Saturday was my special day nilipokuwa Old Moshi.
Nikishafua viguo vyangu inabidi nivisimamie hadi vikauke manake kuna warugaruga walikua wanaiba hadi chupi! Napanda kitandani napiga horizontal kiaina (kusomea kitandani) huku nikisubiri bati (kengele ya msosi), bati likiliita naenda na plate mbili coz mshkaji wangu mtoto wa mama wikiendi lazima aende kwao akanyonye, table leader akiniuliza namwambia "namchukulia mshkaji kenda town!" kiulaiiini najikombea double share japokuwa wengi walikuwa wanajua kuwa na 'forge'.
Baada ya kula najua siku hiyo Ushirika leo inacheza kwenye ligi kuu, siwezi kuikosa hii gemu kwa kuwa vijana walikuwa wanatisha (David Rogers, Venance Mwakalukwa, Often Martin, Martin Mahimbo, etc), nashuka zangu Shengena mbio kumuwahi mshkaji kilema kwenye wheelchair ili nipate kuingia bure uwanjani, mama wee! nakuta washkaji wameshamuwahi walee wanashuka korongoni, inabidi niende nikapande juu ya mti au ukuta, akipigwa bao mtu wakati polisi nao wanashangilia hapo ndo unaruka ndani!
Baada ya mpira ni lazima kutakuwa na harusi, mimi na masela wangu tunaenda kupiga misele kwenye kumbi za ushirka kuangalia uwezekano wa kuzamia, tukishindwa tunaenda zetu kwenye hall la wanachuo kuanagalia TV(KBC tu!), mara jamaa wanatutoa baru. Hatuna jinsi tunaingia kitandu kula mbege, mitumbo inajaa na mikojo kibao, tunaamua kwenda red house kumalizia na gongo ili tuwake vizuri!
Ukirudi school saa 4 usiku unaona washkaji wanashika pua tu, soon unagundua kuwa 'pamenuka', Mdudu mwenguvu amepiga roll call ya nguvu bila kutarajiwa na jumatatu darasani kutakuwa hapakaliki! Monitor ni mshkaji ananitonya usiwe na wasiwasi 'nilikutiki'!
Umbwe,
Siku moja na mamitungi yangu narudi school toka uswekeni, bwii na giza vikanifanya nisione kilichokuwa mbele yangu, kumbe lilikuwa ni jopo la maticha nao wametoka kuutwika! Si nikagongana na mmoja wao uso kwa uso? jamaa akaning'ang'ania na maticha wengine wote wakanirukia huku wakinilazimisha niseme mimi ni nani, I was quite famous and popular! Nikawa nafight niwatoke huku nikiongea kishwahili cha lafudhi ya kichaga na kujitetea kuwa mimi sio mwanafunzi! Nilikuwa nimevaa ki OPP nikawa nakisikia kinachanika taratibu jinsi songombingo linavyoendelea, nilifanikiwa kuponyoka na kuwaacha na kiOPP, nikatoka na moto mkubwa hadi school na ponapona yangu umeme ulikuwa umekatika, giza ndilo lililoniokoa siku hiyo otherwise ningetemwa school.
After one week napita kwenye nyumba za maticha nakaona kaflana kangu mlangoni kwa ticha mmoja anapigia deki, mii kimyaaaaa!
Katika shule zote nakumbuka jinsi ambavyo mabafu yalikuwa yakijaa baada ya debe (disco) kuisha usiku! Wee nanihii nakujua huogagi kabisa, kulikoni huku bafuni saa hizi usiku huu wa manane na kirevola chako mkononi? Blues zilikuwa zinatutesa sana na kutuchafulia suruali kwa kiwango kikubwa!