COVID19 Tanzania: Wagonjwa wapya 35 waongezeka; idadi yafikia 88 (Aprili 15, 2020)

COVID19 Tanzania: Wagonjwa wapya 35 waongezeka; idadi yafikia 88 (Aprili 15, 2020)

Sampuli ngapi? Tunasikia wenzetu kati ya 600 au 800 wagonjwa kadhaa wamepatikana. Hiyo ingetuonesha walau jitihada katika upimaji wa wale contacts na pia kuelewa kama kuna changamoto ya vipimo. Jana nilisikia majirani zetu wakisema wanasambaza vipimo vya corona zaidi ya 1000 lakini sisi tunazidi kusikia sampuli kupelekwa sijui kwa Mkemia Mkuu(kama niko sahihi).

Tunaiona jitihada ya serikali lakini uwazi zaidi unahitajika na kama ni takwa la kimataifa (WHO), ni vizuri tukalitekeleza. Yawezekana hali ya ugonjwa kwa maana ya idadi ya wagonjwa nk ikawa ni kigezo cha kupewa misaada au kusamehewa madeni au kusogezwa muda mbele wa kulipa madeni ili pesa kidogo tuliyonayo itumike kushushughulikia janga hili.

Kama pengine tulianza vibaya si vibaya kurekebisha yale ambayo tunaona hayajatusaidia kwani hali yaweza kuwa mbaya hapo baadaye kama hatukuweka sawa mipango yetu.

Tuchape kazi lakini tukumbuke kuwa ugonjwa huu huonekana baada ya siku 14 na hivyo aliyeambukizwa anaweza akawa anaambukiza wengine kabla ya dalili hazijajitoleza. Leo nilikwenda Kariakoo nikiwa nimevaa Barakowa, katika watu zaidi ya 200 kwa wastani utakutana na mtu mmoja mwingine kavaa Barakowa na watu wanakuwa kama wanakushangaa kama wanaona mzungu katoka nje. Mungu atusaidie lakini inabidi tujisaidie pia.
 
Gallius,
Mkuu hizo na Leso hazina utofauti labda kwa kuwa zimeshonewa vishikizo.Mask ya kuzuia virus inakuwa na content iliyothibitishwa ktk uwezo wa kuchuja virus,bacteria no na zipo kwa namba.N95 ni mfano mzuri
 
Salary Slip, Wewe ni mpumbavu!! Kila kitu kulaumu!!

Tuombeni Mungu kwani wangapi walichukua tahadhari na bado ugonjwa ukasambaa? Unatamani lock down wananchi wataishije? Kisa unalala na kunywa kwa nguvu ya wengine ? Tuombeni Mungu tupunguze lawama!

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu tutaweza kumwomba Mungu kuliko waroma kulikoanzia ukatoliki, au wairan kuliko na misikiti mingi kuliko kwetu, kuliko wasaudia ulikoanzia uislam au waislael wenye vinasaba vya Yesu Kristo?

Tusidanganyane!

Umemwona Ummy na matangazo yake ya bashasha tena kwenye ripoti za Corona? Walitaka sana kutupa habari njema bila kuwajibika.

Hakuna cha maombi kwa Mungu bila kuwajibika.

Corona haitaondoka Tanzania kwa maombi.

Huo ndiyo ukweli mchungu.
 
Taarifa hii ina ukweli kiasi gani? Nawaomba wana Jf tusiwe chanzo cha taharuki.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa Mkuu nimeprove BBC idadi imepanda aswaaa ila kumbuka tuliandaliwa toka wiki iliyopita kwamba tumeingia kwenye wakati wa kuambukizana nje ya maambuzi kutoka nje.Ndio maana ata Serkali imeongeza muda wa wanafunzi na wanachuo kubaki nyumbani kwa muda usiojulikana.
Umeongea Point kubwa sana kiongozi...
 
Gallius,
Mkuu hapa mikoa yenye maambukizi ni muda wa kwenda lockdown kabla hatujachelewa mno.

Historia itakuwapo kutuhukumu.
 
