Tetesi: CUF: Lipumba kuwafuta uanachama wabunge wote wa kuchaguliwa majimbo yote ya Bara

Tetesi: CUF: Lipumba kuwafuta uanachama wabunge wote wa kuchaguliwa majimbo yote ya Bara

Hapa anaweza kuwafukuza halafu na yeye akaondoka huku akisema, nafsi imenisuta
 
Unapaswa kwanza ujue lengo la walio nyuma ya Lipumba.
Walio nyuma ya Lipumba wanataka Kumfuta Maalim uanachama ili;
☞ kumkosesha platform ya kuongelea mambo ya CUF
☞Kudhoofisha madai yake ya urais wa Zanzibar ambayo yamefikia mahali pazuri kwenye jumuiya za Kimataifa.

Ili kujua Maalim afanye nini lazima kujiuliza kwanza ;
Je, walioko nyuma ya Lipumba wakifanikiwa kumfutia Maalim uanachama (Kitu ambacho watafanikiwa ) , Madai ya urais wa Zanzibar ya Maalim kwenye jumuiya za Kimataifa yataathirika kiasi gani?

Kama hayataathirika basi Maalim apractice kile wazungu wanasema -Stop, look, listen, think and wait .

Kama yataathirika basi Maalim anaweza kuchukua ushauri wako hapo juu.
UZEMBE WAKE WAKE WA KUCHELEWA KUMCHUKULIA HATUA LIPUMBA SASA AKUBALI KUJIUNGA NA CHADEMA TU
 
Mnafikiri hizi options CCM hawazijui? Kila moja tayari ina mkakati wake ...dawa ni moja waungane kinafiki na Lipumba then watumie nguvu ya ushawishi wao ndani kuendeleza ajenda zao ....hii ndio options ambayo naamini CCM hawataki itokee na wanaamini kwa hulka za Maalim haitotokea ....CUF inatakiwa busara tu ....tatizo wanachochewa na Chadema kwa faida ya Chadema kuongeza nguvu Zanzibar ....ila hiyo nguvu haitokuwepo ....
 
Siasa sipendi ila Lipumba anavyowafanyia Wapinzani sio sawa alijiondoa ili kudhoofisha upinzani na ameamua kuja kuua kabisa upinzani haswa chama kilichomkaribisha... kama hawataki tena akae tu pembeni kuugua ukimwi sio lazima uambukize na wengine ili mfe wote
mbona hata alipoamua kakaa pembeni aliitwa msaliti acha afanye yake
 
Hiv kitendo alichofanya lipumba 2015 cha kukaa pembeni hamkioni kama alifanya kitendo cha kidemokrasia angekuwa mbowe asingeweza
lipumba alikaa pembeni kwa sababu hakutaka kuwa mmoja wa wanafiki

lowasa alikuwa ni picha ya ufisadi ambayo wapinzani walikuwa wanawaonyesha wananchi
sasa ilipotokea amekuwa mgombea wa urais kupitia umoja wa ukawa hapo lipumba pamoja dr slaa walipoona ugumu wa kumnadi mtu ambaye walishamwitaa fisadi papa
 
True upinzani ni watu siyo chama hapo ndipo wanapo kosea wapuuzii wengi wanadhani ni chama
 
Uprofesa hauna maana kwa ajili ya mtu huyu..!
 
Mbona kuumaliza huu mgogoro nirahis sana,,maalim kumpigia sim lipumba wakutane wenyewe wawili2 wayamalize halafu waite vyombo vyahabar wawaeleze wafuas wao kua hakuna tofaut.ili kama lipumba ametumwa kumuua seif lazima atakataa maana kazi yake itatibuliwa maalim atakaporud ila kama lipumba atakubali nakumaliza tofaut na seif itakula kwa chadema maana wao ndo wanaoivunja cuf.kwamfano mpaka sasa ugomvi mkubwa wa lipumba niule muungano wa ukawa umeimeza cuf na nccr vibaya sana hata kuhatarisha cuf kutoonekana

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio kweli, baada ya kujiunga na Ukawa ndo wakapata walau viti vingi bara. Hivyo usipotoshe ukweli.
 
