zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 20,537
- 31,729
Habari za mchana wana JF natumaini wote humu wazima basi moja kwa moja niende kwenye mada husika.
UTANGULIZI
Wakati nasoma biblia nikakutana na mstari huu ambao ulinipa maswali sana
Mwanzo 1
6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.
7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.
9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.
Mstari huu unaeleza kuwa kulikuwa na maji juu ya anga na chini ya anga hivyo nikajiuliza sana hayo maji ya JUU ni yapi?? Kwa haraka nikafikiri ni mawingu ila muandishi wa zaburi akapigia msumari kuwa ni vitu viwili tofauti
Zaburi 148:4
4 Msifuni, enyi mbingu za mbingu,Nanyi maji mlioko juu ya mbingu.
5 Na vilisifu jina la BWANA,Kwa maana aliamuru, vikaumbwa.
Hapa kaweka wazi kuwa kuna maji juu ya dunia na hapa chini kaonyesha ni tofauti kabisa na mawingu tunayofahamu
Zaburi 147:8
Huzifunika mbingu kwa mawingu,Huitengenezea nchi mvua, Na kuyameesha majani milimani
Baada ya sintofahamu hii Wakati natafuta ukweli wa mambo, nikakutana na nadharia hii ya crystalline canopy theory ambayo ilipewa nguvu na wanatheolojia Dk kent hovind na Dk Henry morris muasisi wa movement ya young earth creationist.
NADHARIA
Kwa kifupi tu nadharia hii inaeleza kwamba anga la Dunia kabla ya gharika la Nuhu ilikuwa imezungukwa na mzingo wa maji yaliyotajwa hapo juu na kwamba hayo maji ndio yaliyokuja kutumika kwenye gharika kwa Mungu kuangusha mzingo huo kwa mfumo wa mvua kupitia mstari huu
Mwanzo 7:11-12
11........ madirisha ya mbinguni yakafunguka.
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi, siku arobaini mchana na usiku.
KAZI YAKE
1. Kuwa na hali ya hewa moja dunia nzima hivyo kuepusha uwezekano wa hali za hewa ya maeneo tofauti kuingiliana ambayo ingesababisha mafuriko,vimbunga,n.k
2. Kazi ya pili ni kuiwekea mzingo dunia ili kuiepusha na mashambulizi ya mionzi mikali ya Jua na hii ilisaidia kuongeza umri wa kuishi wa wanadamu.
3. Kazi kubwa zaidi ni pale ilipotumika kuangamiza dunia nzima kwenye gharika la Nuhu ambapo ilileta mvua kubwa iliosababisha kizazi chote kufutika.
HOJA ZAO
1. Mvua ya siku 40 mfululizo ingehitaji maji ya kutosha ambayo mawingu yakawaida yansingetosheleza maana kijiografia tu haiwezekani pande zote za dunia ziwe na mvua kwa wakati mmoja kama ambavyo haiwezekani jua kuwaka eneo lote la dunia kwa wakati mmoja na kwamba kwa ushahidi wa kisayansi anga letu lote hili likigeuka mvua maji yatajaa dunia nzima kwa urefu wa inchi 1 pekee!! Hivyo wakasema hili lingewezekana kupitia hayo MAJI yaliyokuwa juu ya dunia maana yalikuwa mengi mno!!
2. Pia nadharia inasema hakuna mahala Mawingu yametajwa kabla ya gharika hivyo hiyo mvua ilitokea wapi bila mawingu kuwepo?? Hivyo huenda ni hayo MAJI ya juu ya dunia ndio yalitumika.
Mwanzo 9
14 Hata itakuwa nikitanda mawingu juu ya nchi, upinde utaonekana winguni
3.Pia inasema hakuna mahali mvua imetajwa kabla ya gharika sababu hapakuwa na mawingu wala mfumo wa kawaida wa hali ya hewa kama sasa hivyo huu MZINGO ulikuwa unaleta unyevu nyevu na miti kuota kwa haraka kupitia umande hivyo hiyo wakahoji hiyo mvua ilitoka wapi wakati wa gharika kama sio hayo maji ya JUU ndio kutumika??
Mwanzo 2
5 hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana BWANA Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi.
Kuhusu unyevu;
Mwanzo 2
6. ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.
4.Hoja nyingine ni kwamba kwenye Biblia wanadamu kabla ya gharika walikuwa na maisha marefu kuliko wa baada ya gharika sababu walioishi kabla ya gharika walikuwa chini ya uzio huu hivyo mionzi mibaya ya jua ikawa haiwapati na hivo kuwasaidia kuishi zaidi.
