

Hapa wataruka ruka kufunga mashule, vyuo ila sio mipaka. Wakifunga mikapa watasafocate na kufa njaa.
 
Hufikirii siku unazozipoteza mwezi huu ambao umekatizwa ndugu? Wakifungua unalipa deni na term ya pili hapo hapo hakuna sound.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
na sisi JF tuonyeshe uzalendo. tufunge jf kwa siku 30 kuepuka maambukizi πŸ˜±πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„
 
Sijui kwanini akili yangu inaniambia kuna kitu nyuma ya hili pazia la korona, sitambui kwanini akili yangu imegoma kuishia kwenye tatizo tu la corona, nawaza kimya kimya kama kuna kitu kitafuatia kwa dunia nzima baada ya corona, kwanini nahisi hii ni mipango ya wenye akili ndefu waliotutangulia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu hawajui total lockdown ikoje. EU wanaandaa pesa kulipa watu watakaokuwa nyumbani bila kazi, Tz itaweza? Kuna watu kula mpaka tutoke nje ukahangaike on daily basis, kukaa nyumbani maana yake ni kukosa hela ya kula.

Africa tofauti Mkuu na wanaona sawa tu ila uchumi duniani ndio huo unaporomoka
Hali ni ngumu huku Mkuu
Ukichukua off voluntarily unalipwa Β£29 kwa siku
Leo Kuna kampuni ya Simu Carphone warehouse wamefukuza wafanyakazi 3000
Ni msiba mkubwa huu


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…