Marwa_J_Merengo
JF-Expert Member
- Aug 6, 2018
- 4,512
- 6,882
Nakukubari sana mkubwa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kutoka wuhan mpaka huku..kila siku nahisi tunaacha njia.
sent from Samsung Galaxy A30
the bold ndio mtu pekee alieniingiza JF nilikuwa napita kama guest kitambo tu Ikabidi ni signed in kwa sababu ya huyu mwamba the real definition of the Great thinkerJamii forum imerudi kwenye ubora wake yaani THE BOLD NA MSHANA JR ndo watu wamenifanya nikapendaga JF
Sent using Jamii Forums mobile app
nakubali kamanda 🙏DEEP STATE, COVID-19: Nini Maana ya Uhandisi Jaamii Unaotokea Duniani?
#7
Ni nani yule pembemi ya James Clapper (aliyesimama nyuma ya Robert Gates).
Kwa nini Ikulu ya Marekani wamekataa kumtaja jina mpala leo hii.
Kama umewahi kusoma simulizi yangu ya Vipepeo Weusi mara kadhaa juu kabisa mwanzoni huwa naandika kwamba simulizi ile iko 'inspired by true events'. Simulizi ile ya Vipepeo Weusi ni Riwaya ambayo nimeitengeneza lakini ndani yake kuna matukio ambayo ni ya kweli yaliyo amsha hari ndani yangu na hatimaye kuandika simulizi ya namna ile.
Kwa hiyo next time ukiona nimeiweka simulizi ya Vipepeo Weusi hakikisha unaisoma maana kuna mambo mengi sana adhimu kuhusu nchi yetu ambayo namna pekee naweza kuyaandika ni kwa kuyaweka kwenye simulizi ya namna ile.
Mojawapo ya matukio haya ya kweli… kuna mahala kwenye 'Season One' ya ile Riwaya niliandika kwamba Ray kupitia Taasisi yake ya SOTE HUB alisaidia vijana kadhaa kupata ufadhili wa kuanzisha kampuni. Mojawapo ya vijana hao walioanzisha kampuni kulikuwa na kijana wa Kimasai ambaye alianzisha kampuni ya Ulinzi.
Katika maisha ya halisi ni kwamba… kipindi nasoma Chuo Kikuu Mzumbe, tulifanikiwa 'kunusa' dili fulani hivi. Kuna kampuni toka Australia waliingia pale Morogoro kufanya shughuli fulani maeneo ya Ifakara na Kilosa. Nilikuwa na rafiki yangu anaitwa George tukafanikiwa kuwashawishi wageni hao watupe jukumu la Ulinzi.
Hatukuwa na kampuni, tulikuwa wanafunzi tu.. usiulize tulifanikiwaje kuwashawishi, hakuna linaloshindikana chini ya jua ukiwa na 'motivation'.
Kwa hiyo tukaanza kuhaha kusajili kampuni ya Ulinzi. Kimbembe kikaja urasimu wa namna ya kupata vibali kwa ajili ya silaha za moto (kwa ajili ya vijana watakaokuwa wanalinda).
Kuna vitu vingi sana tulikuwa hatujivui kabla na mchakato ulikuwa ni mgumu kuzidi vile ambavyo tulidhani.
Ndipo kwa mara ya kwanza nikafahamihana na Mstahiki Naibu Meya Isihaka Sengo. Naam huyu Sengo Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro aliyefariki wiki jana akarushwa sana kwenye mitandao ya kijamii.
Huyu bwana ana kampuni kubwa sana ya Ulinzi pale Morogoro inaitwa Sengo Security. Tukamfuata ili atusaidie michakato ya kupata vibali vya vijana wetu kuruhusiwa kubeba silaha.
Hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuonana na nguli huyo na nilijifunza vingi sana toka kwake. Mara ya pili kufanya nae kazi ilikuwa mwala 2017 kwenye uchaguzi wa marudio Kata ya Kiwanja cha Ndege. Diwani wao Godi Mkondya alifariki.. mpwa akasema anautaka udiwani, na si udiwani tu bali Unaibu Meya na hatimaye 2020 Umeya kamili.
Mpwa akaniomba 'nichore mchoro'… mchoro ukachorwa, asubuhi tu saa nne tukatangaza ushindi.