Mbinu waliyotumia ccm ni pigo kwao. UPINZANI sio CUF kama chama Bali ni watu. Na watu hao wanaweza kuamua kuwa chama chochote, na wakiamua kuwa Chadema ccm ndio watajuta!
Kwa nn asianzishe chama kipya ila akiite "CUF Asilia"walau neno CUF liendelee kumtambulisha maana si rahisi kumtenganisha nalo kihistoria...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CUF HAITAKUWA IMARA TENA! MISSION IMEKAMILIKA KWA 80+℅

CUF sasa inaishilia, ni kama mpango unakamilika, mpango mkakati umetengenezwa kimkakati zaidi, kuhakikisha CUF haina nguvu tena, ili kuleta unafuu visiwani. Wabunge wa majimbo wakishavuliwa uanachama, majimbo yao yatakuwa wazi, uchaguzi utarudiwa, kama hujui ni mpango,: kumbuka kauli ya juzi ya mkurugenzi wa tume ya uchaguzi, pale aliposema' ikiwa wabunge wa CUF watavuliwa uanachama, tume imejiandaa kwa dharula yoyote na bajeti ipo! Akili kumkichwa' mkurugenzi wa tume anazungumzia uchaguzi mdogo kwenye majimbo ambayo bado yana wabunge! MISSION

Lipumba sasa anatambuliwa na kila taasisi ya sirikali, anatambuliwa na Bunge, anatambuliwa na Msajili, anatambuliwa mpaka na taasisi ya jikoni! MISSION

Kete kwa upande wa CUF Halisi ilikuwa imebaki moja tu (MAHAKAMA) baada ya makosa kufanyika nyuma! Ndiyo makosa yalifanyika mwanzo kabisa kwa upande wa Maalim Seif kumdharau Lipumba na kumuona ni mtu mmoja tu anayetapatapa kisha atatulia, hawakumuona mapema aliyekuwa nyuma ya Lipumba! Hili lilikuwa Kosa kubwa! Wamekuja kushituka na kuiona nguvu yake kipindi ameingilia bodi ya wadhamini ya CUF! Hapo ndo walishituka na kumbe tayari walikuwa wamechelewa! Walipaswa kumshughulikia mapema!
Sasa kete ya mahakamani nayo inaanza kufeli, kwa nini nasema inafeli?

1😛amoja na kesi ya kutomtambua Lipumba na kauli ya Msajili kuwa mahakamani! Bado Lipumba ameendelea na shughuli za chama kwa kujitanua hadi kufukuza wabunge bila woga na hakuna mhimili unaohoji!

2: Kutupiliwa mbali kwa mapingamizi ya wabunge wa CUF waliovuliwa uanachama, ni pigo kubwa kwa upande wa Maalim Seif! Hata wakirekebisha vifungu walivyotakiwa kuvirekebisha, wao wako mahakamani, Lipumba anaendelea na shuguli za chama huku akijipanga kuwaita na kuwahoji wabunge wa majimbo!

3: Kutotambulika kwa maazimio ya CUF upande wa Maalim wa kuwavua ubunge wabunge wawili ni pigo kubwa pia.

NANI ALAUMIWE

1. Mtatiro;
Ndiyo, huyu ni mtu wa kwanza kabisa kulaumiwa na wana CUF' atanisamehe. Yeye alipewa jukumu kuwa mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya CUF, Lakini amekuwa akifanya siasa za mtandaoni zaidi, kila Lipumba akifanya jambo, yeye huja kulalamika mtandaoni na hukomea kuandika tu bila ya kuelezea njia mbadala ( rejea post zake kwenye plofile yake) Sasa kama yeye kiongozi analalamika na kujibu mapigo ya Lipumba mtandaoni, wengine watafanyeje? Yeye huiongelea CUF baada tu ya Lipumba kufanya kisanga, Lipumba akiwa kimya' na yeye yuko kimya. Kwa hiyo amekuwa akicheza ngoma ya Lipumba!