Wenye magonjwa chronic naomba wajihadhari zaidi, HIV, TB, magonjwa ya moyo, sukari, hypertension, pneumonia etc watu wajihadhari zaidi.

We're heading there....
 
Ngatele,
G 20 wamepanga kutoa $ 20 billion kwa nchi zinazopambana na korona; hasa kwenye msamaha wa madeni. Wameomba na wakopeshaji binafsi kupunguza marejesho.

WB tymekosa kizembe kabisa, na G 20 tunaelekea kukosa. Sikiwahi kudhani kuwa kuna uzembe hivi. Maskini Tz!!
 
Salary Slip, Wewe ni mpumbavu!! Kila kitu kulaumu!!

Tuombeni Mungu kwani wangapi walichukua tahadhari na bado ugonjwa ukasambaa? Unatamani lock down wananchi wataishije? Kisa unalala na kunywa kwa nguvu ya wengine ? Tuombeni Mungu tupunguze lawama!

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu kwenye lockdown wenye kupungukiwa wanasaidiwa.

Tuwe wazalendo kuweka hali zetu sahihi wazi. Kwingine wamefanya hivyo.

Matokeo yake wanaanza tiba za waathirika mapema, hakuna vifo wala wagonjwa ICU.

Rwanda ni case ya kupigiwa mfano.

Dini zenu kaeni nazo. Kila mtu ana yake. Nchi haina dini. Nchi kutokuwa na dini maana yake ni kuwa fumbuzi za nchi zinataka uwajibikaji.

Hatuja wajibika vya kutosha tuleta masuala ya sala na swala?
 
This is sad,mimi nina uhakika serikali inasoma huku mambo na watu walikua wanapinga sana lockdown,kisa tuna cases chache sasa zinaongezeka.mnasemaje..na graph itapanda tuu sababu sio tu hatuchukua hatua kufunga mipaka,ila lockdown pia ilipingwa...Mungu tunusuru
 
Salary Slip,
BRAVOO Salary Slip yaani kwa mara ya kwanza hii imetulia km Mzalendo
yaani hukuweka Siasa kabisa umeelezea ukweli ambao Serikali iache masihara wagonjwa wanaongezeka na bado hatujaanza kuwapima washukiwa kama wenzetu majirani wanavyofanya.

mwisho hata Uchaguzi hukugusia wa Madiwani au Wabunge maana hili karantini linagonga kampeni hivyo hakuna kusogeza kitu.

tutapiga kura na barakoa zetu watuwekee sanitizer na maji Corona ni funga kazi
 
Nimeona video clip ya ITV ya minada ya samaki ferry, yaani ule umati!
Zile picha za Pasaka pia, yaani watu watakuwa wamegawana sana Corona.
Wiki mbili zijazo mambo yanaweza kuwa magumu sana.
Kulikuwa kuna haja gani ya kufanya ibada zenye mikusanyiko mikubwa wakati wa Pasaka?Huku tukijua kuwa kinga ni bora kuliko tiba?
Kwa hali harisi ukichanganya HIV,TB,Kisukari,Pumu,Pressure na magonjwa yote yanayopunguza kinga mwilini ni hatari sana kama utaambukizwa Covid-19.
Fungeni mipaka yote,Achana na mikusanyiko inayozidi watu 10 huku serikali ikitayarisha mpango wa lockdown isiozidi week 2 kama ilivyo shauri WHO kama hali itakuwa mbaya.
 
Dunia iko vitani, Nchi pia inapigana vita yake. Kosa kubwa ni kutotangaza majina ya waliogundulika kuathirika kwa kisingizio cha sheria za kitabibu, ati ugonjwa ni siri ya mgonjwa na serikali. Siri gani nchi iko vitani? Na silaha ya maangamizi zinabebwa na sisi binadamu wenyewe bila kujijua?

Serikali tajeni majina ya waathirika ili ndugu, marafiki na jirani tulio jirani nao tujihadhari na tuliojumuika nao tujitokeze haraka kujisalimisha vituo vya afya kwa upimwaji.
 
Back
Top Bottom