Sasa kipindi kile niko chuo, nguli huyu kwa muda wa siku tatu akatupitisha kwa kila Idara zinayohusika kwa ajili ya vibali na leseni... lakini mwishowe mimi na mwenzangu tukafikia hitimisho kwamba haiwezekani kwa haraka hivyo tupate hivyo vibali.
Wanasema shida mgunduzi… ndio tukaja na wazo la Morani Security. Tuchukue vijana wa kimasai pekee wawe wanalinda na silaha zao za jadi wakiwa ndani ya mavazi yao yale ya asili.
La haula. .Wale wazungu walikoshwa roho kweli kweli na wazo hilo jipya.
Najaribu kusemaje.?
Waona hapa kwetu ni namna ni ngumu kweli kweli na mlolongo mrefu wenye urasimu kupindukia ili kupata leseni na vibali kwa vijana wa kampuni za ulinzi kubeba magobore tu (kama ndio unaanza) pengine kutokana na mazingira ya utete wa nchi zetu hizi..
Lakini wenzetu huko magharibi watu wanamiliki sio tu 'kampuni za Ulinzi'bali wanamiliki 'private military'.
Mara kadhaa kwenye makala hii nimetaja 'private military', nikiongelea private military kichwani usidhani kwamba labda ni kama hizi kampuni za ulinzi kama za kina Sengo. Hawa wa magharibi ninaowaongelea ni majeshi kamili yaliyokamilika ila hayako chini ya umiliki wa nchi.
Yamekamilika katika namna kwamba wana kambi zao kabisa za kijeshi, wana vyuo vyao vya mafunzo, wana ndege za kivita, boti za kivita, makombora, magari ya kivita, idara za intelijensia n.k.
Yaani ni jeshi kamili kabisa ambalo limekamilika lakini haliko chini ya nchi, linamilikiwa na watu binafsi.
Naam, kuna viti hawawezi kumiliki… silaha kama ICBM au nuclear warheads, biowepons… lakini majeshi haya ni majeshi kamilo kabisa. Wanaweza kuchakaza kabisa nchi zetu hizi za ulimwengu wa tatu kwa wiki tu.
Utamu zaidi majeshi haya binafsi mara zote wanaajiri watu toka majeshi ya serikali ambao wametumikia kwenye vikosi vya weledi kama vile Navy Seals, Delta, Rangers, Marine RECON, Air Force ST n.k. yaani wana ajiri wanajeshi ambao walikuwa 'cream' kwenye majeshi ya serikali.
Ndio maana majeshi haya binafsi PMC yamekuwa kiungo adhimu kwenye vita zote ambazo unaona Marekabi anapigana.
Kwa hiyo mara zote nataka ukiona naongelea majeshi binafsi pale Marekani ujue naongelea kitu adhimu na cha weledi wa kiasi gani.
Maana yawezekana wengine waliwaza iliwezekana vipi "ultimate security" wenye magobore wamlinde Obama siku ile ya April 30.
Hawa watu, PMC ni watu wa weledi wa juu kabisa lakini hawako chini ya serikali jambo ambalo huku kwetu haliwezekani abadani.
Sasa,
Yule jamaa pale kwenye picha Situation Room ni nani??
Tuanze kuunga nukta alafu tuelewe ni kwa jinsi gani Deep State inaendesha ulimwengu itakavyo.
Nakutambulisha kwa mtu adhimu mno anaitwa James Steele.
Siku ambayo picha hii inapigwa, yaani May 1, 2011.. kumbukumbu zinainyesha kwamba James Steele alikuwa ni CEO wa Kampuni inayoitwa Buchanan Renewables Energy (BRE).
Unajui hii kampuni iko wapi?
Uarabuni? Hapana..
Marekani? Hapana…
Ulaya? Hapana…
Kampuni hii ya Buchanan Renewables Energy Makao makuu yako 'barazani' kwetu hapa hapa Africa nchini Liberia.
Kwa mujibu wa taarifa zilizo kwenye tovuti ya kampuni hii (kipindi cha mwaka 2012 kurudi nyuma) wanajieleza kwamba wanazalisha umeme kwa kutumia biomass ya miti mikuu kuu ya mpira.
Sasa nianze kwa kukujuza mapema kabisa… kampuni hii ni 'front organisation' ya shughuli za ujasusi na waliingia pale Liberia miezi michache tu baada ta vita ya wenyewe kwa wenyewe kumalizika.