2. Maalim Seif
Yeye namlaumu kwa kutochukua hatua mapema, Lipumba hakupaswa kupewa nafasi mapema, naye sasa amekuwa akijibu mapigo ya Lipumba tu badala ya Lipumba kujibu mapigo yake! Lipumba akiita Baraza lake, naye anaita lake, Lipumba akifukuza wabunge, naye anafukuza! Amechelewa sana!

NINI CUF YA MAALIM IFANYE?
Kwa sasa CUF ya Maalim imebanwa sana na Lipumba, na naona imebakiwa na option mbili tu!

1. Mahakama;
Mahakama pekee kwa sasa ndo imebaki kuweza kuamua kama CUF iwe ya Lipumba au ya Maalim. Na ikitokea mahakama ikaamua kuwa CUF iwe ya Lipumba, Maalim atabaki na option mbili tu, mosi kuungana na Lipumba au

2. Kuongeza nguvu CHADEMA.
Option ya mwisho kabisa kwa Seif ni kutangaza kuachana na siasa za CUF ya Lipumba na kuongeza nguvu upande wa CHADEMA. Faida kubwa kwa upande wa CHADEMA ikiwa hili litatokea, ni kupata wafuasi wengi Zanzibar bila chenga! Na hapo ndipo msemo usemao "Waliokuwa nyuma ya Lipumba waliruka mkojo wakakanyaga kinyesi" utatimia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nakupatia salute aisee. Umeona mbali sana kuliko nilivyokuwa nadhania. Hongera sana
 
Ni kweli kabisa, kwa kauli ya tume ya uchaguzi ambayo badala ya kuangalia namna gani ya kulinda kodi ya wananchi kutumika vibaya, wao ndo kwanza wamekuwa msitari wa mbele kuchochea na kubariki maovu yanayoendelea ndani ya chama cha CUF, hii inadhihirisha ya kwamba tume yetu ya uchaguzi haijawahi kuwa huru toka ianzishwe miaka yote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wabunge hao watahamia chadema na watachaguliwa tena kupitia chadema
Hiki ndicho kinachotakiwa Maalim ndio katumika bila kujijua au kwa makusudi Lipumba kamuita Mara ngapi yeye akawa anashikiwa Akili na watu wenye Akili ndogo.Asilalamike CUF wameshaizika rasmi.Chadema juuuuuuu juuuuuuu zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumuunganisha Maalim Chadema litakuwa kosa kubwa kuliko yote la kimkakati alilofanya Sizonje.
WE WILL BE A LEGION AND NOTHING CAN STOP US!

You never want your enemy to be united against you , Sizonje makes us more than united, he makes us strong.
True
 
Hawa uliosema walaumiwe hawastaili lawama kumbuka Lipumba alujiuzulu uongozi akarudi kwa ajili ya harakati anazozifanya sasa tayari wewe umeshakiri yakuwa Lipumba anajulikana na kila tasisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
new era is coming,2020 ndio mwisho wa cuf kama jina, upinzani ni watu sio chama,upinzani hauwezi kufa, kinachoendelea saivi ni hasara kubwa kwa watawala,wanatumia mbinu zao nyingi sana kwa wakati mmoja ili kupambana na upinzani,

wanachofanya bila ya kujijua ni kujenga nguvu kubwa sana ya upinzani na sio kuua,binadam tulivyo tunajifunza kutokana na makosa,kila ujanja wanaotumia kukandamiza watu,unatafutiwa ufumbuzi, mbinu zao zikishamalizika nao wao watamaliza pia
Mku ni kweli kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom