Uchaguzi 2020 CUF yaapa kuingia Ikulu

Uchaguzi 2020 CUF yaapa kuingia Ikulu

Corticopontine

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2019
Posts
666
Reaction score
1,277
UCHAGUZI WA MWAKA 2020: Chama cha Wananchi CUF chataka mazingira mazuri

Chama cha wananchi CUF kimetoa wito kwa Rais John Magufuli kukutana na viongozi wa Vyama vya Siasa ili kuweka mazingira mazuri ya kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi Cuf Prof Ibrahim Lipumba katika mkutano wake na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam wakati akitoa salamu za mwaka mpya wa 2020

Katika hatua nyingine chama cha Wananchi CUF kimejipanga kuweka wagombea nchi nzima katika ngazi zote madiwani, wabunge na Rais hivyo tunawaomba watanzania wote kuwa imara katika kuhakikisha kuwa uchaguzi Mkuu 2020 unakuwa wa huru na wa haki.

Prof Lipumba amesema kuwa ushiriki wa wananchi katika kuamua mambo yanayogusa maisha yao ni suala muhimu la maendeleo endelevu na ujenzi wa demokrasia ni sehemu muhimu ya maendeleo na kuwanyima wananchi kuchagua viongozi wanaowataka ni kudumaza maendeleo ya kisiasa na kijamii. Sisi Chama cha wananchi CUF ndicho chama kitachoingia IKULU Mwaka 2020
 
Chama cha wananchi CUF kimetoa wito kwa Rais John Magufuli kukutana na viongozi wa Vyama vya Siasa ili kuweka mazingira mazuri ya kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.
Mmoja wa washindani ndie andae mazingira mazuri kwa anaoshindana nao ili wshiriki vizuri. Kweli huyu ni Prof, Made in Tanzania.
 
Kama hawana akili vile,
Waanze kufungua kesi mahakamani kuyapa madai yao uhalali.

Zama hizi haki hudaiwa hasa kwenye mahakama huru
 
Kuingia Ikulu kula Visheti na Kahawa kama Chadema
 
This is a joke.


Anyways.

Kila mtu ashinde mechi zake bwana.
 
Vyama vya kisanii utavijua tu.
Kwani ndio nini kuapa kuingia ikulu?
Haya mie naapa: Haki ya mungu na mtume mwaka 2020 lazima niingie ikulu!
Halafu tuone hata kama nitakanyaga tu bustanini
 
Corticopontine,

Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu. Hamuoni NASA, JUBILEE ya BBI Kenya? Mtakua link kutambua haya mautitiri ya vyama hiyo dili?

Kama adui anajulikana na ni wetu sote kwanini tusiyavunje mavyama haya physically au logically tukamwondosha adui yetu kwanza and the rest baadaye?
 
Daah hizi Ni akili za Prof kweli...
Mzee lipumba apunguze matumizi ya Mihadarati asiwe anaota mchana.

Hajui Kama CUF ilipoteza mwelekeo baada ya yeye kurudi na kuleta mgogoro ndani ya chama mpaka kikagawanyika.

CCM Itemwe, Chadema Itemwe, ACT wazalendo Itemwe.. heti ichaguliwe CUF kwa akili zipi za watanzania?
Prof plz punguza kutumia Mihadarati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lipumba hata ingia tena ikulu kupata kitu chochote zaidi ya alichopata alipokwenda kusaliti UKAWA na kutimkia Rwanda pale ndipo alipo jinajisi, sasa amebaki kukodoa macho tu. Ikulu ataenda kusalimia au kuomba msamaha kama Nape.
 
Badili gia angani kama 2015! Huku CCM ni "Kazi Tu"!
Mnajidanganya mwenzenu muasisi wa hiyo kauli yuko zake Rubondo anakula bata, kazi tu muachieni BASHIRU yule nahisi hana kwao, wala hana hobby.
 
Back
Top Bottom