COVID-19: Nani mkweli kati ya Serikali yetu na Ubalozi wa Marekani? Je, Tanzania tunawaogopa sana Wamarekani? Kwanini waseme uongo huu waachwe?

Jambo jema ni kunyamaza na KUWAPUUZA TU
 
Ila hakupaswa kusema kuhusu Data zetu
 
I wouldn't care less about what the Embassy said. The majority of American citizens will come to visit Tanzania after reading other sources of information. Those with money have other channels to obtain their information they do not depend on the embassy buletins. The new president is coming in October and the acting Ambassador is counting her days. The best way for the Government is to ignore her.
 
Tuna wagonjwa hawafiki 60 hivi. mara tumebakiwa na wagonjwa wanne tunadhani kuwa US embassy nao wanasapoti juhudi za magufuli vilevile sio wanafiki cos wanakusanya data na taarifa tofauti fikiria karibia kila siku watu wanakutwa na corona huko mpakani na serikali haisemi chochote.
 
Nilichojifunza kuhusu hii Corona pia, ni pale maripota wote kuhusu Corona nchini Wapo Imara Tu na Afya zao huku kila siku wakiripoti kuwa Corona inamaliza watu

Unajiuliza, Corona inayolipotiwa na kusemwa kuwa ipo na inauwa wengi Sana, Iweje hawa watoa tarifa wasiripoti kuhusu Wao, ama ndugu zao au rafiki zao, Je Corona, Inauwa na kuwaambukiza Watanzania wa aina gani? Hizi ndizo ajabu za kiumbe Corona Nchini mwangu
 
Njia moja tu chukia waandishi wahabari nenda nao wote kwenye vituo vya walipohifadhiwa wagonjwa wa korona wakikuta hamna mtu si wata aibika wao au pima watu wote kuwa hakikishia tupo salama.tatizo hatuonyeshi kwa vitendo tunasema kwa maneno tu.
 
Unatuchosha! Unatuchosha! Unatuchosha!
 
Wiki hii amekufa nani na nani toka jtatu?
 
Pasco unasahau haraka sana, kumbuka Balozi zote za Marekani Duniani zime jaa mashushu wa CIA ambao jukumulao kubwa ni kuhakikisha ulinzi wa Marekani na Maslai ya Marekani, Sasa tangu mgogoro wa Madini uanze, JPM ali zibana kampuni kubwa za uchimbaji wa Madini katika kila Kona jambo ambalo Marekani haijawai kukutananalo popote katikati uwekezaji wake nje ya Marekani.
Sasa walivyo banwa wakawa hawana namna ila kupitia ma Agent wao (CIA) wanatafuta namna ya kutuharibia, na sehemu amayo wanajaribu kwa muda mrefu ni kwenye utalii kwakua iyo sekta imekua inaafanya vizuri katika kuliingizia taifa fedha nyingi za kigeni.
Kama mnakumbuka kuna kipindi 2019 walianza na kuwataarifu raia wao kutakua na shambulizi la Kigidi apa Bongo lengo ni kuwatisha watalii, wakaja na tishio la Zika ila walimtumia mtanzania mwenzetu, na kwasasa wapo na Corona hapa wametu ng'ang'ania.
kinacho wauma kadri wanavyo tubana kwa kuongopa Hospitali zetu zime jaa wagonjwa na serikali yetu inawajibu kwa kuanza kufungua mashule ,vyuo na michezo iki kitendo kinawatesa kwakua watalii wanaona nchi ipo salama na watakuja.
Nashauri serikali ijipange kwasasa wasiwajibu kwakua wanategemea serikali yetu i panic,
Kuendelea kufungua shughulizetu zilizokua zimefungwa kadri hali ya maambukiziwatakavyo uinavyo endelea kupungua.
ilo ni jiu tosha kwa wageni wanaotaka kuja. jamaa watakuja na Visa na mitego mingi kwakua sisi tulipigania maslai ya madini yetu wao wanasimamia unyonyaji kwa maslai ya Marekani. Kinacho fuatia wanasubiri uchaguzi wetu wa 2020 ili wapate sababu za kutu nyoosha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama majina unayo wewe uliyapata wapi? Na mbona hujayaweka. Una mamlaka gani ya kupata hayo majina?
Familia ya Jaji mmoja ilisema hadharani kwamba jina la baba yao kwenye orodha ya waliokufa kwa corona lilikuwa namba 252 , hii ni kwa mujibu wa wanafamikia walioitwa chemba na kuelezwa kilichomuua baba yao , ambapo walisaini daftari maalum , kuna uzi wa takwimu hii humu humu huku ukihanikizwa na habari moto moto kutoka Aljazeera .

Wewe endelea kumsikiliza Ummy.
 
Ukitaka kujua ukweli nenda Amana , Mwananyamala , Hindu Mandal na Agha Khan , ukisikiliza porojo za ummy utaachwa nyuma sana ! USA inayo idadi ya wagonjwa na majina yao wakiwemo marehemu zaidi ya 300
Ni kweli kabisa hata system ya ku collect most of the data za hospital nchini kwa magonjwa mbalimbali ziko funded na wao so they have all information ya all diseases in Tanzania.Shida yeti ni kuficha ukweli wa mambo ukifikiria una Linda wananchi wako.Jana jirani na kwangu kuna vijana 6 wanafanya kazi ufukwe wa bahati ya hindi wanaumwa hoi wamekimbizwa mwananyamala hospital .I was thinking hii itakuwa outbreak ya sikukuu ya idd kwani walikuwa huko wanafanya biashara ndogondogo .
 
Marekani wako sahihi kabisa, tuache ubishi. Soma AYA ya pili kwenye barua niliyoambatanisha hapo ndiyo utajua mkweli na muongo.

View attachment 1467186
Sawa Hawa 11 madereva wa Tz wamekutwa na virus vya Corona, serikali ilitoa takwimu za wagonjwa walio hospitali kuwa 4 tu, hawajasema kuhusu watu wenye virus lakini hawaoneshi dalili yoyote wako wangapi. Hi inatokana nakwamba hakuna mass testing hapa kwetu. Huko mf Kenya wanapima watu wengi kila na huwapata wenye virus
Ila kwakuwa hata wao wamepima watu wachache tu hivyo hawawezi kusema Wana takwimu sahihi za watu wenye virus lakini hawana dalili. Takwimu sahihi ni za wagonjwa walio hospitali tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma with disbelief hii taarifa ya leo ya ubalozi wa Marekani, kwanini ubalozi unatoa taarifa ya uongo kuhusu hali ya COVID-19 nchini kwetu na wanaachwa hivi hivi?!, Jee hawa Wamarekani tunawaogopa?.
Kwenye darasa moja ninalofundisha, huwa nawaambia wanafunzi wangu "perception matters". Bahati mbaya au nzuri maamuzi mengi hufanyika kwa kutumia (based on) perceptions. Kwenye takwimu za COVID 19 inaelekea tumejikanyaga mahali na matokeo yake iwe kweli au la tunakuwa perceived kuwa tunatumia data za kupika na itachukua muda mrefu hadi tuje kuaminika.
Unaweza ukasema na ni haki yako kusema "Kama mpaka sasa update ya Corona kwa Tanzania ilitolewa mara ya mwisho tarehe 29 April wakati huo idadi ya vifo ni 16, na mpaka leo hakuna update hivyo idadi ya waliokufa kwa Corona Tanzania bara ni huo 16 tuu, na huu ndio ukweli wenyewe........(Pascal hapo juu)". Je ni nani anakuamini? Nasikia hatufi tena kwa COVID19 bali kwa matatizo ya kupumua (yakijumlisha pneumonia, asthma, etc).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…