Nisizunguke sana… nikueleze, huyu James Steele ni nani? Hawa BRE walikuwa wanafanya nini Liberia… kisha tutaelewa kwa nini wengi tunaamini yule bwana mwenye suti nyeusi na tai jeupe ambaye haonekani kwenye picha ni James Steele.
Kama haujasoma simulizi yangu ya Geranimo nakushauri uisome maana kama haujaipitia kwente hivi vitu ambavyo naenda kuelezea hapa baadhi naweza kukuacha Chalinze..
Hapa nitawaeleza wote wawili kwa pamoja… kampuni ya Booz Allen na James Steele ili tusiache kipore chochote.
Ni kwamba..
Karibu nusu ya Intelligence Bugdet ya Marekani inaenda kwa makampuni binafsi ambayo vyombo hivi vya intelijensia vina 'out-source' shughuli na huduma muhimu toka kwao. Fahamu kwamba, mfano kwa mwaka huu 2020 Marekani wanatumia dola bilioni 62 kwa ajili Idara za Intelijensia za 'kiraia' (mfano Central Intelligence Agency CIA, National Security Agency NSA, Bureau of Intelligence and Research INR, Central Security Services CSS na kadhalika).
Pia Marekani kwa mwaka huu inatumia zaidi ya dola bilioni 23 kwa ajili ya idara za intelijensia za jeshi. Kwa hiyo wa jumla ya karibia kama dola bilioni 100 (kama Shilingi Trilioni 230 za Kitanzania) kwa ajili ya Intelijensia tu.
Sasa nusu ya hii bajeti ya intelijensia inakuwa out-sourced nje kwenye makampuni binafsi. Na papo hapo kwenye hiyo nusu ya bajeti ambayo inaenda kwa makampuni binafsi asilimi sabini (70%) inaenda kwa kampuni ya Booz Allen.
Sasa, ni huduma gani hasa Idara za Intelijensia za Marekani wanazipata toka Booz Allen.?
Hawa Booz Allen ni kama "CIA" inayojitegemea binafsi.
Yaani waona pale juu nilieleza juu ya uwepo wa majeshi binafsi PMC kama vile Triple Canopy na Blackwaters… sasa hawa Booz Allen wenyewe ni kampuni inayojihusisha na masuala ya ukusanyaji Intelijensia na Ujausi lakini hawako chini ya serikali.. inamilikiwa na watu binafsi.
Kwenye tovuti yao hawa Booz Allen wanajipambanua kama kampuni ya "Management and Information Technology Consulting Firm". Lakini hawa mabwana wana mkono wao kwenye karibia kila tukio kubwa unaloliona linatokea.
Yaani ni kama vile hapa Tanzania tuna Usalama wa Taifa pale Oysterbay… alafu papo hapo kuwe na kampuni fulani iko pale Victoria iwe yenyewe inafanya kazi kama ya Usalama wa Taifa lakini hawako chini ya serikali.. wanajitegemea.
Unaweza kujiuliza ni kwa namna gani serikali inaweza kuruhusu kuwe na kampuni ya namna hii?
Sababu ni kwamba kuna shughuli ambazo serikali hawawezi kuzifanya inabidi watu toka nje ya serikali wazifanye.
Nikupe mfano mdogo tu…
Unakumbuka lile sekeseke la Arab uprising?
Lile vuguvugu la mwaka 2010 na 2011 wananchi wakipindua serikali zao kwenye nchi za Kiarabu??
Tunaendelea..
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani umeitwa kuja kusoma hizi kitu?Unabore sana maelezo mengi hueleweki hata unataka stori iwe ndefu kuna mdau hapaaa Mizani kaandika shortcut flani lakini kaeleweka mi kuanzia leo sisomi story zako ubabaishaji ni mwingi
Unabore sana maelezo mengi hueleweki hata unataka stori iwe ndefu kuna mdau hapaaa Mizani kaandika shortcut flani lakini kaeleweka mi kuanzia leo sisomi story zako ubabaishaji ni mwingi
Kwani umeitwa kuja kusoma hizi kitu?
Everything is not for everyone!
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama Una CHUKI vaa MIWANI usione GEREUnabore sana maelezo mengi hueleweki hata unataka stori iwe ndefu kuna mdau hapaaa Mizani kaandika shortcut flani lakini kaeleweka mi kuanzia leo sisomi story zako ubabaishaji ni mwingi
Hongera mkuu! Ila unatuweka sana tunapoteza connectivity, Allah akupe wepesi Inshaalah uendelee kushusha nondo hizi nzito.DEEP STATE, COVID-19: Nini Maana ya Uhandisi Jaamii Unaotokea Duniani?
