COVID-19 & DEEP STATE: Nini maana ya Uhandisi Jamii unaotokea Duniani!?

COVID-19 & DEEP STATE: Nini maana ya Uhandisi Jamii unaotokea Duniani!?

Hapa JF kwa muda wa miaka mitano iliyopita nimeandika nyuzi za Intelijensia zaidi ya hamsini. Kama ni msomaji wangu mzoefu utaelewa kwamba, sijawahi ku-lose focus, siwezi ku-lose focus na haitokuja kutokea nika lose focus. NEVER.!!

Huu wali ndio kwanza tumeupalia mkaa.. subiri uive tukwangue ukoko.

Endelea kufuatilia.. kuna jambo jipya kubwa sana utalipata hapa.

Regards
Habib
Mkuu naamini hauwezi kulose focus,utaturudisha kwenye main point maana tumetoka Wuhan,tumeenda Pakistan na sasa tupo Iraq.[emoji16]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu tunasubiri part 3
Hapa JF kwa muda wa miaka mitano iliyopita nimeandika nyuzi za Intelijensia zaidi ya hamsini. Kama ni msomaji wangu mzoefu utaelewa kwamba, sijawahi ku-lose focus, siwezi ku-lose focus na haitokuja kutokea nika lose focus. NEVER.!!

Huu wali ndio kwanza tumeupalia mkaa.. subiri uive tukwangue ukoko.

Endelea kufuatilia.. kuna jambo jipya kubwa sana utalipata hapa.

Regards
Habib

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij addenbwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
Jk12 frank Samuel


Sent using Jamii Forums mobile app
nimeshachukua kiti tayari.... I cant wait kumeza konsi unazotoa Habibu B. Anga 🖊🖊🖊📜📜📜 umesahau. kunitag mkuu😁🙏🙏🙏
 
Nakubaliana na wewe mkuu kabisa Kwani kwa tuliosoma genetics utagundua Leanna DNA ndiyo basic unit of life, but kibiologia zaidi tunarefer cell kama basic and functional unit of life bcoz DNA ipo kwenye nucleus ya cell. Na nyongeza KA kuhusy virus huwa vinatumia materials za kwenye cell za kiumbe ambamo zimeingia ili kujiendesha na kuzaliana kwa wings (replication). kali linux
 
SEHEMU YA TATU


DEEP STATE, COVID-19: Nini Maana ya Uhandisi Jaamii Unaotokea Duniani?




#3


Kuna watu wana wasiwasi kwa nini nagusia matukio kadhaa ambayo yanaonekana hayahusiani. Kama ni msomaji wangu wa siku nyingi utaelewa namna gani naandika Makala zangu... kama mtori... endelea kupakua, fuatana nami.



Kwenye kichwa cha habari ya makala hii nimeandika kuhusi Deep State na COVID-19.
Kabla sijaweka ushahisi wangu kwamba namna gani twapaswa kujiuliza maswali kuhusu hii Covid19 kwanza nataka nikupe ushahidi kuhusu Deep State na namna gani inafanya kazi na kwa nini nina wasiwasi hii Covid-19 inaweza kuwa karata iliyotupwa kwa umahiri kabisa na kwa makusudi.
Imetupwa na nani?


Here we go..


Jana niliwaeleza kwamba katika kitambulisho ambacho Raymond alikutwa nacho kilionyesha kwamba alikuwa ni muajiriwa wa kampuni inayoitwa Hyperion Protective Consultants ambayo nilieleza kuwa hii ilikuwa ni shell Company ya kampuni mama ya Blackwaters Worldwide ambao nikasema hawa ni moja ya 'contractors' wakuu wa CIA.
Kuna jambo la msingi sana kulielewa kuhusu hawa Blackwaters Worldwide kabla sijaendelea mbele sana.


