Crystalline Canopy Theory na gharika la Nuhu

Crystalline Canopy Theory na gharika la Nuhu

Hahahhaa acha tu, naelewa sasa kwanini Mgambilwa ni mntu alitokwa povu kule kwenye uzi wake yaani nimeumiza kichwa kusoma huo mkitabu afu mtu anasema NAPOTOSHA bila hata kunipa jibu wakati nimeuliza swali !! dah kazi sana
Swali lako ni zuri lakn kwbahati mbya mmb ya mungu n mmb tu ya imani hkuna prove yyt ww km umezaliwa bs amini hvyo lkn ukisema tukupe nondo a up to chee ni ngumu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"....siku ile chemchemu zote za vilindi vikuu zilibubujika kwa nguvu,madirisha ya mbinguni yakafunguka.Mvua ikanyesha juu ya nchi...."Mwanzo 7:11
hapa tunaona kuwa gharika ilisababishwa na vyanzo vitatu,kububujika kwa vilindi(vyanzo vya maji ardhini au chini ya bahari),kufunguka kwa madirisha ya binguni hapa ndipo hayo maji ya juu yalianza kumwagika(bila shaka yalikuwa kama maporomoko) na chanzo kingine ni mvua ya kawaida ambayo ilinyesha kwa muda mrefu.
Kwa hiyo hii theory inaukweli ila haiwezi kuaminiwa kwa 100 kwa sababu haiwezi kuwa proved.
 
Mkuu zitto junior hii mada ni nzuri sana ila nasikitika sana kwa baadhi ya wachangiaji kutoa kejeli bila kutoa hoja za msingi.
Hata mimi nlkua na maswali sana ila haya maji ya juu ya anga nadhani yalikua juu mbinguni. Ingawa sina ushahidi wa hilo

sent using samsung galaxy s8
 
Swali lako ni zuri lakn kwbahati mbya mmb ya mungu n mmb tu ya imani hkuna prove yyt ww km umezaliwa bs amini hvyo lkn ukisema tukupe nondo a up to chee ni ngumu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kwanza jifunze kuandika ukaeleweka maana sijui hta umeandika herufi gani hapo.... Pia mie nimeuliza swali MAJI JUU YA ANGA ni nini kama hauna jibu si ukae pembeni wanaojua watakuja sasa kuwahi mada huku ukisema ni mambo ya imani kwani nani hajui biblia ni imani sasa tusiulize swali kisa ni MAMBO YA IMANI?? Sasa mkienda kuhubiri ndio mnajibu watu hivyo wakiuliza swali la biblia??

Kazi kwelikweli
 
Hahahhaa acha tu, naelewa sasa kwanini Mgambilwa ni mntu alitokwa povu kule kwenye uzi wake yaani nimeumiza kichwa kusoma huo mkitabu afu mtu anasema NAPOTOSHA bila hata kunipa jibu wakati nimeuliza swali !! dah kazi sana
Eneo kubwa la Agano la Kale hasa Vitabu 4 vya Torati (Musa), inatumia lugha nyepesi kwa kuwa mlengwa ni Myahudi aliyekuwa mtumwa, ambaye alikuwa masikini, kapuku na asiye na elimu enzi hizo za kutoka utumwani Misri kuelekea Canaan. Shida inakuja kwetu wasomi wa sasa, tunajaribu kutafsiri kifungu kwa kifungu, halafu tuna-relate na uelewa wetu wa kidunia ambao umepatikana kisayansi. Hapo ndo kuna shida.
Wataalamu wa Biblia nao walishakiri wazi kuwa, Biblia iliposema kuwa, Mungu aliumba mbingu na Dunia na vyote vilivyomo ndani ya siku Sita, kamwe hakunaanisha hizo siku za masaa 24. Ndiyo maana kuna uwezekano alikuwa anaongelea namna Dunia ilivyopatikana miaka bilioni 4.5 iliyopita, licha ya kwamba the Big Bang ilitokea miaka zaidi ya Bilioni 12 - 14 iliyopita. Hata Biblia inaposema Mungu akamuumba mwanadamu siku ya Sita, haikumaanisha siku hizo za saa 24, wengi wanakiri kuwa, ni zaidi ya milioni chache (3?) zilizopita.
Kumbuka Biblia inesema kuwa, Mungu alipomaliza kuumba, Dunia ilikuwa haijanyeshewa maji. Hii ni wazi kwa kuwa, baada ya Earth formation miaka bilioni 4.5 iliyopita, ilichukua mamilioni ya miaka (milioni 500) kwa Dunia hiyo kuanza kupoa taratibu mpaka kujitengenezea Atmosphere yake yenye mawingu na Ozone Layer.
So mi nakubaliana kabisa na uchambuzi wao. Hata hivyo, bado kuhusu gharika, siyo kwamba maji yalitoka tu juu. Biblia inaonyesha kuwa, vilindi vya maji vilibubujika maji kutoka ardhini. Hii inaonyesha kuna uwezekano mkubwa sana maji mengi yalitoka chini ya ardhi. Kwenye Conspiracy Theory moja inaelezwa kuwa, maji yaliyomo chini ya Dunia ni zaidi ya mara tano (5) ya maji juu ya uso wa Dunia.