#7
Ni nani yule pembemi ya James Clapper (aliyesimama nyuma ya Robert Gates).
Kwa nini Ikulu ya Marekani wamekataa kumtaja jina mpala leo hii.
Kama umewahi kusoma simulizi yangu ya Vipepeo Weusi mara kadhaa juu kabisa mwanzoni huwa naandika kwamba simulizi ile iko 'inspired by true events'. Simulizi ile ya Vipepeo Weusi ni Riwaya ambayo nimeitengeneza lakini ndani yake kuna matukio ambayo ni ya kweli yaliyo amsha hari ndani yangu na hatimaye kuandika simulizi ya namna ile.
Kwa hiyo next time ukiona nimeiweka simulizi ya Vipepeo Weusi hakikisha unaisoma maana kuna mambo mengi sana adhimu kuhusu nchi yetu ambayo namna pekee naweza kuyaandika ni kwa kuyaweka kwenye simulizi ya namna ile.
Mojawapo ya matukio haya ya kweli… kuna mahala kwenye 'Season One' ya ile Riwaya niliandika kwamba Ray kupitia Taasisi yake ya SOTE HUB alisaidia vijana kadhaa kupata ufadhili wa kuanzisha kampuni. Mojawapo ya vijana hao walioanzisha kampuni kulikuwa na kijana wa Kimasai ambaye alianzisha kampuni ya Ulinzi.
Katika maisha ya halisi ni kwamba… kipindi nasoma Chuo Kikuu Mzumbe, tulifanikiwa 'kunusa' dili fulani hivi. Kuna kampuni toka Australia waliingia pale Morogoro kufanya shughuli fulani maeneo ya Ifakara na Kilosa. Nilikuwa na rafiki yangu anaitwa George tukafanikiwa kuwashawishi wageni hao watupe jukumu la Ulinzi.
Hatukuwa na kampuni, tulikuwa wanafunzi tu.. usiulize tulifanikiwaje kuwashawishi, hakuna linaloshindikana chini ya jua ukiwa na 'motivation'.
Kwa hiyo tukaanza kuhaha kusajili kampuni ya Ulinzi. Kimbembe kikaja urasimu wa namna ya kupata vibali kwa ajili ya silaha za moto (kwa ajili ya vijana watakaokuwa wanalinda).
Kuna vitu vingi sana tulikuwa hatujivui kabla na mchakato ulikuwa ni mgumu kuzidi vile ambavyo tulidhani.
Ndipo kwa mara ya kwanza nikafahamihana na Mstahiki Naibu Meya Isihaka Sengo. Naam huyu Sengo Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro aliyefariki wiki jana akarushwa sana kwenye mitandao ya kijamii.
Huyu bwana ana kampuni kubwa sana ya Ulinzi pale Morogoro inaitwa Sengo Security. Tukamfuata ili atusaidie michakato ya kupata vibali vya vijana wetu kuruhusiwa kubeba silaha.
Hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuonana na nguli huyo na nilijifunza vingi sana toka kwake. Mara ya pili kufanya nae kazi ilikuwa mwala 2017 kwenye uchaguzi wa marudio Kata ya Kiwanja cha Ndege. Diwani wao Godi Mkondya alifariki.. mpwa akasema anautaka udiwani, na si udiwani tu bali Unaibu Meya na hatimaye 2020 Umeya kamili.
Mpwa akaniomba 'nichore mchoro'… mchoro ukachorwa, asubuhi tu saa nne tukatangaza ushindi.
Sasa kipindi kile niko chuo, nguli huyu kwa muda wa siku tatu akatupitisha kwa kila Idara zinayohusika kwa ajili ya vibali na leseni... lakini mwishowe mimi na mwenzangu tukafikia hitimisho kwamba haiwezekani kwa haraka hivyo tupate hivyo vibali.
Wanasema shida mgunduzi… ndio tukaja na wazo la Morani Security. Tuchukue vijana wa kimasai pekee wawe wanalinda na silaha zao za jadi wakiwa ndani ya mavazi yao yale ya asili.
La haula. .Wale wazungu walikoshwa roho kweli kweli na wazo hilo jipya.
Najaribu kusemaje.?
Waona hapa kwetu ni namna ni ngumu kweli kweli na mlolongo mrefu wenye urasimu kupindukia ili kupata leseni na vibali kwa vijana wa kampuni za ulinzi kubeba magobore tu (kama ndio unaanza) pengine kutokana na mazingira ya utete wa nchi zetu hizi..
Lakini wenzetu huko magharibi watu wanamiliki sio tu 'kampuni za Ulinzi'bali wanamiliki 'private military'.
Mara kadhaa kwenye makala hii nimetaja 'private military', nikiongelea private military kichwani usidhani kwamba labda ni kama hizi kampuni za ulinzi kama za kina Sengo. Hawa wa magharibi ninaowaongelea ni majeshi kamili yaliyokamilika ila hayako chini ya umiliki wa nchi.
Yamekamilika katika namna kwamba wana kambi zao kabisa za kijeshi, wana vyuo vyao vya mafunzo, wana ndege za kivita, boti za kivita, makombora, magari ya kivita, idara za intelijensia n.k.
Yaani ni jeshi kamili kabisa ambalo limekamilika lakini haliko chini ya nchi, linamilikiwa na watu binafsi.
Naam, kuna viti hawawezi kumiliki… silaha kama ICBM au nuclear warheads, biowepons… lakini majeshi haya ni majeshi kamilo kabisa. Wanaweza kuchakaza kabisa nchi zetu hizi za ulimwengu wa tatu kwa wiki tu.
Utamu zaidi majeshi haya binafsi mara zote wanaajiri watu toka majeshi ya serikali ambao wametumikia kwenye vikosi vya weledi kama vile Navy Seals, Delta, Rangers, Marine RECON, Air Force ST n.k. yaani wana ajiri wanajeshi ambao walikuwa 'cream' kwenye majeshi ya serikali.
Ndio maana majeshi haya binafsi PMC yamekuwa kiungo adhimu kwenye vita zote ambazo unaona Marekabi anapigana.
Kwa hiyo mara zote nataka ukiona naongelea majeshi binafsi pale Marekani ujue naongelea kitu adhimu na cha weledi wa kiasi gani.
Maana yawezekana wengine waliwaza iliwezekana vipi "ultimate security" wenye magobore wamlinde Obama siku ile ya April 30.
Hawa watu, PMC ni watu wa weledi wa juu kabisa lakini hawako chini ya serikali jambo ambalo huku kwetu haliwezekani abadani.
Sasa,
Yule jamaa pale kwenye picha Situation Room ni nani??
Tuanze kuunga nukta alafu tuelewe ni kwa jinsi gani Deep State inaendesha ulimwengu itakavyo.
Nakutambulisha kwa mtu adhimu mno anaitwa James Steele.
Siku ambayo picha hii inapigwa, yaani May 1, 2011.. kumbukumbu zinainyesha kwamba James Steele alikuwa ni CEO wa Kampuni inayoitwa Buchanan Renewables Energy (BRE).
Unajui hii kampuni iko wapi?
Uarabuni? Hapana..
Marekani? Hapana…
Ulaya? Hapana…
Kampuni hii ya Buchanan Renewables Energy Makao makuu yako 'barazani' kwetu hapa hapa Africa nchini Liberia.
Kwa mujibu wa taarifa zilizo kwenye tovuti ya kampuni hii (kipindi cha mwaka 2012 kurudi nyuma) wanajieleza kwamba wanazalisha umeme kwa kutumia biomass ya miti mikuu kuu ya mpira.
Sasa nianze kwa kukujuza mapema kabisa… kampuni hii ni 'front organisation' ya shughuli za ujasusi na waliingia pale Liberia miezi michache tu baada ta vita ya wenyewe kwa wenyewe kumalizika.
Nisizunguke sana… nikueleze, huyu James Steele ni nani? Hawa BRE walikuwa wanafanya nini Liberia… kisha tutaelewa kwa nini wengi tunaamini yule bwana mwenye suti nyeusi na tai jeupe ambaye haonekani kwenye picha ni James Steele.
Kama haujasoma simulizi yangu ya Geranimo nakushauri uisome maana kama haujaipitia kwente hivi vitu ambavyo naenda kuelezea hapa baadhi naweza kukuacha Chalinze..
Hapa nitawaeleza wote wawili kwa pamoja… kampuni ya Booz Allen na James Steele ili tusiache kipore chochote.
Ni kwamba..
Karibu nusu ya Intelligence Bugdet ya Marekani inaenda kwa makampuni binafsi ambayo vyombo hivi vya intelijensia vina 'out-source' shughuli na huduma muhimu toka kwao. Fahamu kwamba, mfano kwa mwaka huu 2020 Marekani wanatumia dola bilioni 62 kwa ajili Idara za Intelijensia za 'kiraia' (mfano Central Intelligence Agency CIA, National Security Agency NSA, Bureau of Intelligence and Research INR, Central Security Services CSS na kadhalika).
Pia Marekani kwa mwaka huu inatumia zaidi ya dola bilioni 23 kwa ajili ya idara za intelijensia za jeshi. Kwa hiyo wa jumla ya karibia kama dola bilioni 100 (kama Shilingi Trilioni 230 za Kitanzania) kwa ajili ya Intelijensia tu.
Sasa nusu ya hii bajeti ya intelijensia inakuwa out-sourced nje kwenye makampuni binafsi. Na papo hapo kwenye hiyo nusu ya bajeti ambayo inaenda kwa makampuni binafsi asilimi sabini (70%) inaenda kwa kampuni ya Booz Allen.
Sasa, ni huduma gani hasa Idara za Intelijensia za Marekani wanazipata toka Booz Allen.?
Hawa Booz Allen ni kama "CIA" inayojitegemea binafsi.
Yaani waona pale juu nilieleza juu ya uwepo wa majeshi binafsi PMC kama vile Triple Canopy na Blackwaters… sasa hawa Booz Allen wenyewe ni kampuni inayojihusisha na masuala ya ukusanyaji Intelijensia na Ujausi lakini hawako chini ya serikali.. inamilikiwa na watu binafsi.
Kwenye tovuti yao hawa Booz Allen wanajipambanua kama kampuni ya "Management and Information Technology Consulting Firm". Lakini hawa mabwana wana mkono wao kwenye karibia kila tukio kubwa unaloliona linatokea.
Yaani ni kama vile hapa Tanzania tuna Usalama wa Taifa pale Oysterbay… alafu papo hapo kuwe na kampuni fulani iko pale Victoria iwe yenyewe inafanya kazi kama ya Usalama wa Taifa lakini hawako chini ya serikali.. wanajitegemea.
Unaweza kujiuliza ni kwa namna gani serikali inaweza kuruhusu kuwe na kampuni ya namna hii?
Sababu ni kwamba kuna shughuli ambazo serikali hawawezi kuzifanya inabidi watu toka nje ya serikali wazifanye.
Nikupe mfano mdogo tu…
Unakumbuka lile sekeseke la Arab uprising?
Lile vuguvugu la mwaka 2010 na 2011 wananchi wakipindua serikali zao kwenye nchi za Kiarabu??
Tunaendelea..
Sent using Jamii Forums mobile app
Ingawa posti yako
Mkuu Trimmer Ahsante kunivuta shati. Academically ndivyo itakiwavyo.
James J. Angleton. Kama binadam wote tulivyo mapungufu hayakosi hakuna aliekamilika. Huyu Mzee Hana sifa nzuri Marekani kwa wanafuatilia. Nafasi aliodumu nayo ya Jasusi Mkuu wa Counter Intelligence, nafikiri inahitaji hekima ukizingatia Mamlaka ya Top CI officer kifedha (bajeti yake Ni ile inayoitwa blank check andika numba mwenyewe), amri, watumishi, teknolojia na muundo wa taasisi alioyotumikia CIA. Kwa uchache alikua na nguvu nyingi kiasi akataburi na pia alikua mkurupukaji. Mambo mengi ya hovyo aliyafanya bila hata kupewa ruhusa na Taasisi au Kamati zilizowekwa Kuitazama CIA. Na Ndio kilichopelekea William Colby Director wa CIA kumfukuza kazi Desemba 1974. unaweza kugoogle "who fired James Angleton" kupata hii habari. Nitanukuu sources zangu mwisho wa Mantiki au repoti hii. Ni-ukurupukaji wake ambao Umeigharimu Africa Viongozi mahodari na maisha kama yalivyo. Ukizingatia Mauaji ya Patrice Lumumba 1961, kupinduliwa kwa Kwame Nkurumah 1965 wote wawili bila James hajapewa ruhusa na Wala hawakua na Nia mbaya na Marekani. Nkurumah graduated from Massachusetts Institute of Technology, kukamatwa kwa Nelson Mandela 1962 makaburu washashindwa kumnasa Mandela akiwatoka all the times, Hadi walipopata zawadi toka CIA.
Operation/Project MKULTRA au kwa kina lingine Mind Control Program. Ni jitihada zilizoanzishwa kabla James Angleton hajaaza kazi. Marekani waliitwaa toka kwa Wanazi Ujerumani ya Adolf Hitler baada ya Kushinda Vita 1945. Nazi Ndio walikuwa wakifanya experiment ya binadam. Baada ya vita Marekani ikachukua Wanasayansi na kuwapeleka Amerika. Kwa hiyo MK ULTRA ikaendelezwa, Jeshi wakawapa CIA (inawezekana waliona ni upuuzi si unajua majeda hawapotezagi muda). Hata hivo haikufanikiwa, iliishia kuua wamarekani wawili na kilichobaki Ni mbinu za kutesa watu. Lakini, Mzee Angleton aliing'ang'ani kwa Siri hadi iliposhtukiwa na kufishwa. Soma kitabu Operation Paperclip by Anne Jacobsen.
Operation MKCHAOS, ambayo ilianzishwa chini yake, ndiyo iliokua kijipu uchungu Hadi Akatumbuliwa baadha ya New York Times kufichua Siri ambapo Bunge ikabidi wafanye uchunguzi ukiongozwa na Seneta Frank Church na kugundua madudu Ya CIA ikiwemo kifo cha Lumumba, chaos, na kadhalika. William Colby akamtumbua.
CHAOS ilikua Ni program ya kuchunguza raia wa Marekani Activists. CIA ilikua haturuhusiwi kufanya kazi yake ndani. Hadi wapate ruhusa. Basi kwa hii CHAOS wenye maroho mabaya ndo wakapata Sababu ya kugandamiza wanyonge hasa hasa Black Americans ambao walikua Wanapambana juu ya Ubaguzi wa rangi (Ukaburu) enzi za miaka ya sitini 1960s kwa kuwa Neutralized ikiandikwa hivo ujue Ni kuwadedisha. Imprisoned, public humiliated, na Mashtaka ya uongo, katika walikumbwa na UHANDISI JAMII wa Bwana mkubwa ni Mchungaji Martin Luther King Jr, Fred Hampton, Mark Clark, Zayd Shakur, Gerenimo Pratt (Vietnam Green Barret) ambae nadhani kazikwa Arusha Tanzania 2011. listi Ni ndefu Ikiwemo Mumia Abu Jamal
Pia Kuleta Mara kibao tani na tani za Cocaine na Opium kutawanya mitaani hasa mitaa ya Watu weusi
KWA HIO UKISIKIA "UHANDISI JAMII" NDO IVO Wakuu. Baadae Wakawa wanagawa Bunduki kwenye mitaa ya Black Amerika. piga esabu. Mwanangu, Vijana Weusi wasiraruane kama machizi kwa nini
Skando yake nyingine ni failure ya Operation Bay of Pigs Cuba 1961. alikusanya wakyuba karibia 1500 wakafundishwa kutumia silaha na mbinu kidogo wakapewa vifaa na kushushwa sehemu inayoitwa Bays of Pigs (ghuba ya Nguruwe). Castro kashitukia ngoma wote mbaroni. Aibu kubwa. Na kilichoteka baadae hakiwezi kusahaulika. Hadi leo Amerika haivamii cuba Ni maili 280 tu. Matokeo ya ukurupukaji wa Mzee James
Yani kwa kifupi kwa navoona kwa rekodi nafikiri Aliiathiri Taasisi ya CIA kuliko kujenga. na inawezekana alipata kazi Sababu baba yake aliwahi kuwa stesheni chifu Italy. Ukiritimba upo Kila sehemu.
Angleton sie Aliebuni mbinu za hadaa. Mtu alitoa mbinu za hadaa anaitwa JOHN MULLHOLAND aliekua mfanyaji Mazingaombwe kabla ya afisa wa CIA. Yeye Ndio alietunga kitabu Cha Ujanja na Upotezaji) Manual. (Trickery and Misdirection). baadae kikaitwa Kitabu Cha Ujanja na Hadaa (Trickery and Deception). Sasa ikiwa bwa mzee alibadilisha jina la Manual sidhani inampa wadhifa wa Mtungaji.
Ok Kuhusu shehe Ponda. Shehe sio gaidi Wala hahusiani na magaidi wa aina yoyote.
Ponda umaarufu wake umetokana na kukutetea Mali za Waislam ambazo zinahujumiwa na Waislam hao hao waliomo ndani jumuiya yao. kiwastani anatetea haki za kukatiba ya nchi. mfano. Yusuf Manji aliwazuga Viongozi wa kiislam Wamuuzie prime land Mali kinyume Cha sheria Kama alivonunua Bahari Beach Zanzibar. au angetakiwa kutokana na Elimu yake ajue,. nafikiri Ana MBA. Sasa Sheikh Ponda akang'amua na akafanya watu wote hata wasio waislam wajue dhuluma hii (Advocacy). Huyu shehe alekamatwa Italy yeye ngoma yake umeiyona? malengo yao tofauti na visa vyao tofauti. Mtu asiemjua Ponda akisoma mfano ule basi atadhani Ponda gaidi au anata Serikali ya kidini. Hakuna Mtanzania mwenye akili hiyo. Ponda anatetea haki za kikatiba. Soma Katiba ujue haki za Raia. Serikali inakumbushwagwa mjomba na ndo wajibu wa raia. Mchungaji wa Southern Babtist Church Nobel Peace Prize Winner Martin Luther King Jr. alipokua jitahidi kuomba usawa dhidi ubaguzi wa Rangi, James J. Angleton alimuona Kama anahatarisha Amani.
Kwa Waafrika sio tu Usingetakiwa Usimsifie kabisa. Ikiwa wewe sio Mwafrika, I understand. Na Kama ni cut and paste hapo pia I can understand
Ndo maana wanzio wanakuuliza habari umepata wapi. huandiki source ilhali most materials are in public Domain. Yani sio Tena Siri.
bibliography
FIRED DEC. 1974
Documents Reveal the Complex Legacy of James Angleton, CIA Counterintelligence Chief and Godfather of Mass Surveillance/
OPERATION MKCHAOS
Documents Reveal the Complex Legacy of James Angleton, CIA Counterintelligence Chief and Godfather of Mass Surveillance/
HE WAS INSTRAMENTAL ON ASSASSINATION OF PATRICE LUMUMBA, MLK, BLACK NATIONALIST
James Jesus Angleton, the spy whose nightmares propelled the Cold War — Coorabell Ridge
KUMPINDUA KWAME NKURUMAH FEB. 1966. BILA KUIDHINISHWA NA TAASISI HUSIKA. TAYARI TAASISI SIMAMIZI TAYARI ZILIKWISHA KATAA WAZO LA KUMPINDUA
C.I.A. Said to Have Aided Plotters Who Overthrew Nkrumah in Ghana
Four more ways the CIA has meddled in Africa
DRUGS TO AFRICAN AMERICAN LOS ANGELES AND THEN GUNS
Allegations of CIA drug trafficking - Wikipedia
MKULTRA CIA MIND CONTROL PROGRAM
KILLED AT LEAST TWO AMERICANS
Inside the Archive of an LSD Researcher With Ties to the CIA’s MKUltra Mind Control Project/
SOMA KITABU BY ANNE JACOBSEN
OPERATION PAPERCLIP
Operesheni ya Marekani Kuchukua wanasayansi wa Nazi Germany baada ya Kushinda Vita
mm imenishinda nasubiri baadae summaryHii story, msimuliaji ana mambo mengi kichwani anataka kutueleza ila anashindwa kuyaconect... heading ni covid& and deep state ndani kuna story nyingi ambazo hazifiki mwisho na zinakosa connection kabisa
Nimekua msomaji wa makala za The Bold kwa mwaka wa 5 sasa. To be honest hapa kibongo bongo sijaona mwandishi kama The bold(au labda kwa sababu ya usomaji wangu duni wa kazi za watz). Ila brother habib siku hizi naona kama story zako zinakosa udambwiudambwi fulani ivi ulikuoepo enzi zile. Sio kwamba ni mbaya ila kuna ladha fulani inapotea kwa wasomaji wako wa muda watakubaliana na mimi.
You're still one of my fav writers mitaa hii ila check your style mkuu.
Msalimie cheupe