CWT mnaomvimbia kichwa Rais jifunzeni unyenyekevu wa Shaka Hamdu Shaka mtafika mbali vyeo ni dhamana ya muda Tu

CWT mnaomvimbia kichwa Rais jifunzeni unyenyekevu wa Shaka Hamdu Shaka mtafika mbali vyeo ni dhamana ya muda Tu

CM 1774858

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2021
Posts
5,621
Reaction score
5,029
IMG-20230127-WA0186.jpg
Shortly,

Tumesikitishwa sana na hawa vijana wenzetu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) walioamua kuidhalilisha taasisi nyeti ya Urais Tanzania huenda kwa kujua au kutokujua,

Nikweli, Tunafahamu Rais hufanya UTEUZI kwa mtu yeyote anayedhani anaouwezo wa kumsaidia katika kutekeleza majukumu yake ya siku kwa siku bila kumtaarifu.

Uteuzi ni ishara ya imani ya kiwango cha juu toka kwa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuja kwa mteuliwa ikiwa ni pamoja na Ukoo au familia yake.

Hebu fikiri hii, Nchi yenye watu takribani 62M Wewe unateuliwa kisha unamvimbia aliyekupatia hiyo heshima, hakika hili ni jambo baya huenda kuliko Ubaya wenyewe.

Hebu Vijana wa Tanzania bila kujali Itikadi zetu za Kisiasa & dini tujifunze kitu toka kwa aliyekuwa Katibu wa NEC Itikadi & Uenezi wa Chama cha Mapinduzi ( CCM ) Mhe Shaka Hamdu Shaka.

Pamoja na kwamba Mhe Shaka Hamdu Shaka ambae Sasa ni mkuu wa Wilaya ya Kilosa alikuwa ni boss wa ma-RCs, ma-DCs, ma-RAS, Mawaziri wote akihudumu kama kiongozi wa ngazi ya juu wa Chama,

Leo sote tumashahidi baada tu ya kuondoshwa kwenye nafasi hiyo na kuteuliwa kuwa DC Kama ilivyo kwa viongozi hao waandamizi wa CWT Jamaa hakuhoji, hakususa Wala kukunja sura bali alikuwa ndio DC wakwanza kula kiapo miongoni mwa ma -DC wote walioteuliwa katika batch ile.

Tunahitaji kuwa na Taifa lenye vijana wenye nidhamu ya Uongozi na viongozi aina ya akina Shaka Hamdu hasa kwa kulinda Mila na Desturi zetu kama Watanzania kwani ni mbaya kutumwa na mkubwa hata kama hana cheo ukakataa.

 
Hata Mimi niliamini kabisa Shaka angegomea U-DC hawa CWT huenda kuna jambo wanaficha hapo ofisini wanaogopa akiondolewa litabumbuluka
 
View attachment 2502548
Shortly,

Tumesikitisha sana na hawa vijana wenzetu wa Chama cha Mapinduzi walioamua kuidhalilisha Taasisi nyeti ya Urais Tanzania,

Tunafahamu Rais hufanya UTEUZI kwa mtu yeyote anayedhani anaouwezo wa kumsaidia katika kutekeleza majukumu yake ya siku kwa siku bila kumtaarifu,

Uteuzi ni ishara ya imani ya kiwango cha juu toka kwa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuja kwako mteuliwa pamoja na Ukoo au familia yako,

Hebu fikiri nchi yenye watu takribani 62M Wewe unateuliwa then unamvimbia aliyekupatia hiyo heshima hakika hili ni jambo baya huenda kuliko Ubaya wenyewe,

Vijana wa Tanzania bila kujali Itikadi zetu za Kisiasa tujifunze kitu toka kwa aliyekuwa Katibu wa NEC Itikadi & Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Mhe Shaka Hamdu Shaka,

Pamoja na kwamba Shaka Hamdu Shaka alikuwa ni boss wa maRCs,maDCs,Mawaziri wote Kama kiongozi wa Chama mkubwa bado baada ya kuondoshwa na kuteuliwa kuwa DC Kama hao viongozi wa CWT Jamaa hakuhoji Wala kukunja sura bali alikuwa ndio DC wakwanza kula kiapo miongoni mwa ma -DC wote walioteuliwa katika batch ile,

Tunahitaji kuwa na Taifa lenye vijana wenye nidhamu ya Uongozi aina ya akina Shaka Hamdu hasa kwa kulinda Mila na desturi zetu kama Watanzania kwani ni mbaya kutumwa na mkubwa ukakataa,
Rais mwenyewe kachemka kuteua watu kabla ya kuwasiliana nao.

Serikali inabumba na kugangaganga.
 
Za chini chini ni kwamba rais alishapata ABC Zote kuhusu madudu pale CWT. Kwamba mtu na katibu wake hawaelewani pia taasisi Ina perform chini ya kiwango. Akaona awateue kuwa ma DC ili ku solve ile gap lakini wakakaidi na kwenda kula upepo Tanga😀😀

Pia fununu kwamba salary pale cwt ni 7.8m wakati DC ni around 3m Sasa ndo kinawatoa roho.

Kuna hati hati wakakosa vyote baada ya kumparua mama. Mmoja kapewa wiki Moja aripoti bukoba uko.
 
Wewe bwana siyo kila mtu anaongozwa na njaa na kutaka vitu asivyovitolea jasho.

Taaluma ya mtu iheshimike mtu anajisikia secure kuwa mwalimu kuwatoa watoto ujinga aachwe ameridhika na hali yake ujinga wa kwa sababu ni rais unapangia watu kazi unavyotaka uachwe na hii ndo hufikia kusababisha utendaji mbovu kwa sababu mtu ni mwalimu amezoea kusimamia watoto leo umtake akagombane na watu wazima wenzake hiyo haitakiwi.
 
View attachment 2502548
Shortly,

Tumesikitisha sana na hawa vijana wenzetu wa Chama cha Mapinduzi walioamua kuidhalilisha Taasisi nyeti ya Urais Tanzania,

Tunafahamu Rais hufanya UTEUZI kwa mtu yeyote anayedhani anaouwezo wa kumsaidia katika kutekeleza majukumu yake ya siku kwa siku bila kumtaarifu,

Uteuzi ni ishara ya imani ya kiwango cha juu toka kwa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuja kwako mteuliwa pamoja na Ukoo au familia yako,

Hebu fikiri nchi yenye watu takribani 62M Wewe unateuliwa then unamvimbia aliyekupatia hiyo heshima hakika hili ni jambo baya huenda kuliko Ubaya wenyewe,

Vijana wa Tanzania bila kujali Itikadi zetu za Kisiasa tujifunze kitu toka kwa aliyekuwa Katibu wa NEC Itikadi & Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Mhe Shaka Hamdu Shaka,

Pamoja na kwamba Shaka Hamdu Shaka alikuwa ni boss wa maRCs,maDCs,Mawaziri wote Kama kiongozi wa Chama mkubwa bado baada ya kuondoshwa na kuteuliwa kuwa DC Kama hao viongozi wa CWT Jamaa hakuhoji Wala kukunja sura bali alikuwa ndio DC wakwanza kula kiapo miongoni mwa ma -DC wote walioteuliwa katika batch ile,

Tunahitaji kuwa na Taifa lenye vijana wenye nidhamu ya Uongozi aina ya akina Shaka Hamdu hasa kwa kulinda Mila na desturi zetu kama Watanzania kwani ni mbaya kutumwa na mkubwa ukakataa,
NAOMBA HIZO NAFASI MOJA APEWE MTOA MADA CM 1774858 KAMA BADO HAJATEULIWA
 
Kwa maoni yangu wala kujua sheria inasemaje,Naona wameonyesha utovu wa nidhamu uliotukuka.Kwa nn wakatae kazi ya kutumikia wananchi wengi wakomalie hiyo ya waalimu tu?Shaka anaelewa nini wajibu wa kutumikia uma.
 
Au ambitious za CWT leaders ni kupata uongozi wa kitaaluma sio kisiasa
 
View attachment 2502548
Shortly,

Tumesikitisha sana na hawa vijana wenzetu wa Chama cha Mapinduzi walioamua kuidhalilisha Taasisi nyeti ya Urais Tanzania,

Tunafahamu Rais hufanya UTEUZI kwa mtu yeyote anayedhani anaouwezo wa kumsaidia katika kutekeleza majukumu yake ya siku kwa siku bila kumtaarifu,

Uteuzi ni ishara ya imani ya kiwango cha juu toka kwa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuja kwako mteuliwa pamoja na Ukoo au familia yako,

Hebu fikiri nchi yenye watu takribani 62M Wewe unateuliwa then unamvimbia aliyekupatia hiyo heshima hakika hili ni jambo baya huenda kuliko Ubaya wenyewe,

Vijana wa Tanzania bila kujali Itikadi zetu za Kisiasa tujifunze kitu toka kwa aliyekuwa Katibu wa NEC Itikadi & Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Mhe Shaka Hamdu Shaka,

Pamoja na kwamba Shaka Hamdu Shaka alikuwa ni boss wa maRCs,maDCs,Mawaziri wote Kama kiongozi wa Chama mkubwa bado baada ya kuondoshwa na kuteuliwa kuwa DC Kama hao viongozi wa CWT Jamaa hakuhoji Wala kukunja sura bali alikuwa ndio DC wakwanza kula kiapo miongoni mwa ma -DC wote walioteuliwa katika batch ile,

Tunahitaji kuwa na Taifa lenye vijana wenye nidhamu ya Uongozi aina ya akina Shaka Hamdu hasa kwa kulinda Mila na desturi zetu kama Watanzania kwani ni mbaya kutumwa na mkubwa ukakataa,

Ebu tukuulize ww mtoa post, kweli vijana wa CCM wanala kujifunza kwa Shaka? Kweli? Au ww ni Shaka unajipigia promo humu, is there anything CCM youth can learn from Shaka? Do you know this guy had a big big corruption scandal ya mashamba ya UVCCM Iringa na aliuza back in the days. Na Moro pia uchaguzi wa Meya aliacha corruption scandal.

Unasema vijana wa CCM wajifunze kwa Shaka? Stop this worst propaganda za kutaka kuonyesha Shaka is good, of which he is not at all, na angekuwa mzuri, Mh. Rais Samia angempeleka nafasi ya juu kabisa, ila kampa demotion kubwa hiyo, sbb kuna kitu lazima kaharibu, so acha kuleta propaganda za uongo uongo humu, watu wote sio wajinga humu, nothing, zero, we can learn from Shaka, period.
 
We unajuaje kwamba kuteuliwa ni ishara ya kiwango cha juu cha imani ya Raisi juu ya mtu huyo wakati hata sababu za kumteua huwa hatoi?

Tunajua kwamba kuna teuzi hufanywa ili kumuondoa mtu fulani mahali fulani ili awekwe anayemtaka yeye,na wengine huteuliwa ili aondoke kwenye nafasi kubwa kabla ya kuapa anatenguliwa,mbona huwa hatuambiwi sababu,hio huwa ni ishara ya nini?

Msitake kuukuza U-DC hiivyo wakati kwenye katiba ya warioba watu walipendekeza ufutwe tu.Raisi amuulize mtu kabla ya kumteua ili ajue msimamo wake.
 
Back
Top Bottom