Aidha, Mimi sidhani kama mvua ilinyesha kweli Dunia nzima. Kama ingenyesha Dunia nzima na watu wote duniani wakafa, hiyo inamaanisha sisi wote ni uzao wa Noah. Hapa nitakuwa wa mwisho kukubaliana na hii hoja. Ukiniambia gharika ilitokea kabla ya 70,000 BC, hapo nitakubali lakini siyo mwaka 2000 BC.
 
Mkuu zitto junior hii mada ni nzuri sana ila nasikitika sana kwa baadhi ya wachangiaji kutoa kejeli bila kutoa hoja za msingi.
Hata mimi nlkua na maswali sana ila haya maji ya juu ya anga nadhani yalikua juu mbinguni. Ingawa sina ushahidi wa hilo

sent using samsung galaxy s8
Mkuu shida wengi humu wana mahaba ya imani sana yaani ukihoji chochote kwenye vitabu vya dini kwa nia njema tu unaonekana shetani 😀😀 mie nilitegemea hata wataenda download hicho kitabu au hta kuingia google alafu warudi na majibu wameishia kutoa majibu mepesi kazi kwelikweli

anyway ngoja tusubiri wataalam kina mitale na midimu tikakami wa lopelope SALA NA KAZI Son of Gamba wanaweza kuja na majibu ya kueleweka
 
"....siku ile chemchemu zote za vilindi vikuu zilibubujika kwa nguvu,madirisha ya mbinguni yakafunguka.Mvua ikanyesha juu ya nchi...."Mwanzo 7:11
hapa tunaona kuwa gharika ilisababishwa na vyanzo vitatu,kububujika kwa vilindi(vyanzo vya maji ardhini au chini ya bahari),kufunguka kwa madirisha ya binguni hapa ndipo hayo maji ya juu yalianza kumwagika(bila shaka yalikuwa kama maporomoko) na chanzo kingine ni mvua ya kawaida ambayo ilinyesha kwa muda mrefu.
Kwa hiyo hii theory inaukweli ila haiwezi kuaminiwa kwa 100 kwa sababu haiwezi kuwa proved.
Hivyo basi tukiamini nadharia ni uongo je hayo maji JUU YA ANGA ni yapi mkuu na yalitoweka wakati gani if at all hayakuhusika kwenye gharika??
 
Hivyo basi tukiamini nadharia ni uongo je hayo maji JUU YA ANGA ni yapi mkuu na yalitoweka wakati gani if at all hayakuhusika kwenye gharika??
Mkuu haujasoma kwa umakini,binafsi nakubali hayo maji yalikuwepo na nimesema baada ya madirisha ya Mbinguni "hayo maji yalimwagika kama maporomoka"
Nilichofanya ni kuongezea mambo yaliyopelekea gharika na hayo maji yakiwamo.
Kama hautajali soma tena post yangu ya kwanza
 
Habari za mchana wana JF natumaini wote humu wazima basi moja kwa moja niende kwenye mada husika.
View attachment 848708
UTANGULIZI
Wakati nasoma biblia nikakutana na mstari huu ambao ulinipa maswali sana

Mwanzo 1
6 Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.
7 Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
8 Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.
9 Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo
.