Kama umekuwa mfuatiliaji wa vita ya Iraq basi sina shaka utakuwa umewahi kusikia kisanga cha Nisour Square Massacre.
Kisanga hiki cha Nisour Square Massacre pengine ndio moja ya skandali kubwa ya kwanza kufanya Marekani wakosolewe vikali na hatimaye wafanye mabadiliko makubwa katika oparesheni zao za pale Iraq.
Kisanga hiki kinahusu vifo vya Wairaq 17 huku wengine 20 wakijeruhiswa vibaya kwa kupigwa risasi mchana na hadharani kabisa na Wanajeshi wa Marekani ambao walikuwa wanasindikiza msafara wa Balozi wa Marekani pale Iraq. Tukio hili lilitokea mwaka 2007 mwezi Septemba tarehe 16…


Sasa,

Nimegusia kisanga hiki sababu natamani nieleze kidogo kile ninachoelewa kuhusu "Deep State" na namna gani tunapaswa kuwa na hadhari na kutafakari kwa kina kuhusu mlipuko huu wa COVID-19.

Kwenye kisanga hiki cha Nisour Square Massacre baadae baada ya uchunguzi wa tukio hili ambalo lilishitua ulimwengu wakati huo, ikaja kubainika kwamba wanajeshi wale ambao walikuwa wanasindikiza ule msafara wa Balozi wa Marekani pale Iraq hawakuwa hasa "Wanajeshi wa Marekani". Kwamba ndio walikuwa ni raia wa Marekani, na ndio walikuwa ni wanajeshi lakini hawakuwa "Wanajeshi wa Marekani". Ilikuja kubainika kwamba wanajeshi wale walikuwa ni wanajeshi binafsi wa kampuni ya Blackwater Worldwide.
Ilikuwa ni mshituko mkubwa sana, sababu ni ilikiwa inaeleweka wazi juu ya uwepo wa PMCs (Private Millitary Companies) lakini hakuna ambaye alikuwa amewahi hata kuona kwamba ati hizi PMCs zimekuwa na ushawishi na nguvu kiasi kwamba mpaka wao ndio wanalinda 'diplomatic convoys' adhimu kama ya balozi wa Marekani tena kwenye eneo hatari kama Iraq. Na pia wanakuwa na mamlaka bila woga kupiga raia risasi.

Ulikuwa mshituko mkubwa sana kwenye ulimwengu wa Ulinzi na Usalama na kufanya watu waanze kuuliza maswali ambayo awali hayakuwahi kuulizwa.


Kwa utaratibu, umakini mkubwa na ushahidi naomba nieleze kwa undani kuhusu Deep State na kwa namna gani si tu kwamba ni 'conspiracy theory' kama unavyoweza kudhani na vipi tunaunga dot na tukio la mwaka 2011 pale Lahore Pakistan na inatupa tafasiri ipi na hii hamaki ya COVID-19.



Mwaka fulani hivi… miaka kadhaa iliyopita, yuko bwana mmoja hivi (najua kuwa wapwa watauliza ni mimi au si mimi… doesn't matter) alifika kwenye ubalozi wetu wa Tanzania Marekani, jijini Washington D.C ambapo jengo letu la ubalozi lipo mtaa wa North West, 22nd.
Ni miaka kadhaa tu nyuma kama miaka mitano hivi au sita… enzi hizo pale ubalozini wako akina mama Immaculata, akina Abbas Misana kama balozi mdogo, bwamdogo Mugendi Zoka mtoto wa shushushu nguli Jack Zoka akiwa mwambata wa Political Affairs, akina Kanali Mutta mwambata wa masuala ya Ulinzi… watoto wa mjini akina Emmanuel Swere… enzi hizo, miaka kadhaa iliyopita, bwana huyu alifika pale balozini.
Moja ya tongotongo ambayo bwana huyu aliitoa pale ni Washington ni suala dogo sana ambalo awali hakuwa analijua. Suala dogo sana lakini mpaka leo liko kwenye kumbukumbu kichwani… kwamba kwenye maongezi ya kawaida wakazi wa Washington wenyewe huwa lile eneo hawalitamki kama Washington kama sisi wengine.

Yani ni kama miaka ya zamani mtu akitoka mkoani kuja Dar es Salaam anasema anaenda "Bongo", lakini husingeweza kumsikia mkazi wa Dar anasema anaishi "Bongo" akimaanisha Dar es Salaam.
Pale Washington wakazi wa pale wenyewe wanapaita "The District". Yani mfano ukutane naye New York, kwenye maongezi anaweza kukwamba "..tommorow i'm flying back to the district.."
Au mara nyingine wanatumia D.C. Huu ni moja ya ushamba ambao bwana huyu ulimtoka miaka hii kadhaa nyuma.


Lengo sio kuongelea huu ushamba ambao bwana huyu aliutoa bali baadhi ya mambo kadhaa madogo madogo aliyayaona ambayo yalichochea hari ya ndani kufanya tafiti na kuuliza maswali kuhusu ushawishi na mlinganyo wa nguvu kwenye jukwaa la siasa za dunia.

Zaidi ya ushamba huo wa kwanza, kitu cha msingi zaidi ambacho bwana huyu alikiona kwa mara ya kwanza na kuchochea hari nafsini ilikuwa ni barabara inaitwa Beltway iko pale Washington.
Hii Beltway ni sehemu ya "interstate highway system"… yaani twaweza sema kama mfumo wa barabara kuu ambazo zinaunganisha majimbo yote ya Marekani. Sasa kwa pale Washington hii highway inaitwa Beltway.
Barabara hii iko tofauti kidogo sababu yenyewe inazunguka jimbo lote la Washington. Yaani kwamba kwa mfano ukiangalia kwenye ramani alafu tuseme kwa mfano uki-highlight hii barabara (Beltway) mfano kwa kui-bold kwenye ramani utaona inatokea umbo la duara na pale katikati ndio D.C penyewe.
Yaani chukua mfano barabara ya Bagamoyo, nenda mpaka pale Mbezi Beach Masana inapokutana na barabara ya Goba, kisha ukitokea Mbezi nenda na Morogoro Road mpaka Magomeni inapokutana na Barabara ya Kawawa alafu kutoka Magomeni mpakq Morocco. Unaona huo mzingo, hapo katikati sasa ndio iwe Washington na huo mzingo wote ni ndio hiyo highway ya Beltway. Kwamba barabara hii imezungunga kwa mzingo jimbo lote la Washington.

Bwana huyu alikaa muda kadhaa pale ubalozini.. na kama ujuavyo watu wa ubalozi huwa wana alikwa kwenye dhifa na hafla mbali mbali za kiserikali.
Katika maongezi na watu kadhaa kwenye dhifa hizi kapata kusikia jambo jipya ambalo nalo lilimtoa ushamba.. kuna neno alilisikia linatumika sana, "Beltway Politicians".
Binafsi kwenye maisha yangu pengine nafanya vitu viwili tu kwa ufanisi mkubwa… kusoma na kuandika. Nasoma vitu vingi sana kiasi kwamba kuna muda nahisi ni nadra kusikia kitu ambacho sijawahi kukisikia kabisa au sina idea nach hata kidogo… ni nadra mno.
Na kuhisi kwangu kote kwamba nasoma vitu vingi lakimi sikuwahi kulisikia neno hili "Beltway Politician" wala sijawahi hata kuliona limeandikwa mahala na wala sikuwa najua maana yake.

Wajua hata ukienda pale Bungeni Dodoma wana vimisemo vyao, wana vimaneno vyao ambavyo hata huwezi kuvikuta huku mtaani. Ndivyo ambavyo bwana huyu kwa mara ya kwanza naye alilisikia neno hili "Beltway Politician".

Binafsi kwa haraka nilihisi kwamba pengine maana ya neno hilo lina maana ya wanasiasa ambao labda wanafanya kazi zao ndani ya Beltway (Washington) kwa maana ya Maseneta na Congressmen na Congresswomen.
Lakini kadiri ambavyo bwana huyu alikuwa analisikia neno hili baadae ndio akaja kuelewa maana halisi ya "Beltway Politician".
Wanasiasa ndani ya Washington wanalitumia neno hili kuwaelezea wanasiasa wenzao ambao wanawahisi kuwa ni 'insiders' kwenye muhimili ambao sio serikali na wala sio bunge. Kwamba kuna muhimili wenye nguvu sana ndani ya Washington lakini sio serikali, sio mahakama na wala sio bunge na kuna baadhi ya wanasiasa wenzao ambao wanawashuku kuwa sehemu ya 'muhimili' huu.

Sasa, miaka ya hivi karibuni baada ya kuibuka matumizi ya neno "Deep State" akili yangu moja kwa moja zikakumbuka kumbukumbu ile ya miaka ile Washington ambapo kwa mara ya kwanza bwana yule alilisikia neno "Beltway Politicians".
Sasa je, Beltway Politicians ndio Deep State?? Jawabu ni hapana… Beltway Politician ni kasemu kadogo tu ndani ya Deep State. Deep State ni kitu kikubwa zaidi na hakuna muda ambao tunapaswa kuelewa kuhusu Deep State kama sasa..


Tuanze… kwa mara ya kwanza kabisa niiweke hii taarifa.
Nakala iende Kisarawe…


Twafahamu kuwa document yeyote kwenye serikali zetu zote duniani ambazo hazina ruhusa ya kuonwa na watu wengine zaidi ya walengwa huwa zina muhuri wa siri. Mara nyingi documents hizi zinakuwa zimebeba taarifa ambazo ni 'sensitive' na kama ikitokea kuonwa na watu wasiopaswa basi inaweza kuwa na madhara kwenye utunzaji wa usiri wa baadhi ya masuala yenye maslahi ya usalama wa nchi.

Serikali zote na Idara zote za ujasusi duniani wana mamia kama sio maelfu ya documents za namna hii zinazohitaji usiri.

Sasa,
Pale Marekani kama ilivyo kwa nchi nyingine nao wana maelfu ya document za namna hii.
Lakini katika documents hizo ziko documenst mbili ambazo kwa maoni yangu document hizi ni 'sensitive' zaidi kuliko document nyingine zozote zile… lakini ajabu document hizo mbili zote hazina muhuri wa SIRI na jambo la ajabu ni kwamba mpaka leo hii ninapoandika document hizi hazijawahi kuvuja mtandaoni.

Ziko mbili nyaraka hizi.. extremly sensitive lakini hazina muhiri wa siri na hazijawahi kuvuja na ndio maana hujawahi kuzisikia, na kamwe hutokuja kuwahi kuziona popote pale.

Nyaraka ya kwanza kati ya hizi mbili haina jina maalumu/mahususi hasa lakini ingekuwa hapa nchini kwetu kwenye kitengo cha kumlinda Mzee, basi watoto wa kijiweni 'Kisarawe' wageweza kuifahamu kwa jina la “Site Post Assignment Log."
Vijana wetu hapa nchini ya kwao wanaiita jina hilo lakini ile ya pale Marekani inayotumiwa na vijana wa Secret Service haina jina mahususi sana japo dhumuni ni la kufanana kabisa na hata la hawa wa hapa kwetu nyumbani.
Kwa hiyo mniruhusu hata hiyo ya Secret Service niite jina hilo hilo kwa minajiri ya kwenda sambamba kwenye kufanya rejea.

Sasa hii “Site Post Assignment Log" ya pale Marekani inayotumiwa na Secret Service yenyewe ndani yake inakuwa na jina la tukio, tarehe, saa alafu kisha unafuata mfululizo wa namba na herufi ambazo ziko kwenye codes.
Hii “Site Post Assignment Log" yenyewe inatumika kuonyesha maafisa wote wa Secret Service siku ya tukio fulani husika watakuwa wapi, watajipangaje, yupi atakuwa wapi, mbinu zitakazotumika kuimarisha ulinzi, procedures za emergency za kumuokoa Rais kama ikitokea kuna shambulio pamoja na code zote za ulinzi ambazo zitatumila kwenye hiyo siku husika.
Taarifa zote hizi zinakuwa kwenye hiyo nyaraka nyeti ya "Site Post Assignment Log".


Sasa,
Ikulu ya Marekani wana utamaduni kila mwaka wanafanya tukio linaitwa White House Correspondents’ Dinner. Hiki huwa ni chakula cha jioni ambacho kinaandaliwa na Ikulu kwa ajili ya wanahabari ambao wanaripoti habari za Ikulu kutoka kwenye vyombo vyote vya habari.
Mgeni rasmi anakuwa no Rais na anajumuika na wanahabari hao kupata chakula cha jioni lakini pia mara zote huwa anaalika pia na watu mbalimbali mashuhuri.
Tukio hilo japo linaandaliwa na Ikulu lakini huwa halifanyiki Ikulu. Huwa linafanyika kwenye moja ya Hoteli mashuhuri ambayo itachaguliwa kwa mwaka huo.

Kama umewahi kuona video mtandaoni ya Obama 'anampiga madongo' Trump kwa utani na mizaha mpaka Trump anafura na uso kuwa mwekundu kwa hasira, sasa video ile ni ya moja ya matukio kama hilo la Chakula cha jioni enzi za Urais wa Obama.

Sasa, niwapeleke kwenye White House Correspondents’ Dinner ya mwaka 2011. Hii yenyewe ilifanyika tarehe 30 April.
Wahudhuriaji walikuwa hao wanahabari wenyewe, Rais Obama, mkewe Michelle, Mwanasheria Mkuu, Mwenyekiti wa Joint Chief of Staffs, Mkurugenzi wa CIA, Magavana wa majimbo sita walikuwepo, wabunge ishirini na sita wa Congress, Meya wa New York, Waziri mwenye dhamana ya Hazina pamoja na watu wengine kadhaa muhimu.

Wote hawa walikuwa sehemu hii moja kwa wakati mmoja… kwenye hii dhifa.

Sisi tulioko nyumbani ambao tunatazama kwa runinga matukio haya huwa tunaburudika kwa hotuba mwanana pamoja na utani wa comedians ambao mara zote huwa ndio ma-MC wa shughuli hizi. Lakini kiusalama tukio kama hili huwa ni moja la kupasua kichwa kwa wanausalama wanaomlinda rais Secret Service.
Sababu tarehe ya tukio hili na mahala ambapo litafanyika huwa inatangazwa miezi kadhaa kabla. Fikiria kama wewe ni mtu mwenye nia mbaya dhidi ya Rais, yaani miezi kadhaa kabla, unakuwa unafahamu Rais pamoja na karibia nusu ya serikali yote watakuwa wapi, tarehe ngapi na saa ngapi… fursa adhimu iliyoje.


Tukio hili la mwaka 2011 lilikuwa linafanyika Hoteli inayoitwa Washington Hilton (siku hizi inaitwa Hinckley Hilton). Ni hoteli hii hii ambayo mwaka 1981 Rais Ronald Regan alishambuliwa kwa risasi.

Wageni wote waalikwa walikuwa wamewasili, na zilikuwa zimebakia kama dakika ishirini tu kabla msafara wa Rais Obama kuwasili. Wakati wanausalama wanafanya 'sweep' za mwisho mwisho ka la ta msafara wa Rais kuwasili, moja ya Maafisa Usalama walioko Ikulu akawasiliana na wenzake walioko eneo la tukio kwamba moja ya mabinti ambao ni Staff wa Ikulu alikuwa amepoteza PIN za kumpa accesss ya maeneo ambayo Secret Service huyaita 'sensitive areas' ndani ya Ikulu..




Inaendelea…



Habib "The Bold" - 0718 096 811 (WhatsApp)
To Infinity and Beyond

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom