CoViD-19: Siku 30 zijazo ndo muhimu zaidi kujitahadhari, angalia hili jedwali hapa

CoViD-19: Siku 30 zijazo ndo muhimu zaidi kujitahadhari, angalia hili jedwali hapa

Kafrican

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2015
Posts
7,251
Reaction score
7,037
EUcVoy5XsAAVDNn.png




Kwa mwezi mzima, USA ilikua na kesi 15 tu, walidhani wako salama na wameishinda corona!

Siku 22 za kwanza, Italy walikua na kesi tatu tu!!, walidhani wako salama!!!!
Siku 21 za kwanza, Egypt walikua na kesi 3 tu, walidhani hali iko sawa!!!
siku 26 za kwanza, Spain walikua na kesi 7 tu, walidhani hali iko shwari!!!
siku 34 za kwanza, France walikua na kesi 14 tu, walidhani madaktari wako ngangari kuzulia virusi!


Italy, USA, France, Germany, South korea zimekua zikipambana na corona kwa siku zaidi ya 52, Nchi za Africa kando na Egypt na SA, zimekua zikipambana na corona hata siku ishirini hazijapita alafu tunajifanya eti huku kwetu hali si mbaya kama ulaya, kumbe hao jamaa siku ishirini za kwanza hali yao ilikua shwari tu kama vile huku tunadhania.



Alafu, Ukiangalia nchi za USA, Italy, France... kuna mahali flani kwa jedwali utaona kesi zao za siku zilikua zinaongezeka mara mbili ya siku iliopita... Hii ni baada ya wao kuacha kufanyia testing kwa wale walio na dalili (symptoms) za corona pekee na badala yake kufanya mass testing ya watu wote walio safiri hata kama ni kutoka eneo moja la nchi kwenda eneo lengine.....

Kwa mfano, USA sahii ndo inaongoza kwa kesi za crona ikiwa ni kesi 188,000 zilizopatikana positive, lakini ukiangalia USA ilianza kufanya mass testing wiki iliopita, kabla hapo walikua hata hawajui hali kamili



hii tovuti inaonyesha nchi zinazoongoza kwa total tests zilizofanya na nchi by 20th march, wakati huu, USA ilikua haijaripoti kesi nyingi kwasababu walikua wameanya tests 103,000 pekee

1585734901226.png


How many tests for COVID-19 are being performed around the world?


Sahii USA ndo inaongoza kwa kufanya tests kuliko nchi, hakuna nchi inaikaribia kwa test manake wanasema wamefanya 1 million tests, hii ndio maana kesi za USA zimekua zikiongezeka kila uchao hadi kupita kesi za china, Italy, France..etc.....

--------------------
The White House promised an ever-increasing number of coronavirus tests would be available by the end of the month, saying the number of available test kits could be as high as 27 million. But tracking analysts say only about 1 million total tests have been administered nationwide.
The White House promised 27 million coronavirus tests by end of March, but U.S. just hit 1 million
-------------------------


Kenya najua tumefanya tests kama 800 na contact tracing and quaranteen imeika watu 2,000.... Serekali ilitangaza akwamba wataanza kufanya mass testing sijui ni wiki hii au lini, lakini wakianza kufanya, usishtuke ukiona kesi zinaongezeka kwa ma mia kila siku....

current stats as of today, sorted by total cases

1585735245698.png


sorted by total deaths

1585736734314.png





-------------------------------------------------------

Kwahivyo tuwe makini, fwateni maaagizo ya serekali manake hao wengine walikua na kesi chache kwa wiki kadhaa hapo mwanzoni na wakafikiri wako salama, Kumbuka huku Africa tukijaza mahospitali kwasababu ya corona magonjwa mengine ambayo yanaua watu wengi yatawanchwa kutibiwa, watu walio na malaria, ukimwi, watakua hawajisumbui kwenda hospitali manake wanaogopa corona kwahivyo watabaki majumbani waugue kimya kimya... kwahivyo hata kama si watu wengi watauliwa na corona, kuna wengi zaidi watakufa sababu corona ilipewa kipaumbele kwa hospitali zote.


Take care, be safe!
 
Hili Corona baya sana.


Ila naomba Nchi yangu Tz isiingie lockdown, eti tugawiwe wali maharage, hizo kuni za kuivisha maharage, watatuletea?


Ulaya wanaweza cause wamezoea, canned food ambazo viwanda ni vingi huku kwetu, ni viburudisho tu ndivyo canned kwa wingi.


Lockdown iwe kwa baadhi ya miji bado sioni ni suluhisho slums ni mkusanyiko tosha. Muhimu tahadhari muda wote.


Kuna kitu naamini, bila panic it is easy to deal with covid-19 maana mwili unakuwa positively, kwenye panic yaani mwili unashindwa kubalance stress, hofu, uoga, na ugonjwa wenyewe. Hapo ndipo majanga.



Mungu saidia.
 
HOW COVID-19 KILLS--I'm a Surgeon--And Why We Can't Save You



Source : Duc C. Vuong MD

N.B
Gonjwa la Covid-19 lipo hivyo tuzingatie maelekezo tunayopewa na Wizara ya Afya jinsi ya kujikinga na corona kwa kufuata hatua hizi rahisi : epuka misongamano, kukumbatiana, kusogeleana , epuka kuwa abiria wa bodaboda, nawa mikono mara kwa mara kwa maji yanayotiririka n.k
 
Leo tumegonga 81, tunapandisha vinoma, sema nilitegemea hii noma kuanza kuwa balaa kadiri tunavyopima kwa mkupuo.
 
HOW COVID-19 KILLS--I'm a Surgeon--And Why We Can't Save You



Source : Duc C. Vuong MD

N.B
Gonjwa la Covid-19 lipo hivyo tuzingatie maelekezo tunayopewa na Wizara ya Afya jinsi ya kujikinga na corona kwa kufuata hatua hizi rahisi : epuka misongamano, kukumbatiana, kusogeleana , epuka kuwa abiria wa bodaboda, nawa mikono mara kwa mara kwa maji yanayotiririka n.k


Duh! Asante kwa hii video....
 
Hii nineikuta kwenye WhatsApp sehemuu

Hii ni kutufahamisha sisi kuwa pH ya virusi vya corona inatofautiana kutoka 5.5 hadi 8.5.

Wote tunahitaji kufanya, kupinga virusi vya corona, tunahitaji kuchukua zaidi ya vyakula vya alkali ambavyo viko juu ya kiwango cha juu cha pH cha Virusi.

Ambavyo ni:

* Limao- 9.9pH *
* Chenza- 8.2pH *
* Parachichi- 15.6pH *
* Vitunguu - 13.2pH *
* Maembe - 8.7pH *
* Tangerine - 8.5pH *
* Mananasi - 12.7pH *
* Dandelion - 22.7pH *
* chungwa - 9.2pH *

Unajuaje kuwa una coronavirus?
1. * Kuwashwa kwenye koo
2. * kukauka koo
3. * Kikohozi kikavu. *
4. Joto kubwa
5. kupumua kwa tabu

kwa hivyo unapoona vitu hivi haraka chukua maji ya moto kiasi weka limao kisha kunywa

Usibakie na habari hii peke yako. Sambaza kwa familia yako yote na marafiki. Mungu akubariki.
 
Sasa nyie ndo mnahatarisha maisha ya watu zaidi kwa kuokota okota na kusambaza habari za vijiweni.
pH ya virusi vya corona inatofautiana kutoka 5.5 hadi 8.5.
Kirusi kina pH?!! ni sawa na kuniambia pH ya mbuzi ni 8.4!!
* Limao- 9.9pH *
* Chenza- 8.2pH *
* Parachichi- 15.6pH *
* Vitunguu - 13.2pH *
* Maembe - 8.7pH *
* Tangerine - 8.5pH *
* Mananasi - 12.7pH *
* Dandelion - 22.7pH *
* chungwa - 9.2pH *
Chemistry 101....
pH scale unaijua?
Acid ni kati ya 0 hadi 6 na alkaline ni kati ya 8 hadi 14.
Sasa Limao inakuaje 9.9? Chungwa inakuaje 9.2?!
Funga kazi ni parachichi 15.6 na Dandelion ya 22.7!!! Hiyo ni pH scale ya sayari nyingine.
Hivi shule ulienda kufanya nini?!!
 
Sasa nyie ndo mnahatarisha maisha ya watu zaidi kwa kuokota okota na kusambaza habari za vijiweni.

Kirusi kina pH?!! ni sawa na kuniambia pH ya mbuzi ni 8.4!!

Chemistry 101....
pH scale unaijua?
Acid ni kati ya 0 hadi 6 na alkaline ni kati ya 8 hadi 14.
Sasa Limao inakuaje 9.9? Chungwa inakuaje 9.2?!
Funga kazi ni parachichi 15.6 na Dandelion ya 22.7!!! Hiyo ni pH scale ya sayari nyingine.
Hivi shule ulienda kufanya nini?!!
Chem 101, kwani mlisoma Mambo ya Ph how late? Sisi tulifanya back in High school form 1. Kuna vile some bacteria and viruses zinashindwa kumudu au ku-survive under some certain PH level but I am no expert in such.
 
Back
Top Bottom