USHAHIDI WA KISAYANSI
1. Imegundulika na wanasayansi kwamba zamani kulikuwa na oxygen content ya 35% duniani ilihali kwa sasa ni 21% pekee hivyo hii nadharia inasema kutokana na uwepo wa MZINGO huu basi hali ya hewa ikawa na oxygen content kubwa zaidi hivyo kusupport uwepo wa wanyama wakubwa na wanadamu wakubwa (wanefili) waweze kupumua vizuri. Hoja hii imetokana na kugundulika kuwa Mapafu ya dinosaur na viumbe wengine wakubwa wa kale walikuwa na mapafu madogo na nyenzo za kupumulia nyembamba hivyo wasingeweza kuishi sahivi ambapo kupumua ingekuwa shidia kutokana na MZINGO huo kuondoka na oxygen kupungua % zake hivyo hata waliopona kwenye gharika walipoteza kizazi chao hapo.
2. Pia kugundulika kisayansi uwepo wa ice age ambapo barafu ilitanda dunia nzima huko miaka mamillion iliopita hivyo wakajengea hoja kwamba barafu ya huo MZINGO ( barafu kutokana na baridi la nje ya dunia kupiga hayo maji) ulipoyeyuka na baadae kugeuka maji na kumwagika duniani kwa mfumo wa mvua ulisababisha hali ya hewa kubadilika na kuwa na UBARIDI sana hivyo kuweza kuwa chanzo cha ICE AGE (ukizingatia mpaka leo wanasayansi bado hawajapata sababu conclusive ya kilichosababisha).
3. Pia wanasayansi waligundua dunia ya sasa haipigwi na jua kama dunia ya zamani yaani jua lilipiga dunia 30% dhaifu kuliko sasa, hivyo wakajengea hoja kuwa huenda kuna MZINGO ulikuwa unapunguza nguvu ya jua kumulika dunia hivyo kuhalalisha uwepo wa MZINGO huo.
HITIMISHO
Baada ya kusoma mstari huo na baadae kupitia nadharia hii bado nimebaki na maswali mengi nikaona nije kwa great thinkers humu tuchambue pamoja
1.Je nadharia hii ni ya kweli
2. Na tukiamini si kweli basi tujiulize maswali yafuatayo
je hayo maji JUU ya Anga ni yapi?
Kazi yake ilikuwa nini?
Na yalipotelea wapi au kama yapo yakowapi??
SOURCE: The genesis flood by Dr Henry Morris
UTANGULIZI
Wakati nasoma biblia nikakutana na mstari huu ambao ulinipa maswali sana
Mwanzo 1
6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.
7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.
9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.
Mstari huu unaeleza kuwa kulikuwa na maji juu ya anga na chini ya anga hivyo nikajiuliza sana hayo maji ya JUU ni yapi?? Kwa haraka nikafikiri ni mawingu ila muandishi wa zaburi akapigia msumari kuwa ni vitu viwili tofauti
Zaburi 148:4
4 Msifuni, enyi mbingu za mbingu,Nanyi maji mlioko juu ya mbingu.
5 Na vilisifu jina la BWANA,Kwa maana aliamuru, vikaumbwa.
Hapa kaweka wazi kuwa kuna maji juu ya dunia na hapa chini kaonyesha ni tofauti kabisa na mawingu tunayofahamu
Zaburi 147:8
Huzifunika mbingu kwa mawingu,Huitengenezea nchi mvua, Na kuyameesha majani milimani
Baada ya sintofahamu hii Wakati natafuta ukweli wa mambo, nikakutana na nadharia hii ya crystalline canopy theory ambayo ilipewa nguvu na wanatheolojia Dk kent hovind na Dk Henry morris muasisi wa movement ya young earth creationist.
NADHARIA
Kwa kifupi tu nadharia hii inaeleza kwamba anga la Dunia kabla ya gharika la Nuhu ilikuwa imezungukwa na mzingo wa maji yaliyotajwa hapo juu na kwamba hayo maji ndio yaliyokuja kutumika kwenye gharika kwa Mungu kuangusha mzingo huo kwa mfumo wa mvua kupitia mstari huu
Mwanzo 7:11-12
11........ madirisha ya mbinguni yakafunguka.
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi, siku arobaini mchana na usiku.
KAZI YAKE
1. Kuwa na hali ya hewa moja dunia nzima hivyo kuepusha uwezekano wa hali za hewa ya maeneo tofauti kuingiliana ambayo ingesababisha mafuriko,vimbunga,n.k
2. Kazi ya pili ni kuiwekea mzingo dunia ili kuiepusha na mashambulizi ya mionzi mikali ya Jua na hii ilisaidia kuongeza umri wa kuishi wa wanadamu.