Mstari huu unaeleza kuwa kulikuwa na maji juu ya dunia na chini ya dunia hivyo nikajiuliza sana hayo maji ya JUU ni yapi?? Kwa haraka nikafikiri ni mawingu ila muandishi wa zaburi akapigia msumari kuwa ni vitu viwili tofauti

Zaburi 148:4
4 Msifuni, enyi mbingu za mbingu,Nanyi maji mlioko juu ya mbingu.
5 Na vilisifu jina la BWANA,Kwa maana aliamuru, vikaumbwa.


Hapa kaweka wazi kuwa kuna maji juu ya dunia na hapa chini kaonyesha ni tofauti kabisa na mawingu tunayofahamu

Zaburi 147:8
Huzifunika mbingu kwa mawingu,Huitengenezea nchi mvua, Na kuyameesha majani milimani

Baada ya sintofahamu hii Wakati natafuta ukweli wa mambo, nikakutana na nadharia hii ya crystalline canopy theory ambayo ilipewa nguvu na wanatheolojia Dk kent hovind na Dk Henry morris muasisi wa movement ya young earth creationist.
View attachment 848705
NADHARIA
Kwa kifupi tu nadharia hii inaeleza kwamba anga la Dunia kabla ya gharika la Nuhu ilikuwa imezungukwa na mzingo wa maji yaliyotajwa hapo juu na kwamba hayo maji ndio yaliyokuja kutumika kwenye gharika kwa Mungu kuangusha mzingo huo kwa mfumo wa mvua kupitia mstari huu

Mwanzo 7:11-12
11........ madirisha ya mbinguni yakafunguka.
12 Mvua ikanyesha juu ya nchi, siku arobaini mchana na usiku
.

KAZI YAKE
1. Kuwa na hali ya hewa moja dunia nzima hivyo kuepusha uwezekano wa hali za hewa ya maeneo tofauti kuingiliana ambayo ingesababisha mafuriko,vimbunga,n.k

2. Kazi ya pili ni kuiwekea mzingo dunia ili kuiepusha na mashambulizi ya mionzi mikali ya Jua na hii ilisaidia kuongeza umri wa kuishi wa wanadamu.

3. Kazi kubwa zaidi ni pale ilipotumika kuangamiza dunia nzima kwenye gharika la Nuhu ambapo ilileta mvua kubwa iliosababisha kizazi chote kufutika.
View attachment 848716

HOJA ZAO
1. Mvua ya siku 40 mfululizo ingehitaji maji ya kutosha ambayo mawingu yakawaida yansingetosheleza maana kijiografia tu haiwezekani pande zote za dunia ziwe na mvua kwa wakati mmoja kama ambavyo haiwezekani jua kuwaka eneo lote la dunia kwa wakati mmoja na kwamba kwa ushahidi wa kisayansi anga letu lote hili likigeuka mvua maji yatajaa dunia nzima kwa urefu wa inchi 1 pekee!! Hivyo wakasema hili lingewezekana kupitia hayo MAJI yaliyokuwa juu ya dunia maana yalikuwa mengi mno!!

2. Pia nadharia inasema hakuna mahala Mawingu yametajwa kabla ya gharika hivyo hiyo mvua ilitokea wapi bila mawingu kuwepo?? Hivyo huenda ni hayo MAJI ya juu ya dunia ndio yalitumika.

Mwanzo 9
14 Hata itakuwa nikitanda mawingu juu ya nchi, upinde utaonekana winguni

3.Pia inasema hakuna mahali mvua imetajwa kabla ya gharika sababu hapakuwa na mawingu wala mfumo wa kawaida wa hali ya hewa kama sasa hivyo huu MZINGO ulikuwa unaleta unyevu nyevu na miti kuota kwa haraka kupitia umande hivyo hiyo wakahoji hiyo mvua ilitoka wapi wakati wa gharika kama sio hayo maji ya JUU ndio kutumika??

Mwanzo 2
5 hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana BWANA Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi.

Kuhusu unyevu;
Mwanzo 2
6. ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.

