CWT ni Genge la Matapeli wanaokula kwa Mgongo wa Walimu

CWT ni Genge la Matapeli wanaokula kwa Mgongo wa Walimu

OMBI KWA WALIMU WENYE AKILI TIMAMU

Achaneni na CWT bali hamieni CHAKUWAHATA(Chama Cha Kulinda na Kutetea Haki za walimu Tanzania),Huko CWT mtanyonywa hadi mbaki na mafuvu!.

HIKI CHA MA CHA WALIMU HAKINA FAIDA KIFUTWE.
Kumbe hapa Chakuhawata na CWT ,Chakuhawata lini wamemsaidia mwalimu, toka kimeanza 2015 wamefanya jambo gani la utetezi kama sio kula fedha wa walimu tu ..
 
Ndugu mwandishi,

Bahati mbaya umetaja CWT peke yake, labda kwa sababu familia yako inaathirika na chama hicho. Na pia popularity ya hiki chama, kutokana kuwa walimu ni kada yenye watumishi wengi zaidi wa umma Tanzania hii.

Lakini mimi naomba nikuhakikishie kuwa, hili sio CWT peke yake. Ni vyama vyote vya Watumishi (Workers' Union) vinakata mishahara ya watumishi na hakuna kinachofanyika.

Imagine, kila mwezi watumishi wote wanakatwa 2% kutoka kwenye mishahara yao. Na hii ni sheria eti, imepitishwa na bunge letu tukufu.

Mbaya zaidi, kama mtumishi hataki kujiunga chama chochote, anakatwa bila kupenda. Hii inaitwa ada ya uwakala. Ni sheria pia imepitishwa na bunge letu tukufu. Hii ada ya uwakala pia wanakata 2% kama mwanachama.

So hivi vyama vyote, CWT, TALGWU, TUGHE hakuna kitu cha maana sana vinafanya. Ni mpango wa kula fedha za watumishi tu.
 
Kuhusu kuchangia shughuli kama hizo za mwenge nk inawezekana ni mkakati wa wilaya husika kulingana na muktadha wa eneo lao na pia nature ya viongozi wa hapo. Sio kote iko hvyo... ndio maana ni vema kutumia neno “baadhi”. Hata hivyo mapungufu ya cwt yapo na yanahitaji kurekebishwa haraka.
 
Hao Cwt kwakuwa ni chama ambacho kina wanachama wengi kila wilaya bado hakiwezi kuacha wajibu wake wa msingi wa kulikemea hili suala la wanachama wake kuchangia huo mwenge hata kama sio country wide.Kwa bahati mbaya hao Cwt hawawezi kulikemea hilo kwasababu ni wanufaika wa hiyo dhuluma kwa sababu ya kuogopa kuwaudhi watawala na wakakosa teuzi mbeleni
 
Kumbe hapa Chakuhawata na CWT ,Chakuhawata lini wamemsaidia mwalimu, toka kimeanza 2015 wamefanya jambo gani la utetezi kama sio kula fedha wa walimu tu ..
Heri CHAKUHAWATA wanaokula 5000/_ kuliko CWT wanaokeketa 2%ya mshahara wa mtumishi Kila mwezi ambazo ni kati ya shs 10,000/- hadi zaidi ya 50,000/- kwa mwezi kwa baadhi ya watumishi.
 
Back
Top Bottom