3. Kazi kubwa zaidi ni pale ilipotumika kuangamiza dunia nzima kwenye gharika la Nuhu ambapo ilileta mvua kubwa iliosababisha kizazi chote kufutika.
HOJA ZAO
1. Mvua ya siku 40 mfululizo ingehitaji maji ya kutosha ambayo mawingu yakawaida yansingetosheleza maana kijiografia tu haiwezekani pande zote za dunia ziwe na mvua kwa wakati mmoja kama ambavyo haiwezekani jua kuwaka eneo lote la dunia kwa wakati mmoja na kwamba kwa ushahidi wa kisayansi anga letu lote hili likigeuka mvua maji yatajaa dunia nzima kwa urefu wa inchi 1 pekee!! Hivyo wakasema hili lingewezekana kupitia hayo MAJI yaliyokuwa juu ya dunia maana yalikuwa mengi mno!!
2. Pia nadharia inasema hakuna mahala Mawingu yametajwa kabla ya gharika hivyo hiyo mvua ilitokea wapi bila mawingu kuwepo?? Hivyo huenda ni hayo MAJI ya juu ya dunia ndio yalitumika.
Mwanzo 9
14 Hata itakuwa nikitanda mawingu juu ya nchi, upinde utaonekana winguni
3.Pia inasema hakuna mahali mvua imetajwa kabla ya gharika sababu hapakuwa na mawingu wala mfumo wa kawaida wa hali ya hewa kama sasa hivyo huu MZINGO ulikuwa unaleta unyevu nyevu na miti kuota kwa haraka kupitia umande hivyo hiyo wakahoji hiyo mvua ilitoka wapi wakati wa gharika kama sio hayo maji ya JUU ndio kutumika??
Mwanzo 2
5 hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana BWANA Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi.
Kuhusu unyevu;
Mwanzo 2
6. ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.
4.Hoja nyingine ni kwamba kwenye Biblia wanadamu kabla ya gharika walikuwa na maisha marefu kuliko wa baada ya gharika sababu walioishi kabla ya gharika walikuwa chini ya uzio huu hivyo mionzi mibaya ya jua ikawa haiwapati na hivo kuwasaidia kuishi zaidi.
USHAHIDI WA KISAYANSI
1. Imegundulika na wanasayansi kwamba zamani kulikuwa na oxygen content ya 35% duniani ilihali kwa sasa ni 21% pekee hivyo hii nadharia inasema kutokana na uwepo wa MZINGO huu basi hali ya hewa ikawa na oxygen content kubwa zaidi hivyo kusupport uwepo wa wanyama wakubwa na wanadamu wakubwa (wanefili) waweze kupumua vizuri. Hoja hii imetokana na kugundulika kuwa Mapafu ya dinosaur na viumbe wengine wakubwa wa kale walikuwa na mapafu madogo na nyenzo za kupumulia nyembamba hivyo wasingeweza kuishi sahivi ambapo kupumua ingekuwa shidia kutokana na MZINGO huo kuondoka na oxygen kupungua % zake hivyo hata waliopona kwenye gharika walipoteza kizazi chao hapo.
2. Pia kugundulika kisayansi uwepo wa ice age ambapo barafu ilitanda dunia nzima huko miaka mamillion iliopita hivyo wakajengea hoja kwamba barafu ya huo MZINGO ( barafu kutokana na baridi la nje ya dunia kupiga hayo maji) ulipoyeyuka na baadae kugeuka maji na kumwagika duniani kwa mfumo wa mvua ulisababisha hali ya hewa kubadilika na kuwa na UBARIDI sana hivyo kuweza kuwa chanzo cha ICE AGE (ukizingatia mpaka leo wanasayansi bado hawajapata sababu conclusive ya kilichosababisha).
3. Pia wanasayansi waligundua dunia ya sasa haipigwi na jua kama dunia ya zamani yaani jua lilipiga dunia 30% dhaifu kuliko sasa, hivyo wakajengea hoja kuwa huenda kuna MZINGO ulikuwa unapunguza nguvu ya jua kumulika dunia hivyo kuhalalisha uwepo wa MZINGO huo.
HITIMISHO
Baada ya kusoma mstari huo na baadae kupitia nadharia hii bado nimebaki na maswali mengi nikaona nije kwa great thinkers humu tuchambue pamoja
1.Je nadharia hii ni ya kweli
2. Na tukiamini si kweli basi tujiulize maswali yafuatayo
je hayo maji JUU ya Anga ni yapi?
Kazi yake ilikuwa nini?
Na yalipotelea wapi au kama yapo yakowapi??
SOURCE: The genesis flood by Dr Henry Morris