Course gani naweza kusomea kutokana na matokeo yangu

Aqua2

Member
Joined
Nov 22, 2018
Posts
5
Reaction score
4
Habari wanajukwaa
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 19 nilibahatika kumaliza kidato cha 4 mwaka jana lkni bahati mbaya sikufanikiw kufanya vizur kutokan na sababu Mbalimbali(hatanikiwaelezea sababu zenyew haitasidia) lengo la kuleta uzi huu kwenu ni kuomba ushauli course gani naweza kusomea kutokana na matokeo yngu haya

Physics F
Chemistry F
B. Mathematics F
Biology D
Civics D
History D
Geography D
English D
Kiswahili D

Nahitaji ushauli wenu kaka zangu na Dada zangu

ASANTENI
 
nenda kaanze

certifiate ya law(1yr) then diploma(2yrs) ...bachelor LLB (4yrs)...school of law (1yr ukiwa serious)

au nenda mzumbe university kaanze certificate ya Public administration

na kozi zinazofanana na hizo

maana nahisi kwa utawala na waziri yule wa elimu sidhani kama watakuruhusu kufanya kozi za biashara sababu ya F ya math
 
Kasomee ufundi,
Weka mtazamo wako huko kwenye maswala ya veta,

Kisha chagua usome ufundi wa kitu gani.
Ukishindwa kuchagua

Tuone ukileta uzi mwingine wa kutaka kuambiwa ufundi upi mzur kati ya hizo utakazoona zinafaa.

Ila kama nyumbani hela ipo ya kutosha,
Kozi za matajili zipo nyingi tu, waambie wanaokupa hela wakuchagulie.
 
Nashukuru mkuu
 
Shukrani Kwa ushauli
 
Nyie ndo mko siriaz ,heshima kwenu

Mimi nina ndugu yangu mkuu kapata alama hizi

Hisb F
Hist D
CIVC D
BIOS C
CHEM D
KISW C
GEOG D
ENGL D

sasa nimepewa kazi kumtaftia kozi yeyote ya mambo ya afya mkuu.

Nibkozi gani inaweza kumfaa mkuu kwa matokeo hayo?
 
Jimmie Gatsby weka ushauri wako hapo mkuu.
 
Mkuu afya hawataki F ya math
Waambie afya haiweZekan labda kwengine
 
Sina uhakika sana maana kila siku mambo yanabadilika.
Nilikua nikiona wanataka kuanzia D
hii ni prospector ya RUAHA UNIVERSITY.... katika masomo manne math..physics..biology..chemistry.. wanahitaji pass 2 katika course ya certificate in medical laboratory
 
Hyo kozi iko vzuri mkuu,mana sisi wengine shule tulikimbiaga tunawakomalia vijana wetu mkuu.

Iko vipi soko lake la biashara ama ajira?
Na jee kwa zanzibar naweza pata chuo hichp cha kumpeleka mkuu?

Na pia vipi anaanzia certificate miaka mingapi mpaka diploma mkuu?

Samahani kwa miswali ya kiusumbufu nashkuru kwa muda wako mkuu
mkuu nahisi kwa matokeo hayo anakubaliwa kusomea medical laboratory sciences
 
soko lake lipo njema mkuu... siunajua kada ya afya ajira zake huwa hazisumbui

hii kozi certificate ni miaka 2 na diploma ni miwili so atatumia jumla ya miaka 4 kumaliza

ilikuwaga haina ngazi ya degree kwa hapa tanzania ilikuwa ukitaka degree ni lazima uende nje japo miaka miwili nyuma niliskia wizara ya afya wanataka kuanzisha ngazi ya degree kwa hapahapa nchini

kwa zanzibar kwa kweli sijui.. ila kama kuna hospital kubwa kwa hapo zanzibar na ina chuo chake cha masuala ya tiba lazima hii kozi itakuwepo tu... maana hawa ndio huwa wataalamu wa maabara na vipimo kwenye mahospital
 
Ajipange maana pia Lab ni ngumu mkuu.
Pia muhimu kufatilia sifa wanazotaka Nacte na sio chuo fulan.
So fatilia zaidi nacte wanataka nin
Kwa uhakika zaidi nenda kafanye application mwenyewe mtandaoni na sio kuambiwa na chuo kuwa watakusajili tuu.
hii ni prospector ya RUAHA UNIVERSITY.... katika masomo manne math..physics..biology..chemistry.. wanahitaji pass 2 katika course ya certificate in medical laboratoryView attachment 974390
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…