4.Hoja nyingine ni kwamba kwenye Biblia wanadamu kabla ya gharika walikuwa na maisha marefu kuliko wa baada ya gharika sababu walioishi kabla ya gharika walikuwa chini ya uzio huu hivyo mionzi mibaya ya jua ikawa haiwapati na hivo kuwasaidia kuishi zaidi.
View attachment 848715

USHAHIDI WA KISAYANSI
1. Imegundulika na wanasayansi kwamba zamani kulikuwa na oxygen content ya 35% duniani ilihali kwa sasa ni 21% pekee hivyo hii nadharia inasema kutokana na uwepo wa MZINGO huu basi hali ya hewa ikawa na oxygen content kubwa zaidi hivyo kusupport uwepo wa wanyama wakubwa na wanadamu wakubwa (wanefili) waweze kupumua vizuri. Hoja hii imetokana na kugundulika kuwa Mapafu ya dinosaur na viumbe wengine wakubwa wa kale walikuwa na mapafu madogo na nyenzo za kupumulia nyembamba hivyo wasingeweza kuishi sahivi ambapo kupumua ingekuwa shidia kutokana na MZINGO huo kuondoka na oxygen kupungua % zake hivyo hata waliopona kwenye gharika walipoteza kizazi chao hapo.

2. Pia kugundulika kisayansi uwepo wa ice age ambapo barafu ilitanda dunia nzima huko miaka mamillion iliopita hivyo wakajengea hoja kwamba barafu ya huo MZINGO ( barafu kutokana na baridi la nje ya dunia kupiga hayo maji) ulipoyeyuka na baadae kugeuka maji na kumwagika duniani kwa mfumo wa mvua ulisababisha hali ya hewa kubadilika na kuwa na UBARIDI sana hivyo kuweza kuwa chanzo cha ICE AGE (ukizingatia mpaka leo wanasayansi bado hawajapata sababu conclusive ya kilichosababisha).

3. Pia wanasayansi waligundua dunia ya sasa haipigwi na jua kama dunia ya zamani yaani jua lilipiga dunia 30% dhaifu kuliko sasa, hivyo wakajengea hoja kuwa huenda kuna MZINGO ulikuwa unapunguza nguvu ya jua kumulika dunia hivyo kuhalalisha uwepo wa MZINGO huo.

HITIMISHO
Baada ya kusoma mstari huo na baadae kupitia nadharia hii bado nimebaki na maswali mengi nikaona nije kwa great thinkers humu tuchambue pamoja

1.Je nadharia hii ni ya kweli

2. Na tukiamini si kweli basi tujiulize maswali yafuatayo

je hayo maji JUU ya dunia ni yapi?
Kazi yake ilikuwa nini?
Na yalipotelea wapi au kama yapo yakowapi??

SOURCE: The genesis flood by Dr Henry Morris

View attachment 848697
mmmh hii ngumu chief,

hoja za watafiti zina-make sense kwa kiasi fulani.....na Mungu pia inawezekana labda alitumia uwezo wake wa kutoshindwa kitu kufanikisha hilo.
 
Hahahhaa acha tu, naelewa sasa kwanini Mgambilwa ni mntu alitokwa povu kule kwenye uzi wake yaani nimeumiza kichwa kusoma huo mkitabu afu mtu anasema NAPOTOSHA bila hata kunipa jibu wakati nimeuliza swali !! dah kazi sana


JIWE kaleta taabu sana kwenye jamii mkuu wangu...yaani kila unayekutana naye ni HASIRA HASIRA HASIRA...wakati mwingine mtu maneno yanamtoka tu ila akitulia halafu ukamuuliza kwa utaratibu...kulikoni ndugu yangu lile povu lote lilikuwa la nn???...hata mwenyewe anashindwa kukuelezea kilichomkuta...(catalyst ya povu....JIWE) kwa hyo mkuu wakati mwingine inabidi kuwasamehe tu.....Huyu JIWE huyu....acha tu.
 
Mkuu zito you are the best unajaribu kufungua akili za watu lakini siku zote utumwa wa dini ni mbaya sana hata umwambie vipi ni ngumu kukuelewa


ila amini nakuambia hakuna kitabu kibovu ktk biblia kama kitabu cha genesis yaan totally shizophrenia
 
Kuna mmb mengn ni kuumiza tu kchwa lkn hii nadharia cyo ykweli imejaa simuliz na taarifa Za kusafikika na kuunganisha maneno ykweny bible ili story yao iende sw..hv nani leo atakuja na majbu sahh y swali lko?kiufupi tu hlo jmbo lingetokea kiisayansi leo sayans ingeprove lkn kwkuwa limesimuliwa na mmb y kiimani nkushauri tu inatosha kuamini unavyoamn mara zote mmb ydini huendeshwa na imani na s mmb y kuprove

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna ukosefu wa maarifa mkubwa duniani kama kusema hili jambo limesumuliwa tu si la kisansi hivo halifai, lakini mtu huyo huyo anaamini bing bang theory, continental drift, Darwin theory nk ambavyo vyote ni mawazo tu ya watu wengine, kama sayansi inaweza kuprove kila kitu hebu nisaidie kuprove uwepo wa NATURE ambayo sayansi inaamini kuwa ipo
 
Niliwahi kusikia(kusoma) toka kwa bwana mmoja kuwa baada ya dunia kupigwa na Asteroid miaka zaidi ya 65, 000,000 iliyopita athari zilizojitokeza baadaye ni pamoja na kuuwawa kwa viumbe wengi (mass extinction), matetemeko makubwa ya ardhi, kuongezeka kwa joto la dunia, kutanda kwa wingu kubwa la gesi ambalo lilifunika dunia yote na hivyo kuifanya ipoe sana kwa kuwa hata mwanga wa jua ulizuiwa kwa kiasi kiasi kikubwa na kwa muda mrefu kufika duniani.
Inawezekana kupoa huku kulipelekea the so called “ICE AGE” na baadaye kufuatiwa na mvua kubwa kunyesha kutokana na lile wingu kubwa lililokuwa limedanda juu ya duia. Hapa linazungumziwa wingu lililosababishwa na asteroid impact, wingu lililoweza kuzuia mwanga wa jua kuifikia dunia kwa muda mrefu mpaka kusababisha Ice age na baadaya the so called “GHARIKA”.
Theory hii pia naiona una mashiko yake japo sina hakika wa uwiano uliopo kwati ya muda wa kwenye biblia unaokadiria umri wa dunia kuwa miaka 6000 na ule wa kisayansi unaokadiria kuwa miaka 4.543 Bilioni.
Asante.
 
Jamani mambo ya Mungu hayachunguzwi kwa akili hizi za kibinadamu. Lazima uende umuombe Mwenyezi Mungu akupe neema ya kukufunulia atakayo. Haya tunayo ya jua kwa kujidanganya eti ni sayansi ndiyo huyu Mungu aliye tufanya tuyajue kwa kutupa ubongo/akili. Hii sayansi ambayo tunaitumia kujaribu kuhoji na kumkosoa ni Mungu aliyetupa huo uwezo tuwenao na kama asingetaka wala tusingekuwa nao. Kumbuka kilichotokea katika ule mnara babeli.

Tujue tu kuwa Mungu ndiye muweza wa yote na ndiye muwezeshaji wa yote. Haiwezekani eti sayansi tena inayotegemea akili za mwadamu aliye umbwa na Mungu ishinde uwezo wa Mungu au itumike kutilia mashaka uumbaji wa Mungu.

Mimi na omba nikuambie kitu, Biblia au Maneno ya Mungu Matakatifu imeongelea yale Mungu aliyo taka tuyasikie kwa utashi wake yeye basi.

Ni kuulize kwenye Biblia unaweza kuniambia maji au kiza viliumbwa vipi? Hata kwa hiyo sayansi ambayo mnaitumia kumtilia mashaka Mungu inaweza kutuambia giza liliumbwa vipi na vilivyo liumba hilo giza vilitokana na nini?

Wanasayansi wakiwa wamefika ukomo wa uwezo wao watakuambia utafiti unaendelea hawakuambii tumeshindwa katu. Unaendelea mpaka lini? mpaka hapo ufumbuzi utakapo patikana. Hizo nguvu za ufumbuzi mnazozisubiria zipatikane mnategemea kuzitoa wapi? Utaambulia blabla tu za akili za mwanadamu tena aliye jawa na kiburi cha uzima. Hivi kwa nini wanadamu wanaojidai kugundua mambo kibao wanalizwaje na kifo? Uchungu wa kifo umemshinda vipi mwanadamu? Hata baada ya Mungu kumjalia kuona na kufika sayari za mbali?
Mungu anasema yeye jina lake ni " NIKO/YUKO AMBAYE NIKO/YUKO". Hana Asili/Mwanzo wala Mwisho/Hatima.
 
Back
Top Bottom